1. Bei unazoziona sio sahihi, ongea na seller kuhusu bei husika.
2. Postal shipping wanaitumia kwa sample tu, full mzigo wanataka express.
3. Make sure mnanegotiate na kulipana ndani ya Alibaba system (Trade assurance)
 
Imekuwa ni shida sana kwa watanzania wengi kununua bidhaaa katika masoko haya ya mtandaoni kwani mengi huwa hayakupi fursa ya kutumiwa mzigo wako moja kwa moja Tanzania. Baadhi ya thread zilianzishwa na zimeelezea mengi sana kuhusiana na manunuzi haya ya mtandaoni, ila tulipata ufumbuzi mdogo.

Nimejaribu kupitia pitia forums nyingi nichanganue namna mbadala ya kupata mizigo bila ya kutumia gharama nyingi. hii ni kwa kutumia FOWARDING COMPANIES ambazo kazi yake ni;

1: Kukupatia anuani ya Marekani (au popote iliopo ila nashauri marekani au uingereza UK) au US Shipping Address

2: Kupokea mzigo kwenye soko ulilotumia (eidha amazon,ebay au lolote lile lisilo ship Tanzania)

3: Kukutumia mzigo wewe hapo ulipo kwa wakala kama DHL,FEDEX,UPS,USPS NK baada ya kujua kazi ya fowarding company unahitaji kuwa na vigezo vifuatavyo (kwa wageni wasiofahamu/hawajapitia previous threads:

1: CREDIT CARD (KADI YA BENKI) INAYOFANYA ONLINE PURCHASES;
Hii inapatikana almost bank zote hapa Tanzania (kasoro NMB sina uhakika), ni kadi yeyote ya visa au mastercard unachotakiwa ni kwenda kwenye tawi la benki yako na kuomba fomu ya kuruhusu kadi yako ifanye malipo ya mtandaoni(online purchases) na mara nyingi huchukua maximum 24hours kuactivate.

2: KUJIUNGA NA PAYPAL
Hiii ni kampuni inayolinda malipo yako kwa kutomuonesha muuzaji details (nyaraka) za kadi yako kama number na css ambayo vitampa muuzaji access ya kuchukua pesa zako. Ila kwa paypal utalindwa na kurudishiwa pesa pale panapotokea shida au huduma mbaya.

3: KUJIUNGA NA FOWARDING COMPANY
Hii hatua ni ya wewe kwenda kwenye website (tovuti) za hizi fowarding company na kujiunga (sighnup) nazo/nayo ili zianze kukupatia huduma... nitaelezea chini zaidi kuhusu ipi ni ipi na huduma zao zikoje na faida na hasara za kila moja ili ujichagulie wewe mwenyewe binafsi

4: KUTAMBUA SOKO BORA LENYE HUDUMA NZURI(ONLINE MARKET)
Hapa tunazungumzia website za masoko kama ebay,amazon, bestbuy, apple.com, dell.com, toshiba.com nk.. masoko haya ndipo utakapo nunua bidhaa yako.

PROCESS NZIMA KUANZIA UNANUNUA MPAKA MZIGO UNAKUFIKIA IKOJE?

Hii iko hivi....

1: Ingia katika soko lako ulilolichagua au unalopendelea, hapa nasuggest kutumia sana amazon(ndilo ninaloliamini) amazon ukiingia utakuta bidhaa nyingi ila kuwa makini kuchukua zile bidhaa zilizo na alama ya prime chini...alama hiyo inamaanisha kuwa huo mzigo unauzwa, utapakiwa, na kutumwa na amazon wenyewe, so no utapeli hapo, yani u get what u wanted.

2: Nunua na kuagiza kitu kwenda kwenye address ya fowarding company ulioichagua, hivyo mzigo ulioununua utaenda moja kwa moja kwenye company yako, wao wakishaupata watakutumia e-mail uthibitishe au uchague courier wa kukutumia mzigo wako, hapo ndio utachagua either dhl,ups,fedex nk.wao watakutumia na kuchukua kiasi chao cha pesa ya huduma na kukutumia mzigo pamoja na kukupatia tracking number ya kujua mzigo wako ulipo na utaupokea vyema.

FOWARDING COMPANIES ZENYEWE:

1: MYUS.COM link- MyUS.com - #1 International Shipping, Mail and Package Forwarding Service - MyUS.com. Hii ni company niliyoitumia na nina expirience nayo ya mizigo miwili, hawa ni waaminifu wana charge pesa kidogo na huwa hawachukui muda kukutumia mzigo wako. yaani unafika leo hata ukitaka utumwe leo unatumwa, na utafika upesi sana bila ya zengwe lolote.

Ubaya wao: wanatumia sana DHL ambayo kwa mizigo mikubwa ni gharama sana kwa mtanzania wa kawaida, kiasi cha dola kumi kujiunga na huduma zao

Uzuri wao: watakutumia mzigo hata kama utakuwa hauna pesa kwenye account yako, watakujulisha ni duka lipi lina discount ya kutumia huduma zao, watakukumbusha kulipa deni lao, utapewa muda wa miezi miwili kulipa pesa yao,

2: COMGATEWAY
Link: http://comgateway.com/ - Hawa pia ni fowarding company nzuri sana (thanks tu Mwl.RCT), nimepitia site yao na huona wana policy nzuri sana, cha kwanza ni sales tax-free U.S. online shopping yaani punguzo la kodi ya kufanya manunuzi marekani, hii inapelekea huduma zao kuwa nafuu zaidi,pia wana ushirika na shipping courie DHL na FEDEX hivyo kufanya huduma zao kuwa rahisi zaidi.pia wanakupa habari kuhusu discount za masoko mbalimbali kama myus..

3: BORDERLINX
Link: Buy in the USA, ship to Belgium with Borderlinx - Hawa pia ni wazuri sana na hawana tofauti sana na stackry ... Wanawiana ingawa ni competitors wakubwa hivyo inakupa urahisi wa kuwatumia..Hawa pia hawana registration fee na wanakupa option tofauti tofauti za kutumiwa mzigo wako.

4: SHIPITO
Link: USA Address & Mail Forwarding Shipito.com | English - Hii pia ni kampuni kongwe ya fowarding na wao gharama zao ni nafuu sana ingawa wanapokea malalamiko mengi sana kutoka kwa wateja wao ukiangalia kwenye forums nyingi.ila kiujumla ni wazuri kwasababu malalamiko ni madogo kulinganisha na ufanisi na pia wanajua na ni wazoefu sana na kazi yao

5: STACKRY
Link: Stackry - US shopping, global shipping - Hii nayo haina tofauti na myus isipokuwa hawa wao hawana kiasi cha kulipia kujiunga nao na wao pia wanakupa option nyingi za kutumia mizigo yako na mabo yao pia ni mazuri kulinganisha na comment wanazopokea kutoka kwa wateja wao. waungwana ni hayo tu niliyo nayo, kazi kwenu ni kufanya utafiti na pia kuangalia na kuchunguza mabo kabla ya kuchukua uamuzi.

STACKRY na BORDERLINX walikuwa recommended sana na wanasifiwa mno angalia hii link -http://tech-vise.com/10-parcel-forwarding-services-for-international-shoppers/ pitia hizo websites na ujionee mwenyewe chagua moja na utazame kama wanakufaa.

HUU NI MTAZAMO WANGU BINAFSI WAKUU , Please evaluate kindly.

Nilikuwa nataka kuonyesha steps ila naona thread haitoshi maana nimeagiza mzigo na nimechukua hatua zote ili mpate kuona ila I think there are limits..

Help Mwl.RCT
Ahsante mkuu kwani na mimi nilikia nataka ku place order ila nilipata matatizo kidogo kwa namana ya kufanya trusted shipping ila umenifungua akili kwani nilijua forwarding companies ni za magari tuu na bidhaa zingine kubwa
 
Heloo JF.Hakika huko Customs department+TRA kwenye airport zetu kuna shida nyinginyingi, na si mara ya kwanza kusikia complaints kutoka kwa wadau pengine wazoefu watupe tricks.
Package imechukua 4 days kutoka China kufika TZ ila sasa ndio hivo, bongo bahati mbaya madudu lazima yawepo.
Mzigo umefika 15 July Nilijaza c34 form na kutuma documents zote kama invoice, TIN certificate, LOA by 17 July, na kufikia 22 July nikapewa assessment form na payment note yenye gharama za VAT+, TBS, Custom processing fee pamoja na issue nyingine according to TRA, payment receipts nilituma siku hiyogiyo. sasa mara leo naambiwa invoice yako imekataliwa mara nin, najiuliza hilo kadirio la kodi lilifanyikaje kwa kutumia invoice ambayo ni invalid/incomplete ?.
.Leo niliwapandia hewani wame acknowledge makosa yao, I hope this week nitapokea mzigo wangu.
Screenshot_2019-07-30-19-05-57-180_com.android.browser.jpg
 
mm hua natumia Aliexpress ni nzuri saana na ni bonge ya market af iko very simple na wanakata pesa direct kwenye account yako ys master Card
 
Heloo JF.Hakika huko Customs department+TRA kwenye airport zetu kuna shida nyinginyingi, na si mara ya kwanza kusikia complaints kutoka kwa wadau pengine wazoefu watupe tricks.
Package imechukua 4 days kutoka China kufika TZ ila sasa ndio hivo, bongo bahati mbaya madudu lazima yawepo.
Mzigo umefika 15 July Nilijaza c34 form na kutuma documents zote kama invoice, TIN certificate, LOA by 17 July, na kufikia 22 July nikapewa assessment form na payment note yenye gharama za VAT+, TBS, Custom processing fee pamoja na issue nyingine according to TRA, payment receipts nilituma siku hiyogiyo. sasa mara leo naambiwa invoice yako imekataliwa mara nin, najiuliza hilo kadirio la kodi lilifanyikaje kwa kutumia invoice ambayo ni invalid/incomplete ?.
.Leo niliwapandia hewani wame acknowledge makosa yao, I hope this week nitapokea mzigo wangu.
View attachment 1167381
Waweza kunisaidia namna ya kufanya malipo ya kodi Tanzania kwa mzigo ulioingia kutoka nje mkuu? Naona kuagiza mzigo kutoka nje hakuna shida, shida ukishafika hapa Tz namna ya kuupata, wanaohusika wanakuwa ni wa ghali sana kukuhudumia. Nisaidie hapo tu.
 
Waweza kunisaidia namna ya kufanya malipo ya kodi Tanzania kwa mzigo ulioingia kutoka nje mkuu? Naona kuagiza mzigo kutoka nje hakuna shida, shida ukishafika hapa Tz namna ya kuupata, wanaohusika wanakuwa ni wa ghali sana kukuhudumia. Nisaidie hapo tu.
Kampuni ya usafirishaji wakikupigia simu au wewe utaona kwenye tracking kuwa Mzigo umefika Julius Nyerere International Airport (Incase of Air Shipment) kinachofuata ni Customs Clearance, Unahitaji kuwa na TIN Certificate, Commercial Invoice ya bidhaa uliyo nunua ili TRA waweze kukupa kadirio la Taxes/Duties.
kama hutaki kutumia wakala wa clearence mchek members mwenzetu humu anaitwa Mwl RCT atakupa mwongozo maana mimi nilifanyiwa clearance na Sunfresh LTD sababu nipo mbali sana na Dar kwahiyo kama ningesafiri gharama zingekuwa kubwa zaidi.
 
Kampuni ya usafirishaji wakikupigia simu au wewe utaona kwenye tracking kuwa Mzigo umefika Julius Nyerere International Airport (Incase of Air Shipment) kinachofuata ni Customs Clearance, Unahitaji kuwa na TIN Certificate, Commercial Invoice ya bidhaa uliyo nunua ili TRA waweze kukupa kadirio la Taxes/Duties.
kama hutaki kutumia wakala wa clearence mchek members mwenzetu humu anaitwa Mwl RCT atakupa mwongozo maana mimi nilifanyiwa clearance na Sunfresh LTD sababu nipo mbali sana na Dar kwahiyo kama ningesafiri gharama zingekuwa kubwa zaidi.
Basi Mwl RCT popote ulipo naomba unisaidie kwa hili, haiwezekani kufanya clearance mwenyewe online or otherwise hadi ufike Dar es salaam?
 
Basi Mwl RCT popote ulipo naomba unisaidie kwa hili, haiwezekani kufanya clearance mwenyewe online or otherwise hadi ufike Dar es salaam?
Kwangu hawa clearance agents nawaona kama some kinds if vishoka. Ambapo mtu unapewa ugumu wa kupata mzigo wako kama hutaki kutumia hao jamaa.
 
Usaidizi kwa mfano nimenunua labda kama kitabu kimoja au computer moja nayo inahitajika kuilipia kodi na kuufuata hyo computer hadi J.k Airport
 
Kaka
Imekuwa ni shida sana kwa watanzania wengi kununua bidhaaa katika masoko haya ya mtandaoni kwani mengi huwa hayakupi fursa ya kutumiwa mzigo wako moja kwa moja Tanzania. Baadhi ya thread zilianzishwa na zimeelezea mengi sana kuhusiana na manunuzi haya ya mtandaoni, ila tulipata ufumbuzi mdogo.

Nimejaribu kupitia pitia forums nyingi nichanganue namna mbadala ya kupata mizigo bila ya kutumia gharama nyingi. hii ni kwa kutumia FOWARDING COMPANIES ambazo kazi yake ni;

1: Kukupatia anuani ya Marekani (au popote iliopo ila nashauri marekani au uingereza UK) au US Shipping Address

2: Kupokea mzigo kwenye soko ulilotumia (eidha amazon,ebay au lolote lile lisilo ship Tanzania)

3: Kukutumia mzigo wewe hapo ulipo kwa wakala kama DHL,FEDEX,UPS,USPS NK baada ya kujua kazi ya fowarding company unahitaji kuwa na vigezo vifuatavyo (kwa wageni wasiofahamu/hawajapitia previous threads:

1: CREDIT CARD (KADI YA BENKI) INAYOFANYA ONLINE PURCHASES;
Hii inapatikana almost bank zote hapa Tanzania (kasoro NMB sina uhakika), ni kadi yeyote ya visa au mastercard unachotakiwa ni kwenda kwenye tawi la benki yako na kuomba fomu ya kuruhusu kadi yako ifanye malipo ya mtandaoni(online purchases) na mara nyingi huchukua maximum 24hours kuactivate.

2: KUJIUNGA NA PAYPAL
Hiii ni kampuni inayolinda malipo yako kwa kutomuonesha muuzaji details (nyaraka) za kadi yako kama number na css ambayo vitampa muuzaji access ya kuchukua pesa zako. Ila kwa paypal utalindwa na kurudishiwa pesa pale panapotokea shida au huduma mbaya.

3: KUJIUNGA NA FOWARDING COMPANY
Hii hatua ni ya wewe kwenda kwenye website (tovuti) za hizi fowarding company na kujiunga (sighnup) nazo/nayo ili zianze kukupatia huduma... nitaelezea chini zaidi kuhusu ipi ni ipi na huduma zao zikoje na faida na hasara za kila moja ili ujichagulie wewe mwenyewe binafsi

4: KUTAMBUA SOKO BORA LENYE HUDUMA NZURI(ONLINE MARKET)
Hapa tunazungumzia website za masoko kama ebay,amazon, bestbuy, apple.com, dell.com, toshiba.com nk.. masoko haya ndipo utakapo nunua bidhaa yako.

PROCESS NZIMA KUANZIA UNANUNUA MPAKA MZIGO UNAKUFIKIA IKOJE?

Hii iko hivi....

1: Ingia katika soko lako ulilolichagua au unalopendelea, hapa nasuggest kutumia sana amazon(ndilo ninaloliamini) amazon ukiingia utakuta bidhaa nyingi ila kuwa makini kuchukua zile bidhaa zilizo na alama ya prime chini...alama hiyo inamaanisha kuwa huo mzigo unauzwa, utapakiwa, na kutumwa na amazon wenyewe, so no utapeli hapo, yani u get what u wanted.

2: Nunua na kuagiza kitu kwenda kwenye address ya fowarding company ulioichagua, hivyo mzigo ulioununua utaenda moja kwa moja kwenye company yako, wao wakishaupata watakutumia e-mail uthibitishe au uchague courier wa kukutumia mzigo wako, hapo ndio utachagua either dhl,ups,fedex nk.wao watakutumia na kuchukua kiasi chao cha pesa ya huduma na kukutumia mzigo pamoja na kukupatia tracking number ya kujua mzigo wako ulipo na utaupokea vyema.

FOWARDING COMPANIES ZENYEWE:

1: MYUS.COM link- MyUS.com - #1 International Shipping, Mail and Package Forwarding Service - MyUS.com. Hii ni company niliyoitumia na nina expirience nayo ya mizigo miwili, hawa ni waaminifu wana charge pesa kidogo na huwa hawachukui muda kukutumia mzigo wako. yaani unafika leo hata ukitaka utumwe leo unatumwa, na utafika upesi sana bila ya zengwe lolote.

Ubaya wao: wanatumia sana DHL ambayo kwa mizigo mikubwa ni gharama sana kwa mtanzania wa kawaida, kiasi cha dola kumi kujiunga na huduma zao

Uzuri wao: watakutumia mzigo hata kama utakuwa hauna pesa kwenye account yako, watakujulisha ni duka lipi lina discount ya kutumia huduma zao, watakukumbusha kulipa deni lao, utapewa muda wa miezi miwili kulipa pesa yao,

2: COMGATEWAY
Link: http://comgateway.com/ - Hawa pia ni fowarding company nzuri sana (thanks tu Mwl.RCT), nimepitia site yao na huona wana policy nzuri sana, cha kwanza ni sales tax-free U.S. online shopping yaani punguzo la kodi ya kufanya manunuzi marekani, hii inapelekea huduma zao kuwa nafuu zaidi,pia wana ushirika na shipping courie DHL na FEDEX hivyo kufanya huduma zao kuwa rahisi zaidi.pia wanakupa habari kuhusu discount za masoko mbalimbali kama myus..

3: BORDERLINX
Link: Buy in the USA, ship to Belgium with Borderlinx - Hawa pia ni wazuri sana na hawana tofauti sana na stackry ... Wanawiana ingawa ni competitors wakubwa hivyo inakupa urahisi wa kuwatumia..Hawa pia hawana registration fee na wanakupa option tofauti tofauti za kutumiwa mzigo wako.

4: SHIPITO
Link: USA Address & Mail Forwarding Shipito.com | English - Hii pia ni kampuni kongwe ya fowarding na wao gharama zao ni nafuu sana ingawa wanapokea malalamiko mengi sana kutoka kwa wateja wao ukiangalia kwenye forums nyingi.ila kiujumla ni wazuri kwasababu malalamiko ni madogo kulinganisha na ufanisi na pia wanajua na ni wazoefu sana na kazi yao

5: STACKRY
Link: Stackry - US shopping, global shipping - Hii nayo haina tofauti na myus isipokuwa hawa wao hawana kiasi cha kulipia kujiunga nao na wao pia wanakupa option nyingi za kutumia mizigo yako na mabo yao pia ni mazuri kulinganisha na comment wanazopokea kutoka kwa wateja wao. waungwana ni hayo tu niliyo nayo, kazi kwenu ni kufanya utafiti na pia kuangalia na kuchunguza mabo kabla ya kuchukua uamuzi.

STACKRY na BORDERLINX walikuwa recommended sana na wanasifiwa mno angalia hii link -http://tech-vise.com/10-parcel-forwarding-services-for-international-shoppers/ pitia hizo websites na ujionee mwenyewe chagua moja na utazame kama wanakufaa.

HUU NI MTAZAMO WANGU BINAFSI WAKUU , Please evaluate kindly.

Nilikuwa nataka kuonyesha steps ila naona thread haitoshi maana nimeagiza mzigo na nimechukua hatua zote ili mpate kuona ila I think there are limits..

Help Mwl.RCT
Mkubwa,nimejaribu kujiunga na paypal lkn nimekwama pale sehemu ya kujaza adress line 1 na adress line 2. Hizo adress line ndo zp?
 
Nauza Betri za Energizer zinazotumika kwenye Radio, Rimoti za TV, magetin na kwenye magari, pia kwenye tochi, vipimo vya Maabara, vipimo vya uzito na kadhalika


Tupo Calico complex, Tazara Dar
Bei ni poa kabisa
Nipigie 0784112347
0769017151
Unaletewa Popote ulipo
IMG-20190917-WA0001.jpeg
Screenshot_20190914-074305.jpeg
IMG-20190916-WA0019.jpeg
IMG-20190916-WA0021.jpeg
 
- Je ni kampuni kani imesafirisha bidhaa yako?
- Fanya mawasiliano nao, Kuna taarifa wanahitaji, ili taratibu zingine zifuate.
kwenye track nimetumiwa tracking Number
kwenye shipment wameandika
Logistics company:
AliExpress Standard Shipping

Niende nikaulize posta au?
 
129 Reactions
Reply
Back
Top Bottom