Jifunze na uzijue nyayo za kidigitali, tambua namna ya kuzidhibiti uwapo mtandaoni

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
1597519083777.png
Nyayo za Kidigitali au Digital Footprint hizi ni taarifa za kipekee zinazokusanywa kutoka kwa mtumiaji wa Mtandao anapofanya shughuli mbalimbali kwenye mtandao, anapofanya mawasiliano, miamala katika vifaa au majukwaa ya mtandaoni

Taarifa hizi zinaweza kutumika kufuatilia vitu anavyofanya na kupendelea mtu anapokuwa mtandaoni. Aidha, ifahamike kuwa taaifa hizi zikisha wekwa mtandaoni husalia hapo kwa muda mrefu napengine zikawa ni za kudumu. Data hizi zinajumuisha mambo yote unayoyafanya uwapo mtandaoni, kama vile mambo unayoandika, picha zako, video na miamala unayofanya

Uzi huu umelenga kukufahamisha kuhusu hizo Digital Footprint ili uweze kuzidhibiti na pengine kuzipunguza

Njia kubwa ya ukusanyaji wa hizi nyayo za kidigitali ni kwa kupitia kitu kinaitwa Cookies ambazo hujumuisha eneo ulilopo, kifaa unachokitumia, vitu unavyopenda kuvitafuta, tovuti na mitandao unayotembelea, aina ya kifaa unachotumia, browser unayoitumia, eneo ulilopo, barua pepe, bamba ya simu, picha zako na taarifa nyingine nyingi unazoziweka wewe au wanazoweka wengine.

Digital footprint zinaweza kusema nini kuhusu wewe?

Inashauriwa na inapendeza ukiwa na nyayo za kidigitali zilizobeba taarifa chanya kukuhusu kwasababu taarifa hizo ndio hubeba uwakilishi wa wewe ni nani hasa katika mitandao. Ikitokea Mtu akakutafuta au akatafuta jina lako basi apate taarifa chanya kukuhusu

Digital footprint zinaweza kutumika kuamua hatma yako katika nyanja mbalimbali za Maisha. Mfano: waajiri wanaweza kuzitumia kuamua kama wakuajiri au la, wasimamizi na watekelezaji wa sharia wanaweza kuzitumia, unapoomba Visa ya kuingia taifa tofauti na lako zinaweza pia kutumika kuamua kama upewe au unyimwe. Kuwa makini…

1597508228831.png

Je, kuna aina ngapi za Digital Footprints?

Nyayo za hiyari za Kidigitali | Active digital footprints

Hizi hujumuisha taarifa zote ambazo unaziacha wewe mwenyewe kwa kujua pale unapotumia majukwaa na tovuti mbalimbali. Kwa mfano kila unachokiandika na kukiweka kwenye kurasa zako za mitandao ya kijamii hubaki na hutambulika kama Nyayo hai za Kidigitali | Active digital footprints

Hapa nimeweka mifano ya Active Digital Footprints.


  • Unapoweka maudhui kwenye Facebook, Instagram, Snapchat, Twitter, na mitandao mingine ya kijamii
  • Kujaza fomu za mtandaoni na kukubali uwe unatumiwa taarifa kwa njia ya emai kwa jumbe fupi kupitia simu
  • Unapokubali kuweka Cookies kwenye kifaa chako pindi unapoulizwa na mtoa huduma kupitia Browser yako.

Nyayo zisizo za hiyari za Kidigitali | Passive digital footprints

Hizi ni digital footprints ambazo zinachukuliwa kutoka kwako bila ya kujua lengo lake ni nini na bila ya wewe kujua kama zimechukuliwa

Kwa mfano: Kuna tovuti zinachukua taarifa za utembeleaji wako katika tovuti husika na kuziweka kama kumbukumbu kuhusu wewe. Mchakato huu umefichwa na ni wa siri. Matokeo yake taarifa zako hutumika kwa ajili ya matangazo na tafiti mbalimbali

Hapa kuna mifano kadhaa ya passive digital footprints.
  • Tovuti zote ambazo zinakusanya cookies kutoka kwenye kifaa chako bila ya kukutaarifu
  • Application na tovuti zinazotumia Location bila ya kukutaarifu
  • Watangazaji kupitia mitandao ya kijamii. Watu wengi hupokea matangazo kwenye mitandao ya kijamii kwa vitu walivyotafuta kwenye mitandao tofauti na sehemu waliyopokea tangazo. Mfano: Umetafuta kitu kupitia Google lakini wanapokea matangazo kwenye Instagram
Je, ni njia zipi unaweza kuzitumia kulinda Nyayo zako za Mtandaoni?

1597519010461.png

1. Ingia kwenye Search Engen kama vile Google, Bing, Start Page au DuckDuckGo kisha search jina lako. Angalia matokeo yanasema nini kuhusu wewe? Je, yamejazwa taarifa chanya? Aidha, unaweza kuset kwenye google kila linapoandikwa jina lako basi wewe unapata notification ili uweze kujua nini kimeandikwa kuhusu wewe ili kama si taarifa chanya uweze kufuatilia uondoaji wake.

Jinsi ya Kuset : How to Set up Google Alerts (and Use It to Grow Your Business)

2. Angalia upya settings zako za faragha kwenye kifaa chako na browser na application unazozitumia. Hakikisha hazikusanyi taarifa zako kama location, namba ya simu, picha na videos

3. Tengeneza Nywila / passwords imara, hii itakusaidia kulinda vifaa vyako na kuepusha akaunti na kifaa chako kuingiliwa na wahalifu wa mtandaoni wanaoweza kuiba au kuchafua digital footprints zako

4. Hakikisha software na applications zote ziko up to date. Hii itasaidia kuongeza usalama zaidi na kukuepusha na hatari za mtandaoni.

5. Jijengee utamaduni wa kukagua kila unachokiandika na kukifanya mtandaoni hii itakusaidia kujijengea taswira nzuri na yenye manufaa kwako
 
Asante sana aisee, nlikuwa sielewi kuhusu hilo suala la Digital footprint lakini nashukuru hapa umelitolea ufafanuzi wa kina.

Hakika mitandao hii ni suala ambalo kwa pamoja tunapaswa kuwa nalo makini na kuhakikisha tunaacha taarifa chanya kuhusu sisi.

Ntajitahidi nifuate ushauri uliotupa ili uzichunguza taarifa zangu kutokana na nyayo nilizoziacha. Asante Mkuu
 
Ahsante
Nimeshacreate Google Alert naamini wazee wa kutrack wataimba haleluya.

Mkuu shukrani sana
 
Ni muhimu sana watu kuangalia matendo na mienendo yao katika mitandao maana siku hizi tumefikia kuishi katika mazingira ambayo mtu akitaka kujua kitu au kupata taarifa kuhusu mtu mwengine basi jambo la kwanza analofanya ni kuingia google na kusearch jina la mtu anayetaka kujua taarifa zake. Kama hauna umakini katika kuhakikisha uko katika mstari mnyoofu basi taarifa zako za kidigitali zinaweza sababisha ukapishana na fursa kubwa maishani mwako.
 
Aisee hii ni thread bora kwa kipindi hiki cha kidigitali, nimejaribu kuangalia habari zangu aisee ni aibu. Nimeamua kuset google notification na kurclear all data n cookies kwenye browser ya Siku ninayoitumia.
 
Nyayo za Kidigitali au Digital Footprint hizi ni taarifa za kipekee zinazokusanywa kutoka kwa mtumiaji wa Mtandao anapofanya shughuli mbalimbali kwenye mtandao, anapofanya mawasiliano, miamala katika vifaa au majukwaa ya mtandaoni

Taarifa hizi zinaweza kutumika kufuatilia vitu anavyofanya na kupendelea mtu anapokuwa mtandaoni. Aidha, ifahamike kuwa taaifa hizi zikisha wekwa mtandaoni husalia hapo kwa muda mrefu napengine zikawa ni za kudumu. Data hizi zinajumuisha mambo yote unayoyafanya uwapo mtandaoni, kama vile mambo unayoandika, picha zako, video na miamala unayofanya

Uzi huu umelenga kukufahamisha kuhusu hizo Digital Footprint ili uweze kuzidhibiti na pengine kuzipunguza

Njia kubwa ya ukusanyaji wa hizi nyayo za kidigitali ni kwa kupitia kitu kinaitwa Cookies ambazo hujumuisha eneo ulilopo, kifaa unachokitumia, vitu unavyopenda kuvitafuta, tovuti na mitandao unayotembelea, aina ya kifaa unachotumia, browser unayoitumia, eneo ulilopo, barua pepe, bamba ya simu, picha zako na taarifa nyingine nyingi unazoziweka wewe au wanazoweka wengine.

