#COVID19 Jifunze matumizi sahihi ya Barakoa ujikinge na #COVID19

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
2338387_9303D470-96DA-4C5A-8021-5C534339B819.jpeg

MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA MATUMIZI YA BARAKOA

Uvaaji wa barakoa au “mask” ni moja ya njia za kujikinga na maambukizi ya magonjwa mbalimbali ya kuambukiza. Katika kudhibiti kusambaa kwa Virusi vya #Corona

Barakoa inapaswa kuvaliwa endapo unakohoa au kupiga chafya, mtu wa karibu yako ana dalili za #COVID19, uko kwenye mikusanyiko ya watu au muda wote kama ugonjwa umeshatapakaa kwenye jamii

Matumizi ya barakoa yaende sambamba na kunawa mikono kila mara kwa maji tiririka. Barakoa si mbadala wa kunawa mikono

Barakoa ivuliwe na kutupwa mara tu inapoloa au masaa 4 yakipita. Barakoa za kutumiwa mara moja zisitumiwe zaidi ya hapo

Barakoa ivuliwe kwa kushikwa kwenye nyuma (kwenye kamba) na kutupwa kwenye eneo la taka lililo na mfuniko au mbali na makazi ya watu bila kushika eneo la katikati ili kuepuka kuhamisha maambukizi

Mikono itakaswe kwa maji tiririka na sabuni au kitakasa mikono mara baada ya kutupa barakoa kabla ya kufanya jambo lolote

20200421_235148_0000.png

NI WAKATI GANI NATAKIWA KUVAA BARAKOA?

Wataalam wanaeleza kuwa Virusi vya Corona vinaenea kutoka kwa Mtu mmoja kwenda kwa mwingine pale mmoja wao anapokuwa amepata maambukizi

Mtu mwenye maambukizi anaweza kumuambukiza mwingine pale anapokohoa, kupiga chafya na majimaji yatakayomtoka muathirika na kumrukia Mtu mwingine

Maelekezo ya Uvaaji wa Barakoa;

Vaa Barakoa: Unapolazimika kwenda kwenye maeneo yenye mkusanyiko wa watu wengi. Aidha, kama huna sababu ya kwenda maeneo haya unashauriwa kukaa nyumbani kwako

Vaa Barakoa: Watu wenye maambukizi pia wanashauriwa kuvaa Barakoa ili kuwalinda wengine dhidi ya maambukizi ya #COVID19

Vyanzo: WHO na John Hopkins Medicine
 
mi sipendi mshike mshike hizi kila wakati mambo mapya utafikiri tutaishi milele
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom