AbuuMaryam
JF-Expert Member
- Dec 26, 2015
- 2,537
- 4,513
Salamu zenu...
Dini ya kiislaam ni dini ambayo hakuna kitu kuhusu maisha ya mwanadam hakijawekwa wazi utaratibu wake...
KILA KITU KATIKA MAISHA YA MWANADAM KIMEWEKEWA UTARATIBU KATIKA UISLAAM...KUANZIA KWENYE QUR-AN HADI HADITH ZA MTUME MUHAMMAD صلى الله عليه وسلم.
NDOA, TALAKA, NA MIRATHI NI KATIKA MAMBO HAYO.
Sheria ya kiislaam inaitambua NDOA ni kama agano zito ambalo watu wawili wa jinsia mbili tofauti walioridhiana kihisia,katikati yao YAKAZALIWA MAPENZI NA KUHURUMIANA, Agano hilo huliingia mbele ya Allaah kwa mujibu wa taratibu alizo ziweka Allaah Mtukufu.
QUR-AN 4:21
"mmekwisha ingiliana nyinyi kwa nyinyi, na wao wanawake wamechukua kwenu ahadi iliyo madhubuti(Agano zito)?"
Taratibu hizo tunaita NGUZO ZA NDOA...tunaita nguzo kwa sababu nguzo ndizo husimamisha jengo...na bila nguzo hizo jengo halitosimama tena...hivyo basi...NGUZO ZA NDOA YA KIISLAAM NI HIZI ZIFUATAZO(Bila nguzo hizo HAKUNA NDOA HAPO):-
1. UWEPO WA MKE NA MUME, UWEPO WA MARIDHIANO BAINA YAO, UWEPO WA MAPENZI BAINA YAO.
* Kwenye nguzo hii...tunamaanisha katika UISLAAM HAKUNA NDOA YA KULAZIMISHANA...Kuna ile ada mitaani wanasema eti NDOA YA MKEKA...huu utaratibu kwenye uislaam haupo...ni uhuni tu uliosambaa.
* Lazima MKE aulizwe ni kweli amemridhia na amempenda MUME anayetajwa kuolewa nae...? Na lazima majibu yake LAZIMA YAZINGATIWE. Hali kadhalika kwa MUME. Kinyume chake hakuna ndoa.
*Hivyo basi uislaam umekataza kabisa MZAZI, MLEZI, KIONGOZI au mtu yeyote yule kumlazimisha mtu kuingia katika ndoa asiyoitaka.
Ushahidi ni hoja hizi katika hadith za Mtume Muhammad صلى الله عليه وسلم:
Kauli ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Bikira haozeshwi mpaka atakiwe idhini”. Akaulizwa: “Ewe Mtume wa Allaah! Idhini yake ni vipi?” Akajibu: “Kunyamaza kwake” (al-Bukhaariy na Muslim).
Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas (Radhiya Allaahu ‘anhuma) kuwa msichana mmoja bikira alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na kumuarifu kuwa babake amemuozesha naye anachukia hilo. Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akampa hiari (yaani baina kukubali na kukataa) {Abu Daawuud, Ibn Maajah, ad-Daraqutwniy na al-Bayhaqiy}.
Na mfano wake ni ile Hadiyth ya Jaabir (Radhiya Allaahu ‘anhuma), ambayo ndani yake ipo ibara: “…akawatenganisha” (an-Nasaa’iy).
Hapa tunajifunza kutoka kwa Mtume صلى الله عليه وسلم kuwa aliivunja ndoa ambayo BINTI ALIOZESHWA KWA KULAZIMISHWA.
Inaendelea...
Dini ya kiislaam ni dini ambayo hakuna kitu kuhusu maisha ya mwanadam hakijawekwa wazi utaratibu wake...
KILA KITU KATIKA MAISHA YA MWANADAM KIMEWEKEWA UTARATIBU KATIKA UISLAAM...KUANZIA KWENYE QUR-AN HADI HADITH ZA MTUME MUHAMMAD صلى الله عليه وسلم.
NDOA, TALAKA, NA MIRATHI NI KATIKA MAMBO HAYO.
Sheria ya kiislaam inaitambua NDOA ni kama agano zito ambalo watu wawili wa jinsia mbili tofauti walioridhiana kihisia,katikati yao YAKAZALIWA MAPENZI NA KUHURUMIANA, Agano hilo huliingia mbele ya Allaah kwa mujibu wa taratibu alizo ziweka Allaah Mtukufu.
QUR-AN 4:21
"mmekwisha ingiliana nyinyi kwa nyinyi, na wao wanawake wamechukua kwenu ahadi iliyo madhubuti(Agano zito)?"
Taratibu hizo tunaita NGUZO ZA NDOA...tunaita nguzo kwa sababu nguzo ndizo husimamisha jengo...na bila nguzo hizo jengo halitosimama tena...hivyo basi...NGUZO ZA NDOA YA KIISLAAM NI HIZI ZIFUATAZO(Bila nguzo hizo HAKUNA NDOA HAPO):-
1. UWEPO WA MKE NA MUME, UWEPO WA MARIDHIANO BAINA YAO, UWEPO WA MAPENZI BAINA YAO.
* Kwenye nguzo hii...tunamaanisha katika UISLAAM HAKUNA NDOA YA KULAZIMISHANA...Kuna ile ada mitaani wanasema eti NDOA YA MKEKA...huu utaratibu kwenye uislaam haupo...ni uhuni tu uliosambaa.
* Lazima MKE aulizwe ni kweli amemridhia na amempenda MUME anayetajwa kuolewa nae...? Na lazima majibu yake LAZIMA YAZINGATIWE. Hali kadhalika kwa MUME. Kinyume chake hakuna ndoa.
*Hivyo basi uislaam umekataza kabisa MZAZI, MLEZI, KIONGOZI au mtu yeyote yule kumlazimisha mtu kuingia katika ndoa asiyoitaka.
Ushahidi ni hoja hizi katika hadith za Mtume Muhammad صلى الله عليه وسلم:
Kauli ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Bikira haozeshwi mpaka atakiwe idhini”. Akaulizwa: “Ewe Mtume wa Allaah! Idhini yake ni vipi?” Akajibu: “Kunyamaza kwake” (al-Bukhaariy na Muslim).
Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas (Radhiya Allaahu ‘anhuma) kuwa msichana mmoja bikira alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na kumuarifu kuwa babake amemuozesha naye anachukia hilo. Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akampa hiari (yaani baina kukubali na kukataa) {Abu Daawuud, Ibn Maajah, ad-Daraqutwniy na al-Bayhaqiy}.
Na mfano wake ni ile Hadiyth ya Jaabir (Radhiya Allaahu ‘anhuma), ambayo ndani yake ipo ibara: “…akawatenganisha” (an-Nasaa’iy).
Hapa tunajifunza kutoka kwa Mtume صلى الله عليه وسلم kuwa aliivunja ndoa ambayo BINTI ALIOZESHWA KWA KULAZIMISHWA.
Inaendelea...