Mndali ndanyelakakomu
JF-Expert Member
- Dec 14, 2016
- 13,992
- 31,695
Kwa kweli MUNGU awape utambuzi wa mapemaKabisa aisee, mpaka unamwonea huruma. Kuna mwalimu mwez wa nane aliamua kuacha kazi kimya kimya ili asishauliwe chochote. Amepigiwa simu pamoja na kufuatwa nyumbani mara nyingi kumsihi arudi kazini, akasema wamwache na maamuzi yake.
Baadae wakaja wakaguzi wakaambiwa kuhusu huyo mwalimu, wakampa wiki awe amerudi kazini. Lakini hakurudi.
Baadae ndio katika kutafuta watu wengine wa kujiunga na Qnet ndio siri ikafichuka. Maama alianza kuwashawishi walimu wenzake wajiunge na hiyo network.
In short mwalimu kapauka sana. Anatamani apigiwe simu tena arudi kazini.
Walimu Mungu awasaidie sana. Maana pamoja na malalamiko haya, bado kunawatyu wanaendelea kujiunga. Manaigana sana. Mwalimu mmoja akikopa woote wanaenda kukopa hata kama huna project yoyote. Ngoja waendelee kupigwa tu
Unajua watu wengi wamejikuta wanatafuta njia ya mkato hapo ndio wanapo pigwa kama hawa