Mimi natumia alibaba na naagiza kila mwezi mizigo ka meli au ndege Inategemea na aina ya mizigo. SI KWELI KAMA kutuma western ni tatizo, muda wote mpaka sasa natumia western union na pia wire transfer. Kwa zaidi ya 80% suppliers wa Alibaba ni halisi hakuna Utapeli hata kidogo. Kuna, ni wewe tu how you negotiate nao na aina ya bidhaa utakazo. Their trustworthy kabisa, vitu muhimu unaangalia kwa supplier pale alibaba ni kuwa ana nembo ya trade assurance, pili kama ni gold suppluer wa miaka kadhaa kuanzia mmoja nk. Endelea kufanya biashara.... More info itanicheki kwa wakati wako..
Kaka naomba na mm muongozo nahitaji kuagiza kitu kupitia ali baba my namba ni 0712262322
 
Mimi natumia alibaba na naagiza kila mwezi mizigo ka meli au ndege Inategemea na aina ya mizigo. SI KWELI KAMA kutuma western ni tatizo, muda wote mpaka sasa natumia western union na pia wire transfer. Kwa zaidi ya 80% suppliers wa Alibaba ni halisi hakuna Utapeli hata kidogo. Kuna, ni wewe tu how you negotiate nao na aina ya bidhaa utakazo. Their trustworthy kabisa, vitu muhimu unaangalia kwa supplier pale alibaba ni kuwa ana nembo ya trade assurance, pili kama ni gold suppluer wa miaka kadhaa kuanzia mmoja nk. Endelea kufanya biashara.... More info itanicheki kwa wakati wako..
Mkuu nilikuwa nahitaji kununua mashine fulani kutoka alibaba....but naona kama nimekwama kwenye suala la usafirishaji maana kwenye calculation zao za kwenye mtandao inaonekana kama vile inakuwa bei ya mashine ni cheap kuliko ya usafirishaji coz mashine yenyewe ni kama $650 but wakifanya calculation za usafirishaji inaonekana kama vile transportation itacost kama $1300. Naomba nijuze hapa kwenye usafirishaji huwa mnatumia utaratibu gani. Nawakilisha mkuu
 
Kuna issue inanitatiza!
Ukitaka kutumiwa mzigo wako ulionunua mfano duka la Marekani,ni lazima mzigo upitie Forward company then courier yeyote mf. Myus..Lakin nimejaribu kupitia baadhi ya suppliers wa Alibaba group nimeona hawana forward companies,wenyewe wanasema wanashipp bidhaa kwa kupitia courier mf. Fedex,DHL au EMS.

Je,hapa ni mim tu ni mbumbumbu au kunakitu sijakielewa..
Kwa wenye exposure,msaada tafadhali!!!
 
Kuna issue inanitatiza!
Ukitaka kutumiwa mzigo wako ulionunua mfano duka la Marekani,ni lazima mzigo upitie Forward company then courier yeyote mf. Myus..Lakin nimejaribu kupitia baadhi ya suppliers wa Alibaba group nimeona hawana forward companies,wenyewe wanasema wanashipp bidhaa kwa kupitia courier mf. Fedex,DHL au EMS..Je,hapa ni mim tu ni mbumbumbu au kunakitu sijakielewa..
Kwa wenye exposure,msaada tafadhali!!!

unataka kuagiza mzigo wa aina gani na maybe ni wa ukubwa gani!?!?
 
Ukitaka kutumiwa mzigo wako ulionunua mfano duka la Marekani,ni lazima mzigo upitie Forward company then courier yeyote mf. Myus..
#1. Sio lazima, waweza kutumwa moja kwa moja.
Lakin nimejaribu kupitia baadhi ya suppliers wa Alibaba group nimeona hawana forward companies,wenyewe wanasema wanashipp bidhaa kwa kupitia courier
#2. Wauzaji alibaba hutuma moja kwa moja Tanzani (africa). Kwa kutumia shipping agent tajwa hapo juu

Angalizo:
- Kwa kuwa mzigo wako ni mkubwa 25kg. shipping cost ni kubwa iwapo utatumia courier agent tajwa hapo juu
- Omba seller atume mzigo kwa njia ya Posta.
- Sabau [1] Utaokoa kiasi kikubwa cha fedha, [2] Hiyo fedha utakayo okoa sehemu yake utatumia kulipia ushuru
 
#1. Sio lazima, waweza kutumwa moja kwa moja.

#2. Wauzaji alibaba hutuma moja kwa moja Tanzani (africa). Kwa kutumia shipping agent tajwa hapo juu

Angalizo:
- Kwa kuwa mzigo wako ni mkubwa 25kg. shipping cost ni kubwa iwapo utatumia courier agent tajwa hapo juu
- Omba seller atume mzigo kwa njia ya Posta.
- Sabau [1] Utaokoa kiasi kikubwa cha fedha, [2] Hiyo fedha utakayo okoa sehemu yake utatumia kulipia ushuru
Nimekupa vizur sana,asante sana mdau!
 
Mimi sunawahi tumia eBay, natumia Alibaba tu. Ukiwa akibaba kila supplier wana nembo ZA trade assurance na limit ya pesa alibaba anazikugurantee kufanya nae kazi., pia ni vema udeal na supplier ambaye ni gold member, ikiwezekana supplier akutumie video clip ya office yake, na ukitaka bei nzuri deal na supplier ambaye ni manufucturer, na wanajionesha pale.

Ndio ni kweli ukituma pesa alibaba wao wenyewe ndipo wamlipe suppllier sawa, but mzunguko mrefu labda kama huna haraka, na pia ukimtumia supplier mwenyewe sawa na nirahisi sana kwa uharaka. Mimi Mara zote namtumia supplier tu. Na Mimi na washirika wangu hatujawahi experience utapeli wowote. Anyway more ukihitaji zaidi nicheki...
Check me 0766530478 kama hutojali Kuna vitu ningependa kujua zaid
 
Mkuu nilikuwa nahitaji kununua mashine fulani kutoka alibaba....but naona kama nimekwama kwenye suala la usafirishaji maana kwenye calculation zao za kwenye mtandao inaonekana kama vile inakuwa bei ya mashine ni cheap kuliko ya usafirishaji coz mashine yenyewe ni kama $650 but wakifanya calculation za usafirishaji inaonekana kama vile transportation itacost kama $1300. Naomba nijuze hapa kwenye usafirishaji huwa mnatumia utaratibu gani. Nawakilisha mkuu
Kuna watu wanaosafirisha kwa gharama ndogo sana, achana na huyo, mwambie utalipia tu hiyo 650$ then kuna mtu atampelekea machine na tutakuletea mpaka home kwa si zaidi ya $500 inategemea na ukubwa wake. Nipe details za kutosha.
 
mi nimemwelewa huyo muuzaji..

itakuwa amekupa gharama ya express.. yaani airfreight... mara nyingi ni kubwa kuliko bei ya mashine..

mwambie akupe sea freight bei gani? kusafirisha kwa meli ni nafuu sana.

na pia lazima ujue ukubwa wa hiyo mashine.. ujazo wake

Mkuu nilikuwa nahitaji kununua mashine fulani kutoka alibaba....but naona kama nimekwama kwenye suala la usafirishaji maana kwenye calculation zao za kwenye mtandao inaonekana kama vile inakuwa bei ya mashine ni cheap kuliko ya usafirishaji coz mashine yenyewe ni kama $650 but wakifanya calculation za usafirishaji inaonekana kama vile transportation itacost kama $1300. Naomba nijuze hapa kwenye usafirishaji huwa mnatumia utaratibu gani. Nawakilisha mkuu
 
  • Katika list ya forwarding company ongeza hii " ComGateway"
  • Iko safi zaidi - ukilinganisha na myusu.com
  • Tena wana application yao ya android inayokuwezesha kufanya ulinganifu wa bei toka masoko tofauti tofauti.
  • Iko salama zaidi, hakuna charges zilizojificha, Kujiunga ni free JZHOELO
comgateway.png
Ko ndgu ipi ni best amng the above
 
Salaam wadau nilikua nauliza kama kuna njia ya kushop online shop za UAE kama SOUQ....
 
Guys nmecheki kwenye shipping calculator kwa baadhi ya sites zilizotajwa hapo juu ni gharama sana kuship even a package ya 0.5 kg, mfano Comgateway gharama ya kuship 0.5kg ni around 77 USD
 
Imekuwa ni shida sana kwa watanzania wengi kununua bidhaaa katika masoko haya ya mtandaoni kwani mengi huwa hayakupi fursa ya kutumiwa mzigo wako moja kwa moja Tanzania. Baadhi ya thread zilianzishwa na zimeelezea mengi sana kuhusiana na manunuzi haya ya mtandaoni, ila tulipata ufumbuzi mdogo.

Nimejaribu kupitia pitia forums nyingi nichanganue namna mbadala ya kupata mizigo bila ya kutumia gharama nyingi. hii ni kwa kutumia FOWARDING COMPANIES ambazo kazi yake ni;

1: Kukupatia anuani ya Marekani (au popote iliopo ila nashauri marekani au uingereza UK) au US Shipping Address

2: Kupokea mzigo kwenye soko ulilotumia (eidha amazon,ebay au lolote lile lisilo ship Tanzania)

3: Kukutumia mzigo wewe hapo ulipo kwa wakala kama DHL,FEDEX,UPS,USPS NK baada ya kujua kazi ya fowarding company unahitaji kuwa na vigezo vifuatavyo (kwa wageni wasiofahamu/hawajapitia previous threads:

1: CREDIT CARD (KADI YA BENKI) INAYOFANYA ONLINE PURCHASES;
Hii inapatikana almost bank zote hapa Tanzania (kasoro NMB sina uhakika), ni kadi yeyote ya visa au mastercard unachotakiwa ni kwenda kwenye tawi la benki yako na kuomba fomu ya kuruhusu kadi yako ifanye malipo ya mtandaoni(online purchases) na mara nyingi huchukua maximum 24hours kuactivate.

2: KUJIUNGA NA PAYPAL
Hiii ni kampuni inayolinda malipo yako kwa kutomuonesha muuzaji details (nyaraka) za kadi yako kama number na css ambayo vitampa muuzaji access ya kuchukua pesa zako. Ila kwa paypal utalindwa na kurudishiwa pesa pale panapotokea shida au huduma mbaya.

3: KUJIUNGA NA FOWARDING COMPANY

Hii hatua ni ya wewe kwenda kwenye website (tovuti) za hizi fowarding company na kujiunga (sighnup) nazo/nayo ili zianze kukupatia huduma... nitaelezea chini zaidi kuhusu ipi ni ipi na huduma zao zikoje na faida na hasara za kila moja ili ujichagulie wewe mwenyewe binafsi

4: KUTAMBUA SOKO BORA LENYE HUDUMA NZURI(ONLINE MARKET)
Hapa tunazungumzia website za masoko kama ebay,amazon, bestbuy, apple.com, dell.com, toshiba.com nk.. masoko haya ndipo utakapo nunua bidhaa yako.

PROCESS NZIMA KUANZIA UNANUNUA MPAKA MZIGO UNAKUFIKIA IKOJE?


Hii iko hivi....

1: Ingia katika soko lako ulilolichagua au unalopendelea, hapa nasuggest kutumia sana amazon(ndilo ninaloliamini) amazon ukiingia utakuta bidhaa nyingi ila kuwa makini kuchukua zile bidhaa zilizo na alama ya prime chini...alama hiyo inamaanisha kuwa huo mzigo unauzwa, utapakiwa, na kutumwa na amazon wenyewe, so no utapeli hapo, yani u get what u wanted.

2: Nunua na kuagiza kitu kwenda kwenye address ya fowarding company ulioichagua, hivyo mzigo ulioununua utaenda moja kwa moja kwenye company yako, wao wakishaupata watakutumia e-mail uthibitishe au uchague courier wa kukutumia mzigo wako, hapo ndio utachagua either dhl,ups,fedex nk.wao watakutumia na kuchukua kiasi chao cha pesa ya huduma na kukutumia mzigo pamoja na kukupatia tracking number ya kujua mzigo wako ulipo na utaupokea vyema.

FOWARDING COMPANIES ZENYEWE:

1: MYUS.COM link- MyUS.com - #1 International Shipping, Mail and Package Forwarding Service - MyUS.com. Hii ni company niliyoitumia na nina expirience nayo ya mizigo miwili, hawa ni waaminifu wana charge pesa kidogo na huwa hawachukui muda kukutumia mzigo wako. yaani unafika leo hata ukitaka utumwe leo unatumwa, na utafika upesi sana bila ya zengwe lolote.

Ubaya wao: wanatumia sana DHL ambayo kwa mizigo mikubwa ni gharama sana kwa mtanzania wa kawaida, kiasi cha dola kumi kujiunga na huduma zao

Uzuri wao:
watakutumia mzigo hata kama utakuwa hauna pesa kwenye account yako, watakujulisha ni duka lipi lina discount ya kutumia huduma zao, watakukumbusha kulipa deni lao, utapewa muda wa miezi miwili kulipa pesa yao,

2: COMGATEWAY
Link: Shop US Stores and Ship Internationally | comGateway - Hawa pia ni fowarding company nzuri sana (thanks tu Mwl.RCT), nimepitia site yao na huona wana policy nzuri sana, cha kwanza ni sales tax-free U.S. online shopping yaani punguzo la kodi ya kufanya manunuzi marekani, hii inapelekea huduma zao kuwa nafuu zaidi,pia wana ushirika na shipping courie DHL na FEDEX hivyo kufanya huduma zao kuwa rahisi zaidi.pia wanakupa habari kuhusu discount za masoko mbalimbali kama myus..

3: BORDERLINX
Link: Buy in the USA, ship to Belgium with Borderlinx - Hawa pia ni wazuri sana na hawana tofauti sana na stackry ... Wanawiana ingawa ni competitors wakubwa hivyo inakupa urahisi wa kuwatumia..Hawa pia hawana registration fee na wanakupa option tofauti tofauti za kutumiwa mzigo wako.

4: SHIPITO
Link: USA Address & Mail Forwarding – Shipito.com | English - Hii pia ni kampuni kongwe ya fowarding na wao gharama zao ni nafuu sana ingawa wanapokea malalamiko mengi sana kutoka kwa wateja wao ukiangalia kwenye forums nyingi.ila kiujumla ni wazuri kwasababu malalamiko ni madogo kulinganisha na ufanisi na pia wanajua na ni wazoefu sana na kazi yao

5: STACKRY
Link: Stackry - US shopping, global shipping - Hii nayo haina tofauti na myus isipokuwa hawa wao hawana kiasi cha kulipia kujiunga nao na wao pia wanakupa option nyingi za kutumia mizigo yako na mabo yao pia ni mazuri kulinganisha na comment wanazopokea kutoka kwa wateja wao. waungwana ni hayo tu niliyo nayo, kazi kwenu ni kufanya utafiti na pia kuangalia na kuchunguza mabo kabla ya kuchukua uamuzi.

STACKRY na BORDERLINX walikuwa recommended sana na wanasifiwa mno angalia hii link -http://tech-vise.com/10-parcel-forwarding-services-for-international-shoppers/ pitia hizo websites na ujionee mwenyewe chagua moja na utazame kama wanakufaa.

HUU NI MTAZAMO WANGU BINAFSI WAKUU , Please evaluate kindly.

Nilikuwa nataka kuonyesha steps ila naona thread haitoshi maana nimeagiza mzigo na nimechukua hatua zote ili mpate kuona ila I think there are limits..

Help Mwl.RCT
Umenifungua macho nilokuwa natumia njia ndefu sana
 
Back
Top Bottom