Losambo
JF-Expert Member
- Nov 8, 2011
- 2,612
- 864
Ndg WanaJF,
Itakumbukwa kuwa mikoa ya Mwanza, Mbeya, Arusha, Dar – es – Salaam n.k ilikuwa ikiwakilishwa na wabunge toka CCM bila shaka kabla ya uchaguzi wa 2010. Mara baada ya uchaguzi, baadhi ya majimbo mengi makubwa yaliangukia chini ya upinzani. Baadhi ya majimbo hayo ni Mbeya Mjini, Arusha Mjini, Mwanza Mjini n.k
Tokea matokeo hayo yatangazwe mikoa hiyo hususani majimbo niliyoyataja hapo juu yamekuwa yakikabiliwa na vurugu za mara kwa mara. Vurugu hizo zimepelekea wabunge wanaowakilisha majimbo hayo kupakwa matope kuwa ndiyo wanaochochea vurugu na hivyo kuzorotesha maendeleo ya majimbo yao!
Hili limeanza kuingia akilini kwa baadhi ya wananchi. Lakini mimi leo hii naomba nipingane na propaganda hiyo ambayo haina mantiki kabisa kwa muono wangu kama Losambo kwa kuangalia mikoa yote mitatu yaani Arusha, Mwanza na Mbeya.
ARUSHA
Kama upo makini matokeo ya mikoa yote niliyoitaja nguvu kubwa sana ilitumika kutangaza matokeo hali iliyoashiria kulikuwa na dalili mbaya ya kutaka kuchakachua matokeo. Baada ya matokeo kutangazwa ni wazi kulikuwa na juhudi za makusudi kuhakikisha majimbo hayo hayaongozwi na mameya kutoka upinzani!
Hiki ndicho kiini cha tatizo la vurugu Arusha. Baada ya meya wa Arusha kupatika katika mazingira yenye utata, CDM waliandaa maandamano yaliyopelekea watu watatu (03) kufa na mamia kujeruhiwa.
Hili lilipelekea waziri mkuu Pinda kuingilia kati kwa lengo la kutafuta suluhu ambayo hadi leo bado haijapatikana.
Wakati kiini cha mgogoro hakijapatiwa ufumbuzi yaani mgogoro wa meya, hivi majuzi tena kumetokea vurugu zilizopelekea viongozi wa CDM, Dr. W. Slaa, F. Mbowe, T. Lissu pamoja na wafuasi wao kufunguliwa mashitaka kwa kosa la uchochezi na kufanya mkutano kinyume na sheria.
Ukichunguza kwa makini kuna madai ya msingi ambayo serikali ya CCM haitaki kuyapa nguvu kwa kigezo cha kuipa nguvu CDM. Kiukweli, katika vurugu za majuzi ni ujinga wa hakimu kushindwa kutumia busara kwa kumnyima dhamana mbunge wa Arusha Ndg G. Lema tu ndiko kulikopelekea mambo yote hayo! Tujiulize kwa nini Lema alinyimwa dhamana;
MWANZA
Tatizo la Mwanza ni la Wamachinga. Kumekuwa na tabia kabla ya uchaguzi vitu kuacha vifanywe kiholela hata kama watu wanavunja sheria kwa kigezo cha kutokosa kura.
Ukichunguza masoko mengi Arusha, Mwanza na hata Mbeya kuna biashara za wamachinga na akina mama zinazofanywa katika maeneo yasiyoruhusiwa. Wafanyabiashara hao wamekuwa wakipata usumbufu wa mara kwa mara toka kwa mgambo wa jiji licha ya kulipa kodi za manispaa kama kawaida.
Mara baada ya uchaguzi serikali husahau kuwa iliwaachia huru kipindi cha uchaguzi na sasa wameshajenga mazoea na kuamua kuwafukuza ghafla.
Inapotokea mvutano kuwa mkubwa, serikali hutumia mwanya huo kisiasa kwa kusema kuna mkono wa viongozi wa vyama vya upinzani hususani CDM. Lakini imesahau kiini cha mgogoro ni ukosefu wa ajira na udhaifu wa serikali kukurupuka kuwafukuza watu bila kuwaonyesha maeneo mbadala ambayo yanakidhi haja.
Hili serikali haitaki kulisemea na kukimbilia vurugu hizo kusababishwa na wabunge wa CDM waliowachagua ili watu wajutie maamuzi yao, japokuwa si dhambi kujutia maamuzi kama kweli umekosea.
MBEYA
Kinachotokea Mbeya kinafana kidogo na Mwanza hivyo sioni haja ya kuongelea kitu kinachofanana. Mbeya iliunguliwa na masoko karibu mawili hivi karibuni, hivyo ni tumaini langu wamachinga wengi watakuwa wamekimbilia eneo moja na kuonekana kama vurugu.
Naomba sasa niunganishe nilichokisema kwa title ya thread yangu na hayo hapo juu.
Ni ukweli usiopingika kuwa hivi sasa hali ya serikali kifedha ni mbaya na hivyo inachohangaika saizi siyo vurugu zinazoendelea bali kujinasua na aibu ya kushindwa kujiendesha! Serikali inahangaika ipate wapi fedha za kulipa wafanyakazi wake wasiozidi million moja na matumizi mengine.
Hili la kuwa serikali ina hali mbaya kifedha limeshaanza kuonekana kwa baadhi ya wafanyakazi kuchelewa kupata mishahara, wizara nyingi kutopata migawo kama ilivyo kawaida na kusimama kwa miradi mingi ya maendeleo kwa kuwa serikali haijalipa madeni ya wakandarasi kwa muda mrefu! Mengine ni siri lakini wajio jikoni wanajua serikali ipo ICU kimapato.
Sasa hili la vurugu linafurahiwaje na serikali ya CCM? Ni rahisi kwa sababu serikali yenyewe inatambua hata kama kungekuwa na amani kiasi cha mtu yoyote kutopigwa hata kibao isingefanya chochote cha maana, hivyo vurugu hizo zinawapunguzia kujibia maswali na hoja nzito kwa nini imeshindwa kuleta maendeleo licha ya amani na utulivu uliotawala.
Kitakachofanyika ni kuvuna matunda ya mbegu inayopandwa saizi kwa wananchi kuwa wameshachemsha kuwachagua wabunge wanaohamasisha vurugu na migogoro hivyo wasahau maendeleo. Na hili litachagizwa na viongozi vichwa ngumu ambao hawataisha kuanzisha migogoro ya mara kwa na wabunge hao ili wahemkwe na kuanzisha vurugu na kufunguliwa makesi yasiyokwisha.
Suala la maendeleo yatapatika kwa kuwa miradi mingi haifadhiliwi na serikali ya Tanzania bali ama ni mikopo au misaada toka banki ya dunia au vinginevyo. Hebu jiulize ni miradi mingapi iliyoendeshwa na serikali yenyewe mpaka ikakamilika bila msaada toka taasisi hizo nilizozitaj ahapo juu. Halafu kinachoitwa vurugu ambazo zinaweza kutishia katika mikoa hiyo bado hazionekani kuwa ni tishio kiasi cha kuhatarisha maendeleo, bali ni propaganda tu.
Mwisho, nawakilisha wanaJF. Hii ni kwa kadiri ya uelewa wangu na vyanzo vyangu.
Naomba mtakanijibu msini quote kwa sababu ya urefu wa maada na kuleta usumbufu kwa wasomaji. Nategemea changamoto nyingi kutoka kwenu.
Itakumbukwa kuwa mikoa ya Mwanza, Mbeya, Arusha, Dar – es – Salaam n.k ilikuwa ikiwakilishwa na wabunge toka CCM bila shaka kabla ya uchaguzi wa 2010. Mara baada ya uchaguzi, baadhi ya majimbo mengi makubwa yaliangukia chini ya upinzani. Baadhi ya majimbo hayo ni Mbeya Mjini, Arusha Mjini, Mwanza Mjini n.k
Tokea matokeo hayo yatangazwe mikoa hiyo hususani majimbo niliyoyataja hapo juu yamekuwa yakikabiliwa na vurugu za mara kwa mara. Vurugu hizo zimepelekea wabunge wanaowakilisha majimbo hayo kupakwa matope kuwa ndiyo wanaochochea vurugu na hivyo kuzorotesha maendeleo ya majimbo yao!
