Jimbo la Segerea ni mali ya CHADEMA ndani ya UKAWA au nje ya UKAWA

obama sererea

Senior Member
Mar 13, 2012
101
37
Jimbo la Segerea ni moja ya majimbo nane (8) yaliyoko mkoa wa Dar es salaam, ni jimbo jipya lililoanzishwa mwaka 2010 kwa kugawa jimbo la Ukonga, na sasa kuna jimbo la Ukonga na jimbo la Segerea.

Jimbo la Segerea limepata Umaarufu baada ya Uchaguzi wa mwaka 2010 kwa chama cha Chadema kufanya vizuri kwenye uchaguzi huo na kuweza kupata madiwani wawili wakuchaguliwa toka kata ya Segerea na kata ya Kimanga na moja wa viti mwalimu.

Lakini umaarufu zaidi ulipatikana pale ngombea wa nafasi ya Ubunge bw Frey Mpendazoe kuchakachuliwa wazi wazi mchana kweupe.
Matokeo ya kura kwa uchakachuaji huo:-
Ccm walipata kura 43,0000
Chadema kura 39,0000
Cuf kura 18,

Chadema waliendelea kupiga Kazi kubwa na uchaguzi wa mwaka Jana wa serikali za mitaa Chadema walipata mitaa 16 na Cuf mitaa 11 pia chadema walipata uwakirishi wa wajumbe kila kata tofauti na Cuf wao watipata ushindi kata tatu tu nazo ni Buguruni, Vingunguti na Kiwalani pekee.

Kwa matokeo hayo chadema inakila sababu na vigezo vya kuweka mgombea Ubunge Jimbo la Segerea kupitia Ukawa, lakini kwa propaganda inayoendelea sasa ya Cuf kuanza kufikiria kusimamisha kugombe Segerea basi kuna kila sababu Chadema kusimama wenyewe nje ya ukawa na kushinda kwa kishindo.

Wazungu wanamsemo wao "let's agree disagree" tukubaliane kuto kukubaliana.
Hii ndio dawa ya mzizi wa fitna ya hizi propaganda zinazojengwa mpaka na wahariri wa magazeti makubwa hapa nchini eti" Jimbo Segerea waachiwa Cuf"

Nimeamua kuandika hivi kwasababu uongo ukiendelea kusambaa watu wanaweza fikiri ni kweli. Segerea ni Jimbo lenye watu wenye uwezo mkubwa wa kisiasa wasiopenda sifa na kimbelembele cha front page, pia sio kama Chadema haina mgombea wa ubunge Jimbo la Segerea watu wapo ni swala la wakati tu.
 
Jimbo la Segerea ni moja ya majimbo nane (8) yaliyoko mkoa wa Dar es salaam,
Wazungu wanamsemo wao "let's agree disagree" tukubaliane kuto kukubaliana.
Hii ndio dawa ya mzizi wa fitna ya hizi propaganda zinazojengwa mpaka na wahariri wa magazeti makubwa hapa nchini eti" Jimbo Segerea waachiwa Cuf"

Nimeamua kuandika hivi kwasababu uongo ukiendelea kusambaa watu wanaweza fikiri ni kweli. Segerea ni Jimbo lenye watu wenye uwezo mkubwa wa kisiasa wasiopenda sifa na kimbelembele cha front page, pia sio kama Chadema haina mgombea wa ubunge Jimbo la Segerea watu wapo ni swala la wakati tu.

Asante kwa taarifa hii, itasaidia vyombo vingi kupata ukweli wa mambo kwa upande wa uchambuzi wa matokeo ya 2010 na 2014. Kama kuna mwenye takwimu tofauti na hizi za kwako ni vyema akaziweka. Kwa upande mwingine, mpaka sasa mgombea aliyejitangaza ni Mtatiro wa CUF, kwa kuwa umeandika CHADEMA watu wapo wa kugombea Segerea, ina maana unajua kabisa ni wakina nani, hivyo; tutajie baadhi ya majina hata kama hawajatangaza kwenye vyombo vya habari lakini wewe unajua kwa taarifa zako za ndani kwamba wanakusudia kugombea kupitia CHADEMA katika Jimbo hilo.

PM
 
Asante kwa taarifa hii, itasaidia vyombo vingi kupata ukweli wa mambo kwa upande wa uchambuzi wa matokeo ya 2010 na 2014. Kama kuna mwenye takwimu tofauti na hizi za kwako ni vyema akaziweka. Kwa upande mwingine, mpaka sasa mgombea aliyejitangaza ni Mtatiro wa CUF, kwa kuwa umeandika CHADEMA watu wapo wa kugombea Segerea, ina maana unajua kabisa ni wakina nani, hivyo; tutajie baadhi ya majina hata kama hawajatangaza kwenye vyombo vya habari lakini wewe unajua kwa taarifa zako za ndani kwamba wanakusudia kugombea kupitia CHADEMA katika Jimbo hilo.

PM

Sizani Kama ni vema kuwataja kwa sasa ila wapo na ni watu wenye uwezo mkubwa
 
tatizo la ukawa muungano wao unaendeshwa na kuratibiwa na viongozi badala ya kwenda ngazi za chini binafsi nikiangalia historia ya chadema na jimbo la segerea sikuamini kama cuf wanaweza kuweka mgombea kuna hatari ya kugawana kura
 
Jimbo la Segerea ni moja ya majimbo nane (8) yaliyoko mkoa wa Dar es salaam, ni jimbo jipya lililoanzishwa mwaka 2010 kwa kugawa jimbo la Ukonga, na sasa kuna jimbo la Ukonga na jimbo la Segerea.

Jimbo la Segerea limepata Umaarufu baada ya Uchaguzi wa mwaka 2010 kwa chama cha Chadema kufanya vizuri kwenye uchaguzi huo na kuweza kupata madiwani wawili wakuchaguliwa toka kata ya Segerea na kata ya Kimanga na moja wa viti mwalimu.

Lakini umaarufu zaidi ulipatikana pale ngombea wa nafasi ya Ubunge bw Frey Mpendazoe kuchakachuliwa wazi wazi mchana kweupe.
Matokeo ya kura kwa uchakachuaji huo:-
Ccm walipata kura 43,0000
Chadema kura 39,0000
Cuf kura 18,

Chadema waliendelea kupiga Kazi kubwa na uchaguzi wa mwaka Jana wa serikali za mitaa Chadema walipata mitaa 16 na Cuf mitaa 11 pia chadema walipata uwakirishi wa wajumbe kila kata tofauti na Cuf wao watipata ushindi kata tatu tu nazo ni Buguruni, Vingunguti na Kiwalani pekee.

Kwa matokeo hayo chadema inakila sababu na vigezo vya kuweka mgombea Ubunge Jimbo la Segerea kupitia Ukawa, lakini kwa propaganda inayoendelea sasa ya Cuf kuanza kufikiria kusimamisha kugombe Segerea basi kuna kila sababu Chadema kusimama wenyewe nje ya ukawa na kushinda kwa kishindo.

Wazungu wanamsemo wao "let's agree disagree" tukubaliane kuto kukubaliana.
Hii ndio dawa ya mzizi wa fitna ya hizi propaganda zinazojengwa mpaka na wahariri wa magazeti makubwa hapa nchini eti" Jimbo Segerea waachiwa Cuf"

Nimeamua kuandika hivi kwasababu uongo ukiendelea kusambaa watu wanaweza fikiri ni kweli. Segerea ni Jimbo lenye watu wenye uwezo mkubwa wa kisiasa wasiopenda sifa na kimbelembele cha front page, pia sio kama Chadema haina mgombea wa ubunge Jimbo la Segerea watu wapo ni swala la wakati tu.
Mkikubaliana kutokubaliana kutakuwa hakuna makubaliano kwa maana hiyo UKAWA iatakuwa imeparaganyika. Dalili za UKAWA kuwa kama UDETA yetu kwa sababu ya uroho wa vyama ambavyo vyenyewe vinajiona ni vikubwa.
 
Chadema acheni kuleta uroho wenu wa madaraka na kujifanya eti nyie ndiyo mnapendwa sana kuliko wenzenu, kwani huyo Mtatiro ana dosari gani mpaka muanze kumuwekea zengwe? Ukawa ni mjumuiko wa vyama 4 kikiwemo chama chenu hivyo ni wajibu wenu cdm kumpa kura zenu mgombea wa Ukawa, hakuna ulazima wowote was nyie kuweka mgombea.
 
Kusema kweli kwa vigezo vya uimara was chama katika eneo na matokeo yaliyopita inashangaza kidpgo kuambiwa eti cuf wanaweza segerea kuliko chadema ama labda kama tunaweka rekodi chini
 
narudia tena, naanza kupata shida juu ya UKAWA,
Ni vyema dalili za uroho wa madaraka zikaondolewa,
Tukiamua tunaweza kumuondoa shetani SISIEM
 
Cha msingi ni kukaa na kuchambua wagombea yule anayefaa na kukubalika kwa wananchi ndio apitishwe. Haijalishi katoka chama gani kwa sababu kampeni zitamlenga yeye na vyama vyote ndani ya UKAWA vitampa kura.
Msipokubaliana CCM itapeta kwa sababu UKAWA mtagawana kura. Na muwe macho maana kutokubaliana kwenu kutakuwa na mkono wa mtu...ESCROW cash inafanya kazi!
 
Cha msingi ni kukaa na kuchambua wagombea yule anayefaa na kukubalika kwa wananchi ndio apitishwe. Haijalishi katoka chama gani kwa sababu kampeni zitamlenga yeye na vyama vyote ndani ya UKAWA vitampa kura.
Msipokubaliana CCM itapeta kwa sababu UKAWA mtagawana kura. Na muwe macho maana kutokubaliana kwenu kutakuwa na mkono wa mtu...ESCROW cash inafanya kazi!

Hakuna suala la Escrow cash wala nini. Chama kimoja kimejijenga kitaasisi wakati kingine kinatumia 'ukubwa'wa jina la mgombea wao.
Pamoja na nia ya kupata mgombea anayekubalika ni muhimu pia kuzingatia uwepo na uwezo wa chama husika katika jimbo husika.
Vinginevyo hakuna maana yoyote ya wengine kujitoa kujenga chama halafu wengine watunie mwavuli wa UKAWA kujipatia madaraka bila kuvuja jasho.
 
Hakuna suala la Escrow cash wala nini. Chama kimoja kimejijenga kitaasisi wakati kingine kinatumia 'ukubwa'wa jina la mgombea wao.
Pamoja na nia ya kupata mgombea anayekubalika ni muhimu pia kuzingatia uwepo na uwezo wa chama husika katika jimbo husika.
Vinginevyo hakuna maana yoyote ya wengine kujitoa kujenga chama halafu wengine watunie mwavuli wa UKAWA kujipatia madaraka bila kuvuja jasho.

Tata Maranya hakyamama waache mchezo, watu tumeishajipanga, tumeweka mtandao na kujenga chama na kujijenga jimboni harafu vishabani vitoke huko na kutaka jimbo eti kwa tiketi ya UKAWA, hakyamama hatukubali.
 
Hakuna suala la Escrow cash wala nini. Chama kimoja kimejijenga kitaasisi wakati kingine kinatumia 'ukubwa'wa jina la mgombea wao.
Pamoja na nia ya kupata mgombea anayekubalika ni muhimu pia kuzingatia uwepo na uwezo wa chama husika katika jimbo husika.
Vinginevyo hakuna maana yoyote ya wengine kujitoa kujenga chama halafu wengine watunie mwavuli wa UKAWA kujipatia madaraka bila kuvuja jasho.
umeeleweka mkuu, kila chama kitumie nguvu sake kujijenga na si kusubiri kubebwa kwa jasho LA wengine
 
Hakuna suala la Escrow cash wala nini. Chama kimoja kimejijenga kitaasisi wakati kingine kinatumia 'ukubwa'wa jina la mgombea wao.
Pamoja na nia ya kupata mgombea anayekubalika ni muhimu pia kuzingatia uwepo na uwezo wa chama husika katika jimbo husika.
Vinginevyo hakuna maana yoyote ya wengine kujitoa kujenga chama halafu wengine watunie mwavuli wa UKAWA kujipatia madaraka bila kuvuja jasho.
Hapa zinapenyezwa propaganda huku ukeli ukibaki pale pale, ni jinsi gani ya kudelete ccm.
Kwani Mtatiro makazi yake ya kawaida yako wapi ndani ya jiji la Dar es Salaam, ni ndani ya hili jimbo!?

 
Kwani yule wa sisi em HATOGOMBEA?Yule mh anaiba kura na kuchakachua matokeo HAKUNA MF WAKE NDAN YA HII NCHI!
 
Msisitizo na Msimamo uwe kuiondoa CCM madarakani ... Kugawana Majimbo kutafanyika via kura za Maoni za UKAWA!!! Thanks ...
 
Back
Top Bottom