jihadhari na polisi wala rushwa magomeni

babukijana

JF-Expert Member
Jul 21, 2009
13,087
15,981

Nlitokea Jangwani kwenda Magomeni juzi tarehe 17/8/10 mchana na kujaribu kuingia barabara ya kulia bondeni hapo Magomen Mapipa karibu na kwa Macheni bila kuona alama inayozuia. Kutaharuki nikakutana na Traffiki wa pikipiki na sub-machine walovalia kama FFU.
Magari matatu yalikamatwa kwa mpigo na kuongozwa kituo cha Magomeni. Wakachukua cadi za magari na leseni. Wakasimamisha magari barabara kuu. Pikipiki mbili zilituswaga harakaharaka hadi kituo Magomeni. Kufika tukabanwa kwenye magari mengine.
Askari maarufu mviziaji kumbe anaitwa White (Cheupe), IGP na Kova lazima wamfahamu. Haraka kachukua funguo na kutishia kesho ni mahakamani na faini ni Sh. 250,000 au kifungo/au vyote. Kuona niko kibosi na gari imeshehena mzigo wa nguvu wa duka nikaitwa kwanza (si unajua ..deal/mteja) ndani ya ofisi kulia karibu na kimgahawa chao mbele ya ile ya top boss.
Akaketi kushoto mwa chumba na kuamuru watuhumiwa wengine watolewe nje haraka. Akaagiza copy ya fomu mashitaka. Askari wa kike wakabaki wanatazama kusubiri mgawo. Akasema nikodishe gari ya kubeba mizigo yangu na langu lilale hapo. Ama sivyo tuongee kimila au….. Muonekano wake ni kiSingida/Kikaskazini type.
Eti mahabusu walijaa watu kama sisi. Jamaa kadai elfu 50 ndani ya ofisi. Nilitakiwa nikamchukue mtoto mchanga shuleni, ikabidi ……….(KK). Seems he fraudulently collects not less than TAS 1.0m per day and shares with his … because all took place infront and under the noses of his top guys. Serikali haiambulii senti.
Inakuwaje gari kuingizwa kituoni mchana na kutoka bila kibali cha wakubwa?? Si deal ya wengi??. Kazi kwako Mheshimiwa sana IGP Mwema na Mhe.Kamanda Kova utusaidie hili. How come that a traffic offender is arrested by sub-machine gun armed cops??. Bunduki ya nini kwenye kosa la traffic??.. I was seriously intimidated, frightened and fragmented!
This is pure day light robbery by few corrupt traffic men. Through this peoples blog am appealing to the Honorable Mwema na Kova to clean Magomeni Station and send Mr White “ or Cheupe to where he belongs best .. apelekwe zima moto or aadabishwe. Ni rushwa tu inaendelea hapo. Tuna imani na Jeshi letu bado, lakini maboresho ni lazima.
Mdau aliyelizwa Magomeni

from:michuzi post
 
Back
Top Bottom