Jifunze kutunza position yako!!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,462
21,334
Bwana yesu asifiwe wapendwa
habarini za jumapili ..natumaini mmerudi salama toka kanisani,mlioshindwa mungu awawezeshe wiki ijayo kuwepo madhabahuni..nimewiwa kukumbushana jambo hili si jipya bali vyema kujua na kuweza kuishi kwa furaha jinsi ya ""kutunza position yako"""
adam alipokula lile tunda aliulizwa na mungu adam uko wapi akajibu niko uchi,,akuulizwa umefanya nini ..hii inatufundisha mungu akijua adam ameshapoteza position yake kwenye bustan ya eden ndio maana akashindwa hata kujibu kwa ufasaha swali aliloulizwa..
Ester wa modekai alipoteza nafasi yake kwa mfalme
turudi kwetu sie tuliopo duniani,ndugu zangu wengi sana wanauwezo mkubwa wa kusali kufunga na kuomba wakiwa awana kazi mungu awape kazi nzuri lakini wengi kazi nzuri wanayopata awajui jinsi ya kuilinda wakijua wameshapata akuna mwingine ten..hiili ni kosa kubwa sana sana na wengi wamepoteza nafasi zao nzuri aijalishi umeokoka ujaokoka kama ujui jinsi ya kutunza position yako watu watakusaidia kukutunzia...

Kuna walokole wengi wanapata kazi nzuri sana lakini kutokana na shetan kuwaingia wanafika hali ya kuwagandamiza watu hata kama ni haki zao hili mradi watunze nafasi zao..hii sio nzuri tunaitaji mungu atupe njia halisi ya kupingana na vizingiti kama hivi vinavyokufanya ushindwe kuona ufalme wa mungu..

Turudi kwenye lililotuweka hapa swala la mapenzi
usione umebahatika kumuoa huyo binti ukahisi wewe ni mzuri kuliko wote la hasha huyo mungu alikuweka kwa ajili yake na naomba tujue wale wote tunaoenda kuoa ama tuliooa ama kuolewa wengi wanasali sana sana mungu awape mke mwema ama mume mwema lakini awaombi mungu awasaidie kujua jinsi gani ya kuwatunza wenza wao..na hili limefany shetan kusambaratisha ndoa nyingi sana sana na leo mahakamani kila baada ya kesi 10 ,1 ya ndoa...
Unaposali upate mwenza aliemwema kumbuka mungu akuongoze ujue jinsi gani ya kumtunza na kuishi pamoja..aijalishi ulizaliwa kwenye kichaka aijalishi baba na mama walitunga mimba yako chooni la hasha kinachotakiwa ni wewe jinsi gani ujue kutunza na kufanya yale mungu aliokuitia hapa duniani

lazima ujue mpaka unampata huyo wako wengi waliohonga hata na magri lakiniwaliishia kuambiwa muda bado..na hata wanapojua ameolewa ama ameoa ujue wako nje wanapigana kuhakikisha akuna amani kwenye ndoa zenu..kuna watu awaachi kuloga hata ukioa mpka waasikie mko mahakamani mnagaiana talaka ndio anatulia...

Nini maanake naomba tujue jinsi gani ya kutunza position tunazopata siweezi kusema unaitwa mume ama mke kwa bahati mbaya la hasah mapenzi ya mungu uwe hivyo lazima ujue jinsi gan ya kutunza hiyo position..wanaume wengi wanaoa awajui majukumu yao nini nini na mwisho kupoteza nafasi waliopewa ..leo hii wanawake wengi wanafanya majukumu ya wanaume..amka tunza position yako

wale mliooana ni wakati wenu sasa kuendeleea kuomba mungu awalinde sehemu zenu za ndoa muweze kuishi na amani na upendo..hali sii kwenye ndoa tu jifunze kutunza nafasi yako na za ofisini pia..ukiwa unaomba mke ama mume mwambie mungu akusaidie ujue jinsi gani ya kusihi nae ..usikimbilie tu oohh nimechoka nimechoka wakati ujafanya jukumu lako
usisubiri kufukuzwa kazi ndio uanze kumwambia mungu naomba nipe sehemu sahihi sahihi hiyo ulioondolewa tatizo umeshindwa kuitunza kuiombea na mwisho utaishia kuhama kila ofisi..same to mapenzi usipojua kutunza ndoa yako utaishia kubadilisha size kama mwehu

mungu awape nguvu ya maombi muweze kutunza nafasi zenu mlizokuwa nazo kwenye ndoa ..kazini na makanisani mkawe ushuhuda wa roho mtakatifu

mungu awabariki kwa mliocchoka kusoma basi kidogo mkakifanyie kazi
 
Amen Mpendwa, kweli sijaenda ibadani leo naomba nisamehewe tu.
 
Nimeipenda hii, tuwajibike huku tukimkumbuka Mungu na sio tusubiri mambo yakiharibika ndo tuanze kupiga magoti na kufunga!! Lol!
 
Asante p.ddy kwa kushare ujumbe mzur namna hii, kweli 2kumbuke ku2nza position zetu, vinginevyo ukijisahau utalala mojakwamoja na hauta amka. wakat ndo huu
 
Japo nimeishia katikati naona wa2 wanasema asante ngoja na mimi nifuate mkumbo! .......asante pdidy.
 
Pdidy
Asante sana kwa kutukumbusha,yote ni kweli wala hamna cha kupunguza ubarikiwe sana pia Roho mtakatifu azidi kukupa mafunuo zaidi ili tuelimishane zaidi.Ila nimejifunza kitu hapa Jf watu wengine hawaamini kuwa Mungu anahusika na mahusiano hasa ya ndoa hawajui kuwa Mungu ndiye aliyeyaweka na pia anajishugulisha mno pale anapoachiwa aongoze.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom