Jinsi hukumu ya Jaji wa Rufaa ilivyookoa Maisha ya Hakimu na Mkuu wa Taasisi

Carlos The Jackal

JF-Expert Member
Feb 6, 2017
24,036
71,267
Ninakuandikia wewe hakimu ambaye umehamishwa miezi michache ilopita, kufuatia rushwa zako zinazosababisha mlundikano wa kesi mahakama ya rufaa pale.

Haya maisha kuna wanaoamini kisasi sio chako, na kuna sisi tunaoamini ya duniani tunamalizana hapa hapa wenyewe kisha tunatubu.

Kila upande uheshim mwengine kwa sababu ni uchaguzi wa maisha. Wewe wakulipiza kisasi kikubwa ukumbuke kutokucha alama.

Nyie wenye nafasi ambazo utendaji wenu unahitaji kua watu wa haki, usawa, basi fanya ivo. Kutoka nje ya njia hiyo maana yake ni kuumiza na hata kuua watu wengine, sababu ya tamaa ya pesa.

Ukitaka kufa mapema, dhulumu mali ya mtu/watu, shiriki kudhulumu mali ya mtu.

Ipo hivi mazeee, kila mmoja wetu humu ana kijijin kwao huko kwa mababu, na mababu zenu huko wana maeneo makubwa makubwa ya ardhi.

Sasa iko hivi, mababu zangu upande fulani wa mzazi mmoja, huko kijijini walikua na maeneo makubwa makubwa sana, mwaka fulani mababu hao waliigawia taasisi fulani sehem ya ardhi heka 20 ivi bure, miaka ikasogea masuala ya kupima maeneo, mipaka nini kila kitu kikawa sawa yaan wazee wakawa wamiliki kisheria.

Sasa kizazi cha mababu yaan sisi hapa kuanzia wazazi mpaka vijukuu, tukawa watu wa mjini ,na ivo yale maeneo yakawapo tu kwaajili ya atakayekua anashindwa mjini anaenda kulima ila kwakua tulikua tunapishana nahiyo taasisi kimipaka, tukawa tunawaruhusu wafanye shughuli za kilimo eneo zima.

Mwaka fulan ndugu wawili wakaona wakalime ilikua 201...

Sasa ile taasisi kwakutumia pesa vibaya, wakaanzisha chokochoko, wakidai eneo zima ni lao, kwamba wao ndio walikua wanatukodisha, aiseeee taasisi ilijipanga chapchap, wakawaonga baadhi ya wazee vijijin, viongozi, mara kesi mahakamani.

Sasa kama nilivyosema, ndugu wengi tuko mjini, kwahiyo masuala ya shamba hamna mwenye mpango nayo.

Lkn wale ndugu wawili walorudi, aisee wana familia, lkn shamba bado ni kielelezo chetu, basi wazee wakubwa wakasema wacha kesi iendelee n.k lkn wakawa hawaifatilii, unajua wakili analipwa eehh!

Basi mimi na kaka mwingine tukasimama kwelikweli, lakini ile taasisi ilikua na hela mazee, licha ya vielelezo viingi tulopeleka n.K lkn kesi ikawa inaelekea kwao.

Hakimu akawa anataka tumpe kiasi fulani cha pesa ili atupe ushinde. Nikasema hapana.

Nikakumbuka nina mwanangu tulipiga naye chuo, ni Muha, nikamuelezea wee akanipa namba za baba yake mdogo, naye akaniunga na mganga mmoja wa jadi yupo Kibondo.

Mganga akaniambia niende, nikapanda bus nikafika Kigoma - Kibondo.

Kumbuken wakati huo kesi inaendelea mganga akaniambia kwanza tuweke nyoka shamban ,ili asikanyage yoyote zaidi ya wa uko wetu, hapo nikaanza 1m)

Nakumbuka tukapanga safari na kurudi shambani huku kijijin mimi na mganga, yule mganga alienda kuzindika shamba usiku wa saa saba , basi baada ya siku mbili tatu tetesi zikaanza , kwenye shamba kuna joka, anafukuza. Mganga akaondoka zake kurudi.

Kesi, imeenda wee, taasisi kwa kuhonga, hakimu mpenda hela, si akawapa taasisi ushindi.

Mwanasheria wetu nguli, wawili msomi akaamua kukata rufaa.

Huku kesi ya rufaa ikiendelea, ile taasisi ikawa inajitapa sanaaa wakasema hakimu ni wakwao lazima wangeshinda ,maneno ya dhihaka kwelikweli.

Nikasema kwakua babu marehem alishakufa, nayeye ndio aliwapa sehem ya eneo lake, leo wanamdhihaki lazima tusiwaache.

Nikamtafuta mganga yule, mganga akasema unatakaje? Nikamwambia nataka umuondoe hakimu, na mkuu wa hii taasisi.

