Jihadhari na tapeli huyu anayejiita Beka Mfaume

lutayega

JF-Expert Member
Feb 29, 2012
1,288
552
Kuna utapeli unafanyika kupitia page ya facebook inayoitwa kona ya riwaya reloded. mi nimetapeliwa na mtu anayejiita BEKA MFAUME mwenye namba 0754893247 niliwasiliana naye akajitambulisha kwa jina hilo tukakubaliana nimtumie sh 5600 kwa njia ya mpesa ili anitumie soft copy ya kitabu chake cha siku ya utakaso ambacho aliahidi kukituma ndani ya siku mbili.

Toka nimemtumia hiyo pesa sasa ni mienzi miwili na nusu imepita na kila nikimkumbusha ananiahidi kunitumia ila hatumi. Nawapa angalizo kuwa makini na mtu huyo na kona ya riwaya reloded ili msije tapeliwa kama mimi.
 
kuwa makini kwa kila kitu mjini hapa.we unatuma tu kirahisi.lakini umejifunza kutokana na kosa.
 
mwenzio aliweka salio akapata bando akaendelea kuchat fb duh pole sana
 
Huyu jamaa ni Mtunzi maarufu wa riwaya,mtafute,je nini yeye kweli au wajanja wanatumia jina lake...
 
beka mfaume ni mtu mzima mwenye heshima zake . hapo wahuni wamekuchezea akili.. je hiyo namba imesajiliwa jina lake!?
 
Cha msingi jaribu kumtafuta Beka mfaume mwenyewe umwelezee yaliyokukumba, naamini atachukua hatua stahiki na pia itasaidia na wengine wasije kutapeliwa hapa mjini kunamijitu imezoea kula kupitia migongo ya wenzao.
 
Kuna utapeli unafanyika kupitia page ya facebook inayoitwa kona ya riwaya reloded. mi nimetapeliwa na mtu anayejiita BEKA MFAUME mwenye namba 0754893247 niliwasiliana naye akajitambulisha kwa jina hilo tukakubaliana nimtumie sh 5600 kwa njia ya mpesa ili anitumie soft copy ya kitabu chake cha siku ya utakaso ambacho aliahidi kukituma ndani ya siku mbili.

Toka nimemtumia hiyo pesa sasa ni mienzi miwili na nusu imepita na kila nikimkumbusha ananiahidi kunitumia ila hatumi. Nawapa angalizo kuwa makini na mtu huyo na kona ya riwaya reloded ili msije tapeliwa kama mimi.
Sina hakika kama atakuwa Beka Mfaume ninayemfahamu, lakini kama ni yeye
basi mfuate kwenye ofisi za magazeti ya Sani na Kiu pale Shaurimoyo...
 
Sina hakika kama atakuwa Beka Mfaume ninayemfahamu, lakini kama ni yeye
basi mfuate kwenye ofisi za magazeti ya Sani na Kiu pale Shaurimoyo...

kaka nisaidie mawasiliano yake kama unayo. Naomba unitumie kwenye pm
 
Back
Top Bottom