Kilasi Mkuu
JF-Expert Member
- Nov 25, 2013
- 2,325
- 719
CCm ina zidi kupata wakati mgumu majimbo mbalimbali nchini likiwemo hili linalo ongozwa na spika Anne Makinda.viongozi wa ccm wanajaribu kuiokoa hali hiyo lakini bado mambo ni magumu muno!Ikumbukwe ni majuzi tu Katibu mkuu wa ccm mwenyewe alijionea hali hiyo alipo jaribu kwenda kubadili upepo lakini wale wa bena walimkatalia katakata kuhutubiwa.Kwa watu wanao fahamu tabia ya wabena nasikia ni wagumu muno kudanganywa.Kumbuka hata jaribio la kusomba watu watu jimbo la jirani la Deo Sanga kule Lupembe napo ilishindikana baada ya mafuso kukwama kutokana na mvua kubwa iliyo nyesha. Ali sikika mtu mmoja akisema tatizo wa bena wakiona unawadanganya hata ukiwasalimia Kamwene hawakuitikii.Mtu aliye karibu na siasa za Njombe anasema huenda ndiyo sababu Anne Makinda hataki kugombea tena.Aliongeza kusema afadhali kidogo Wahehe wanaweza kupokea hela ingawa nao kura hakupi.Lakini mbena akikukataa hata hela hawataki.Mama Makinda anawajua sana ndiyo maana hataki kurudia akihofu kuaibika