Wanasema ukistaajabu ya Mussa utaona ya Mwigulu,
Wakati mbunge wa Singida magharibi Mhe. Mwigulu Mnchemba anapasua masafa ya nchi wapiga kura wake wanamlilia kweli aende akawasikilize matatizo yao kwani shida zimewakaba hadi shingoni. Wanamstaajabu mbunge wao ambae wakati rais wake anachanja mbuga duniani yeye mbunge anachanja mbuga inchini akiwawakilisha wanainchi ambao hawakumchagua akiwaacha wao katikati ya lindi la matatizo. Nimepita jimboni mwa huyo mbunge wapiga kura wake wakanieleza yafuatayo kwa mdomo wao:-
Shida zinazowakabili-
1. Njaa kali.
Wana uhaba mkubwa wa chakula mvua zilikuwa haba sana ukitilia maanani wenywe wako kwenye bonde la ufa inabidi kupata mvua za kutosha ili wavune mtama (lugugu) wacha mahindi, kwa hiyo wanauhaba mkubwa wa chakula familia nyingi karibu % 90 katika jimbo la Mwigulu wanakula mlo mmoja na huo mlo mmoja hawashibi. Watoto wa shule wanashindwa kwenda shule shauri ya njaa, pia wakirudi nyumbani saa 6 wanalala inje ya nyumba shauri ya njaa kali ndani hamna kitu na wazazi wao hawapo wamekwenda kutafuta vibarua, wengine wanazirahi.
2. Umasikini wa kipato.
Wanaumaskini mkubwa wa kipato wachilia mbali njaa inayowakabili, hawana zao lolote la maana la biashara,ajira wanayoitegemea ingalao kupata kipato ili kutatua matatizo yao ni ombaomba kwenye treni, na biashara za ovyoovyo kwenye treni yakati biashara kama kuuza ujugu, vikapo , vindege, vifilimbi vya miti, ukwaju na ubuyu, ni vibiashara vya kijinga jinga tu, vijana wengi wamekimbia jimbo wasichana kwa wavulana wameenda kutafuta ajira mjini na wengine wameenda kutafuta vibarua vya kulima tumbaku katika vijiji kata ya Igwisi urambo.
3. Ukame mkali.
Kuna ukame wa hali ya juu, ukame unawakabili watu na mifugo, mifugo kuanzia vijiji vya Kintinku, Igose, Makutupora Kirimatinde Salanda, Ulyampiti, Msigili hadi Sherui mifugo wanakunywa mgwao, yaani wanakunywa leo siku inayofuata hawanywi maji.Maji yenyewe wanayapata kwa kuesea kwa kutumia Nkosi,wanadamka usiku kwenda kwenye visima walivyochimba wenyewe ili kuchotelea maji kwa kutumia nkosi na kujaza mrambo ili mchana mifugo waje wanywe, kazi hiyo ni ngumu sana inawafanya vijana wengi kukimbia makazi yao au kuwa ni ajira kwa wenye uwezo, mtu unafanya kazi hiyo ngumu halafu anaishia kupewa chakula tu jioni.
4. Wizi wa mifugo.
Kuna wizi wa mifugo wa hali ya juu, hii ni kutokana na njaa kali, mifugo inaibiwa nyumbani usiku au mchungaji ananyang`anywa mchana kweupe machungani, mifugo inaibiwa kiasi kuna tishio la mifugo kwisha kwa wizi, wengine huiba mbuzi na kwenda kuchinja polini na kuishia kula nyama shauri ya njaa.
5. Magonjwa:
Tunakabiliwa na magonjwa ya kuambikiza, magonjwa yanayotusumbua ni Malaria na kichocho, malaria inatusumbua kwa ajili ya joto hapa jimboni kwa Mwigulu ni bonde la ufa yaani ardhi imetitia chini hivyo joto kweli usiku na mbu ni wengi , kwenye vituo vya kutolea huduma ya afya kama zahanati na vituo vya afya hamana dawa mseto kuna paracetamo tu, pia uwezo wa kukata bima ya afya hatuna kwa sababu ya umasikini wa kipato, Kichocho kinasumbua sana hasa wanafunzi ,shule kama Ulyampiti karibu wanafunzi wote wana kichocho dawa ya Parazenguantel hamana katika vituo vyote hadi hospitali ya mkoa ya Singida, halafu dawa yenyewe ni ghali.
