Jikoki na tigo-hyundai za voda mchanga wa macho watanzania-watchout

Ivi na yule mwakilishi wa bahati nasibu yuko pale kufanya nini? ana uelewa gani wa maswala ya computer au software inayotumika?
Ivi namber haiwezi kuwa set kabla wakuu?
Ivi wakifika studio na kuambiwa muda ukifika, we bonyeza hapa, wanauwezo wa kukataa?? Wanashiriki vipi kutengeneza software au wao ndo wanaziuza??????
Mbona huwa wanaoneka hawajiamnini na ni mbumbumbu kwenye IT issues?

Wako kama geresha flani ivi, siwaone wakiichezea kwanza computer!!
 
Hiyo ni gambling kama zilivyo gambling zingine zozote. Ukitaka kupata hivyo vitu vifanyie kazi, ila hii tabia ya watanzania ya kupenda vitu vya bure ndiyo inayowa-cost watu. Eti unakuta wanakutumia swali: kifupi cha chama cha mapinduzi ni A.ccm B. pondolo C. mwanza............sasa unajiuliza hivi kuna mtu wa kukosa hili swali kweli.........kaaaaaazi. Wajinga ndio wamegwao na itabaki kuwa hivyo forever and ever.
 
Mimi Nishishaandika mada ya hizi promosheni za simu na jinsi zinavowatapeli watu .....sasa safari hii nitaandika kila kona product ambayo naamini itazi-twist kampuni za simu zisi-rely sana kwenye promosheni ...especially inapotokea Revenue imeyumba
 
Its better hizo hela wanazonunulia zawadi watoe msaada kwa watu wasiojiweza au kwa watoto yatima...au wafanye kitu ambacho kitakuwa na faida kwa wananchi wengi eg: kujenga hospitali,kununua madawati kwa ajili ya mashule mbalimbali au kununua vitabu vya kwenye mashule nk....wasitupige changa la macho na bahati nasibu zao...
 
Kuna jamaa yangu alishinda droo ya kampuni moja kubwa hapa Dar kwenda South Africa kuangalia baadhi ya mechi za kombe la dunia, lakini ukweli ilikuwa dili na alichangia kiasi cha fedha kwenda huko.
 
Hiyo ni gambling kama zilivyo gambling zingine zozote. Ukitaka kupata hivyo vitu vifanyie kazi, ila hii tabia ya watanzania ya kupenda vitu vya bure ndiyo inayowa-cost watu. Eti unakuta wanakutumia swali: kifupi cha chama cha mapinduzi ni A.ccm B. pondolo C. mwanza............sasa unajiuliza hivi kuna mtu wa kukosa hili swali kweli.........kaaaaaazi. Wajinga ndio wamegwao na itabaki kuwa hivyo forever and ever.


Au hukujua kuwa na wewe umejitukana?? Umejuaje hilo swali?
 
Jamaa katoa Tshs.160,000/- na aliyeshinda katoa Tshs.32,000/=sasa huo si wizi wa kimachomacho?
 
Hizi sio promosheni kama wanavyopenda kuziita! Kimsingi hizi bahati nasibu wanadanganya ni promoshen....its simple wengi wanawachangia wachache zawadi!
 
Bora hata Voda wanatoa magari hayo tunaona watu wanapata. Tigo wanadai wanatoa milioni 2 na simu kila siku, milioni tano kila wiki lakini hata mara moja hakuna ushahidi kama kweli maneno hayo. Mbona ya kujisajili walikuwa wanaonyesha? Kujikoki nadhani kweli ni wizi. Nilienda nao kujikoki nikashituka dili lao nikaachana nao, lakini ni baada ya kuliwa pesa nyingi sana. Kuna usiri usio wa kawaida katika michezo yao. Voda kla siku wanaonyesha, ukikosa ni bhati isiyo yako. Kujikoki wanafika wakati wanadai unaongoza kwa mbali sana endelea kujikoki, ukiwa unajiweka sawa wanaanza kupunguza points kwa kila 360 wanayokukata, ghafla wanakuambia usijiamini kuna watu wamegundua mbinu zako wanakusogelea. Kisha wananyamaza au wanakuambia usijali ukikosa leo utapata kesho.

Ujinga wetu ndio unaotutafuna. Labda umasikini wetu ndio chanzo cha mahangaiko yote haya. Mnagombania gri moja la milioni 100 kwa miezi zaidi ya mitatu na kama ukipiga hesabu ya makisio ya haraka haraka unakuta wanakusanya faida kubwa mno! Tigo sio rahisi, ni wajanja zaidi wakiegemea kwa walalahoi wanaodanganyika kirahisi.

Yawezekana kuna watu wanapata, lakini kama milioni 2 zinatoka kila siku kwa mtanzania yeyote kwelikweli inaweza kuinua walio wengi sana. Usiri wa zoezi zima una utata. Ina maana mtu anaweza kupata milioni 2 kila siku kwa kijirudiarudia, maana kama umepata ya kwanza si unawekeza kwa mchezo huo tu kiwango kikubwa? asiyewahi kupata ataweza vipi kushindana katika hali hiyo? Twaongopeana, ni DECI nyingine hiyo.
 
.

Ujinga wetu ndio unaotutafuna.

Pole baba kumbe mimi na wewe tunatafunwa kupitia sms na kupiga simu! Duh tutaponaje?

Labda umasikini wetu ndio chanzo cha mahangaiko yote haya.

Ndo maana tunashindana sana kuonesha urefu wa status zetu kupitia mishahara!

Mnagombania gri moja la milioni 100 kwa miezi zaidi ya mitatu na kama ukipiga hesabu ya makisio ya haraka haraka unakuta wanakusanya faida kubwa mno!

Inauma sana!!

Tigo sio rahisi, ni wajanja zaidi wakiegemea kwa walalahoi wanaodanganyika kirahisi.

Tutazidi kuliwa tu maana hatujui namna ya kujikinga nayo!!

Yawezekana kuna watu wanapata,

Ndo maana mishahara ya huko ni balaa!!!

lakini kama milioni 2 zinatoka kila siku kwa mtanzania yeyote kwelikweli inaweza kuinua walio wengi sana. Usiri wa zoezi zima una utata. Ina maana mtu anaweza kupata milioni 2 kila siku kwa kijirudiarudia, maana kama umepata ya kwanza si unawekeza kwa mchezo huo tu kiwango kikubwa? asiyewahi kupata ataweza vipi kushindana katika hali hiyo? Twaongopeana, ni DECI nyingine hiyo.

Kweli kabisa!!
 
Magavila wa Zain anatuletea "TEJA" Eti Baba yake kashinda! "TEJA" adai Baba yangu ni dereva wa gari yupo Burundi LOL!! Kisha "TEJA" anaenda na mtoto.mdogo ili kuweka imani kwa wanawake washiriki... Duuh! Maskini hvi wanaohusika na haki za watoto wako wapi??? ..
 
Haya yote tunajitakia wenyewe, hivi unategemea hizo Hyundai zinanunuliwa na nini kama sio pesa hiyo ya promosheni!
In fact siyo tu wananunulia na hiyo pesa ya promosheni, bali pia wanapata faida big tyme katika kila siku. My understanding ni kwamba hiyo ni biashara kama zilivyo biashara nyingine za gambling... jamaa wanakusanya tuseme milioni 50 kwa siku then wanatoa gari lenye thamani ya sh milioni 10 faida milioni 40. sasa kwa kuwa mtu hulazimishwi kushiriki, sidhani kama ni busara kulalamika. Ila for heaven's sake watu wapewe chance ya kushinda basi!!! maana nina wasiwasi watu wananunua ushindi.----kale kaprogram wanachotumia inawezekana kabisa ku-determine namba unayotaka ishinde kabla ya kubofya kitufe cha kompyuta.... siyo mtaalam wa IT kwa saana lakini najua inawezekana. Tafakari chukua hatua.....
 
Jamani mbona ni vita tu na makampuni ya simu tuuuuuuuuuu, mbona Coke na Pepsi wakifanya bahati nasibu zao hamsemi?
 
Makosa ni ya kwetu Watanzania,tunapenda rahisi kupita kiasi.Kama ilivyo kwenye utapeli mtu anayependa rahisi ndiye anayeingia mkenge haraka.
Angalieni bei ya used microwave na brand new,tofauti ni ndogo lakini watu wanakimbilia used.
 
jamaa wanakusanya tuseme milioni 50 kwa siku then wanatoa gari lenye thamani ya sh milioni 10 faida milioni 40. sasa kwa kuwa mtu hulazimishwi kushiriki, sidhani kama ni busara kulalamika. Ila for heaven's sake watu wapewe chance ya kushinda basi!!! maana nina wasiwasi watu wananunua ushindi.----kale kaprogram wanachotumia inawezekana kabisa ku-determine namba unayotaka ishinde kabla ya kubofya kitufe cha kompyuta.... siyo mtaalam wa IT kwa saana lakini najua inawezekana. Tafakari chukua hatua.....
Goma Kushiriki ndo suluhisho...kwa ufupi makampuni ya simu yanafaida kubwa sanaa especially hawa Vodacom..
 
Ndo maana ya ubepari, ubepari ni mfumo unaotegemea sana
ubinafsi
tamaa
kujilimbikizia
kufanya kazi kidogo faida kubwa
kutokujali wenzio hata kama ni masikini
kuonea
kukapitalise kwenye ujinga wa wenzio
nk
nk
Angalia biashara yoyote inayothrive kwenye ubepari, lazima owner awe na tamaa kubwa ya mali, otherwise ataishia tu kusurvive na mwishowe atakufa kwa presha.
huwa inaitwa:
aggreessiveness
ambition
focus
nk
nk
Hakuna cha Voda, Tigo, Zain wala TTCL, Zantel si tanzania wala UK au Italy, wote ni hao hao tu!!
 
Ole wao wenye PUPA hawata uridhi uzima wa milele. Pupa maana yake ni tamaa ya kuwa tajiri kiurahisi kama kucheza kamari na michezo ya bahati na sibu. Kuelewa hili unahitaji uwe deep katika vitabu vya Mungu.
 
ndio sababu lazima wacheki umri wako, lazima uwe zaidi ya miaka 18.
Usiweze kuwashtaki kwa kukudanganya!!!
 
Back
Top Bottom