Jinsi CCM inavyowachezesha Wapinzani kwa rimoti

Mzalendo_Mwandamizi

JF-Expert Member
Dec 12, 2007
1,117
4,764
Moja ya mapungufu makubwa ya Wapinzani wetu ni suala lile lile wanaloilalamikia CCM kila kukicha, kwamba ukiikosoa CCM unaonekana mhaini. As if wao ni wazuri katika kukubali kukosolewa.

Katika hili la kumuona kila anayekosoa ni mhaini au anataka u-DC, tofauti kati ya CCM na Upinzani ni jina tu. Na utakuwa na bahati kama utawakosoa na wakakuita mhaini au mtaka u-DC bila matusi, another janga la kitaifa katika political conversations zetu.

Lakini kwa vile si kuitwa mhaini wala mtaka u-DC kunakoweza kumdhuru mtoa hoja, basi hakuna sababu ya kuchelea kuzungumzia masuala mbalimbali kuhusu Tanzania yetu.

Na ni katika mantiki hiyo, naamsha tafakuri kuhusu jinsi Wapinzani wetu wanavyoendeshwa kwa rimoti na CCM.

Mfano hai: ishu ya Membe. Kwa sie tunaokwenda mbali zaidi ya kusoma mabandiko mtandaoni (au/na ku-like/reply/comment) trend moja imejitokeza bayana tangu Bashiru atoe tamko kuhusu Membe.

Na trend hiyo ipo katika sura mbili. Kwanza, suala hilo linaongelewa zaidi na wapinzani kuliko CCM. Labda ni wishful thinking ya wapinzani kudhani suala hilo litaivuruga CCM. But they are wrong. It won't.

Membe is damaged goods. Mtu aliyefeli mchakato uliokuwa in his favour (he's one of the forces behind Lowassa's downfall kwenye kinyang'anyiro cha urais 2015) hawezi kufanikiwa thru "vita ya msituni."

Linalohusiana na sura hii ya kwanza ni ukweli kwamba japo upinzani wa kisiasa si uadui, kila mwenye akili timamu anafahamu kuwa CCM sio tu inawaona wapinzani kuwa ni maadui bali pia kama watu hatari zaidi ya wahalifu/wahaini/magaidi (you name it).

Na hilo halijaanza na Jiwe. Chuki ya CCM dhidi ya upinzani ilikuwapo from word go in 1992. Tofauti kati ya Jiwe na watangulizi wake ni kwamba yeye hahangiki kuficha chuki yake/ya chama chake vs Wapinzani.

Wakati CCM ya Jiwe inanunua wapinzani waziwazi, ya JK ilipandikiza watu kibao ndani ya upinzani walionawiri na kugeuka kansa inayoutafuna upinzani leo hii. Je wafahamu kuwa mbunge mmoja wa upinzani ni afisa kamili (sio source) wa Idara ya Usalama wa Taifa? Huo ni ndio "ununuzi wa wapinzani" uliofanyika kabla ya Jiwe, na ni wa hatari zaidi kuliko huu wa "nunua nunua" aka "hama hama."

Pointi yangu hapa ni kwamba japo upinzani wa kisiasa haupaswi kuwa uadui, "adui" wa kwanza wa Upinzani ni CCM...as chama cha siasa kilichopo madarakani, na ambacho wapinzani wanapaswa kujibidiisha kuking'oa. Kwahiyo iwe Membe, au Mwandosya, au Mwigulu au aendelee Jiwe madarakani, CCM itaendelea kuwa "CCM adui wa wapinzani."

Na la ziada hapo ni ukweli kwamba "vita ya jirani haimaanishi amani kwako." Kwamba kweli kuna vita inayoendelea chini chini huko CCM kuhusu urais 2020, kama ilivyokuwa 1995, 2005, 2015 na sasa 2020 (ilipaswa kuwa 2025 lakini sote twajua sababu za mabadiliko haya).

So, vita hizi zimekuwepo kila baada ya miaka 10. In fact huanza kila baada ya uchaguzi mkuu. JK na Lowassa walianza mkakati wa Ikulu mara baada ya kuwekewa zengwe na baba wa Taifa 1995 na wakaunda mtandao uliofanikiwa kuwaingiza madarakani miaka 10 baadaye yaani 2005.

Sawa, "adui yako mwombee njaa" but only if njaa hiyo itakuwa na faida kwako. Hakuna ushahidi wowote kuwa misukosuko ndani ya CCM huwanufaisha wapinzani. Kwa sababu kama ilivyo kwenye boxing, udhaifu wa opponent wako haumaanishi ubora wako. Ili kumtwanga bondia dhaifu shurti uwe bora zaidi yake na sio dhaifu kama yeye au zaidi yake.

