Hivi juzi kati nimefanikiwa kuuza banda langu ambalo nimetangaza sana hapa JF.
Nilichogundua wanunuzi wana nia ya kutapeli pia sawa sawa na wauzaji wengine. Mnunuzi alikuja yuko full na mwanasheria na dalali mwenye ofisi yake posta huko sio hawa wa mitaani. Baada ya kuelewana mipaka na kila kitu tukaenda benk moja mjini
Kwanza tulimwambia afanye Bank transfer ya hela yote iende kwenye account,tukisoma salio ndio tuta sain mkataba wa muuziano.
Tulipofika benki; yeye pale ni maruufu, tukaenda ofisi ya meneja moja kwa moja akampa karatasi meneja na dak 5 tu meneja akaja na bahasha kubwa ya kaki imejaa mabunda kibao, halafu meneja akaondoka ofisini kwake tukabaki mimi na mke wangu na wanununzi na timu yake. Akatuambia mzigo huu hapa weka sain tumalize.
Mimi nadhani yule Bwana alizani sijawai kamata hela nyingi kiasi kile sasa naona alidhani mimi kuona lile loba la hela ningepata kiwewe.
Tukamwambia mkataba unasema hela ilipwe kwenye account. Basi tukatoka pale na sababu ya foleni tukatembea mtaa mwingine kabisa na sababu ya foleni ilibidi abebe kile kiroba cha hela mkononi. Tulipofika benki mle ndani akaniomba niweke sain tena nikamwambia hela haijaingia mjomba . Basi akamtuma jamaa yake apange foleni ya kuweka hela. Wakati bado watu wawili mbele kufika zamu ya jamaa yake kufika kaunta akaniomba tena niweke sain ili muda tuwai kwani ana mambo mengi. Hapo nikaona moja kwa moja huyu bwana ana nia ya kutapeli. Nikwambaia sitii mkono mpaka nisome salio, Na ndivyo ilivyokuwa
Sijui kama ningeweka sain yangu mapema ingekuwaje, ila mi nadhani wangetawanyika na hela wangebaki nazo wao na MIMI NINGEBAKI NASHANGAA
mjini hapa.
Nilichogundua wanunuzi wana nia ya kutapeli pia sawa sawa na wauzaji wengine. Mnunuzi alikuja yuko full na mwanasheria na dalali mwenye ofisi yake posta huko sio hawa wa mitaani. Baada ya kuelewana mipaka na kila kitu tukaenda benk moja mjini
Kwanza tulimwambia afanye Bank transfer ya hela yote iende kwenye account,tukisoma salio ndio tuta sain mkataba wa muuziano.
Tulipofika benki; yeye pale ni maruufu, tukaenda ofisi ya meneja moja kwa moja akampa karatasi meneja na dak 5 tu meneja akaja na bahasha kubwa ya kaki imejaa mabunda kibao, halafu meneja akaondoka ofisini kwake tukabaki mimi na mke wangu na wanununzi na timu yake. Akatuambia mzigo huu hapa weka sain tumalize.
Mimi nadhani yule Bwana alizani sijawai kamata hela nyingi kiasi kile sasa naona alidhani mimi kuona lile loba la hela ningepata kiwewe.
Tukamwambia mkataba unasema hela ilipwe kwenye account. Basi tukatoka pale na sababu ya foleni tukatembea mtaa mwingine kabisa na sababu ya foleni ilibidi abebe kile kiroba cha hela mkononi. Tulipofika benki mle ndani akaniomba niweke sain tena nikamwambia hela haijaingia mjomba . Basi akamtuma jamaa yake apange foleni ya kuweka hela. Wakati bado watu wawili mbele kufika zamu ya jamaa yake kufika kaunta akaniomba tena niweke sain ili muda tuwai kwani ana mambo mengi. Hapo nikaona moja kwa moja huyu bwana ana nia ya kutapeli. Nikwambaia sitii mkono mpaka nisome salio, Na ndivyo ilivyokuwa
Sijui kama ningeweka sain yangu mapema ingekuwaje, ila mi nadhani wangetawanyika na hela wangebaki nazo wao na MIMI NINGEBAKI NASHANGAA
mjini hapa.