Jimbo Jipya Katoliki La Kayanga laundwa

Kamakabuzi

JF-Expert Member
Dec 3, 2007
2,853
1,296
Leo saa saba mchana Baba Mtakatifu Benedict wa 16 ametangaza kuanzishwa kwa Jimbo jipya nalo ni Jimbo Katoliki la Kayanga.
Jimbo hilo limemegwa kutoka jimbo la Rulenge na litachukua eneo zima la Wilaya ya Karagwe yenye dekania za Karagwe na Kyerwa.
Pia baba Mtakatifu amemteua Padre Almichius Rwechungura kuwa Askofu wa Jimbo hilo. Kabla ya uteuzi huo, alikuwa makamu wa askofu wa Jimbo la Bukoba.
Askofu wa sasa wa Jimbo la Rulenge amewatangazia rasmi habari hiyo waumini wa Parokia ya Kayanga itakayokuwa makao makuu ya JImo hilo.
Jimbo la zamani la Rulenge linahamisha makao makuu kwenda Ngara mjini na kuitwa Jimbo la Rulenge- Ngara.
WOTE HONGERENI NA MUWE TAYARI KUTIMIZA YOTE TANAYOEDANA NA TUKIO HILI
TUMSIFU YESU KRISTU.
 
Last edited by a moderator:
Habari Hii Ni Sawa Na Rostam Alivyoamua Kwenda Kanisani Kuzindua Album

Si sahihi kabisa kulinganisha habari hizi mbili. Ya Rostam alikwenda kwa nia ya kutumia kanisa kujisafisha wakati hili ni tangazo la uanzishwaji wa jimbo jipya na uteuzi wa Askofu mpya.
Halina uhusiano wowote na ufisadi.
Anyway asante kwa mchango wako kwani kila mtu ana namna yake ya kufikiri.
 
Mi naomba mtu anisaidie na maelezo zaidi kwanini Vigango na kwanini "vigango" vimekuja kwa kasi sana huku mitaa ya waKatoliki. Kuna vi-eligibility vya ku-maintain Catholism ambavyo vimeanza kuleta mgongano na ratiba zangu za maisha. (Hasa mtu kama mimi ambaye sina Kigango)

What's up with that?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom