Jiji la Mwanza wagomea sensa, Makarani hawana sare wala vitambulisho!

Kieleweke

Member
Jun 23, 2009
79
8
Udhaifu wa zoezi la sensa jijini Mwanza umeingia hatua nyingine tofauti na ya jana ya kuchelewesha malipo ya makarani wa sensa iliyowekwa hapa.

Udhaifu huo wa jana haukuishia kufanya makarani wachelewe kupatiwa posho yao ya kuanzia kufanya sensa, lakini pia hawakupewa sare yaani utambulisho utakaowarahisishia kujulikana na kupokelewa majumbani.

Matokeo yake ni kwamba, makarani wameenda nyumba hadi nyumba huku hawana sare na hivyo kufanywa wafukuzwe na baadhi kudhaniwa vibaka, majambazi au machangudoa. Hivyo, si tu kwamba wamekataliwa sehemu nyingi bali pia wamefukuzwa kwa vitisho kadhaa kwa kuelezwa wazi kwamba kuingia eneo la mtu bila kitambulisho au sare ukjifanya wewe ni karani wa sensa.

Hivyo, inaweza kutoka picha kwamba Mwanza wamegoma kuhesabiwa lakini ukweli ni kwamba maafisa wengi hawana sare kama ilivyo kwa mikoa mingine na kwa hili wananchi wa Mwanza wana haki ya kulinda miji yao isivamiwe na mtu asiyejulikana kwa kisingizio cha kuwa karani wa sensa.
 
Hii nchi ni ya sanaa na wasanii...Hawa maafisa wa Takwimu walianza kuzitumbua hizi fedha kuanzia 2010 kwa kuzunguka nchi nzima ...Wamezunguka si chini ya siku 500 kwa kanda tofauti piga hesabu hizo padiemu na mafuta sijui inaitwaje ikizidi siku 30. Leo hii hakuna fedha za vifaa na za kuwalipa makarani posho.Hii ni fedhea kwa kweli.
 
...idadi yao itabaki ile ile kama ya sensa iliyofanyika mwaka 2002....au hii Serikali ya kisanii itacheza na namba na kisha kuanika uongo wake hadharani.
 
Hivi kwenye dodoso hakuna sehemu ya kuuliza kama mtu ana akili timamu?

Unaweza kukuta tupo 46m lakini mwezi mchanga ni 28m. Na maana ccm inachaguliwa kila uchwao.
 
sare zitakuja next month, ziliagzwa kutoka ughaibuni.

Kumbuka sare za mei mosi zilikuja july
 
Mleta uzi ni muongo! Hivi watanzania tumelogwa kupenda uzushi? Leo nimeshinda eneo la Igombe jijini Mwanza, asubuhi mvua imenyesha kidogo lakini pamoja na mvua kunyesha makarani wa sensa wameamka mapema kweli! Nilipanda basi la kwenda Igombe saa moja kamili na ndani niliwaona makarani kama sita hivi(nimewatambua kwasababu wengi ni watumishi wenzangu wa jiji). Ili kuepuka kuchafua sare zao wengi walikuwa wamezitunza kwenye mikoba yao. Saa saba mchana nilikutana na mwalimu mmoja aliyekuwa na sare kamili na kibebeo cha madodoso.

Kwa wasiofahamu Igombe ni eneo la pembezoni sana mwa jiji(kupita uwanja wa ndege kama km 8 hivi).
My take: kama makarani wa Igombe ,Sangabuye, nk wamepata sare iweje wa katikati ya mji?
 
Mleta uzi ni muongo! Hivi watanzania tumelogwa kupenda uzushi? Leo nimeshinda eneo la Igombe jijini Mwanza, asubuhi mvua imenyesha kidogo lakini pamoja na mvua kunyesha makarani wa sensa wameamka mapema kweli! Nilipanda basi la kwenda Igombe saa moja kamili na ndani niliwaona makarani kama sita hivi(nimewatambua kwasababu wengi ni watumishi wenzangu wa jiji). Ili kuepuka kuchafua sare zao wengi walikuwa wamezitunza kwenye mikoba yao. Saa saba mchana nilikutana na mwalimu mmoja aliyekuwa na sare kamili na kibebeo cha madodoso.

Kwa wasiofahamu Igombe ni eneo la pembezoni sana mwa jiji(kupita uwanja wa ndege kama km 8 hivi).
My take: kama makarani wa Igombe ,Sangabuye, nk wamepata sare iweje wa katikati ya mji?
acha uzushi wewe mimi ninaishi kwenye hii milima ya kwenye mawe hapa mabatini sijamwona mtu wa sensa
 
Ni rahisi kugawa sare za kijani na kofia zake nchi nzima kuliko kugawa sare za sensa. Unaona umakini walionao watu wa Kijani??????
 
acha uzushi wewe mimi ninaishi kwenye hii milima ya kwenye mawe hapa mabatini sijamwona mtu wa sensa

Umepunguza munkari wangu wa kumjibu huyo jamaa. Nilitaka kumuuliza kama hao sita aliowaona ndiyo idadi ya makarani wa Mwanza nzima.
 
sare zitakuja next month, ziliagzwa kutoka ughaibuni.

Kumbuka sare za mei mosi zilikuja july

Sare .....vitambulisho,...na baadhi ya vifaa maafisa wa ofisi iliyoratibuu ununuziii Huu ndani ya ofisi ya Rais ....wamepeana tenda,....wanataka kuuza hewa.....kila karani anastahili yafuatayoooo..

Kofia
fulana
koti
bag
kalamu
Posho...

Kila Kifaa hapo Huu zinatakiwa Jozi...150,000......Taarifa ni kuwa Jozi zilizoletwa hazifiki hata 50'000 .....na zilizobaki....wanamgoja watu wasahau....walipe...hewa...hii Taarifa tumeshampa onyooo...CaG..,PPRA..,BUnge..TISs....na wabunge wanasubiri BUnge la November wale leek Hoja juu ya malpractice kwenye ununuzi wa vifaa vya sensa......tunatambua kuna ambao itabidi kusubiri watoke madarakani...ili nao waunganishwee kwenye kesi ya matumizi mabaya ya billions 120 za sensa ...maana watu ni walafii na hawatosheki...
 
Mleta uzi ni muongo! Hivi watanzania tumelogwa kupenda uzushi? Leo nimeshinda eneo la Igombe jijini Mwanza, asubuhi mvua imenyesha kidogo lakini pamoja na mvua kunyesha makarani wa sensa wameamka mapema kweli! Nilipanda basi la kwenda Igombe saa moja kamili na ndani niliwaona makarani kama sita hivi(nimewatambua kwasababu wengi ni watumishi wenzangu wa jiji). Ili kuepuka kuchafua sare zao wengi walikuwa wamezitunza kwenye mikoba yao. Saa saba mchana nilikutana na mwalimu mmoja aliyekuwa na sare kamili na kibebeo cha madodoso.

Kwa wasiofahamu Igombe ni eneo la pembezoni sana mwa jiji(kupita uwanja wa ndege kama km 8 hivi).
My take: kama makarani wa Igombe ,Sangabuye, nk wamepata sare iweje wa katikati ya mji?
Unachobisha nn wewe? hapo ni Mza uliza Kigoma kama wamepata hata hilo begi,lazma mkubali kukosole
 
Back
Top Bottom