Ushauri kwa Mbunge wa Mwigulu
Aje akae jimboni ili waweze kusaidiana kukabili matatizo haya , huko unakozurula kwani ndiko walio mchagua? Aache kuhangaika na LEMA kwani mbunge huyo hamwezi wanaweza wenyewe waliomchagua. Kupenda ni sehemu ya uhai , kumeambatana na uhai kupenda hakuwezi kwisha mpaka uhai umetoweka kwa hiyo kama Arusha wanampenda mbunge wao Mwigulu hata ufanyeje unajisumbua tu njoo jimboni utusaidie wapiga kura wako tunakwisha. Huyo LEMA unayempiga vita yeye anawapigania wapiga kura wake hadi saa ingine bungeni haendi hadi anafungwa jela mahabusu wewe Mwigulu unazurula tu unatusahau,
Kama mbunge una uwezo kutusaidia kupata dawa hasa za kichocho, kulobe chakula kije jimboni ingalao tutanua, Kwenye jimbo la Tundu Lisu mashuleni wanafunzi wanapata mlo wa mchana kupitia Pragram ya WFP, Mbunge wetu Mwigulu yuko wapi na sisi tupate mpango huu. Njoo tusaidiane kuandaa mkakati wa kukabiliana na wizi wa mifugo, njoo tujipange tuweze kukata bima za afya kwa watendaji wa kata ingalao zituwezeshe kupata matibabu hata hayo kiduchu.
Mbunge wetu Mwigulu njoo jimboni sisi wapiga kura wako tunakulilia kwani hiyo jeuri uliyopewa na Rais kwamba wewe unakabiliana na wapinzani hukimbilii polisi isikuvimbishe kichwa kiasi unasahau wajibu wako.
Wakati mbunge wa Singida magharibi Mhe. Mwigulu Mnchemba anapasua masafa ya nchi wapiga kura wake wanamlilia kweli aende akawasikilize matatizo yao kwani shida zimewakaba hadi shingoni. Wanamstaajabu mbunge wao ambae wakati rais wake anachanja mbuga duniani yeye mbunge anachanja mbuga inchini akiwawakilisha wanainchi ambao hawakumchagua akiwaacha wao katikati ya lindi la matatizo. Nimepita jimboni mwa huyo mbunge wapiga kura wake wakanieleza yafuatayo kwa mdomo wao:-
Shida zinazowakabili-
1. Njaa kali.
Wana uhaba mkubwa wa chakula mvua zilikuwa haba sana ukitilia maanani wenywe wako kwenye bonde la ufa inabidi kupata mvua za kutosha ili wavune mtama (lugugu) wacha mahindi, kwa hiyo wanauhaba mkubwa wa chakula familia nyingi karibu % 90 katika jimbo la Mwigulu wanakula mlo mmoja na huo mlo mmoja hawashibi. Watoto wa shule wanashindwa kwenda shule shauri ya njaa, pia wakirudi nyumbani saa 6 wanalala inje ya nyumba shauri ya njaa kali ndani hamna kitu na wazazi wao hawapo wamekwenda kutafuta vibarua, wengine wanazirahi.
2. Umasikini wa kipato.
Wanaumaskini mkubwa wa kipato wachilia mbali njaa inayowakabili, hawana zao lolote la maana la biashara,ajira wanayoitegemea ingalao kupata kipato ili kutatua matatizo yao ni ombaomba kwenye treni, na biashara za ovyoovyo kwenye treni yakati biashara kama kuuza ujugu, vikapo , vindege, vifilimbi vya miti, ukwaju na ubuyu, ni vibiashara vya kijinga jinga tu, vijana wengi wamekimbia jimbo wasichana kwa wavulana wameenda kutafuta ajira mjini na wengine wameenda kutafuta vibarua vya kulima tumbaku katika vijiji kata ya Igwisi urambo.