Hili limeanza kuingia akilini kwa baadhi ya wananchi. Lakini mimi leo hii naomba nipingane na propaganda hiyo ambayo haina mantiki kabisa kwa muono wangu kama Losambo kwa kuangalia mikoa yote mitatu yaani Arusha, Mwanza na Mbeya.
ARUSHA
Kama upo makini matokeo ya mikoa yote niliyoitaja nguvu kubwa sana ilitumika kutangaza matokeo hali iliyoashiria kulikuwa na dalili mbaya ya kutaka kuchakachua matokeo. Baada ya matokeo kutangazwa ni wazi kulikuwa na juhudi za makusudi kuhakikisha majimbo hayo hayaongozwi na mameya kutoka upinzani!
Hiki ndicho kiini cha tatizo la vurugu Arusha. Baada ya meya wa Arusha kupatika katika mazingira yenye utata, CDM waliandaa maandamano yaliyopelekea watu watatu (03) kufa na mamia kujeruhiwa.
Hili lilipelekea waziri mkuu Pinda kuingilia kati kwa lengo la kutafuta suluhu ambayo hadi leo bado haijapatikana.
Wakati kiini cha mgogoro hakijapatiwa ufumbuzi yaani mgogoro wa meya, hivi majuzi tena kumetokea vurugu zilizopelekea viongozi wa CDM, Dr. W. Slaa, F. Mbowe, T. Lissu pamoja na wafuasi wao kufunguliwa mashitaka kwa kosa la uchochezi na kufanya mkutano kinyume na sheria.
Ukichunguza kwa makini kuna madai ya msingi ambayo serikali ya CCM haitaki kuyapa nguvu kwa kigezo cha kuipa nguvu CDM. Kiukweli, katika vurugu za majuzi ni ujinga wa hakimu kushindwa kutumia busara kwa kumnyima dhamana mbunge wa Arusha Ndg G. Lema tu ndiko kulikopelekea mambo yote hayo! Tujiulize kwa nini Lema alinyimwa dhamana;
- Kwanza kitendo chake cha kukataa dhamana wakati alikuwa na uwezo wa kujidhamini ilikuwa dharau kwa mahakama. Ok, nakubaliana na hakimu lakini ndiyo nae alipize kisasi eti kwa sababu G. Lema aliidharau mahakama kwa kumwambia siku hiyo haikuwa siku ya kesi yake hivyo wadhamini wake waje 14.11.2011 ambapo ndipo shauri lake lilipangwa kusikilizwa? Hekima yake kukosekana ndiyo imesababisha vurugu zile pale NMC. Pamoja na hayo G. Lema alikuwa na madai yake na kwa mujibu wa akili yake aliona ndiyo njia labda ya kuyafikisha kwa wahusika kwa urahisi zaidi.
- Pili na kubwa, ni serikali kuzima shamra shamra za G. Lema kupokelewa kama shujaa toka jela. Ni wazi G. Lema alikuwa ameandaliwa maandalizi makubwa sana Arusha na Dodoma kiujumla! Sasa ili kuvuruga hayo, ikaonekana Lema anyimwe dhamana technically siku ile.
MWANZA
Tatizo la Mwanza ni la Wamachinga. Kumekuwa na tabia kabla ya uchaguzi vitu kuacha vifanywe kiholela hata kama watu wanavunja sheria kwa kigezo cha kutokosa kura.
Ukichunguza masoko mengi Arusha, Mwanza na hata Mbeya kuna biashara za wamachinga na akina mama zinazofanywa katika maeneo yasiyoruhusiwa. Wafanyabiashara hao wamekuwa wakipata usumbufu wa mara kwa mara toka kwa mgambo wa jiji licha ya kulipa kodi za manispaa kama kawaida.