Sura ya pili ya trend hii ni jinsi suala la Membe lilivyopelekea kwa kiasi kikubwa tu kusahaulika kwa masahibu yanayomkabili Mbowe na Esther Matiko, ambao wapo jela kwa siku kadhaa sasa, huku danadana ya kimahakama ikiendelea.

Lengo la danadana hiyo ni wanasiasa hao wawili wawe jela hadi baadaye mwakani. Why? Partly ni mkakati dhidi ya upinzani tarajiwa kwenye mjadala ujao bungeni kuhusu muswada ya vyama vya siasa.

Partly kuwakumbusha wapinzani kwamba "kama tunaweza kumfanyia hivi huyu kiongozi wenu mkuu, ninyi wengine ni akina nani haswa?" It's all wrong lakini it really doesn't matter kwa CCM, wazoefu wa kila mbinu chafu za kisiasa.

Samahani kwa andiko refu, lakini nihitimishe kwa kuwakumbusha ndugu zangu wa upinzani kuwa hizi sideshows za CCM zisiwafanye mjisahau.

Ni haki yenu kujadili kuhusu mustakabali wa siasa za Tanzania including kinachoendelea ndani ya CCM, lakini la muhimu msitolewe kwenye reli kirahisi hivyo.

Whether Membe anatendewa haki au la, haijalishi kwani mwajua fika kuwa Mbowe na Matiko wananyimwa haki zao. Epukeni kuendeshwa na matukio.

I stand to be corrected.
 
Mission ni moja tu, ni kumtoa Jiwe magogoni.

Awe CCM awe upinzani ila jiwe hatakiwi tena baada ya 2020.

Wapinzani wanajua dhahiri hawana chao kwenye urais kwasababu hawana tume huru ya uchaguzi na dola yote ipo CCM.

Cha kwanza jiwe atoke 2020. Mengine Wapinzani watahangaikia baada ya 2020.
 
Moja ya mapungufu makubwa ya Wapinzani wetu ni suala lile lile wanaloilalamikia CCM kila kukicha, kwamba ukiikosoa CCM unaonekana mhaini. As if wao ni wazuri katika kukubali kukosolewa.

Katika hili la kumuona kila anayekosoa ni mhaini au anataka u-DC, tofauti kati ya CCM na Upinzani ni jina tu. Na utakuwa na bahati kama utawakosoa na wakakuita mhaini au mtaka u-DC bila matusi, another janga la kitaifa katika political conversations zetu.

Lakini kwa vile si kuitwa mhaini wala mtaka u-DC kunakoweza kumdhuru mtoa hoja, basi hakuna sababu ya kuchelea kuzungumzia masuala mbalimbali kuhusu Tanzania yetu.

Na ni katika mantiki hiyo, naamsha tafakuri kuhusu jinsi Wapinzani wetu wanavyoendeshwa kwa rimoti na CCM.

Mfano hai: ishu ya Membe. Kwa sie tunaokwenda mbali zaidi ya kusoma mabandiko mtandaoni (au/na ku-like/reply/comment) trend moja imejitokeza bayana tangu Bashiru atoe tamko kuhusu Membe.

Na trend hiyo ipo katika sura mbili. Kwanza, suala hilo linaongelewa zaidi na wapinzani kuliko CCM. Labda ni wishful thinking ya wapinzani kudhani suala hilo litaivuruga CCM. But they are wrong. It won't.

Membe is damaged goods. Mtu aliyefeli mchakato uliokuwa in his favour (he's one of the forces behind Lowassa's downfall kwenye kinyang'anyiro cha urais 2015) hawezi kufanikiwa thru "vita ya msituni."

Linalohusiana na sura hii ya kwanza ni ukweli kwamba japo upinzani wa kisiasa si uadui, kila mwenye akili timamu anafahamu kuwa CCM sio tu inawaona wapinzani kuwa ni maadui bali pia kama watu hatari zaidi ya wahalifu/wahaini/magaidi (you name it).

Na hilo halijaanza na Jiwe. Chuki ya CCM dhidi ya upinzani ilikuwapo from word go in 1992. Tofauti kati ya Jiwe na watangulizi wake ni kwamba yeye hahangiki kuficha chuki yake/ya chama chake vs Wapinzani.

Wakati CCM ya Jiwe inanunua wapinzani waziwazi, ya JK ilipandikiza watu kibao ndani ya upinzani walionawiri na kugeuka kansa inayoutafuna upinzani leo hii. Je wafahamu kuwa mbunge mmoja wa upinzani ni afisa kamili (sio source) wa Idara ya Usalama wa Taifa? Huo ni ndio "ununuzi wa wapinzani" uliofanyika kabla ya Jiwe, na ni wa hatari zaidi kuliko huu wa "nunua nunua" aka "hama hama."

Pointi yangu hapa ni kwamba japo upinzani wa kisiasa haupaswi kuwa uadui, "adui" wa kwanza wa Upinzani ni CCM...as chama cha siasa kilichopo madarakani, na ambacho wapinzani wanapaswa kujibidiisha kuking'oa. Kwahiyo iwe Membe, au Mwandosya, au Mwigulu au aendelee Jiwe madarakani, CCM itaendelea kuwa "CCM adui wa wapinzani."

Na la ziada hapo ni ukweli kwamba "vita ya jirani haimaanishi amani kwako." Kwamba kweli kuna vita inayoendelea chini chini huko CCM kuhusu urais 2020, kama ilivyokuwa 1995, 2005, 2015 na sasa 2020 (ilipaswa kuwa 2025 lakini sote twajua sababu za mabadiliko haya).

So, vita hizi zimekuwepo kila baada ya miaka 10. In fact huanza kila baada ya uchaguzi mkuu. JK na Lowassa walianza mkakati wa Ikulu mara baada ya kuwekewa zengwe na baba wa Taifa 1995 na wakaunda mtandao uliofanikiwa kuwaingiza madarakani miaka 10 baadaye yaani 2005.

Sawa, "adui yako mwombee njaa" but only if njaa hiyo itakuwa na faida kwako. Hakuna ushahidi wowote kuwa misukosuko ndani ya CCM huwanufaisha wapinzani. Kwa sababu kama ilivyo kwenye boxing, udhaifu wa opponent wako haumaanishi ubora wako. Ili kumtwanga bondia dhaifu shurti uwe bora zaidi yake na sio dhaifu kama yeye au zaidi yake.

Sura ya pili ya trend hii ni jinsi suala la Membe lilivyopelekea kwa kiasi kikubwa tu kusahaulika kwa masahibu yanayomkabili Mbowe na Esther Matiko, ambao wapo jela kwa siku kadhaa sasa, huku danadana ya kimahakama ikiendelea.

Lengo la danadana hiyo ni wanasiasa hao wawili wawe jela hadi baadaye mwakani. Why? Partly ni mkakati dhidi ya upinzani tarajiwa kwenye mjadala ujao bungeni kuhusu muswada ya vyama vya siasa.

Partly kuwakumbusha wapinzani kwamba "kama tunaweza kumfanyia hivi huyu kiongozi wenu mkuu, ninyi wengine ni akina nani haswa?" It's all wrong lakini it really doesn't matter kwa CCM, wazoefu wa kila mbinu chafu za kisiasa.

Samahani kwa andiko refu, lakini nihitimishe kwa kuwakumbusha ndugu zangu wa upinzani kuwa hizi sideshows za CCM zisiwafanye mjisahau.

Ni haki yenu kujadili kuhusu mustakabali wa siasa za Tanzania including kinachoendelea ndani ya CCM, lakini la muhimu msitolewe kwenye reli kirahisi hivyo.

Whether Membe anatendewa haki au la, haijalishi kwani mwajua fika kuwa Mbowe na Matiko wananyimwa haki zao. Epukeni kuendeshwa na matukio.

I stand to be corrected.
WAPINZANI TZ n janga... ni matusi, hawataki ushauri, hawakosoleki, wanajenga taswira mbaya ktk nchi kwamba CCM n MAshwetani wao n ANGELS, wanaamnisha watu kuwa wao wanajua kila kitu na wengne wote n wajinga... Wanataka democracy, wao wenyewe hawana democracy ndani ya vyama vyao, na wanabadilibadili gia angani mara kwa mara!

WAPINZANI WETU TUWAOMBEE, MAANA TUNAWATAKA, N MUHIMU SANA. TUWAOMBEE (1) wakosoe kwa hekima na busara, (2) wapate sera mbadala, (3) wawe serikali mbadala inayoonekana yenye sura ya kitaifa, siyo kikanda. This is because to be trusted with power, they have to be at their best!
 
Mission ni moja tu, ni kumtoa Jiwe magogoni.

Awe CCM awe upinzani ila jiwe hatakiwi tena baada ya 2020.

Wapinzani wanajua dhahiri hawana chao kwenye urais kwasababu hawana tume huru ya uchaguzi na dola yote ipo CCM.

Cha kwanza jiwe atoke 2020. Mengine Wapinzani watahangaikia baada ya 2020.
Asipotoka hyo 2020??
 
Mission ni moja tu, ni kumtoa Jiwe magogoni.

Awe CCM awe upinzani ila jiwe hatakiwi tena baada ya 2020.

Wapinzani wanajua dhahiri hawana chao kwenye urais kwasababu hawana tume huru ya uchaguzi na dola yote ipo CCM.

Cha kwanza jiwe atoke 2020. Mengine Wapinzani watahangaikia baada ya 2020.
Hata 2015 plan ilikua kama hii; wakafeli ni jambo gani linalowapa matumaini ya kufanikiwa this time
 
Evarist Chahali nakubaliana na ww katika makala yote.

Zitto sio mpinzani...na nimewaambia watu hili suala mara nyingi sana..ajabu watu hawaoni hata yaliyo wazi.

Katika namna zote membe is so pooor na hana ubavu wowote. Kwanza sijui wafuasi wa membe ni kina nani?

Leo kuna mambo ya msingi tumeacha kujadili kama taifa..isshu ya sheria ya mafao..ishu ya katiba mpya..sheria ijayo ya vyama vya siasa. Eti tunakomaa kujadili propaganda wanazotengeneza CCM Ili ki divert mwelekeo wa mijadala

Mungu atusaidie walau tupate upinzani makini wa kina lissu na heche....mbowe amezidiwa na amezungukwa na ma ajent wa ccm...walewale...kina lowasa
 
Mission ni moja tu, ni kumtoa Jiwe magogoni.

Awe CCM awe upinzani ila jiwe hatakiwi tena baada ya 2020.

Wapinzani wanajua dhahiri hawana chao kwenye urais kwasababu hawana tume huru ya uchaguzi na dola yote ipo CCM.

Cha kwanza jiwe atoke 2020. Mengine Wapinzani watahangaikia baada ya 2020.
Mnarudia kile kile mlichofanya 2015... Mlisema mlipo mbeba Lowassa, "kinachotakiwa n CCM watoke...mengine baadaye. " Hakuna kitu kama hicho, my dear friend!

Ktk kitu kinachonshangazaga n madai ya wizi wa kura! Hv kweli, mtu na akl zako unategemea ushinde urais 2015 kwa kufanya kampeni dakika 10 kumi na helicopter kwenye makao makuu ya wilaya na mikoa tu? Da! Unafikia asilimia 30 ya wapiga kura, utashindaje?
 
Mkuu wengine si kama tunaipenda CCM ila ni kwamba tunaona kinachoendelea upande wa pili ni uhuni uhuni.............

Tulipigania tukijua tupo nao ila tulipoona rangi zao 2015 atukuamin tukakaa pemben na kumsupot huyu ambae japo anakosa vitu flan ila ni bora na afadhali.......!
 
"Membe is damaged goods. Mtu aliyefeli mchakato uliokuwa in his favour (he's one of the forces behind Lowassa's downfall kwenye kinyang'anyiro cha urais 2015) hawezi kufanikiwa thru "vita ya msituni.", (Shushushu, Evarist Chahali, 2018)
 
Mission ni moja tu, ni kumtoa Jiwe magogoni.

Awe CCM awe upinzani ila jiwe hatakiwi tena baada ya 2020.

Wapinzani wanajua dhahiri hawana chao kwenye urais kwasababu hawana tume huru ya uchaguzi na dola yote ipo CCM.

Cha kwanza jiwe atoke 2020. Mengine Wapinzani watahangaikia baada ya 2020.
upinzani huu hauna uwezo hata wa kumtoa mbunge yeyote wa ccm madarakani , eti ndio mnawaza kuitoa CCM madarakani.
 
Mnatuchanganya wananchi. Na mnataka siasa tuzifanye yanga na Simba
Kwa taarifa yenu hatuna permanet interest lolote nafuu kwetu tunaunga mkono. Hao wapakuaji wajijua kuwa masinia mengine huyapeleka wapi
Imagine wabunge wote wapo kwenye kamati
Wakitoka nje wanaanza kulalamila ooh nyama hawakuleta.
 
Yani ni nini au kipi alichokiandika Evarist Chahali kisichojulikana. Kama ni zitto inajulikana tangu mwanzo kuwa sio mpinzani na ndio maana chadema walimfukuza. Alianzisha chama kwa support ya ccm, maana ACT ilianzishwa kuidhoofisha chadema 2015, ingawa hilo halikufananikiwa. Kuhusu ccm kuwa adui wa upinzani hilo liko wazi halikuhitaji makala kulielezea. Ni sawa na mtu kuandika makala kuelezea kwamba chadema ni chama cha upinzani Tanzania, sijui ni nini au kipi itakuwa ujumbe hapo.
Anyway ni uzi wake, nasi ni wasomaji na wachangiaji.
 
Back
Top Bottom