Jimbo la Buhigwe lageuka kitendawili baada ya Dkt. Philip Mpango kuteuliwa kuwa Makamu wa Rais

mwanzo wetu

JF-Expert Member
May 4, 2014
1,581
461
Nianze moja kwa moja kusema kuwa siasa Sasa imegeuka kuwa bidhaa Bora na biashara Bora katika maisha ya viongozi wengi hapa duniani hasa Tanzania Bila kuwaza kuwa watanzania wanahitaji maendeleo kupitia wawakilishi wao ila zaidi kujineemesha pekee.

Kufuatia mh. Mpango kuteuliwa kuwa Makamu wa Rais kikatiba Jimbo lake la Buhigwe lilikuwa wazi toka siku hiyo anateuliwa.

Tume ya Taifa ilitangaza kuanza kufanyiwa mchakato wa upatikanaji wa mbunge mpya.

Na ndani ya Chama Cha mapinduzi ikatolewa ratiba ya kufanyika utaratibu wa kuchukua fomu ndani ya Chama ambapo April 17 na mwisho ikiwa April 19 ambapo ni leo hii na hatua ya uchukuaji fomu inaendelea na ikielezwa kuwa uchaguzi wa kumpata wa kupeperusha kijiti hicho ndani ya Chama ktk uchaguz huo mdogo ni siku ya jumatano ya wiki hii ya Aprill 21 mwaka huu.

Mpaka Sasa wanaotajwa kuchukua fomu ktk uchaguz huo huenda wakafika 40 ambapo mpaka Sasa wameshachukua fomu watu 27 Jambo ambalo unaweza kuona siasa jinsi ilivyo ktk kusaka mkate kupitia siasa nje na lengo la kuwatumikia wananchi, hatukatai ndio Demokrasia ila siyo kwa mtindo huo.

Mpaka Sasa ni nikupigana vibega wao kwa wao wengine wakiungana kumkabili mtu mmoja pengine mwenyenguvu ingawa wengi wamekuwa wakiona mwenye Nguvu na mwenye uwezo wa kumrithi mh. Mpango huenda akawa Injinia Aron Sisiye Zabron kutokana yeye kuwa na Nguvu katika ukanda wa Buhigwe maana inasadikiwa Jimbo hilo kuwa na tatizo la ukwetu yaani ukanda ambapo ukandanda wa manyovu wametoka wengi hivyo kugawana kura na kuangukia patupu ukilinganisha na waliochukua fomu kutwaa kugombania nafasi hiyo kwa ukanda wa Buhigwe yaani ule ukanda wa mh. Mpango anakotoka.

Ukanda wa Manyovu mpaka Sasa wamefika 23 huku ukanda ule wa Buhigwe anakotoka mh. Mpango wakiwa wa nne tu ambapo ametajwa mwenye nguvu kuwa ni Aron Zabron.

Utitiri wa Wagombea wengi hii inaleta zaidi picha kuwa siasa imekuwa kitu cha kuwa weka wengi mjini kuliko Jambo lolote maana wengi wamekuwa wakiacha kazi nzuri tu na kukimbilia upande huu wa siasa.

Nawasilisha kwenu wadau pengine huenda mkawa na mtazamo zaidi juu ya kuwepo kwa utitiri mkubwa wa Wagombea.
 
Nani asiependa kazi ya kudemka bungeni halafu mwisho wa mwezi 12milion inasoma.
Halafu sasa wa la Saba ndio wanapewa udokta huko Bungeni unategemea nini tena na Spika mwenyewe.
 
Kud
Nani asiependa kazi ya kudemka bungeni halafu mwisho wa mwezi 12milion inasoma.

Halafu sasa wa la Saba ndio wanapewa udokta huko Bungeni unategemea nini tena na Spika mwenyewe.
Kuna haja mama Samia kutembea na mkalimani wa kutafusilia sisi watu wa bara kiswahili Cha pwani atuelewi maana tunapiga makofi sehemu ya kusikitika , Mimi kudemka ndio naisikia😊
 
Zitto Kabwe naye anakuja!
Nasikia hivo ila aache tu asijidhalilishe coz lazima achapwe maana naona mpaka Sasa ameandaa propaganda kubwa Sana mm inapota inamuseva zito , Kama ka Gingle Furani hivi , Jimbo la Buhigwe Ni la CCM kwa garama yoyote na wananchi wanaitaka ccm tu maana wameanza kuonja matunda kutoka kwa mpango yaan hawaambiwi lolote wao ni CCM tu.
 
Nasikia hivo ila aache tu asijidhalilishe coz lazima achapwe maana naona mpaka Sasa ameandaa propaganda kubwa Sana mm inapota inamuseva zito , Kama ka Gingle Furani hivi , Jimbo la Buhigwe Ni la ccm kwa garama yoyote na wananchi wanaitaka ccm tu maana wameanza kuonja matunda kutoka kwa mpango yaan hawaambiwi lolote wao ni ccm tu.
CCM wakimpitisha mtu wa Ukanda wa humo kwa Mpango na Zitto akatia nia, Zitto anashinda saa 4 asubuhi. Huo Ukanda population yake ni ndogo. Ukanda wa Manyovu ndio una watu wengi na miaka yote ndo unaoamua Nani awe Mbunge. Dr. Mpango kilichombeba hata kwenye kura za maoni ni nafasi aliyokuwepo na hali halisi ya saisa za 2020. CCM wakitaka Jimbo libaki wahakikishe mgombea anatoka Ukanda wa Manyovu. Ushauri wa bure Kabisa huu.
 
Naona umeamua kumtaja jamaa aliyekutuma umpigie kampeni huyo injinia maana hata mantiki ya hii thread siioni kabisa.
 
Mi nashauri serikali iangalie swala hili kwa upya, kwani ni kweli kabisa asilimia 99.99% ya wanao wania nafasi hizi za kisiasa kama za ubunge n.k, ni kwaajili ya kujinufaisha na kutuliza njaa za matumbo yao na familia zao, na sio kutumikia wananchi.

Inabidi serikali ipitishe utaratibu wa kukagua mali na kipato cha wagombeaji wa nafasi za kisiasa, walau kwa kila mgombea awe na mali isiyo hamishika yenye thamani ya kuanzia billion 1.5 mpaka 2 na kipato kisichopungua million 250 hadi 350 million kwa mwaka, kwani hii itasaidia kuweka watu walioshiba na kujitosheleza wasio na njaa wala tamaa na itasaidia kupunguza ufisadi, uporaji na wizi wa mali za umma.

Mara nyingi hii hufanywa zaidi na nchi zinazojielewa na ndo maana ziliendelea na zinazidi kuendelea mfano wa nchi hizo au mataifa hayo ni USA, China na Russia.
 
Nianze moja kwa moja kusema kuwa siasa Sasa imegeuka kuwa bidhaa Bora na biashara Bora katika maisha ya viongozi wengi hapa duniani hasa Tanzania Bila kuwaza kuwa watanzania wanahitaji maendeleo kupitia wawakilishi wao ila zaidi kujineemesha pekee.

Kufuatia mh. Mpango kuteuliwa kuwa Makamu wa Rais kikatiba Jimbo lake la Buhigwe lilikuwa wazi toka siku hiyo anateuliwa.
Tume ya Taifa ilitangaza kuanza kufanyiwa mchakato wa upatikanaji wa mbunge mpya.

Na ndani ya Chama Cha mapinduzi ikatolewa ratiba ya kufanyika utaratibu wa kuchukua fomu ndani ya Chama ambapo April 17 na mwisho ikiwa April 19 ambapo ni leo hii na hatua ya uchukuaji fomu inaendelea na ikielezwa kuwa uchaguzi wa kumpata wa kupeperusha kijiti hicho ndani ya Chama ktk uchaguz huo mdogo ni siku ya jumatano ya wiki hii ya Aprill 21 mwaka huu.

Mpaka Sasa wanaotajwa kuchukua fomu ktk uchaguz huo huenda wakafika 40 ambapo mpaka Sasa wameshachukua fomu watu 27 Jambo ambalo unaweza kuona siasa jinsi ilivyo ktk kusaka mkate kupitia siasa nje na lengo la kuwatumikia wananchi, hatukatai ndio Demokrasia ila siyo kwa mtindo huo.

Mpaka Sasa ni nikupigana vibega wao kwa wao wengine wakiungana kumkabili mtu mmoja pengine mwenyenguvu ingawa wengi wamekuwa wakiona mwenye Nguvu na mwenye uwezo wa kumrithi mh. Mpango huenda akawa Injinia Aron Sisiye Zabron kutokana yeye kuwa na Nguvu katika ukanda wa Buhigwe maana inasadikiwa Jimbo hilo kuwa na tatizo la ukwetu yaani ukanda ambapo ukandanda wa manyovu wametoka wengi hivyo kugawana kura na kuangukia patupu ukilinganisha na waliochukua fomu kutwaa kugombania nafasi hiyo kwa ukanda wa Buhigwe yaani ule ukanda wa mh. Mpango anakotoka.

Ukanda wa Manyovu mpaka Sasa wamefika 23 huku ukanda ule wa Buhigwe anakotoka mh. Mpango wakiwa wa nne tu ambapo ametajwa mwenye nguvu kuwa ni Aron Zabron.

Utitiri wa Wagombea wengi hii inaleta zaidi picha kuwa siasa imekuwa kitu cha kuwa weka wengi mjini kuliko Jambo lolote maana wengi wamekuwa wakiacha kazi nzuri tu na kukimbilia upande huu wa siasa.

Nawasilisha kwenu wadau pengine huenda mkawa na mtazamo zaidi juu ya kuwepo kwa utitiri mkubwa wa Wagombea.
Wasiuane tu
 
mi nashauri serikali iangalie swala hili kwa upya, kwani ni kweli kabisa asilimia 99.99% ya wanao wania nafasi hizi za kisiasa kama za ubunge n.k, ni kwaajili ya kujinufaisha na kutuliza njaa za matumbo yao na familia zao, na sio kutumikia wananchi.

Inabidi serikali ipitishe utaratibu wa kukagua mali na kipato cha wagombeaji wa nafasi za kisiasa, walau kwa kila mgombea awe na mali isiyo hamishika yenye thamani ya kuanzia billion 1.5 mpaka 2 na kipato kisichopungua million 250 hadi 350 million kwa mwaka, kwani hii itasaidia kuweka watu walioshiba na kujitosheleza wasio na njaa wala tamaa na itasaidia kupunguza ufisadi, uporaji na wizi wa mali za umma.

Mara nyingi hii hufanywa zaidi na nchi zinazojielewa na ndo maana ziliendelea na zinazidi kuendelea mfano wa nchi hizo au mataifa hayo ni USA, China na Russia.
Mpaka iwepo sheria inayobana kuchukuliwa hatua wadanganyifu wa maadili hayo, bila hivyo ni kazi bure.

Mbona wengi tu wanaingia huko kisha wanatangaza kwenye tume ya maadili mali chache lakini hakuna ufuatiliaji wa ziada na hatua stahiki kuchukuliwa? Je, kuna kumbukumbu zozote ambazo kuna mtumishi wa umma ambaye alishawahi kuenguliwa kwa sababu za kudanganya taarifa za kutangaza mali na madeni? Kama hakuna unataka muujiza gani utatokea kutokana na unavyopendekza?
 
Nianze moja kwa moja kusema kuwa siasa Sasa imegeuka kuwa bidhaa Bora na biashara Bora katika maisha ya viongozi wengi hapa duniani hasa Tanzania Bila kuwaza kuwa watanzania wanahitaji maendeleo kupitia wawakilishi wao ila zaidi kujineemesha pekee.

Kufuatia mh. Mpango kuteuliwa kuwa Makamu wa Rais kikatiba Jimbo lake la Buhigwe lilikuwa wazi toka siku hiyo anateuliwa.

Tume ya Taifa ilitangaza kuanza kufanyiwa mchakato wa upatikanaji wa mbunge mpya.

Na ndani ya Chama Cha mapinduzi ikatolewa ratiba ya kufanyika utaratibu wa kuchukua fomu ndani ya Chama ambapo April 17 na mwisho ikiwa April 19 ambapo ni leo hii na hatua ya uchukuaji fomu inaendelea na ikielezwa kuwa uchaguzi wa kumpata wa kupeperusha kijiti hicho ndani ya Chama ktk uchaguz huo mdogo ni siku ya jumatano ya wiki hii ya Aprill 21 mwaka huu.

Mpaka Sasa wanaotajwa kuchukua fomu ktk uchaguz huo huenda wakafika 40 ambapo mpaka Sasa wameshachukua fomu watu 27 Jambo ambalo unaweza kuona siasa jinsi ilivyo ktk kusaka mkate kupitia siasa nje na lengo la kuwatumikia wananchi, hatukatai ndio Demokrasia ila siyo kwa mtindo huo.

Mpaka Sasa ni nikupigana vibega wao kwa wao wengine wakiungana kumkabili mtu mmoja pengine mwenyenguvu ingawa wengi wamekuwa wakiona mwenye Nguvu na mwenye uwezo wa kumrithi mh. Mpango huenda akawa Injinia Aron Sisiye Zabron kutokana yeye kuwa na Nguvu katika ukanda wa Buhigwe maana inasadikiwa Jimbo hilo kuwa na tatizo la ukwetu yaani ukanda ambapo ukandanda wa manyovu wametoka wengi hivyo kugawana kura na kuangukia patupu ukilinganisha na waliochukua fomu kutwaa kugombania nafasi hiyo kwa ukanda wa Buhigwe yaani ule ukanda wa mh. Mpango anakotoka.

Ukanda wa Manyovu mpaka Sasa wamefika 23 huku ukanda ule wa Buhigwe anakotoka mh. Mpango wakiwa wa nne tu ambapo ametajwa mwenye nguvu kuwa ni Aron Zabron.

Utitiri wa Wagombea wengi hii inaleta zaidi picha kuwa siasa imekuwa kitu cha kuwa weka wengi mjini kuliko Jambo lolote maana wengi wamekuwa wakiacha kazi nzuri tu na kukimbilia upande huu wa siasa.

Nawasilisha kwenu wadau pengine huenda mkawa na mtazamo zaidi juu ya kuwepo kwa utitiri mkubwa wa Wagombea.
Ndani ya ccm hata uwe darasa la nne C unachukua jimbo.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom