Jihadhari na Wajanja kwenye Uuzaji hasa Nyumba

wakurochi

JF-Expert Member
Dec 4, 2017
2,647
2,936
Hivi juzi kati nimefanikiwa kuuza banda langu ambalo nimetangaza sana hapa JF.

Nilichogundua wanunuzi wana nia ya kutapeli pia sawa sawa na wauzaji wengine. Mnunuzi alikuja yuko full na mwanasheria na dalali mwenye ofisi yake posta huko sio hawa wa mitaani. Baada ya kuelewana mipaka na kila kitu tukaenda benk moja mjini

Kwanza tulimwambia afanye Bank transfer ya hela yote iende kwenye account,tukisoma salio ndio tuta sain mkataba wa muuziano.
Tulipofika benki; yeye pale ni maruufu, tukaenda ofisi ya meneja moja kwa moja akampa karatasi meneja na dak 5 tu meneja akaja na bahasha kubwa ya kaki imejaa mabunda kibao, halafu meneja akaondoka ofisini kwake tukabaki mimi na mke wangu na wanununzi na timu yake. Akatuambia mzigo huu hapa weka sain tumalize.

Mimi nadhani yule Bwana alizani sijawai kamata hela nyingi kiasi kile sasa naona alidhani mimi kuona lile loba la hela ningepata kiwewe.

Tukamwambia mkataba unasema hela ilipwe kwenye account. Basi tukatoka pale na sababu ya foleni tukatembea mtaa mwingine kabisa na sababu ya foleni ilibidi abebe kile kiroba cha hela mkononi. Tulipofika benki mle ndani akaniomba niweke sain tena nikamwambia hela haijaingia mjomba . Basi akamtuma jamaa yake apange foleni ya kuweka hela. Wakati bado watu wawili mbele kufika zamu ya jamaa yake kufika kaunta akaniomba tena niweke sain ili muda tuwai kwani ana mambo mengi. Hapo nikaona moja kwa moja huyu bwana ana nia ya kutapeli. Nikwambaia sitii mkono mpaka nisome salio, Na ndivyo ilivyokuwa

Sijui kama ningeweka sain yangu mapema ingekuwaje, ila mi nadhani wangetawanyika na hela wangebaki nazo wao na MIMI NINGEBAKI NASHANGAA
mjini hapa.
 
Uoga tuu..mi nshshuhudia mtu anauza eneo kwa ajili ya sheli 400mil kwenye mabag ya kusafir bila mbwembwe hzo,tho ishu ilifanyika bank
 
Uoga tuu..mi nshshuhudia mtu anauza eneo kwa ajili ya sheli 400mil kwenye mabag ya kusafir bila mbwembwe hzo,tho ishu ilifanyika bank
Je kama ningesain kwamba nimepokea mpunga kabla sijashika mkononi wangenibadilika unadhani ningeweza kupata haki yangu ?
 
Uoga tu ulikujaa. Kama mkataba ubasema atalipa benki bado asingeweza kukutapeli maana angeulizwa pay slip iliyokulipa kama angetaka akutapeli na shauri likaenda mahakamani.
 
Uoga tu ulikujaa. Kama mkataba ubasema atalipa benki bado asingeweza kukutapeli maana angeulizwa pay slip iliyokulipa kama angetaka akutapeli na shauri likaenda mahakamani.
ok kesi itachukua miezi kibao na hela inatoka pia na mambo ya nenda rudi we unaonaje hapo mahakama zetu si unazijua
 
Uoga tu ulikujaa. Kama mkataba ubasema atalipa benki bado asingeweza kukutapeli maana angeulizwa pay slip iliyokulipa kama angetaka akutapeli na shauri likaenda mahakamani.
Mahakamani utapoteza muda wako mwiingi bila sababu za msingi. Huyu Bwana yuko sahihi kugoma kusaini mpaka pesa ilivyowekwa kwenye akaunti.
 
Uko sahihi mkuu.
Nishaqahi shuhudia jamaa ambaye mnunuaji wa kiwanja kaja na majambazi na bastola. Baada ya kupewa 3M tu na kusaini hati ya mauziano wakapiga risasi hewani kila mtu akakimbia na kwake. Bahati nzuri hawakufanikiwa kumuibia yule ndugu.
 
Ungemixiwa na hela fake
Hivi juzi kati nimefanikiwa kuuza banda langu ambalo nimetangaza sana hapa JF.

Nilichogundua wanunuzi wana nia ya kutapeli pia sawa sawa na wauzaji wengine. Mnunuzi alikuja yuko full na mwanasheria na dalali mwenye ofisi yake posta huko sio hawa wa mitaani. Baada ya kuelewana mipaka na kila kitu tukaenda benk moja mjini

Kwanza tulimwambia afanye Bank transfer ya hela yote iende kwenye account,tukisoma salio ndio tuta sain mkataba wa muuziano.
Tulipofika benki; yeye pale ni maruufu, tukaenda ofisi ya meneja moja kwa moja akampa karatasi meneja na dak 5 tu meneja akaja na bahasha kubwa ya kaki imejaa mabunda kibao, halafu meneja akaondoka ofisini kwake tukabaki mimi na mke wangu na wanununzi na timu yake. Akatuambia mzigo huu hapa weka sain tumalize.

Mimi nadhani yule Bwana alizani sijawai kamata hela nyingi kiasi kile sasa naona alidhani mimi kuona lile loba la hela ningepata kiwewe.

Tukamwambia mkataba unasema hela ilipwe kwenye account. Basi tukatoka pale na sababu ya foleni tukatembea mtaa mwingine kabisa na sababu ya foleni ilibidi abebe kile kiroba cha hela mkononi. Tulipofika benki mle ndani akaniomba niweke sain tena nikamwambia hela haijaingia mjomba . Basi akamtuma jamaa yake apange foleni ya kuweka hela. Wakati bado watu wawili mbele kufika zamu ya jamaa yake kufika kaunta akaniomba tena niweke sain ili muda tuwai kwani ana mambo mengi. Hapo nikaona moja kwa moja huyu bwana ana nia ya kutapeli. Nikwambaia sitii mkono mpaka nisome salio, Na ndivyo ilivyokuwa

Sijui kama ningeweka sain yangu mapema ingekuwaje, ila mi nadhani wangetawanyika na hela wangebaki nazo wao na MIMI NINGEBAKI NASHANGAA
mjini hapa.
 
Anakupa hela anatuma masela wanazichukua then anakuja kukupa pole tu.
Uoga tu ulikujaa. Kama mkataba ubasema atalipa benki bado asingeweza kukutapeli maana angeulizwa pay slip iliyokulipa kama angetaka akutapeli na shauri likaenda mahakamani.
 
Hivi juzi kati nimefanikiwa kuuza banda langu ambalo nimetangaza sana hapa JF.

Nilichogundua wanunuzi wana nia ya kutapeli pia sawa sawa na wauzaji wengine. Mnunuzi alikuja yuko full na mwanasheria na dalali mwenye ofisi yake posta huko sio hawa wa mitaani. Baada ya kuelewana mipaka na kila kitu tukaenda benk moja mjini

Kwanza tulimwambia afanye Bank transfer ya hela yote iende kwenye account,tukisoma salio ndio tuta sain mkataba wa muuziano.
Tulipofika benki; yeye pale ni maruufu, tukaenda ofisi ya meneja moja kwa moja akampa karatasi meneja na dak 5 tu meneja akaja na bahasha kubwa ya kaki imejaa mabunda kibao, halafu meneja akaondoka ofisini kwake tukabaki mimi na mke wangu na wanununzi na timu yake. Akatuambia mzigo huu hapa weka sain tumalize.

Mimi nadhani yule Bwana alizani sijawai kamata hela nyingi kiasi kile sasa naona alidhani mimi kuona lile loba la hela ningepata kiwewe.

Tukamwambia mkataba unasema hela ilipwe kwenye account. Basi tukatoka pale na sababu ya foleni tukatembea mtaa mwingine kabisa na sababu ya foleni ilibidi abebe kile kiroba cha hela mkononi. Tulipofika benki mle ndani akaniomba niweke sain tena nikamwambia hela haijaingia mjomba . Basi akamtuma jamaa yake apange foleni ya kuweka hela. Wakati bado watu wawili mbele kufika zamu ya jamaa yake kufika kaunta akaniomba tena niweke sain ili muda tuwai kwani ana mambo mengi. Hapo nikaona moja kwa moja huyu bwana ana nia ya kutapeli. Nikwambaia sitii mkono mpaka nisome salio, Na ndivyo ilivyokuwa

Sijui kama ningeweka sain yangu mapema ingekuwaje, ila mi nadhani wangetawanyika na hela wangebaki nazo wao na MIMI NINGEBAKI NASHANGAA
mjini hapa.
Hongera sana Mkuu..

Kupitia hilo umewafunza na wasio kuwa wakijua taratibu hizo, binadamu sa hivi wamekuwa wajanja sana kiasi usipokuwa makini basi UTALIA NA KUSAGA MENO.

Sometimes subira yavuta heri
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom