Jinsi gani tunayaishi maisha feki

Christiba

Member
May 27, 2020
24
32
Kipindi ambacho mtoto ujifunza KUWA sauti/neno analolisikia mara kwa mara kutoka kwa wazazi wake ni jina lake, mtoto uanza kujilinganisha yeye na neno hilo, ambalo huja kuwa wazo kwenye fikra zake kuwa yeye ni hilo neno nakuwa neno hilo linamuwakilisha 100% hakika. kipindi hicho ndipo binadamu upata utambuzi feki kuwa wao ni kina nani hapa binadamu ujitambua kwa jina lake na kuwa jina hilo ni yeye 100%, kwa kuwa mtoto huwa bado ajapotea moja kwa moja kwenye utu wa jina au neno hilo kuna kesi za watoto kutumia majina yao au neno analoitwa sana kwa kuliweka kwenye mfumo wa nafsi ya tatu kujimaanisha yeye mwenyewe mfano kama jina lake ni James atasema, " James ananjaa" au mtoto ananjaa. Hii inaonesha kwamba anaemuongelea James ni utu mkubwa ulio ndani ya mtoto na James ni utu mdogo wa nje wenye mahitaji ya kimwili. Hapa jina James utumiwa na mtoto kuelezea hali, matakwa na uhitaji unaohusu utu wake wa nje mdogo ambao sio yeye halisi.

Baadaye mtoto ujifunza neno moja la ajabu sana ambalo awali linaanza kama neno masikioni mwake kisha uingia kwenye mchakato wa ubongo kama wazo ambalo matunda yake hubadili fikra za mtoto na utu wake kiujumla, kisha uanza kulitumia neno hilo kujiwakilisha au kuurejelea utu wake neno hilo ni " nina". Neno hilo ulitumia kwa ulinganifu wa jina lake mfano; James ambalo awali alilinganisha Jina hilo na yeye mwenyewe. Hapa mtoto uacha kutumia jina kuurejelea utu wake wa nje na uanza kutumia neno "nina", kwenye fikra zake akidhani yeye ni "nina", mfano hapa ataanza kusema "ninanjaa". Neno "nina" hubadilisha taswira nzima ya fikra ya mtoto na kwa haraka udhoofisha ule utu mkubwa wa ndani na uupa utu mdogo wenye mahitaji ya kimwili nguvu na utawala wa hisia ya kujitambua kwake. Neno mbalo mtoto alielewa kimakosa kuwa ndio yeye halisi linakuja kuchepua maneno mengine kama yangu, changu na vyangu ambayo yanakuja kuwa sehemu ya "nina". Maneno hayo yanakuja kuwakilisha vitu ambavyo moja kwa moja vitakuwa sehemu ya "nina" au sehemu ya utu wa kimakosa, utu huo unaanza kujitambulisha na vitu, usishangae mtoto akiwa analia akisema "nimepoteza mdoli ^wangu^", inamaana kapoteza sehemu ya utu wake ndio maana analia.

Mpaka unaona neno nina linajitanua na kujitambulisha kuwa yeye ndie mtu halisi, ukubwani linakuja kuzaa utambulisho mbali mbali kama; Taifa langu, dini yangu, ninapenda hiki, sikipendi kile, stori yangu, mali zangu na watoto wangu. Kumbuka nina lilianza kama neno ambalo likaja kuwa wazo kwenye fikra ya mtu, nina ni wazo tu wala sio wewe halisi mtoto mara anapozaliwa si ni mtu sio? Mtoto huanza kuzaliwa kabla ya nina kwahiyo ni wazi mtu anaanza kabla ya neno "nina".

"Nina" ni mental construct imetengenezwa na ubongo tu ni wazo lako tu sio Mungu aliekuumba uje kuwa "nina", "yangu", "changu", "vyangu" na "wangu". Yesu alijua hilo aliposema ukitaka kuona kunifuata ujikane nafsi ("nina") yako yaani kuacha kuishi kwenye maisha yasio halisi maisha ya starehe "yangu", mali "zangu" na gari langu na kumfuata. Yesu aliposema ni vigumu tajiri kuuona ufalme wa Mungu alimaanisha matajiri wamezama kwenye utambulisho huu fake wa utu na ni vigumu wao kuishi maisha yao halisi ambayo hayana maneno yangu na changu, langu na vyangu ambayo msingi wake ni neno "nina"ni vigumu kwa wao kuishi maisha yao ya ndani ambayo hayana muunganiko na umiliki wa vitu, utu usio na muunganiko na mali ambao huo uonesha utukufu wa Mungu ndani yetu.

Wewe sio neno nina, wewe sio huyu wa nje, wewe sio hizo mali, wewe sio hiyo furaha feki ya nje, wewe sio hiyo huzuni ya utu nina, wewe umefichwa na neno nina, wewe upo ndani sana nyuma ya huu utu wa nina.

Kwa kumalizia.
• Tunaona unapouhusianisha neno au wazo kwenye ubongo na utu wake ndivyo unavyokimbia uhalisia, ubongo umeonganisha utu na neno "nina" matokeo yake umeleta ubinafsi na kutokujitambua sisi ni akina nani.

• Neno nina limebadilisha maana halisi ya upendo, furaha, na huzuni kwa kuwa tunaishi kwenye utu fake basi hata furaha na upendo baina yetu ni fake, kwa mfano, kama nyumba zinavunjwa kwenye mtaa wako bahati nzuri yako isipovunjwa utafurahi si ndio? Utasema nashukuru Mungu nyumba "yangu" haikuvunjwa. Jiulize ulipaswa ufurahie jambo hilo?

• Je sisi si zaidi ya lile neno "nina" ambalo ndio chanzo cha yangu, vyangu na changu. Maneno yanaundwa na irabu tano tu a, e, i, o na u, je sisi si zaidi ya a, e, i, o na u? Tujitafute leo sisi ni kina nani na inabidi tuishije hapa duniani.
 
Kipindi ambacho mtoto ujifunza KUWA sauti/neno analolisikia mara kwa mara kutoka kwa wazazi wake ni jina lake, mtoto uanza kujilinganisha yeye na neno hilo, ambalo huja kuwa wazo kwenye fikra zake kuwa yeye ni hilo neno nakuwa neno hilo linamuwakilisha 100% hakika. kipindi hicho ndipo binadamu upata utambuzi feki kuwa wao ni kina nani hapa binadamu ujitambua kwa jina lake na kuwa jina hilo ni yeye 100%, kwa kuwa mtoto huwa bado ajapotea moja kwa moja kwenye utu wa jina au neno hilo kuna kesi za watoto kutumia majina yao au neno analoitwa sana kwa kuliweka kwenye mfumo wa nafsi ya tatu kujimaanisha yeye mwenyewe mfano kama jina lake ni James atasema, " James ananjaa" au mtoto ananjaa. Hii inaonesha kwamba anaemuongelea James ni utu mkubwa ulio ndani ya mtoto na James ni utu mdogo wa nje wenye mahitaji ya kimwili. Hapa jina James utumiwa na mtoto kuelezea hali, matakwa na uhitaji unaohusu utu wake wa nje mdogo ambao sio yeye halisi.

Baadaye mtoto ujifunza neno moja la ajabu sana ambalo awali linaanza kama neno masikioni mwake kisha uingia kwenye mchakato wa ubongo kama wazo ambalo matunda yake hubadili fikra za mtoto na utu wake kiujumla, kisha uanza kulitumia neno hilo kujiwakilisha au kuurejelea utu wake neno hilo ni " nina". Neno hilo ulitumia kwa ulinganifu wa jina lake mfano; James ambalo awali alilinganisha Jina hilo na yeye mwenyewe. Hapa mtoto uacha kutumia jina kuurejelea utu wake wa nje na uanza kutumia neno "nina", kwenye fikra zake akidhani yeye ni "nina", mfano hapa ataanza kusema "ninanjaa". Neno "nina" hubadilisha taswira nzima ya fikra ya mtoto na kwa haraka udhoofisha ule utu mkubwa wa ndani na uupa utu mdogo wenye mahitaji ya kimwili nguvu na utawala wa hisia ya kujitambua kwake. Neno mbalo mtoto alielewa kimakosa kuwa ndio yeye halisi linakuja kuchepua maneno mengine kama yangu, changu na vyangu ambayo yanakuja kuwa sehemu ya "nina". Maneno hayo yanakuja kuwakilisha vitu ambavyo moja kwa moja vitakuwa sehemu ya "nina" au sehemu ya utu wa kimakosa, utu huo unaanza kujitambulisha na vitu, usishangae mtoto akiwa analia akisema "nimepoteza mdoli ^wangu^", inamaana kapoteza sehemu ya utu wake ndio maana analia.

Mpaka unaona neno nina linajitanua na kujitambulisha kuwa yeye ndie mtu halisi, ukubwani linakuja kuzaa utambulisho mbali mbali kama; Taifa langu, dini yangu, ninapenda hiki, sikipendi kile, stori yangu, mali zangu na watoto wangu. Kumbuka nina lilianza kama neno ambalo likaja kuwa wazo kwenye fikra ya mtu, nina ni wazo tu wala sio wewe halisi mtoto mara anapozaliwa si ni mtu sio? Mtoto huanza kuzaliwa kabla ya nina kwahiyo ni wazi mtu anaanza kabla ya neno "nina".

"Nina" ni mental construct imetengenezwa na ubongo tu ni wazo lako tu sio Mungu aliekuumba uje kuwa "nina", "yangu", "changu", "vyangu" na "wangu". Yesu alijua hilo aliposema ukitaka kuona kunifuata ujikane nafsi ("nina") yako yaani kuacha kuishi kwenye maisha yasio halisi maisha ya starehe "yangu", mali "zangu" na gari langu na kumfuata. Yesu aliposema ni vigumu tajiri kuuona ufalme wa Mungu alimaanisha matajiri wamezama kwenye utambulisho huu fake wa utu na ni vigumu wao kuishi maisha yao halisi ambayo hayana maneno yangu na changu, langu na vyangu ambayo msingi wake ni neno "nina"ni vigumu kwa wao kuishi maisha yao ya ndani ambayo hayana muunganiko na umiliki wa vitu, utu usio na muunganiko na mali ambao huo uonesha utukufu wa Mungu ndani yetu.

Wewe sio neno nina, wewe sio huyu wa nje, wewe sio hizo mali, wewe sio hiyo furaha feki ya nje, wewe sio hiyo huzuni ya utu nina, wewe umefichwa na neno nina, wewe upo ndani sana nyuma ya huu utu wa nina.

Kwa kumalizia.
• Tunaona unapouhusianisha neno au wazo kwenye ubongo na utu wake ndivyo unavyokimbia uhalisia, ubongo umeonganisha utu na neno "nina" matokeo yake umeleta ubinafsi na kutokujitambua sisi ni akina nani.

• Neno nina limebadilisha maana halisi ya upendo, furaha, na huzuni kwa kuwa tunaishi kwenye utu fake basi hata furaha na upendo baina yetu ni fake, kwa mfano, kama nyumba zinavunjwa kwenye mtaa wako bahati nzuri yako isipovunjwa utafurahi si ndio? Utasema nashukuru Mungu nyumba "yangu" haikuvunjwa. Jiulize ulipaswa ufurahie jambo hilo?

• Je sisi si zaidi ya lile neno "nina" ambalo ndio chanzo cha yangu, vyangu na changu. Maneno yanaundwa na irabu tano tu a, e, i, o na u, je sisi si zaidi ya a, e, i, o na u? Tujitafute leo sisi ni kina nani na inabidi tuishije hapa duniani.
Wewe jifunze matumizi ya h
 
Hapo unazungumzia aina ya maneno.

Kati ya Nomino
Kiwakilishi na Kitenzi.

Ninanjaa
Jokajeusi ananjaa

Ni- ni nafsi ya kwanza umoja ikiniwakilisha Mimi.
A- nafsi ya tatu umoja kumrejelea huyo huyo Jokajeusi.

Hakuna mahusiano katika ya Majina na kitu halisi.
Zingatia lugha ni sauti za Nasibu.

Unachokifanya ninaweza kukiita Nadharia ambazo ni changamsha Genge.

Leo unaweza ukajiita Jokajeusi, kesho Simba, kesho kutwa jiwe lakini Roho ni ile ile. Majina hubadilika, lakini roho haibadiliki.

Hata ungejiita Mungu, bado hakuna uhusiano wa istilahi Mungu na Roho yako.

Ulivyo ndivyo ulivyo. Hubadilishwi kwa majina, au namna ujiitavyo
 
Hapo unazungumzia aina ya maneno.

Kati ya Nomino
Kiwakilishi na Kitenzi.

Ninanjaa
Jokajeusi ananjaa

Ni- ni nafsi ya kwanza umoja ikiniwakilisha Mimi.
A- nafsi ya tatu umoja kumrejelea huyo huyo Jokajeusi.

Hakuna mahusiano katika ya Majina na kitu halisi.
Zingatia lugha ni sauti za Nasibu.

Unachokifanya ninaweza kukiita Nadharia ambazo ni changamsha Genge.

Leo unaweza ukajiita Jokajeusi, kesho Simba, kesho kutwa jiwe lakini Roho ni ile ile. Majina hubadilika, lakini roho haibadiliki.

Hata ungejiita Mungu, bado hakuna uhusiano wa istilahi Mungu na Roho yako.

Ulivyo ndivyo ulivyo. Hubadilishwi kwa majina, au namna ujiitavyo
Fikra zako zimetokana na maneno na sentensi mbali mbali ambazo unazisikiaga katika maisha yako ya kila siku pasipo maneno hakuna fikra na bila fikra hakuna personality jinsi unavyofikiria ndivyo wewe ulivyo. Maneno ya umilikishi ambayo tunayaskia toka udogoni yalitujengea fikra za umimi ambazo ndani yake kuna changu na vyangu bila maneno hayo binadamu asingekuwa mbinafsi, asingeishi maisha yake kwa kuangaikia kumiliki vitu na kusahau utu wake wa ndani. Yangu ni hayo bro mjuaji
 
Chai niliokunywa asubuh hii haijansaidia kitu maana nimetoka KAPA hapa.Sijaelewa kitu
Simply cha kujua hapo ni kuwa maneno unayoyasikia ndio huzaa fikra na fikra huzaa utu fulani( personality), unachofikiri ndivyo utakavyokuwa, kwa kusikia maneno ya umilikishi na kujirejelea tokea utotoni kulitengeneza fikra ya kujihisi bora kuliko wengine na fikra ya kuona thamani ya utu wetu ipo kwenye vitu tunavyomiliki kitu ambacho ni tofauti na kusudi letu la kuishi duniani, ni maneno sana sana neno hili "nina" / "I am" tu yaliobadilisha zumuni la maisha hapa duniani. Sisi ni watu na kitu cha thamani kwetu ni utu, utu ni upendo, umoja na amani
 
Fikra zako zimetokana na maneno na sentensi mbali mbali ambazo unazisikiaga katika maisha yako ya kila siku pasipo maneno hakuna fikra na bila fikra hakuna personality jinsi unavyofikiria ndivyo wewe ulivyo. Maneno ya umilikishi ambayo tunayaskia toka udogoni yalitujengea fikra za umimi ambazo ndani yake kuna changu na vyangu bila maneno hayo binadamu asingekuwa mbinafsi, asingeishi maisha yake kwa kuangaikia kumiliki vitu na kusahau utu wake wa ndani. Yangu ni hayo bro mjuaji


Fikra hazijengwi na maneno Boss, zipo jamii hazitumii lugha ya sauti na zijafikra
 
Fikra zako zimetokana na maneno na sentensi mbali mbali ambazo unazisikiaga katika maisha yako ya kila siku pasipo maneno hakuna fikra na bila fikra hakuna personality jinsi unavyofikiria ndivyo wewe ulivyo. Maneno ya umilikishi ambayo tunayaskia toka udogoni yalitujengea fikra za umimi ambazo ndani yake kuna changu na vyangu bila maneno hayo binadamu asingekuwa mbinafsi, asingeishi maisha yake kwa kuangaikia kumiliki vitu na kusahau utu wake wa ndani. Yangu ni hayo bro mjuaji
Mbona wanyama wengine hawana hizi lugha lakini bado wana ubinafsi?
 
Nikajua unajibu la hiyo Nina,wangu,yangu n.k kumbe nawe watubwabwajia tu!..
Hizo ni lugha tu na hata huko unapokimbilia kwa Mungu nae kwenye vitabu vyake amempa binadamu umilikishi Ee nendeni mkatawale dunia sijui na vilivyomo na tumepewa mamlaka ya kukanyaga ng'e na nyoka(watumishi wabwana mtasaidia hapo neno kidogo)😅

Sasa Kama hapo binadamu kapewa umiliki wa dunia unataka tuiteje isipokuwa kusema dunia yangu au yetu n.k

Lugha ni kama utohoaji tu.. namaanisha kiunge kama mguu utakiona kwa macho au kwa kukishika n.k ila sasa tutakiita vipi kwa lugha tusipoweka jina..? Lugha inarahisisha maelewana kama njia ya mawasiliano inamaana neno limesimama kwa maana ya kitu fulani Sasa tunarepresent kitu fulani kwa kitu fulani..😅
Napata ugumu hata kueleza!..

Umilikishi nao pia tumeuleta kwenye lugha ambapo ndo tunasema yangu,changu,yetu,vyao,vyetu n.k
Ili kuthibitisha mada yako tuonyeshe au tueleweshe kilicho nyuma ya pazia huenda mwenzetu umeng'amua kitu...? Ukiwa nawe hujui basi unatuchezesha kanyabazongo tu hapa kwa utata wa maneno!.
 
Maisha ni nini?
Maisha ni uhai mkuu.. tunahadisia historia ya maisha ya marehemu pindi akiwa hai lkn baada ya kukosa uhai tunahadisia nini alitendewa marehemu!.. hivyo kukosa uhai ni kukosa sifa za utendaji wa maisha so maisha ni ni uhai.
 
Nikajua unajibu la hiyo Nina,wangu,yangu n.k kumbe nawe watubwabwajia tu!..
Hizo ni lugha tu na hata huko unapokimbilia kwa Mungu nae kwenye vitabu vyake amempa binadamu umilikishi Ee nendeni mkatawale dunia sijui na vilivyomo na tumepewa mamlaka ya kukanyaga ng'e na nyoka(watumishi wabwana mtasaidia hapo neno kidogo)

Sasa Kama hapo binadamu kapewa umiliki wa dunia unataka tuiteje isipokuwa kusema dunia yangu au yetu n.k

Lugha ni kama utohoaji tu.. namaanisha kiunge kama mguu utakiona kwa macho au kwa kukishika n.k ila sasa tutakiita vipi kwa lugha tusipoweka jina..? Lugha inarahisisha maelewana kama njia ya mawasiliano inamaana neno limesimama kwa maana ya kitu fulani Sasa tunarepresent kitu fulani kwa kitu fulani..
Napata ugumu hata kueleza!..

Umilikishi nao pia tumeuleta kwenye lugha ambapo ndo tunasema yangu,changu,yetu,vyao,vyetu n.k
Ili kuthibitisha mada yako tuonyeshe au tueleweshe kilicho nyuma ya pazia huenda mwenzetu umeng'amua kitu...? Ukiwa nawe hujui basi unatuchezesha kanyabazongo tu hapa kwa utata wa maneno!.
Nakubaliana na wewe japo sijabase sana kwenye dini.
Kuhusu kwenda kuimiliki dunia Mungu aliwaagiza watu wote wakaitawale dunia but unaona leo dunia inatawaliwa na wachache, kwanini? Sababu ya umimi ambao tuliuweka kichwani tokea tukiwa wadogo kutokana na maneno ya umilikishi binafsi (yangu,changu n.k) na sio wa ushirika

Nije kwenye point ya msingi Safari ya maisha yako imejengwa kwenye sehemu kuu mbili; maisha ya kiroho yasionekana kwa macho na maisha ya kimwili ambayo uhisiwa na milango ya fahamu. Maisha ya kiroho ni safari ya yakuutambua utu wako halisi na kutambua wewe ni nani hasa( true self/ being).Maisha ya kimwili ni safari ya matarajio ya kuwa na hadhi, nafasi au nguvu fulani katika jamii inayokuzunguka(future).

Maneno hayareflect utu wetu halisi wa kiroho unaposema hili gari ni langu, unareflect mwili na sio wewe halisi ambae ni roho, maneno hureflect hali zetu za kimwili tu na sio hali zetu halisi unajua wewe ni nani soma chini

Ulimwengu umeundwa na nguvu ya uwepo wa uelewa mkuu (being) ambao hauonekani, uwepo huo wa uelewa uliingia wenyewe kwenye vitu (maumbo ya kifiziki au linaloshikika/ miili) na lengo la mageuzi ya kuingia kwenye vitu (miili) ni kujidhihilisha( kuweza kuonekana) wenyewe kwenye maumbo ya vitu mbalimbali yanayoonekana. Ili uwepo wa uelewa ujidhihilishe ( uonekane) kutoka kwenye utumwa wa kutoonekana, uelewa huo ukaingia kwenye maumbo na kutengeneza mifumo wa maisha kwenye maumbo hayo(miili). Hivyo ni jukumu la miili kuishi katika kudhihilisha uwepo wa uelewa (roho) katika maisha yanayoonekana. Je ni sahii sisi kupewa maana na maneno? Hapana sio sahii maneno kutumaanisha sisi kwa sababu hayatoshi kutumaanisha, ni sahii kuyatumia kutaja tu na sio kueleza maana ya ndani ya kitu. Kosa letu tunatumia maneno kama mimi, langu na changu kwa dhana kuwa tunajimaanisha sisi kwa 100% kumbe sivyo, tunamaanisha hali zetu za kimwili na fikra tu .

SIJATULIA KUELEZA KWA UREFU ILA NAHISI UTANIELEWA KIDOGO
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom