Jinsi Mbunge Katani(CUF) alivyobadili gia angani kuhamia CCM. Mbatia na Bwege walimsihi asihame

NGolo Kante

Member
Feb 28, 2017
80
131
Nanai anahama na nani anabali lilikuwa ni swali linalogonga vichwa vya wengi Alhamisi iliyopita ya Novemba 15 ambayo kwa mujibu wa CCM iliuwa ni siku ya mwisho kwa Wabunge na Madiwani kutoka upinzani wanaotaka kuhamia ndani ya chama hicho.

Joto lilipanda na kuwavuruga wabunge hasa baada ya Mbunge wa Temeke CUF, Abdalah Mtolea kutagaza kujiuzulu Ubunge na kuhamia CCM

Duru za Siasa zinadai kuwa Katani Katani mapema siku hiyo alionekana katika viunga vya Bunge akiwa na Mtolea jambo hilo liliwahusisha wawili hao kujiuzulu na baadaye ikatajwa kuwa Wabunge wawili James Mbatia (NCCR) na Seleman Bungara 'Bwege' (CUF) walimnasua Katani

- ''Ni kweli Katani alikuwa miongoni mwa waliotakiwa kuhama siku hiyo(Alhamis) lakini kuna Wabunge wawili walizungumza naye na kumsihi sana asihame, alikuwa njiani kuhama kama alivyofanya Mtolea Bungeni'' Alisema Mbunge mmoja ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini.

Katani alipozungumza na Mwananchi alisema hana wazo la kuhama na hata akihama hawezi kwenda CCM waliosema anaondoka walikuwa na hoja zao

Mbatia ambaye imeelezwa kuwa alihusika kumshawishi Katani asihame, alipoulizwa kuhusiana na sakata hilo alisema ni kweli alizungumza na Katani kipindi ambacho tayari 'nilishatoka Ikulu kuzungumza na Rais Magufuli mbali na mengine nilimwambia 'Hekima, umoja na amani inalisimamisha taifa'

Kuhusu Katani Mbatia anasema ''Ni kweli Katani aliniambia anataka afanye uamuzi mgumu kwasababu anaona kuna giza nene katika chama chake(CUF)''

Baada ya kunieleza hayo nilimweleza mambo manne ambayo ni majukumu ya Bunge tuliyofundishwa na Spika Mstaafu Pius Msekwa yanayopaswa kuzingatiwa kabla ya kufanya maamuzi

Mambo hayo ni taifa lake, jimbo lake, chama chake na dhamira yake binafsi..

Chanzo: Mwananchi
 
Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kusini Selemani Bungara “Bwege” amefunguka juu ya mazungumzo yake na Mbunge wa Tandahimba Katani Katani yalivyopelekea mbunge mwenzake kubadilisha msimamo wa kuhamia Chama Cha Mapinduzi.



KATANI.jpg

Mbunge wa Tandahimba Katani Katani.​
Kauli hiyo ya Mbunge Bwege imekuja kufuatia tetesi zilizozagaa wiki iliyopita zikimtaja Mbunge wa Jimbo la Tandahimba, Katani Katani kutaka kuhamia Chama cha Mapinduzi CCM kutoka CUF.
Akizungumza na www.eatv.tv Mbunge Bwege amekiri kuzungumza na Mbunge huyo siku ambayo Mbunge wa Temeke Abdallah Mtolea alitangaza kukihama chama chake cha CUF.
Mheshimiwa Katani alinambia yeye ahami, lakini nilimfuata kumuuliza kuhusu kuhamia CCM akanijibu hawezi kuhama, kama kumshawishi, nilimshawishi kwa njia hiyo japo tuliongea kwa muda mrefu na nikaongea kwa muda mrefu sana kuanzia saa 7 hadi saa 11,” amesema Selemani Bungala.
Na Kwa mujibu wa maelezo yake alivyotoka kwangu kabla ya kwenda bungeni alinambia anaenda kwa Mbunge wa Vunjo James Mbatia japo sikujua alizungumza nini, ila baada ya hapo alikanusha bungeni kuwa hawezi kuhama chama,” ameongeza.
Novemba 15 mwaka huu ikiwa ni siku ya mwisho ya Chama Cha Mapinduzi kuwapokea Mbunge mmoja wa Chama Cha Wananchi CUF Abdallah Mtolea alitangaza kujiuzulu nafasi yake na baadaye kutangaza kujiunga na Chama Cha Mapinduzi.
 
Maelezo hayako vizuri, nani alimshawishi nani?
Au CUF kwa CUF wanashawishiana kuingia CCM?
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom