Jinsi CCM inavyowachezesha Wapinzani kwa rimoti

Watanzania tunataka serikali inayojali watu wote! inayojali maslai ya wafanyakazi,wakulima,walimu na wengineo! watanzania wamechoka na awajui kesho nini kitawakuta! wana Dar es salaam awajui kesho jumatatu wataambiwa nn na mkuu wao wa mkoa! watumishi wa Serikali awajui atma yao! askari wote(police,jeshi,magereza) awaju lini watenda course ili wapande cheo! Wewe TISS namba moja sema usikike umesikia nn kuhusu watu kupanda vyeo na lini mshahara utapanda na lini Watumishi watalipwa malimbikizo yao,je ni Lini MSD na wengine wanaodai (madeni ya ndani) yatalipwa ila usilete usanii!!! Membe ajatweet na bado ajatweet
 
mkuu Evarist Chahali hawa wapinzani wa nchi hii ni sikio la kufa...Tuliwaambia kuhusu EL hawakusikia.
Hapa ni kuwa ccm itatawala miaka yote nami namsapoti Jpm na serikali yake.
chADEma ni wahuni flulani
Unapo walaumu Chadema /Upinzani huku tukiwa tuna katiba na Tume ya hii ya uchaguzi. Wewe pia ni msanii kama walivyo CCM na hao Wapinzani . Hali halisi ya siasa hapa Tanzania mpinzani kushinda hutegemea busara na hekma ya Raisi aliyepo madarakani. Wakulaumiwa ni sisi wananchi kuto dai katiba mpya na Tume huru ya uchaguzi, usiufiche uboya wako mgongoni kwa wanasiasa. Hivyo basi kwa ujinga wetu hatuna budi kuomba apatikane Raisi mwenye busara na hekma huko CCM.
 
Watanzania tunataka serikali inayojali watu wote! inayojali maslai ya wafanyakazi,wakulima,walimu na wengineo! watanzania wamechoka na awajui kesho nini kitawakuta! wana Dar es salaam awajui kesho jumatatu wataambiwa nn na mkuu wao wa mkoa! watumishi wa Serikali awajui atma yao! askari wote(police,jeshi,magereza) awaju lini watenda course ili wapande cheo! Wewe TISS namba moja sema usikike umesikia nn kuhusu watu kupanda vyeo na lini mshahara utapanda na lini Watumishi watalipwa malimbikizo yao,je ni Lini MSD na wengine wanaodai (madeni ya ndani) yatalipwa ila usilete usanii!!! Membe ajatweet na bado ajatweet
I second you mkuu!!!
Bahati mbaya sana nchi hii wananchi wasiotetewa kwa nguvu ( wanatetewa kisaniii Sana maslahi yao) na wanasiasa wao ndio watetezi wakubwa wa maslahi ya wanasiasa, pengine pasipo kujua ya kwamba wanachezeshwa ngoma isiyo yao huku wanasiasa wakijineemesha!
 
Hivi wewe pia una amini Tweet ni za Membe??? maana Account original ya Membe aijapostiwa toka 2015!!! Wenyewe kwa Wenyewe mtafute mchawi acheni usaniii! au kweli Mweshimiwa Mbowe ana simu ya Mbunge Lema???? mpaka sasa Membe (ukipitia acc yake original AJAJIBU NA WALA AJAMWELEZA BASHIRU CHOCHOTE sasa nashangaaa wewe TISS nguli pia umeingia choo cha mabasha bora ingekuwa cha kike)
Msome na mfuatilie vizuri. Ukila hela ya mtu lazima umfanyie kazi bila kujali kama inakuvunjia heshima.
 
Well umejitahidi kuandika, ila haya yangekuwa na maana zaidi kama tuna ccm kama chama sias, bahati mbaya hatuna chama cha siasa cheje jina la.ccm hapa Tanzania.

Sikuzote upinzani kama vyama vya siasa huwa vinapambana na tiss,jwtz, na policeccm na ndugu zao NEC wanaotumia jina la ccm, na hili ninaamini unalijua vizuri sana, hivyo ukija na hoja zinazoweza kuwasaidia upinzani kupambana na huyo imporster itakuwa vizuri sana, vingenevyo unachofanya hakuna tofauti na wanachofanya huyo imposter.
 
CCM baada ya Magufuli itakua na miaka mingine kama 10 ikiwa ya kupumua kabla ya kupata upinzani unaojitambua tena.
Huu wa sasa kwishney..eti wanampost membe leo kama hero wao upinzani..kuna usemi unasema ukiona adui yako anakusifia jiangalie mara mbili..upinzani wameshaona siasa za magu kama wao hawaziwezi tena..na wameona kwao hawana cha kupoteza tena..pengine wameona membe angekuwa size yao kwa maana wangemmudu maana kama ilivyoonekana membe ni copy ya jk kiuongozi na jk walimmudu, wasingeshindwa kwa membe.
Ila wanachofanya sasa ni kama fisi anayevizia mkono wa.mtu anayetembea pengine utaanguka aule..wamepoteza ramani ya gemu ya siasa tz..
 
Upinzani unatia aibu na bahati mbaya kuna watu bado wanawaendekeza pamoja na huu ujinga.

Wanatumia njia zile zile zilizoshindwa kwa Kikwete 2005 , zikashindwa kwa Lowasa ambaye alitumia ujasiri wa kimasai kuvuka mstari! Wanatia hasira mno! Sana!

Unatamani uwaite wote uwalambe mboko! Alafu washabiki wao ndio mfu kabisa! Leo wanamshabikia Membe! Ex spy! , hawajui hata wanacheza ngoma gani! aibu aibu!

Bora niandike ili siku moja mje mpime nilichoandika! Mbowe yupo gerezani, wako nae kuweza kufanya lolote! Huku wanamtandao tunaowajua wanapambana na mada za Membe! Hawajui hata wafanye nini!
 
upinzani huu hauna uwezo hata wa kumtoa mbunge yeyote wa ccm madarakani , eti ndio mnawaza kuitoa CCM madarakani.
Yaani mtu unajisifu umeshinda huku umemfunga kamba mpinzani wako baharini (jela) kisha unamwambia aogolee?wekeni katiba mpya na tume huru ili sie wananchi tujue pumba na mchele na sio mnategemea policcm kushinda.
 
Linalohusiana na sura hii ya kwanza ni ukweli kwamba japo upinzani wa kisiasa si uadui, kila mwenye akili timamu anafahamu kuwa CCM sio tu inawaona wapinzani kuwa ni maadui bali pia kama watu hatari zaidi ya wahalifu/wahaini/magaidi (you name it).
Unasahau vitu viwili. Kwanza, tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi, hakuna chama kingine kimewahi kuwa madarakani isipokuwa CCM. Pili, wako Watanzania wengi ambao hawajawahi kuwa wanachama wa chama chochote cha siasa kiwe CCM au vyama vya upinzani ila ni Watanzania wasioridhishwa na uongozi wa taifa hili na hatma yake. CCM imetumia nafasi yake kama chama tawala utadhani wana hatimiliki ya nchi hii. Hii ndiyo sababu ya chuki dhidi ya CCM kutoka kwa baadhi ya wananchi na vyama vya upinzani kwani kuipinga kunatafsiriwa kama uhaini.
Na hilo halijaanza na Jiwe. Chuki ya CCM dhidi ya upinzani ilikuwapo from word go in 1992. Tofauti kati ya Jiwe na watangulizi wake ni kwamba yeye hahangiki kuficha chuki yake/ya chama chake vs Wapinzani.
Jiwe ni muoga kwa sababu pamoja na majigambo anajua moyoni kwamba aliupata uongozi wa nchi hii kwa hila. Ndio maana hata yeye mwenyewe anakiri kuwa alisukumiziwa madaraka ambayo hakujua ni makubwa kiasi hicho. Wewe unasema wapinzani wananunuliwa, are you kidding me? Kama vilivyokuwa vikundi vya kigaidi kama Mafia, you are given an offer you cannot refuse, je wewe kama mwanausalama kama unavyodai, hao wapinzani wana alternative gani? Hivi kweli hujui yaliyompata Mbunge wa Singida, Mh. Tundu Antiphas Lissu ? Bila shaka risasi za kumuangusha tembo ndio ilikuwa alternative!
Pointi yangu hapa ni kwamba japo upinzani wa kisiasa haupaswi kuwa uadui, "adui" wa kwanza wa Upinzani ni CCM...as chama cha siasa kilichopo madarakani, na ambacho wapinzani wanapaswa kujibidiisha kuking'oa.
Hii ni tafsiri yako lakini sisi Watanzania wengine tunaamini CCM ndiye adui mkubwa wa taifa na si upinzani tu. I hate CCM, I dont hate individuals, hao wote naamini ni matunda ya mfumo. Hata malaika akiingia CCM hawezi kufanya tofauti, sana sana ataharibu zaidi kama tulivyoshuhudia kwa awamu zote toka 1992, it gets worse with every new leadership. Mgombea wa CCM kwa mfumo tulio nao hata akiwa kichaa atatangazwa mshindi na huo ndio ukweli taka usitake.
 
Moja ya mapungufu makubwa ya Wapinzani wetu ni suala lile lile wanaloilalamikia CCM kila kukicha, kwamba ukiikosoa CCM unaonekana mhaini. As if wao ni wazuri katika kukubali kukosolewa.

Katika hili la kumuona kila anayekosoa ni mhaini au anataka u-DC, tofauti kati ya CCM na Upinzani ni jina tu. Na utakuwa na bahati kama utawakosoa na wakakuita mhaini au mtaka u-DC bila matusi, another janga la kitaifa katika political conversations zetu.

Lakini kwa vile si kuitwa mhaini wala mtaka u-DC kunakoweza kumdhuru mtoa hoja, basi hakuna sababu ya kuchelea kuzungumzia masuala mbalimbali kuhusu Tanzania yetu.

Na ni katika mantiki hiyo, naamsha tafakuri kuhusu jinsi Wapinzani wetu wanavyoendeshwa kwa rimoti na CCM.

Mfano hai: ishu ya Membe. Kwa sie tunaokwenda mbali zaidi ya kusoma mabandiko mtandaoni (au/na ku-like/reply/comment) trend moja imejitokeza bayana tangu Bashiru atoe tamko kuhusu Membe.

Na trend hiyo ipo katika sura mbili. Kwanza, suala hilo linaongelewa zaidi na wapinzani kuliko CCM. Labda ni wishful thinking ya wapinzani kudhani suala hilo litaivuruga CCM. But they are wrong. It won't.

Membe is damaged goods. Mtu aliyefeli mchakato uliokuwa in his favour (he's one of the forces behind Lowassa's downfall kwenye kinyang'anyiro cha urais 2015) hawezi kufanikiwa thru "vita ya msituni."

Linalohusiana na sura hii ya kwanza ni ukweli kwamba japo upinzani wa kisiasa si uadui, kila mwenye akili timamu anafahamu kuwa CCM sio tu inawaona wapinzani kuwa ni maadui bali pia kama watu hatari zaidi ya wahalifu/wahaini/magaidi (you name it).

Na hilo halijaanza na Jiwe. Chuki ya CCM dhidi ya upinzani ilikuwapo from word go in 1992. Tofauti kati ya Jiwe na watangulizi wake ni kwamba yeye hahangiki kuficha chuki yake/ya chama chake vs Wapinzani.

Wakati CCM ya Jiwe inanunua wapinzani waziwazi, ya JK ilipandikiza watu kibao ndani ya upinzani walionawiri na kugeuka kansa inayoutafuna upinzani leo hii. Je wafahamu kuwa mbunge mmoja wa upinzani ni afisa kamili (sio source) wa Idara ya Usalama wa Taifa? Huo ni ndio "ununuzi wa wapinzani" uliofanyika kabla ya Jiwe, na ni wa hatari zaidi kuliko huu wa "nunua nunua" aka "hama hama."

Pointi yangu hapa ni kwamba japo upinzani wa kisiasa haupaswi kuwa uadui, "adui" wa kwanza wa Upinzani ni CCM...as chama cha siasa kilichopo madarakani, na ambacho wapinzani wanapaswa kujibidiisha kuking'oa. Kwahiyo iwe Membe, au Mwandosya, au Mwigulu au aendelee Jiwe madarakani, CCM itaendelea kuwa "CCM adui wa wapinzani."

Na la ziada hapo ni ukweli kwamba "vita ya jirani haimaanishi amani kwako." Kwamba kweli kuna vita inayoendelea chini chini huko CCM kuhusu urais 2020, kama ilivyokuwa 1995, 2005, 2015 na sasa 2020 (ilipaswa kuwa 2025 lakini sote twajua sababu za mabadiliko haya).

So, vita hizi zimekuwepo kila baada ya miaka 10. In fact huanza kila baada ya uchaguzi mkuu. JK na Lowassa walianza mkakati wa Ikulu mara baada ya kuwekewa zengwe na baba wa Taifa 1995 na wakaunda mtandao uliofanikiwa kuwaingiza madarakani miaka 10 baadaye yaani 2005.

Sawa, "adui yako mwombee njaa" but only if njaa hiyo itakuwa na faida kwako. Hakuna ushahidi wowote kuwa misukosuko ndani ya CCM huwanufaisha wapinzani. Kwa sababu kama ilivyo kwenye boxing, udhaifu wa opponent wako haumaanishi ubora wako. Ili kumtwanga bondia dhaifu shurti uwe bora zaidi yake na sio dhaifu kama yeye au zaidi yake.

Sura ya pili ya trend hii ni jinsi suala la Membe lilivyopelekea kwa kiasi kikubwa tu kusahaulika kwa masahibu yanayomkabili Mbowe na Esther Matiko, ambao wapo jela kwa siku kadhaa sasa, huku danadana ya kimahakama ikiendelea.

Lengo la danadana hiyo ni wanasiasa hao wawili wawe jela hadi baadaye mwakani. Why? Partly ni mkakati dhidi ya upinzani tarajiwa kwenye mjadala ujao bungeni kuhusu muswada ya vyama vya siasa.

Partly kuwakumbusha wapinzani kwamba "kama tunaweza kumfanyia hivi huyu kiongozi wenu mkuu, ninyi wengine ni akina nani haswa?" It's all wrong lakini it really doesn't matter kwa CCM, wazoefu wa kila mbinu chafu za kisiasa.

Samahani kwa andiko refu, lakini nihitimishe kwa kuwakumbusha ndugu zangu wa upinzani kuwa hizi sideshows za CCM zisiwafanye mjisahau.

Ni haki yenu kujadili kuhusu mustakabali wa siasa za Tanzania including kinachoendelea ndani ya CCM, lakini la muhimu msitolewe kwenye reli kirahisi hivyo.

Whether Membe anatendewa haki au la, haijalishi kwani mwajua fika kuwa Mbowe na Matiko wananyimwa haki zao. Epukeni kuendeshwa na matukio.

I stand to be corrected.
Idiot
 
Hivi huyo mbunge full agent na sio informer ni nani? Tunaweza kuwataja na kuwachambua hapa kwa jinsi wanavyobehave ? Tunatamani tumfahamu kwa mustakabali wa watanzania na sio wachache wa tabaka tawala.......................FUNGUKENI PLEASE 1. NI ZITO KABWE 2.NI JOHN MNYIKA 3.NI JOSHUA NASARI 4.NI ESTER BULAYA 5.NI HALIMA MDEE AU NI NANI?


Haitakusaidia.


Serikali inatekeleza wajibu wake kukuwekea huduma. Kazi kwako kufanya kazi. Acha kupoteza muda kwa yasiyo kuletea faida zaidi ya kukuvuruga
 
Nashukuru umekubali kukosolewa,kuna kitu umekosea ktk kuwa judge wapinzani,kwanza utambue kuwa ishu ya Mbowe kuwekwa gerezani na kunyimwa dhamana si jambo la kuwapa wapinzani tension as if huo ni unyama mpya kati ya unyama mwingi ambao Serikali ovu ya CCM imekuwa ikiwafanyia wapinzani.
Watu hawajatoka kwenye reli eti kwa sababu ya Membe,kuna jambo umeshindwa kujifunza hapo,kwa sasa adui mkubwa wa upinzani ni Magufuli,sasa adui yoyote wa Magufuli ni rafiki mkubwa wa wapinzani... no matter what!
Membe anaweza kuwa mbaya kwa wapinzani pia,lakini ni mzuri nyakati hizi ambazo wapinzani wana tabu kuu...
Ni ule msemo wa ndugu zangu waislamu,Nguruwe ni haramu,lakini ukizidiwa na njaa na hakuna chakula popote basi unaruhusiwa kumla Nguruwe,baada ya kushiba Nguruwe ataendelea kuwa haramu.
Nadhani hadi hapo umenisoma,jambo lingine umekosea kumtuhumu Membe kuwa ni mtu anaye fail mipango yake mingi kama alivyo fail kuupata urais 2015.
Hapo umechemka sana,2015 halikuwa kosa la Membe,sote tunajua kilichotokea,Tanzania ipo mikononi mwa mtu ambaye hata anajua fika kuwa hakupaswa kuwa rais.
Dhambi ya kikwete kumchafua Lowassa tangu akiwa waziri mkuu,kumtengenezea kashfa feki ya Richmond ili kumwondelea nguvu aliyokuwa nayo CCM,kwa lengo tu la kumwandaa Membe ili aje kuwa rais,kisha Membe ampe uwaziri wa mambo ya nje Ridhwani ili aandaliwe naye kuwa rais.
Mambo hayakuwa kama alivyotaka kikwete,nashangaa wewe mtu ulitumikia kitengo nyeti unashindwa kutambua hili,au unapuuza na kumdharau Membe kwa Sababu zako binafsi.
Halafu you should think beyond,mkuu niishie hapa kwa Leo,not everything that you plan will be successful... And nobody knows tomorrow, usipuuze mambo usiyoyajua kesho take,we're all blindfolded about our tomorrows.
Jiwe anaweza kutoka 2020 na huyu huyu Membe unayemdharau leo akashika nchi.
Soma mapinduzi ya Romania,uone kilichomtokea Nicolae Ceasecue .

Duuu!
 
Wanajiremotisha/ jichezesha wenyewe. Huku kwetu sijaona dirisha la dawa la wanachama pekee, bei ya debe la mahindi ni 6 kwa wote uwe Cuf, chadema au CCM. HHt
 
Yaani mtu unajisifu umeshinda huku umemfunga kamba mpinzani wako baharini (jela) kisha unamwambia aogolee?wekeni katiba mpya na tume huru ili sie wananchi tujue pumba na mchele na sio mnategemea policcm kushinda.
tume huru na katiba mpya ndio limekuwa chaka la kuficha udhaifu wenu
 
tume huru na katiba mpya ndio limekuwa chaka la kuficha udhaifu wenu
Ccm hamtaki katiba mpya na tume huru ndio chaka la kuficha udhaifu wenu,eti mwenyekiti wa ccm anateuwa tume ya uchaguzi,mkuu wa polic,mkuu wa majeshi kisha mnadai kuna uchaguz hapo kuhadaa wananchi.
 
Wanajirimotisha/jichezesha wenyewe. Huku kwetu sijaona dirisha la dawa la wanachama wa CCM pekee, bei ya mahindi debe elfu 6 ni kwa wote na mwaka jana kunde na choroko tuliongeza protein wote baada ya kukosa soko.
Wakati mwingie huwatunafikiri mbunge anaakili kwa kununua kura ya mwananchi kwa nusu lita ya pombe ya kienyeji. Lakini kimsingi mdanganya ndiyo mjinga zaidi kuliko mdanganywa kwa sababu mdangana anajua kuwa anadanganya wakati mdanganywa hajui.
Mkuu chahali mimi ni mdogo kwako kwa kila kitu hata hadhi lakini in Madela's voice "hakuna kitu kisichokuwa na faida kabisa, kwani hata vibaya kwa sura hutumika kama models wakati wa kutofautisha ubaya na uzuri mwalimu anapofundisha watoto. Hivyo, naomba nijibu swali langu kwenye post yako iliyopita. Hivi hawa Chahali wa kivukoni - Ifakara ni nduguzo?
 
Watumishi fanyeni hujuma indirect dhidi ya serikali hii onevu kwenu ni miaka 3 hakuna ongezeko la mishahara na maslahi yenu yanazidi kukandamizwa.
 
Ccm hamtaki katiba mpya na tume huru ndio chaka la kuficha udhaifu wenu,eti mwenyekiti wa ccm anateuwa tume ya uchaguzi,mkuu wa polic,mkuu wa majeshi kisha mnadai kuna uchaguz hapo kuhadaa wananchi.[/QUOT
mwenyekiti wa CCM ni rais pia wa tanzania. anafanya teuzi hizo kutokana na mamlaka yake ya kikatiba kama rais na si mwenyekiti wa CCM. nitajie nchi walau moja tu duniani rais hateui mkuu wa polisi, mkuu wa majeshi ama mwenyekiti wa tume ya uchaguzi?

Nchi zote rais anapewa mamlaka kikatiba kuteua hao watu na ambacho wanafanya tofauti ni kwamba wanaidhinishwa na bunge ama senata. sasa , kama rais kashinda urais na chama chake kinaongoza kwa idadi ya wabunge, unadhani hawataidhinishwa?
 
Back
Top Bottom