Mheshimiwa_Mtemi
JF-Expert Member
- Oct 27, 2014
- 288
- 215
Asalaam
Nimekuza najiuliza Jinamizi ni nini hasa? He ni Jini? Mizimu? Pepo au mashetani?
Nyakati za usiku hasa usiku wa manane inatokea upo kwenye ndoto ambayo huwezi kupumua wala kuongea lakini unasikia kila kitu.
Mbaya zaidi unakua unatamani hata mtu akuguse ili uzinduke. Kifupi ni kama umekabwa au kubanwa na kitu.
Wengine hali hii huwapata nyakati za mchana wakiwa wamelala.
Hivi Jinamizi ni nini?
Nawasilisha.
=====
Tafadhali Blasto Ngeleja pia soma Kukabwa na jinamizi wakati usiku umelala
Nimekuza najiuliza Jinamizi ni nini hasa? He ni Jini? Mizimu? Pepo au mashetani?
Nyakati za usiku hasa usiku wa manane inatokea upo kwenye ndoto ambayo huwezi kupumua wala kuongea lakini unasikia kila kitu.
Mbaya zaidi unakua unatamani hata mtu akuguse ili uzinduke. Kifupi ni kama umekabwa au kubanwa na kitu.
Wengine hali hii huwapata nyakati za mchana wakiwa wamelala.
Hivi Jinamizi ni nini?
Nawasilisha.
=====
MAELEZO YA KISAYANSI KUHUSU KULALA KUPOOZA.
Kwa mujibu wa Ryan Hurd kwenye makala yake ya "The sleeping paralysis report" kulala kupooza ni hali impatayo mtu pale muingiliano wa taswira za kwenye mazingira ya ndoto kutokea katika mazingira ya mtu akiwa macho au anaufahamu na mazingira yake halisi au ya nje ya usingizi(ndoto).Kwa kifupi ni hali impatayo mtu pale ubongo au akili yake ikiwa macho lakini mwili wake umelala au kupooza. Kulala kupooza au sleeping paralysis humpata mtu pindi tu anaanza kupata usingizi (wakati akiwa ubongo wake ukiwa bado na ufahamu na mazingira yake yamzungukayo) au humpata mtu pindi tu anapotaka kuamka kutoka usingizini ( akiwa tayari ubongo wake umeanza rejea ufahamu wa mazingira yake ya nje au halisi) na hivyo kumfanya mtu huyo ashindwe kujisogeza mwili wake na kupatwa maono (hallucinations) ya taswira mbalimbali.
Tafadhali Blasto Ngeleja pia soma Kukabwa na jinamizi wakati usiku umelala