Mganga akaniambia nimpe siku nzima awatazame kama wanaingilika.

Basi siku ya kwanza kimya, yapili akanitafuta, akaniambia watu wake wamemwambia wanaingilika kwakua tayari kiroho wana dhuluma.

Gharama akaniambia milioni 4, watu wawili.

Basi akasafiri akaja, kwanza tukamhitaj amshugulikie mkuu wa taasisi, mganga nakumbuka ule usiku wa manane alienda kwenye nyumba ya mkuu wa taasisi akaondoka na mchanga,akarudi kwetu.

Akachukua jogoo mweupe, tukaingia shamban, tukachimba kaburi la urefu wa mita moja.

Kisha mganga aka tumia zaidi ya nusu saa kufanya ulozi mle ndani ya kaburi na jogoo, akamchinja, alivyo toka juu tukaanza kufukia kisha akasema, nitamuita huyu jogoo, akitoka mavumbin akiwa hai, basi jamaa ndani ya miezi miwili anakufa.

Mganga akaanza kuita, mara jogoo hilo likaibuka, akalishika na kulirusha hewan, jogoo alipaa kama ndege hatukumuona teeeeena .

Wakati huoo rufaa inaendeleaaa kusikilizwa kwenye tarehe tunazopangiwa.

Ilichukua siku kama sita, tukapata taarifa mkuu wa taasisi kalazwa.

Tukahamia kwa hakimu, nayeye bila kustuka, ile siku alienda mganga mwenyewe mpaka ofisin kwa hakimu kuzuga ana mambo binafsi

Mwendo uleule, safari hii mganga alimuua paka mweusi kwa kumvuta kichwa tuu nakutenganisha kiwili wili na kichwa, akafanya ulozii.

Nmechoka kuandika, kwa ufupi.

Hakimu baada ya wiki chache, naye akakumbwa na dhoruba la afya, akalazwa hosp

Sasa mganga akauliza, aminye wakate pumzi?

Nikamwambia siku fulani ni hukumu, wacha hukumu tuione.

Hukumu, Jaji akatupatia ushindi na ndio ikawa pona pona ya hakimu na mkuu wa taasisi kufa

Msiniambie habari za mganga wala mwanasheria
Sitaki PM inbox
Mkijifanya watakatifu sana, hakikisheni mnapenda haki.
Sitaki mambo ya jamaa una roho mbaya (Mimi ni mtu mmoja mwana sana, ila nachukia uonevu kwa mtu au mimi mwenyewe)

KIKUBWA ACHENI DHULUMA, DHULUMA INAUA, NA UTAKUFA TUUU, UTAKUFA, WATU WATAKUZIKA, UTASAHAULIKA, TENDENI HAKI, ACHENI TAMAA ZA VIJISENT NA RUSHWA AMBAZO HUENDA KUUMIZA WENGINE

NARUDIA, KWA DHULUMA?? LAZIMA UFE MAPEMA.
 
Nasema hivi uchawi upo kama mtu atabisha kuhusu jogoo kufufuka kuna ndugu yangu aliumwa saa 8 usiku tulienda makaburini tukaliuliza kaburi mgonjwa atapona kaburi likasema sema ndio

Hiyo tisa funga kazi kuna mtu alienda kuizika kesi kwenye kaburi na akashinda ilikuwa madai ya nyumba huyo mganga ni kiboko yy anadeal na makaburi tu ila sifanyi promo za waganga mimi na sitaki usumbufu
 
Nakumbuka kuna jamaa anaitwa mng'oa kucha aliwahi kuleta uzi hapa jf miaka ya nyuma kidogo akimlalamikia hakimu wa mahakama ya ilala Marehamu Juma kasailo na akasema wazi bila chenga kwamba hakimu huu ndio mwezi wake wa mwisho.

kama kawaida mods wakafuta uzi kumbe kuna watu wamescreenshot na baada ya siku kadhaa hakimu akakata moto kweli uzi ukaletwa hapa jamvini. Sina kumbukumbu nao vizuri ule uzi ngoja nikautafute.
UPDATE: Uzi wenyewe ulifutwa nimefanikiwa kupata huu

Thread 'Familia yataja sababu za kifo cha Hakimu Juma' Familia yataja sababu za kifo cha Hakimu Juma
 
Nakumbuka kuna jamaa aliwahi kuleta uzi hapa jf miaka ya nyuma kidogo akimlalamikia hakimu wa mahakama ya Temeke na akasema wazi bila chenga kwamba hakimu hatoboi miezi mitatu.

kama kawaida mods wakafuta uzi kumbe kuna watu wamescreenshot na baada ya miezi kadhaa hakimu akakata moto kweli uzi ukaletwa hapa jamvini. Sina kumbukumbu nao vizuri ule uzi ngoja nikautafute.
qmqmqq
 
Ungeminya mzee baba ili uwafundishe kazi wanaopenda dhulma.... Ningekuwa mimi ningefyeka familia nzima ya hakimu na mkuu wa taasisi mama eee😊😊😊😊
Ukizingatia na 1m plus 4m zimetumika kumlioa mganga aisee angeminya tuuuu hawa wataleta choko chokk mbele ya safari
 
Nasema hivi uchawi upo kama mtu atabisha kuhusu jogoo kufufuka kuna ndugu yangu aliumwa saa 8 usiku tulienda makaburini tukaliuliza kaburi mgonjwa atapona kaburi likasema sema ndio

Hiyo tisa funga kazi kuna mtu alienda kuizika kesi kwenye kaburi na akashinda ilikuwa madai ya nyumba
huyo mganga ni kiboko yy anadeal na makaburi tu ila sifanyi promo za waganga mimi na sitaki usumbufu
Pm kama kawa dhuluma tunafanyiwa sana
 
" Yule Mganga alienda kuzindika shamba usiku wa saa Saba , basi baada ya siku mbili tatu Tetesi zikaanza , kwenye shamba kuna Joka, anafukuza,... Mganga akaondoka zake kurudi." 😀😃😀

Noma sana
 
Nakumbuka kuna jamaa anaitwa mng'oa kucha aliwahi kuleta uzi hapa jf miaka ya nyuma kidogo akimlalamikia hakimu wa mahakama ya ilala Marehamu Juma kasailo na akasema wazi bila chenga kwamba hakimu huu ndio mwezi wake wa mwisho.

kama kawaida mods wakafuta uzi kumbe kuna watu wamescreenshot na baada ya siku kadhaa hakimu akakata moto kweli uzi ukaletwa hapa jamvini. Sina kumbukumbu nao vizuri ule uzi ngoja nikautafute.
UPDATE: Uzi wenyewe ulifutwa nimefanikiwa kupata huu

Thread 'Familia yataja sababu za kifo cha Hakimu Juma' Familia yataja sababu za kifo cha Hakimu Juma
Hawa wapenda rushwa wajinga sana, hawajui uamuzi wao unaumiza WATU kiasi gani .


Na Wakili Wetu alimwandikia barua ya kumtaka kujitoa kwenye hiii kesi maana Hakim alikua nayeye mwanachama wa hiyo Taasisi.


Tukaenda mpaka Takukuru, haikutosha Ikatumwa Barua kutoka Dodoma ..

(Nisiingie ndani zaidi)


Lkn bado Jamaa akawa jeuri .


Hata kama ni wewe , LAZIMA UMSHUGULIKIE AFE .
 
Kuna binadamu wana roho mbaya sana na wameteketeza familia nyingi kwa tamaa zao
Hakimu amekula kiapo kuwa muadilifu katika kazi zake ila kwa tamaa zake anaamua kupindisha haki

Hajali huyo mtu anamuachia ameuwa mtu au wengine kama nyie kudhulumiwa haki yenu

Kwa kweli mahakimu wengi wataingia motoni ila kama kuna njia za kuwashughulikiwa hapa hapa nalo sawa tu

Hawana Utu kabisa wao hela wanaona ndio muhimu kuliko dhuluma wanazofanya

Nimeumia sana
 
Nasema hivi uchawi upo kama mtu atabisha kuhusu jogoo kufufuka kuna ndugu yangu aliumwa saa 8 usiku tulienda makaburini tukaliuliza kaburi mgonjwa atapona kaburi likasema sema ndio

Hiyo tisa funga kazi kuna mtu alienda kuizika kesi kwenye kaburi na akashinda ilikuwa madai ya nyumba
huyo mganga ni kiboko yy anadeal na makaburi tu ila sifanyi promo za waganga mimi na sitaki usumbufu
Siyo vizur Kaka hujuw watu wanaumizwa kiac gani hebu tufungulie dunia tupate tuanchotaka
 
Mkuu mimi nakuja PM taka usitake nataka kumnyoosha mtu, maisha magumu halafu anatokea kenge mmoja anakuletea stress No!
 
emoji818.png
KIKUBWA ACHENI DHULUMA, DHULUMA INAUA, NA UTAKUFA TUUU, UTAKUFA, WATU WATAKUZIKA, UTASAHAULIKA, TENDENI HAKI, ACHENI TAMAA ZA VIJISENT NA RUSHWA AMBAZO HUENDA KUUMIZA WENGINE
Hebu muulize kama anaweza kuwatenda wahalifu kama CCM na Akina Kingai. Niko tayari kuchangia pesa, Niko hapa Kibondo kijijni Kilemba, mchana nitasogea Hadi pale Busunzu. Nipe connection
 
Back
Top Bottom