Jimboni Hai hali ni tete, mhe. Mbowe haya huyajui?

HAMY-D

JF-Expert Member
Sep 18, 2011
7,149
3,817
Mhe Mbowe, mbali na uenyekiti wa CHADEMA taifa ila wewe ni mbunge wa Hai, jitihada zako kubwa za kukitumikia chama chako kila mtanzania ana ziona, ila hoja ya msingi ni kwamba, umesahau kuwa wewe ni mbunge?

Mhe Mbowe wananchi wa Hai wana taabika mno chini ya uongozi wako kama mbunge wao, kama mambo yamekushinda ni busara ukae pembeni kuliko kuendelea kung'ang'ania nafasi usiyo iweza.

Tangu umerudi tena bungeni mwaka 2010 ni mara chache mno umekuwa ukihimiza serikali kukumbuka jimbo lako katika mgao wa bajeti, mara nyingi wewe umekuwa ukihimiza wabunge wako waombe miongozo isiyo na tija ili ukitangaze chama chako cha CHADEMA kupitia bunge.

Mhe Mbowe angalau basi uwe una taja taja hata jimbo lako la Hai, wananchi wana kero nyingi sana ambazo wewe kama mbunge ni jukumu lako kuhakikisha zina tatuliwa na serikali, usipo wasemea wewe atawasemea nani?

Wana-JF, jioneeni wenyewe jinsi wananchi wa jimbo la Hai wanavyo pata hadha chini ya uongozi wa bwana Mbowe!


hai.jpg
 
Mhe Mbowe, mbali na uenyekiti wa CHADEMA taifa ila wewe ni mbunge wa Hai, jitihada zako kubwa za kukitumikia chama chako kila mtanzania ana ziona, ila hoja ya msingi ni kwamba, umesahau kuwa wewe ni mbunge?

Mhe Mbowe wananchi wa Hai wana taabika mno chini ya uongozi wako kama mbunge wao, kama mambo yamekushinda ni busara ukae pembeni kuliko kuendelea kung'ang'ania nafasi usiyo iweza.

Tangu umerudi tena bungeni mwaka 2010 ni mara chache mno umekuwa ukihimiza serikali kukumba jimbo lako katika mgao wa bajeti, mara nyingi wewe umekuwa ukihimiza wabunge wako waombe miongozo isiyo na tija ili ukitangaze chama chako cha CHADEMA kupitia bunge.

Mhe Mbowe angalau basi uwe una taja taja hata jimbo lako la Hai, wananchi wana kero nyingi sana ambazo wewe kama mbunge ni jukumu lako kuhakikisha zina tatuliwa na serikali, usipo wasemea wewe atawasemea nani?

Wana-JF, jioneeni wenyewe jinsi wananchi wa jimbo la Hai wanavyo pata hadha chini ya uongozi wa bwana Mbowe!


View attachment 97319

Nape yupo Arusha. Kachukue 7 zako kabla hanaishiwa. Maana machalii wameanza kudai mgao wa kula CCM kura CHADEMA.
 
HAMY-D kweli wewe kilaza..Ukiacha mbali Mnyika,Lema na Msigwa hakuna mbunge wa bunge la Jamhuri aliye karibu na wapiga kura wake kama Mbowe mbali na majukumu yake...pole sana kakilaza ketu!! nenda ukakate gogo ulale basi maana ndo muda wenu mliochoka akili!!
 
mbona humuulizi Fuya Kimbita aliyekuwepo kabla ya Mbowe? Kama una uchungu sana mwaka 2015 sio mbali jipange ukagombee ili ukajenge hilo daraja? ni mbunge wangu na Hai siyo TETE ndio Wilaya yenye maendeleo kuliko zote Tanzania kama hujui go back to your STD I history book!!!!!! pmf..:A S embarassed::A S embarassed::A S-omg::A S-omg::A S-omg::A S-omg::A S-omg::A S-omg::A S-omg::A S-omg:
 
Unataka Mh.Mbowe ajenge daraja hilo kubwa kiasi hicho?kwa pesa zipi kama sii za halmashauri?kilimanjaro kuna mito mingi toka mlimani.Hivyo huwezi jenga daraja kila kijiji.Zinajengwa kwenye barabara kuu au kubwa
 
mbona humuulizi Fuya Kimbita aliyekuwepo kabla ya Mbowe? Kama una uchungu sana mwaka 2015 sio mbali jipange ukagombee ili ukajenge hilo daraja? ni mbunge wangu na Hai siyo TETE ndio Wilaya yenye maendeleo kuliko zote Tanzania kama hujui go back to your STD I history book!!!!!! pmf..:A S embarassed::A S embarassed::A S-omg::A S-omg::A S-omg::A S-omg::A S-omg::A S-omg::A S-omg::A S-omg:


Upo tayari kupindisha ukweli ili tu umtetee bwana Mbowe?

Kweli CHADEMA ni zaidi ya miujiza, watanzania mmekuwaje?
 
Hilo daraja ni Daraja la Kiungi maarufu kama DARAJA LA MNEPO.

Tatizo la daraja hilo ni la tangu tupate uhuru.

Mara kwa mara
DIWANI wa CCM wa Kata ya Machame Weruweru, Adris Mandrai amekuwa akihujumu ujenzi wa daraja hilo.

Awali, aliwataka wananchi wa kata hiyo kuhakikisha wanaunga jitihada za Serikali ya wilaya kuchangia fedha kwa ajili ya ujenzi wa Daraja la Mnepo, kila mwananchi alitakiwa kuchangia Sh 5,000, ambapo halmashauri hiyo imeidhinisha Sh milioni 20 kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo.

Alisema pamoja na jitihada za Serikali, pia aliyekuwa Mbunge wa Hai, Fuya Kimbita, aliwahi kuchangia Sh milioni tano kupitia fedha za Mfuko wa Jimbo.

Kiwanda cha TPC walishajitolea kulijenga ila hela walizotoa kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo zikaliwa na Diwani huyo wa CCM na washirika wake.

Kanisa Katoliki ililo karibu na eneo hilo kwa ufadhili wa wazungu walitaka kulijenga daraja hilo ila Diwani huyo akaleta udini na kukwamisha taratibu za ujenzi huo.

Kosa la watu wa Kiyungi ni kuendelea kuikumbatia CCM na kuchelewesha maendeleo ktk eneo lao.

Natamani Daraja hilo lingekuwa ndani ya Manispaa ya Moshi lingekuwa limeshatengenezwa.

Mbunge asiyajue yote hayo? basi Mbowe hajui wajibu wake.


Katika kikao cha bunge kilichofanyika
June 13, 2011, katika kuonesha kwamba Mh Mbowe analipigania daraja hilo alimuuliza Naibu waziri kama ifuatavyo;
Question from : Hon. Freeman Aikaeli Mbowe
Question: KIONGOZI WA KAMBI YA UPINZANI BUNGENI:

Mheshimiwa Spika nakushukuru, kwa kuwa suala la madaraja ni suala la msingi ambalo linaweza likahatarisha maisha ya watumiaji na kwa sababu tatizo la Iringa lililozungumzwa hapa na Mheshimiwa Mbunge linafanana sana na tatizo la daraja ambalo linaitwa daraja la Mnepo linalounganisha Jimbo la Hai Mkoa wa Kilimanjaro na Jimbo la Moshi Vijijini katika Kata ya Machame Weruweru, katika Kijiji cha Mijongweni. Ni daraja ambalo limepata kutolewa ahadi mara kadhaa na viongozi wa Kitaifa akiwemo Mheshimiwa Rais Benjamin Mkapa na ahadi hiyo hadi leo haijatekelezwa.

Je, Waziri atatusaidiaje katika kutatua hili la daraja la daraja la Mnepo linaloounganisha Kata na vilevile Majimbo mawili ambayo ni muhimu na linatumiwa na wananchi walio wengi wakiwemo wanafunzi?


Answered by: Hon. Aggrey Deaisile Joshua Mwanri
Answer: NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI):

Mheshimiwa Spika, daraja ninalifahamu, mimi ninamwomba Mheshimiwa Mbowe kwamba tutoke tuende tukaiangalie status ya jambo hili tujue vizuri anapozungumza hapa anazungumza nini, kwa sababu daraja moja hapa lile la kwanza lililouliziwa swali hapa ni shilingi bilioni 1.9 ni hela nyingi.

Sasa nikisema kwamba aingize katika Bajeti ya Halmashauri, hela zinazopelekwa katika Halmashauri sana sana hazizidi milioni mia nne na hamsini, kule kwangu Siha ni milioni mia tatu na hamsini, hela tunazokupelekea Hai ni milioni mia nne na ishirini ndizo zinazopelekwa kwa ajili ya barabara. Sasa haya yote ni lazima tuende tukaketi tuangalie kwa pamoja mimi na yeye.

Mheshimiwa Spika, huyu namwita homeboy wangu kwa hiyo tutakwenda kuzungumza tutaelewana katika jambo hili ili tujue kwamba itakuwaje.

Nadhani mpaka hapo umeelewa kwamba tatizo ni CCM na Serikali yake kwa dhati kabisa hawana mpango madhubuti wa kutaka kutatua tatizo la daraja hilo.
 
Upo tayari kupindisha ukweli ili tu umtetee bwana Mbowe?

Kweli CHADEMA ni zaidi ya miujiza, watanzania mmekuwaje?

hata jimbo la Mk .were pale magogoni lina kero nyingi sana, na yeye km kiranja mkuu hajaweza kutatua hata 1, Mbowe anajitahidi sana
 
Hilo daraja ni daraja la kiungi maarufu kama DARAJA LA MNEPO. Tatizo la daraja hilo ni la tangu tupate uhuru Mara kwa mara Diwani wa CCM wa kata hiyo ya kiungi amekuwa akihujumu ujenzi wa daraja hilo. Kiwanda cha TPC walishajitolea kulijenga ila hela walizotoa kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo zikaliwa na Diwani huyo wa CCM na washirika wake. Kanisa Katoliki ililo karibu na eneo hilo kwa ufadhili wa wazungu walitaka kulijenga daraja hilo ila Diwani huyo akaleta udini na kukwamisha taratibu za ujenzi huo. Kosa la watu wa Kiungi ni kuendelea kuikumbatia CCM na kuchelewesha maendeleo ktk eneo lao. Natamani Daraja hilo lingekuwa ndani ya Manispaa ya Moshi lingekuwa limeshatengenezwa.

Mbunge asiyajue yote hayo? basi Mbowe hajui wajibu wake.
 
HAMY-D kweli wewe kilaza..Ukiacha mbali Mnyika,Lema na Msigwa hakuna mbunge wa bunge la Jamhuri aliye karibu na wapiga kura wake kama Mbowe mbali na majukumu yake...pole sana kakilaza ketu!! nenda ukakate gogo ulale basi maana ndo muda wenu mliochoka akili!!

Huyu jamaa ni kilaza kweli kweli. Uthibitisho ni michango yake au post zake. Nyingi hazina mwelekeo wa aina yo yote. Nina wasiwasi na elimu yake. Isije ikawa anamudu KKK?

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Upo tayari kupindisha ukweli ili tu umtetee bwana Mbowe?

Kweli CHADEMA ni zaidi ya miujiza, watanzania mmekuwaje?

Mambo ya Hai yanakuhusu nini?Mijanamume mingine ka
mishoga yaani.
 
Daraja kama ili lipo Mbeya kwenye jimbo la Mhe Mwakyembe ambaye ni waziri wa Uchukuzi! Sasa sembuse kwa mbunge wa upinzani? Labda kama unataka atumie fedha zake za mfukoni! Bado haujaongea kitu changa bongo zaidi. By the way mtoto wa Nape(wa kufikia) yupo Arusha kawahi mgawo!
 
Tutaaminije kuwa ni Hai kwa hyo picha.
Kikwete alipofungua barabara ya lami pale Hai hilo hakuliona kupitia au hakuna Dc na mkurugenzi wa Wilaya?
 
Embu soma hii thread Mbowe hatetewi ni huyo diwani wa chama chako cha mashaitwani wa kijani ndo alikula fedha za kujenga daraja sasa unataka akapigane?
 
me hapo ndiyo siasa huwa inanichosha kabisa hata ufanye vpi wanafiki hawakosi yani ni tatizo watu wanapenda watu na vyama na si maendeleo yani ili mradi ni wa chama chake tu hata kama hana mipango ya mana yeye anashabikia tu. yani watanzania tunahitaji idadi kubwa sana ya watu wasiokuwa wanachama wa vyama vya siasa ili tuweze kuwa na uwezo wa kuchagua watu wanaotufaa na si watu tunaowashabikia na vyama tunavyovipenda ahsanteni sana.
 
Back
Top Bottom