JIFUNZE: Tengeneza Mwili wa chini bila kuingia Gym

Asante sana mkuu, labda kwa kuongezea uelewa wako nikitumia whey protein ili mwili ukae vizuri nichanganye na steroid au mega mass?
Kwa uelewa wangu kwa mhitaji wa mwili wa level ya Jason Statham kwenye Transporter 1 whey protein pekee inatosha unachotakiwa kufanya ni mazoezi ya uhakika.
8eff73f15cc96f815e32c7b0a7461a49.jpg


Kama unataka kuwa na mwili wa levo ya Michael Jai White changanya na mega mass.
undisputed-ii-0.jpg


Kama unataka kuwa na mwili levo ya Phil Heath changanya na steroids.
28K0954.jpg


NB.
Hizo supplements siyo replacement ya chakula usiache kuendelea kula na kunywa maji.

Steroids zimepigwa marufuku nchi nyingi na katika baadhi ya michezo ukigundulika umetumia unaondolewa kwenye mchezo husika. Nchi zingine hupati steroids mpaka uandikiwe na daktari na sidhani kama Tz zipo (kama upo Tz).

Kwa kadri nionavyo steroids zina madhara ambayo hayaepukiki ingawa inasemwa ni mpaka ukiwa unaabuse.

Fuatilia side effects ya mega mass utakayokua unatumia na namna ya kuziepuka kama ni risk sana nashauri achana nazo.

Picha zimetoka mtandaoni.
 
Na-assume unaongelea supplements za kutengeneza mwili (kutokana na kuuliza zinaongeza au zinakata). Pia nina-assume wewe ni me.

Supplements zipo za kuongeza mwili halafu zipo za kukata mwili. Zinazofanya kazi ya kuongeza na kukata mwili zipo pia zinaitwa steroids (zimepigwa marufuku sehemu nyingi sijui Tz) sidhani kama steroids zipo Tz.

Mimi hua situmii supplements lakini nimeshuhudia wengi wakitumia hivyo nina mawili matatu.

Supplements zinareplace seli nyekundu za damu na kurepair tissue muda wote wa mazoezi, mtu anakua hachoki na ana nguvu.

Of course zitaubadilisha mwili lakini nashauri jifunze na side effects zake na namna ya kuziepuka.

Watu wote ninaowajua waliotumia supplements walipata wanachotaka, ikiwa utaanza kutumia usifanye mazoezi kwa kutegea utakua unarisk kuwa na tumbo na makalio makubwa sana.
mkuu hivi kutengeneza mazoezi ya chini kupitia gym kama yapi
 
mkuu hivi kutengeneza mazoezi ya chini kupitia gym kama yapi
Haya mazoezi niliyoonesha hapa, tofauti yake na ukiyafanyia gym ni kwamba ukiwa gym utakua umebeba uzito mabegani hivyo utafanya kama hapa ila ukiwa una mzigo.

Ukimaliza hayo matatu unafuatia calf raise (gym zingine nilikuta wanaita donkey raise na wanaifanya tofauti), leg press, leg extension na leg curls.

Watu wengine huendesha baiskeli kabla au baada, hayo mazoezi nimepangilia kuanzia utakachoanzia na utakachomalizia.
 
Haya mazoezi niliyoonesha hapa, tofauti yake na ukiyafanyia gym ni kwamba ukiwa gym utakua umebeba uzito mabegani hivyo utafanya kama hapa ila ukiwa una mzigo.

Ukimaliza hayo matatu unafuatia calf raise (gym zingine nilikuta wanaita donkey raise na wanaifanya tofauti), leg press, leg extension na leg curls.

Watu wengine huendesha baiskeli kabla au baada, hayo mazoezi nimepangilia kuanzia utakachoanzia na utakachomalizia.
nataka chura wangu akae mkao mzuri pia aongezeke kidogo na tumbo liishe mkuu.pia mikono ipungue nifanyeje?
 
nataka chura wangu akae mkao mzuri pia aongezeke kidogo na tumbo liishe mkuu.pia mikono ipungue nifanyeje?
Kuhusu tumbo, kuna uzi niliwahi kuuanzisha bonyeza username ya Castr cheki nyuzi ambazo zimeanzishwa na Castr utakuta uzi unasema 'Unataka tumbo flat na six packs...'

Kuhusu chura, mimi ni me hivyo sijawahi kuprove kama mazoezi yanayokua promoted yanamkuza na kumtengeneza chura kama yanafanya kazi kweli, ingawa fitness gurus wanaonyesha kua mazoezi hayo yapo.

Kwenye mikono sijaelewa, kwamba ni mikubwa ukilinganisha na mwili wako? Au ina nyama zinazoning'inia?
 
Kuhusu tumbo, kuna uzi niliwahi kuuanzisha bonyeza username ya Castr cheki nyuzi ambazo zimeanzishwa na Castr utakuta uzi unasema 'Unataka tumbo flat na six packs...'

Kuhusu chura, mimi ni me hivyo sijawahi kuprove kama mazoezi yanayokua promoted yanamkuza na kumtengeneza chura kama yanafanya kazi kweli, ingawa fitness gurus wanaonyesha kua mazoezi hayo yapo.

Kwenye mikono sijaelewa, kwamba ni mikubwa ukilinganisha na mwili wako? Au ina nyama zinazoning'inia?
ok mikono ni mimene sana
 
ok mikono ni mimene sana
Napendekeza mazoezi ya kupunguza mwili. Kwa kuyafanya utakua unaondoa fat ya tumboni na hiyo iliyo kwenye mikono, hivyo utakua unafikia malengo yako yote mawili.

Napendekeza kujog, kuruka kamba, kuendesha baiskeli, cardio na kuhakikisha diet yako inaendana na malengo yako.

Kama ni beginner anza pole pole na utaongeza ukubwa wa mazoezi unayofanya kadri utakavyozoea.
 
castr leo nimepiga push up zile pana,nimepiga 30 awamu ya kwanza nikapumzika dakika 3 nikapiga 20 baada ya hapo nikapiga kumikumi na kutimiza miamoja,baada ya dakika 5 nikachukua roller yangu a.k.a kitairi nimekwenda mara 30 yaani kila set ni kumikumi.
 
castr leo nimepiga push up zile pana,nimepiga 30 awamu ya kwanza nikapumzika dakika 3 nikapiga 20 baada ya hapo nikapiga kumikumi na kutimiza miamoja,baada ya dakika 5 nikachukua roller yangu a.k.a kitairi nimekwenda mara 30 yaani kila set ni kumikumi.
Mkuu hongera kwa mwanzo wenye nguvu kama huo, maintain hiki unachokifanya kwa muda kisha punguza muda wa kupumzika mpaka utakapoweza kufanya seti na raundi ambazo nilizionesha.

Nakugarantii mabadiliko.
 
Heshima kwenu wadau.

Katika uzi wangu uliopita nilielezea jinsi unavyoweza kutengeneza mwili bila kuingia gym. Mazoezi yale yalilenga mwili wa juu, yaani kifua, mikono na mabega.

Jinsi ya kutengeneza mwili bila kuingia Gym

Leo tutaangalia namna ya kutengeneza mwili wa chini yaani miguu, mapaja na nguvu za miguu yote.

Ili kufikia malengo yetu tutaifuata kanuni ile ile ya Tabata Protocol. Na zoezi letu litakua ni squats.

Hivyo zoezi letu litakua na kanuni ifuatayo;
Zoezi moja litakua na seti nne.
Seti moja itakua na reps ishirini.
Kupumzika kati ya seti moja na nyingine ni sekunde kumi.
Kupumzika kati ya zoezi moja na jingine ni dakika moja.

Tuanze.

Squats za kawaida.
Tanua miguu yako usawa wa mabega yako, mikono inaweza kushikilia kichwa ama ukainyoosha kwa mbele.
View attachment 464617
Utaanza kwa kuchuchumaa kwenda chini, ukirudi juu hiyo ni moja.
Utafanya hivyo mara 20 kwa seti nne. Kisha tunaenda zoezi la pili.

Visigino Viwe Vimeinuka.
Mkao wako utakua kama wa hapo juu ila kwenye visigino utakua umeweka kitu cha kufanya visigino viwe kwa juu (unakua umekikanyaga kitu husika). Mfano mimi huwa naweka mbao.
View attachment 464618
Utaanza kwa kuchuchumaa kwenda chini, ukirudi juu hiyo ni moja.
Utafanya hivyo mara 20 kwa seti nne. Kisha tunaenda zoezi la tatu.

One Step Squats.
Mkao wako utakua kama wa kufanya zoezi la kwanza, ila mbele yako utaweka kitu ambacho mguu wako utaweza kukikanyaga, mfano tofali au ngazi.
Umbali wa hiko kitu uwe kuanzia hatua mbili kutoka uliposimama.
View attachment 464619
Kutokea uliposimama, utaanza na mguu mmoja kuwa kama unapiga hatua na kutua kwenye hiko kitu kisha utarudi square kama ulivyokua mwanzo. Utamalizia na wa pili hapo unakua umepiga moja, yaani mfano umeanza na mguu wa kushoto, utapiga na wa kulia hapo utakua umepiga moja.
Fanya hivyo mara 20 na tutakua tumemaliza zoezi letu.

NB;
-Ukiwa unachuchumaa usiwe kama unataka kutua mzigo, usiupinde mgongo, nyooka.
-Kama una maumivu ya mgongo au kiuno punguza idadi ya reps na ongeza muda wa kupumzika.
-Ushauri wangu ni kutokana na uzoefu wangu na kujifunza kwa wengine, sijasomea, na siyo wa kidaktari.
-Comment workout yako tujifunze.
Mkuu na kareti uko vizuri? Combat? Mm hii minyama bila ujuzi siyataki, au sheria ya ugaidi inakataza?
 
Mkuu na kareti uko vizuri? Combat? Mm hii minyama bila ujuzi siyataki, au sheria ya ugaidi inakataza?
Hapana sijawahi kufanya mafunzo ya karet, nilifanya boxing zamani.

Ila unaweza kua fit bila hata kutaka kujua ngumi au ukajua ni uchaguzi wako, na kadri ninavyojua sheria haikatazi.
 
Heshima kwenu wadau.

Katika uzi wangu uliopita nilielezea jinsi unavyoweza kutengeneza mwili bila kuingia gym. Mazoezi yale yalilenga mwili wa juu, yaani kifua, mikono na mabega.

Jinsi ya kutengeneza mwili bila kuingia Gym

Leo tutaangalia namna ya kutengeneza mwili wa chini yaani miguu, mapaja na nguvu za miguu yote.

Ili kufikia malengo yetu tutaifuata kanuni ile ile ya Tabata Protocol. Na zoezi letu litakua ni squats.

Hivyo zoezi letu litakua na kanuni ifuatayo;
Zoezi moja litakua na seti nne.
Seti moja itakua na reps ishirini.
Kupumzika kati ya seti moja na nyingine ni sekunde kumi.
Kupumzika kati ya zoezi moja na jingine ni dakika moja.

Tuanze.

Squats za kawaida.
Tanua miguu yako usawa wa mabega yako, mikono inaweza kushikilia kichwa ama ukainyoosha kwa mbele.
View attachment 464617
Utaanza kwa kuchuchumaa kwenda chini, ukirudi juu hiyo ni moja.
Utafanya hivyo mara 20 kwa seti nne. Kisha tunaenda zoezi la pili.

Visigino Viwe Vimeinuka.
Mkao wako utakua kama wa hapo juu ila kwenye visigino utakua umeweka kitu cha kufanya visigino viwe kwa juu (unakua umekikanyaga kitu husika). Mfano mimi huwa naweka mbao.
View attachment 464618
Utaanza kwa kuchuchumaa kwenda chini, ukirudi juu hiyo ni moja.
Utafanya hivyo mara 20 kwa seti nne. Kisha tunaenda zoezi la tatu.

One Step Squats.
Mkao wako utakua kama wa kufanya zoezi la kwanza, ila mbele yako utaweka kitu ambacho mguu wako utaweza kukikanyaga, mfano tofali au ngazi.
Umbali wa hiko kitu uwe kuanzia hatua mbili kutoka uliposimama.
View attachment 464619
Kutokea uliposimama, utaanza na mguu mmoja kuwa kama unapiga hatua na kutua kwenye hiko kitu kisha utarudi square kama ulivyokua mwanzo. Utamalizia na wa pili hapo unakua umepiga moja, yaani mfano umeanza na mguu wa kushoto, utapiga na wa kulia hapo utakua umepiga moja.
Fanya hivyo mara 20 na tutakua tumemaliza zoezi letu.

NB;
-Ukiwa unachuchumaa usiwe kama unataka kutua mzigo, usiupinde mgongo, nyooka.
-Kama una maumivu ya mgongo au kiuno punguza idadi ya reps na ongeza muda wa kupumzika.
-Ushauri wangu ni kutokana na uzoefu wangu na kujifunza kwa wengine, sijasomea, na siyo wa kidaktari.
-Comment workout yako tujifunze.
Hii ipo vizur sana
 
Tafadhali usiniquote na kuniuliza juu ya hii mada
 
Back
Top Bottom