Mara baada ya uchaguzi serikali husahau kuwa iliwaachia huru kipindi cha uchaguzi na sasa wameshajenga mazoea na kuamua kuwafukuza ghafla.
Inapotokea mvutano kuwa mkubwa, serikali hutumia mwanya huo kisiasa kwa kusema kuna mkono wa viongozi wa vyama vya upinzani hususani CDM. Lakini imesahau kiini cha mgogoro ni ukosefu wa ajira na udhaifu wa serikali kukurupuka kuwafukuza watu bila kuwaonyesha maeneo mbadala ambayo yanakidhi haja.
Hili serikali haitaki kulisemea na kukimbilia vurugu hizo kusababishwa na wabunge wa CDM waliowachagua ili watu wajutie maamuzi yao, japokuwa si dhambi kujutia maamuzi kama kweli umekosea.
MBEYA
Kinachotokea Mbeya kinafana kidogo na Mwanza hivyo sioni haja ya kuongelea kitu kinachofanana. Mbeya iliunguliwa na masoko karibu mawili hivi karibuni, hivyo ni tumaini langu wamachinga wengi watakuwa wamekimbilia eneo moja na kuonekana kama vurugu.
Naomba sasa niunganishe nilichokisema kwa title ya thread yangu na hayo hapo juu.
Ni ukweli usiopingika kuwa hivi sasa hali ya serikali kifedha ni mbaya na hivyo inachohangaika saizi siyo vurugu zinazoendelea bali kujinasua na aibu ya kushindwa kujiendesha! Serikali inahangaika ipate wapi fedha za kulipa wafanyakazi wake wasiozidi million moja na matumizi mengine.
Hili la kuwa serikali ina hali mbaya kifedha limeshaanza kuonekana kwa baadhi ya wafanyakazi kuchelewa kupata mishahara, wizara nyingi kutopata migawo kama ilivyo kawaida na kusimama kwa miradi mingi ya maendeleo kwa kuwa serikali haijalipa madeni ya wakandarasi kwa muda mrefu! Mengine ni siri lakini wajio jikoni wanajua serikali ipo ICU kimapato.
Sasa hili la vurugu linafurahiwaje na serikali ya CCM? Ni rahisi kwa sababu serikali yenyewe inatambua hata kama kungekuwa na amani kiasi cha mtu yoyote kutopigwa hata kibao isingefanya chochote cha maana, hivyo vurugu hizo zinawapunguzia kujibia maswali na hoja nzito kwa nini imeshindwa kuleta maendeleo licha ya amani na utulivu uliotawala.
Kitakachofanyika ni kuvuna matunda ya mbegu inayopandwa saizi kwa wananchi kuwa wameshachemsha kuwachagua wabunge wanaohamasisha vurugu na migogoro hivyo wasahau maendeleo. Na hili litachagizwa na viongozi vichwa ngumu ambao hawataisha kuanzisha migogoro ya mara kwa na wabunge hao ili wahemkwe na kuanzisha vurugu na kufunguliwa makesi yasiyokwisha.
Suala la maendeleo yatapatika kwa kuwa miradi mingi haifadhiliwi na serikali ya Tanzania bali ama ni mikopo au misaada toka banki ya dunia au vinginevyo. Hebu jiulize ni miradi mingapi iliyoendeshwa na serikali yenyewe mpaka ikakamilika bila msaada toka taasisi hizo nilizozitaj ahapo juu. Halafu kinachoitwa vurugu ambazo zinaweza kutishia katika mikoa hiyo bado hazionekani kuwa ni tishio kiasi cha kuhatarisha maendeleo, bali ni propaganda tu.
Mwisho, nawakilisha wanaJF. Hii ni kwa kadiri ya uelewa wangu na vyanzo vyangu.
Naomba mtakanijibu msini quote kwa sababu ya urefu wa maada na kuleta usumbufu kwa wasomaji. Nategemea changamoto nyingi kutoka kwenu.