Jihadhari na matapeli wanaojifanya kama wafanyakazi wa TRA

Pianist

JF-Expert Member
Nov 7, 2010
679
370
Kuna matapeli wanapita mitaani na gari na kujifanya wao wametumwa na TRA kuangalia biashara ndogondogo kama saluni, stationery, magenge na maduka kama zimesajiliwa. Hawana vitambulisho na gari wanayotumia ina namba za usajili za kiraia. Wakikuta hauna leseni na TIN number wanatoa vitisho vya faini kubwa (laki tano, milioni) na kisha kuomba rushwa (elfu hamsini) na kuchukua baadhi ya bidhaa unazouza kama; kopo la maziwa ya unga, dumu la mafuta ya kula bila ya kuwa na aibu. Hawa ni wezi na matapeli kama walivyo wengine. Siku ukiwaona wapo kwenye sehemu ya biashara ya mtu mjulishe mhusika kwamba hao ni wezi asiwape rushwa.
 
Kuna matapeli wanapita mitaani na gari na kujifanya wao wametumwa na TRA kuangalia biashara ndogondogo kama saluni, stationery, magenge na maduka kama zimesajiliwa. Hawana vitambulisho na gari wanayotumia ina namba za usajili za kiraia. Wakikuta hauna leseni na TIN number wanatoa vitisho vya faini kubwa (laki tano, milioni) na kisha kuomba rushwa (elfu hamsini) na kuchukua baadhi ya bidhaa unazouza kama; kopo la maziwa ya unga, dumu la mafuta ya kula bila ya kuwa na aibu. Hawa ni wezi na matapeli kama walivyo wengine. Siku ukiwaona wapo kwenye sehemu ya biashara ya mtu mjulishe mhusika kwamba hao ni wezi asiwape rushwa.

Mkuu, taarifa muafaka sana hii, hasa katika kipindi hiki ambacho TRA wameamua kuwazungukia wafanyabiashara katika maeneo yao ya biashara. Kimsingi, mtumishi yeyote wa Serikali (TRA) anapokutembelea katika biashara yako basi muombe AKUONYESHE KITAMBULISHO. Usibabaishwe na uniform
 
Back
Top Bottom