Digital footprint zinaweza kusema nini kuhusu wewe?

Inashauriwa na inapendeza ukiwa na nyayo za kidigitali zilizobeba taarifa chanya kukuhusu kwasababu taarifa hizo ndio hubeba uwakilishi wa wewe ni nani hasa katika mitandao. Ikitokea Mtu akakutafuta au akatafuta jina lako basi apate taarifa chanya kukuhusu

Digital footprint zinaweza kutumika kuamua hatma yako katika nyanja mbalimbali za Maisha. Mfano: waajiri wanaweza kuzitumia kuamua kama wakuajiri au la, wasimamizi na watekelezaji wa sharia wanaweza kuzitumia, unapoomba Visa ya kuingia taifa tofauti na lako zinaweza pia kutumika kuamua kama upewe au unyimwe. Kuwa makini…

Je, kuna aina ngapi za Digital Footprints?

Nyayo za hiyari za Kidigitali | Active digital footprints

Hizi hujumuisha taarifa zote ambazo unaziacha wewe mwenyewe kwa kujua pale unapotumia majukwaa na tovuti mbalimbali. Kwa mfano kila unachokiandika na kukiweka kwenye kurasa zako za mitandao ya kijamii hubaki na hutambulika kama Nyayo hai za Kidigitali | Active digital footprints

Hapa nimeweka mifano ya Active Digital Footprints.


  • Unapoweka maudhui kwenye Facebook, Instagram, Snapchat, Twitter, na mitandao mingine ya kijamii
  • Kujaza fomu za mtandaoni na kukubali uwe unatumiwa taarifa kwa njia ya emai kwa jumbe fupi kupitia simu
  • Unapokubali kuweka Cookies kwenye kifaa chako pindi unapoulizwa na mtoa huduma kupitia Browser yako.

Nyayo zisizo za hiyari za Kidigitali | Passive digital footprints

Hizi ni digital footprints ambazo zinachukuliwa kutoka kwako bila ya kujua lengo lake ni nini na bila ya wewe kujua kama zimechukuliwa

Kwa mfano: Kuna tovuti zinachukua taarifa za utembeleaji wako katika tovuti husika na kuziweka kama kumbukumbu kuhusu wewe. Mchakato huu umefichwa na ni wa siri. Matokeo yake taarifa zako hutumika kwa ajili ya matangazo na tafiti mbalimbali

Hapa kuna mifano kadhaa ya passive digital footprints.
  • Tovuti zote ambazo zinakusanya cookies kutoka kwenye kifaa chako bila ya kukutaarifu
  • Application na tovuti zinazotumia Location bila ya kukutaarifu
  • Watangazaji kupitia mitandao ya kijamii. Watu wengi hupokea matangazo kwenye mitandao ya kijamii kwa vitu walivyotafuta kwenye mitandao tofauti na sehemu waliyopokea tangazo. Mfano: Umetafuta kitu kupitia Google lakini wanapokea matangazo kwenye Instagram
Je, ni njia zipi unaweza kuzitumia kulinda Nyayo zako za Mtandaoni?


1. Ingia kwenye Search Engen kama vile Google, Bing, Start Page au DuckDuckGo kisha search jina lako. Angalia matokeo yanasema nini kuhusu wewe? Je, yamejazwa taarifa chanya? Aidha, unaweza kuset kwenye google kila linapoandikwa jina lako basi wewe unapata notification ili uweze kujua nini kimeandikwa kuhusu wewe ili kama si taarifa chanya uweze kufuatilia uondoaji wake.

Jinsi ya Kuset : How to Set up Google Alerts (and Use It to Grow Your Business)

2. Angalia upya settings zako za faragha kwenye kifaa chako na browser na application unazozitumia. Hakikisha hazikusanyi taarifa zako kama location, namba ya simu, picha na videos

3. Tengeneza Nywila / passwords imara, hii itakusaidia kulinda vifaa vyako na kuepusha akaunti na kifaa chako kuingiliwa na wahalifu wa mtandaoni wanaoweza kuiba au kuchafua digital footprints zako

4. Hakikisha software na applications zote ziko up to date. Hii itasaidia kuongeza usalama zaidi na kukuepusha na hatari za mtandaoni.

5. Jijengee utamaduni wa kukagua kila unachokiandika na kukifanya mtandaoni hii itakusaidia kujijengea taswira nzuri na yenye manufaa kwako
Nitarudi
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom