Jinsi gani nitajiunga na chuo kusoma USA

shafii77

Member
Mar 18, 2019
45
73
Habarini wanaJF,

Mimi ni mhitimu wa kidato chasita mwaka 2017 lengo la kuja hapa mbele yenu ni kuomba ushauri kwa wenye experience ya kusoma nchini USA kwa maana mwakani nataka nijiunge katika chuo mojawapo hasa katika state ya FLORIDA advance na secondary nmesoma masomo ya arts HKL na matokeo yangu ni ya wastani, division 2, for both secondary na primary. Je, hii haitoathiri application yangu?

Napenda nifahamu vigezo gan wanazingatia ili kusajili international students maana nmeskia tu kuna baadhi ya tests inabidi nzifanye kama TOEFL, ACT, SAT, GRE na mingineyo, nahitaji nijiunge either in diploma in business au kozi za social science.

Nakaribisha maoni na msaada wenu pia
 
Kwa ulichokisoma A-level mdogo wangu anza tu kutafuta hela uendeshe maisha yako!

Hakuna sponsor atakufadhili ukasome kozi za sanaa labda awe nduguyo.
Nisikuvunje moyo sana kuna shirika la ki-israel (lakidini) kila mwaka hufadhili wanafunzi kwenda Minnesota kusoma na mimi ni mmoja wa wanufaika.

Kwa taarifa zaidi usinijie PM nenda SUA utapata taarifa zote kuwahusu na huenda ukawa na nyota ukafanikiwa licha ya sanaa yako.
 
Kwa ulichokisoma A-level mdogo wangu anza tu kutafuta hela uendeshe maisha yako!

Hakuna sponsor atakufadhili ukasome kozi za sanaa labda awe nduguyo.
Nisikuvunje moyo sana kuna shirika la ki-israel (lakidini) kila mwaka hufadhili wanafunzi kwenda Minnesota kusoma na mimi ni mmoja wa wanufaika.

Kwa taarifa zaidi usinijie PM nenda SUA utapata taarifa zote kuwahusu na huenda ukawa na nyota ukafanikiwa licha ya sanaa yako.
Ndiyo maana hata mimi nimemuuliza hayo maswali mawili hapo juu. Kama anajilipia hakuna tatizo tena nitamuunganisha na watu wa admission na kumpatia info zote anazohitaji.

Bado uko Minnesota mkuu? Libaridi hilo limewaanza. Niliwahi kufika huko wakati wa Winter nikakimbia asubuhi na mapema na kuapa kutorudi tena. Si kwa baridi ile aisee. Yaani makende mpaka yanapotea duh!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio sponsor yupo anaishi hapo FLORIDA ndo maana nkapendekeza hyo state by the way nataka nkasomee diploma either masomo ya biashara ama political science
kwanini huyo sponsor asikulipe ada usomee hapahapa bongo uanze diploma ya masomo ya biashara?
Alafu pia usisomee political science, soma biashara itakufungua angalau akili hata ya kuendesha maisha yako political sayansi itakufanya uwe mpiga kelele tu.
 
Ndiyo maana hata mimi nimemuuliza hayo maswali mawili hapo juu. Kama anajilipia hakuna tatizo tena nitamuunganisha na watu wa admission na kumpatia info zote anazohitaji.

Bado uko Minnesota mkuu? Libaridi hilo limewaanza. Niliwahi kufika huko wakati wa Winter nikakimbia asubuhi na mapema na kuapa kutorudi tena. Si kwa baridi ile aisee. Yaani makende mpaka yanapotea duh !

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapana Nahmala sipo Minnesota kwa sasa nilirejea Tanzania wakati Corona ndio imeanza kupamba moto.

Kwa baridi Minnesota ni kiboko nilikuwa najaribu kucheza mpira na washikaji kwenye ice wenyewe wametoka Brazil, S.Korea na India wamezoea hali ile nilikuwa naona naweza kurudisha namba kwa Mungu sio muda na sikutaka kujitenga😂

Huyu mdogo wetu kwa alichokisoma akafungue M-pesa tu au akomae na ushauri aliopewa hapo juu na EllySkyWilly
 
Ndiyo maana hata mimi nimemuuliza hayo maswali mawili hapo juu. Kama anajilipia hakuna tatizo tena nitamuunganisha na watu wa admission na kumpatia info zote anazohitaji.

Bado uko Minnesota mkuu? Libaridi hilo limewaanza. Niliwahi kufika huko wakati wa Winter nikakimbia asubuhi na mapema na kuapa kutorudi tena. Si kwa baridi ile aisee. Yaani makende mpaka yanapotea duh!

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimekukamata leo kumbe upo huko?
 
kwanini huyo sponsor asikulipe ada usomee hapahapa bongo uanze diploma ya masomo ya biashara?
Alafu pia usisomee political science, soma biashara itakufungua angalau akili hata ya kuendesha maisha yako political sayansi itakufanya uwe mpiga kelele tu.
Bongo naeza jilipia mwenyew na kuwalipia wengine ata watatu
 
Hongera sana kama utafanikiwa kwenda kusoma florida, maana kuwa gator ama seminoles ni heshima kubwa...
 
Back
Top Bottom