complex31
JF-Expert Member
- Jun 15, 2016
- 379
- 1,208
Sauli ni kampuni ya bus za kusafirisha abiria kutoka Mbeya kuja Dar na Dar kwenda Mbeya, kampuni hii ina takriban miaka miwili toka ianze kazi rasmi katika ardhi ya Tanzania.
Katika miaka miwili hiyo kumekuwepo na changamoto mbalimbali lakini kikubwa ni haijawahi kupata ajali.
Mmiliki wa hii kampuni anaweza kua ni mfano mzuri wa kuigwa kwani ameweza kutonesha wengi biashara ni kitu ambacho huanzia mbali sana.
Miaka zaidi ya saba nyuma njia ya Nyanda juu Kusini Dar - Iringa - Mbeya - Tunduma - Sumbawanga na Songea kampuni kutoka China ya NEW FORCE na GOLDEN DEER walifanya mapinduzi makubwa sana kwa kuweza kuteka masoko haya na kua na abiria wa uhakika.
Mwaka 2018 SAULI ilianza kazi rasmi kukiwa na bus mbili tu moja inaanzia Dar kwenda Mbeya na nyingine inaanzia Mbeya kurudi Dar na kwa nauli ya 44,000 ambayo mpinzani wake wa karibu New Force na Golden Deer kwa nauli hii ya 44,000 aliweza kwenda Dar mpaka Tunduma.
Mwanzo hua mgumu sana lakini Sauli alikuja na itikadi zake za kufanya abiria wachague gari lake waache kupanda ya mpinzani
Kwanza aliweza kujali muda kitu ambacho kilifanya apendwe sana na kuanza kua na jina ingali ana gari mbili tu
Alitumia mbinu ya SCANIA pamoja na BENZ ni gari za luxury na bora kuliko gari za michina kitu ambacho pia ni kweli hivo pia iliweza khmuongezea credit ya biashara yake
Kampuni hii ya SAULI iliweza kupata jina na umaarufu katika kipindi kichache sana hivo kupelekea kuongeza bus zingine mbili aina na kufanya kua na total fleet ya bus 4 ambazo tatu ni Scania Gemilang na moja ni Mercedes Benz
Mzee huyu mwenye kampuni ameweza kutufundisha kuamini kwa kile tunachoona kinafaa kutokubali kuyumbishwa na kumuangalia mpinzani wako kwa jicho la karibu ili kujua wapi pa kumuovertake katika biashara