3. Ukame mkali.
Kuna ukame wa hali ya juu, ukame unawakabili watu na mifugo, mifugo kuanzia vijiji vya Kintinku, Igose, Makutupora Kirimatinde Salanda, Ulyampiti, Msigili hadi Sherui mifugo wanakunywa mgwao, yaani wanakunywa leo siku inayofuata hawanywi maji.Maji yenyewe wanayapata kwa kuesea kwa kutumia Nkosi,wanadamka usiku kwenda kwenye visima walivyochimba wenyewe ili kuchotelea maji kwa kutumia nkosi na kujaza mrambo ili mchana mifugo waje wanywe, kazi hiyo ni ngumu sana inawafanya vijana wengi kukimbia makazi yao au kuwa ni ajira kwa wenye uwezo, mtu unafanya kazi hiyo ngumu halafu anaishia kupewa chakula tu jioni.
4. Wizi wa mifugo.
Kuna wizi wa mifugo wa hali ya juu, hii ni kutokana na njaa kali, mifugo inaibiwa nyumbani usiku au mchungaji ananyang`anywa mchana kweupe machungani, mifugo inaibiwa kiasi kuna tishio la mifugo kwisha kwa wizi, wengine huiba mbuzi na kwenda kuchinja polini na kuishia kula nyama shauri ya njaa.
5. Magonjwa:
Tunakabiliwa na magonjwa ya kuambikiza, magonjwa yanayotusumbua ni Malaria na kichocho, malaria inatusumbua kwa ajili ya joto hapa jimboni kwa Mwigulu ni bonde la ufa yaani ardhi imetitia chini hivyo joto kweli usiku na mbu ni wengi , kwenye vituo vya kutolea huduma ya afya kama zahanati na vituo vya afya hamana dawa mseto kuna paracetamo tu, pia uwezo wa kukata bima ya afya hatuna kwa sababu ya umasikini wa kipato, Kichocho kinasumbua sana hasa wanafunzi ,shule kama Ulyampiti karibu wanafunzi wote wana kichocho dawa ya Parazenguantel hamana katika vituo vyote hadi hospitali ya mkoa ya Singida, halafu dawa yenyewe ni ghali.
Ushauri kwa Mbunge wa Mwigulu
Aje akae jimboni ili waweze kusaidiana kukabili matatizo haya , huko unakozurula kwani ndiko walio mchagua? Aache kuhangaika na LEMA kwani mbunge huyo hamwezi wanaweza wenyewe waliomchagua. Kupenda ni sehemu ya uhai , kumeambatana na uhai kupenda hakuwezi kwisha mpaka uhai umetoweka kwa hiyo kama Arusha wanampenda mbunge wao Mwigulu hata ufanyeje unajisumbua tu njoo jimboni utusaidie wapiga kura wako tunakwisha. Huyo LEMA unayempiga vita yeye anawapigania wapiga kura wake hadi saa ingine bungeni haendi hadi anafungwa jela mahabusu wewe Mwigulu unazurula tu unatusahau,
Kama mbunge una uwezo kutusaidia kupata dawa hasa za kichocho, kulobe chakula kije jimboni ingalao tutanua, Kwenye jimbo la Tundu Lisu mashuleni wanafunzi wanapata mlo wa mchana kupitia Pragram ya WFP, Mbunge wetu Mwigulu yuko wapi na sisi tupate mpango huu. Njoo tusaidiane kuandaa mkakati wa kukabiliana na wizi wa mifugo, njoo tujipange tuweze kukata bima za afya kwa watendaji wa kata ingalao zituwezeshe kupata matibabu hata hayo kiduchu.
Mbunge wetu Mwigulu njoo jimboni sisi wapiga kura wako tunakulilia kwani hiyo jeuri uliyopewa na Rais kwamba wewe unakabiliana na wapinzani hukimbilii polisi isikuvimbishe kichwa kiasi unasahau wajibu wako.