kitunguu saumu
New Member
- Apr 23, 2020
- 4
- 8
JJIWE HILI JIWE GANI HAPA KWETU KIJIJINI?
Kwenye mwanga waliona, kwenye giza hulioni,
Waliokwisha liliona, wakatoa zao warn,
Wa kijiji wakagoma, wakaziba zao mboni,
Jiwe hili Jiwe gani, hapa kwetu kijijini?
Wale waliolileta, nao sasa wanajuta,
Linawapiga mieleka, na viuno kuvunjika,
Wasotaka fedheheka, wanalipaka mafuta,
Jiwe hili Jiwe gani, hapa kwetu kijijini?
Waandishi wa habari, wajua madhara yake,
Kulipamba ni hiari, na picha zake uweke,
Kutofanya ni kiburi, akili kando uweke,
Jiwe hili Jiwe gani, hapa kwetu kijijini?
Tukatoboa na tundu, ila nalo likazibwa,
Gwanda, bendera,vifungu, saa nane vikaibwa,
Pakajawa na ukungu, kuliona kawa shida
Jiwe hili Jiwe gani, hapa kwetu kijijini?
Upande wa mashariki, linapo tokea jua,
Hua hauathiriki,hata inyeshe mvua,
Eti hakuna riziki, mbolea imekwangua,
Jiwe hili Jiwe gani, hapa kwetu kijijini?
Wakazi kwenye kijiji, nao wamegawanyika,
Wasemao hawashibi,jiwe shamba lafunika,
Na wenginewaahidi, nguo zao waanika
Jiwe hili Jiwe gani, hapa kwetu kijijini?
Lilipachokwa kwa chuma, halikupaswa liwepo,
Wengi walolisukuma, wana enjoy upepo,
Waloachaga huruma, upande wao si heko.
Jiwe hili Jiwe gani, hapa kwetu kijijini?
Jiwe hili ni kimondo, jiwe hili ni dhahabu?
Jiwe hili lina mambo, jiwe hili kama dubu,
Lapaswa liwekwe kando, watu wasilihusudu,
Jiwe hili Jiwe gani, hapa kwetu kijijini?
Ona najihatarisha,nataja mambo ya jiwe,
Hili jiwe linatisha, hupenda sifa lipewe,
Mabayake nakanusha, kwa jiwe vigelegele
Ali li li li li li li li li li li li li li li li li li
Jiwe jiwe jiwe jiwe jiwe jiwe jiwe jiwe.
Kwenye mwanga waliona, kwenye giza hulioni,
Waliokwisha liliona, wakatoa zao warn,
Wa kijiji wakagoma, wakaziba zao mboni,
Jiwe hili Jiwe gani, hapa kwetu kijijini?
Wale waliolileta, nao sasa wanajuta,
Linawapiga mieleka, na viuno kuvunjika,
Wasotaka fedheheka, wanalipaka mafuta,
Jiwe hili Jiwe gani, hapa kwetu kijijini?
Waandishi wa habari, wajua madhara yake,
Kulipamba ni hiari, na picha zake uweke,
Kutofanya ni kiburi, akili kando uweke,
Jiwe hili Jiwe gani, hapa kwetu kijijini?
Tukatoboa na tundu, ila nalo likazibwa,
Gwanda, bendera,vifungu, saa nane vikaibwa,
Pakajawa na ukungu, kuliona kawa shida
Jiwe hili Jiwe gani, hapa kwetu kijijini?
Upande wa mashariki, linapo tokea jua,
Hua hauathiriki,hata inyeshe mvua,
Eti hakuna riziki, mbolea imekwangua,
Jiwe hili Jiwe gani, hapa kwetu kijijini?
Wakazi kwenye kijiji, nao wamegawanyika,
Wasemao hawashibi,jiwe shamba lafunika,
Na wenginewaahidi, nguo zao waanika
Jiwe hili Jiwe gani, hapa kwetu kijijini?
Lilipachokwa kwa chuma, halikupaswa liwepo,
Wengi walolisukuma, wana enjoy upepo,
Waloachaga huruma, upande wao si heko.
Jiwe hili Jiwe gani, hapa kwetu kijijini?
Jiwe hili ni kimondo, jiwe hili ni dhahabu?
Jiwe hili lina mambo, jiwe hili kama dubu,
Lapaswa liwekwe kando, watu wasilihusudu,
Jiwe hili Jiwe gani, hapa kwetu kijijini?
Ona najihatarisha,nataja mambo ya jiwe,
Hili jiwe linatisha, hupenda sifa lipewe,
Mabayake nakanusha, kwa jiwe vigelegele
Ali li li li li li li li li li li li li li li li li li
Jiwe jiwe jiwe jiwe jiwe jiwe jiwe jiwe.