Jide na Gadner acheni hizooo!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,144
Mhhhh wamependeza sana sana kwanza napenda kuwapa hongera baada ya hapo nimeshangaa mmejitahidi kuelzea vyakula mlivyokuta na picha za menu...mbona hamjawahi kupiga picha zile pweza za feri jamani na umuhimu wake katika jamii hamuoni mnatangaza soko la watu wakati kwenu wanakimbia....haya Zanzibar nako ndio hivyo wamarekani no.

Asalaleh!

Mwisho nawapongeza maisha na raha wajipe jamani msisubiri kupewa na kampuni ama mashirika

=====================


SAFARI YA KUELEKEA JELA ALIPOFUNGWA MWANAMAPINDUZI WA KWELI COMRADE MADIBA

DSC06842.JPG


Vivutio mbali mbali ambavyo vipo Waterfront ni pamoja na huyu mtu wa Gold ambae akisimama hatingishiki unaweza ukadhani ni sanamu ila ukimtupia pesa kwenye ki box kidogo kilichopo pembeni ndio ana swing kama ishara ya kushukuru


DSC06713.JPG


Kuna duka linalouza suvenir mbali mbali za Mandela zikiwemo tshirts, keyholders, magnet za kwenye fridge n.k mi nilikamata ya kwangu...size zote hazikunitosha ikabidi ninunue ya size ya watoto wa miaka 7-8 ndio ikanikaa...kazi kweli kweli

DSC06704.JPG

Mlango wa kuingilia sehemu ya kupandia Boat kuelekea Robben Island,(Nelson Mandela GetAway)


DSC06703.JPG


Huku nako kumbe mpaka kuna cha kiswahili nimepanga nitarudi kukila


DSC06841.JPG


Manka na Mtu wa dhahabu

DSC06846.JPG


Manka na mtu wa silver


DSC06724.JPG


Berna na Gardner kuelekea katika boat (Sikululekhile)


DSC06723.JPG


Mkiwa nje ya boat kabla ya kupanda mnapigwa picha wakati wa kurudi mnazichukua kwa kumbu kumbu, kama bongo vile


DSC06715.JPG


Tuko kwenye foleni kabla ya kuingia kwenye boat, sio unampita tu mwenzio ukikuta amesimama...na utake kuhudumiwa wewe kwanza huku wa kila sehemu unapanga foleni

DSC06694.JPG


Sio lazima kungoja wadosi wakuuzie, kama wanazingua sio mbaya kwenda front mwenyewe..African Marimba Band wanapiga na kuuza Cd's zao wenyewe hapo hapo, pia watu wanaopendezewa wanawapa chochote kila wanapopita


DSC06709.JPG


Duka la Suvenir za Comrade Madiba, ...wadau wachache nimewachukulia zawadi nikirudi tu nawacheki msikonde



DSC06829.JPG


Lango kuu la kuingia jela alipofungwa Comrade Nelson Mandela miaka 18 kabla ya kuhamishiwa magereza mengine mawili tofauti ambapo alikamilisha miaka 27.


Gereza la Posmo alifungwa miaka 7 na Gereza la Paarl alifungwa miaka 2

DSC06747.JPG


Moja kati ya watu waliokuwa Tour guide wetu ambae alifungwa miaka 2 katika gereza la Robben Island na sasa ndio anawaelezea watalii vizuri kuhusu yaliokuwa yanajiri humo ndani...


Aliwahi kuchapwa viboko mwili mzima. Lakini alipojaribu kuwaonyesha wahusika wakuu na doctors kuwa ameumizwa sana hawakujali na walikuwa wanamfukuza na kumuita muongo, na kudai kuwa ni stress tu za yeye kutokulala usiku, huyu guide ni moja kati ya wanaoitwa coloured (halfcast)
Alipona kwa kudra za mwenyezi MUNGU

Kumbukeni gereza hili walikuwa wanafungwa watu weusi, Asians na Coloured tuuu, hakuna mzungu aliekuwa anafungwa humu.
Pia wanawake walikuwa hawafungwi humu
Ubaguzi ulikuwa wazi wazi, kabla Comrade hajaachiwa na kuibadili Afrika Kusini

DSC06831.JPG


Moja ya Picha za kumbukumbu zilizopo kwenye kisiwa hicho, ya wafungwa waliokuwa wakiingizwa huku wamefungwa minyororo miguuni na mikononi tayari kwa mateso.

Mkono wa kulia katikati ni askari weusi waliokuwa wanapewa mikuki na rungu tu kwaajili ya kuwalinda weusi wenzao wasitoroke,
Wakati askari wa kizungu walikuwa na bunduki,
Askari mweusi hakuruhusiwa kuwa na bunduki

DSC06763.JPG


Tukiwa kwenye Bus kuelekea gereza kuu hii ni moja ya barabara za ndani ya gereza hilo


DSC06772.JPG


Kulikuwa hakuna vitanda gerezani humo wafungwa wetu walikuwa wanalala kwenye matandiko kama haya, na hapo juu pichani ni Tour Guide mwingine akituelezea habari zote kuhusiana na gereza hilo


DSC06768.JPG


Menu ya chakula ilikuwa kama hivi, Coloured na Asians walikuwa wanapewa chakula cha afadhali, na Chakula cha wabantu (watu weusi) kilikuwa kibaya kuliko vya wote.


Soma Menu vizuri utaona, upande wa kushoto ndio chakula cha Coloured na Asians na upande wa kulia ni chakula cha mtu mweusi, gerezani humo

DSC06778.JPG


Watalii mbali mbali hufika gerezani hapo kutembelea, na gereza limefungwa kuwa kama gereza limebaki kuwa kivutio cha kitalii ambacho kinaingizia South Africa pesa za kuisaidia nchi.


DSC06788.JPG


Hiki ndicho chumba alichofungiwa Comrade Nelson Madiba Mandela (Our Miracle Father)

Tanzania pia tulikuwa nae wa kujivunia Our Miracle father J.K Nyerere

DSC06792.JPG


Hapa ndipo alipokuwa akijiegesha, maana humu huwezi kuita ni sehemu ya kulala wala kujipumzisha, unaweza ukalia mwanzo mpaka mwisho wa safari unapokwenda kisiwani humo.

Ukielezewa story ya kusikitisha kama hii

DSC06800.JPG


Captain akishuhudia jela aliofungwa Madiba miaka 18, kabla ya kuhamishiwa jela zingine alizokamilisha miaka 27

DSC06803.JPG


Berna, Flower la Venture ndani ya gereza la Mandela

DSC06806.JPG


Manka ndani ya Gereza alilofungwa Madiba


DSC06824.JPG


Mlango mkuu wa kutokea ukiwa umeachiwa huru, na picha ya gereza kwa nje kama linavoonekana


DSC06823.JPG


Tour Guide aliekuwa akituhadithia yaliojiri, yeye alifungwa miaka 7 ndani ya gereza hilo. Mwanaharakati wa mapinduzi, ambae alibambikiwa kosa la ugaidi lakini hivi leo yuko huru na anatuelezea makaburu walivowatesa


DSC06802.JPG


Watalii mbali mbali tulioongozana nao, wakipiga picha gereza la Komandoo wa Afrika, COMRADE NELSON MADIBA MANDELA.

Miaka 27 gerezani, katoka akiwa hai na kawasamehe wote waliomtesa na kumfunga?????????

Mungu nisaidie niwe na roho ya hivo...eeehhhhhhhhh!!
Na hakutaka kufukuza wazungu kaamua taifa liwe la amani kwani binadamu wote ni sawa, Wazungu na weusi wote ni sawa hapa Afrika ya Kusini na hii yote ni kwasababu ya Mandela...we love you tata Madiba

DSC06821.JPG


Berna na Manka nje ya gereza
 
Hapa hata sijaelewa kitu kama vp jaribu kuweke sawa mwana!
 
it is good to have vacation like this, wakirudi waende mkumi au serengeti watangaze na utalii wa ndani
 
2namshauri dada yetu hana uwezo wa kutumia pesa kijinga asije akayavaa makubwa awe makini, ni kijana mdogo sana anahitaji kutulia...hayo mambo ya akina britney spears wenzao wana mabilioni na mabilioni...yeye hata m 100 kwenye account hana, afu anatuzingua hapa na mambo eti ya edgers, nani asiyepajua cape town bwana mpaka picha kibaoooo.nawewe pia hapo juuu usimsemee.mwambie ajibu yeye.pumbav
 
mbona wabongo mnakuwa hampendi wanayofanya wenzenu,kwanini hamuwaelezi wageni wanaokuja kutalii kwetu wasiweke pesa zao badala ya kuja huku nyie mnawaona jide na Gardner tu?acheni wivu,je kwa mimi ambaye niliamua kwenda vacation makkah mtasemaje?
 
mimi ni mkristo lakini sasa hivi nipo makkah kwa mapumziko mafupi,mtasema vipi?
 
ningeona wamuhim sana angepiga picha ngorongoro au serengeti ambazo ni maarufu duniani na zingeisaidia TZ kuliko hiyo robbin island,kwi kwi kwi kwi..afu anavaaaaa manguo ya SA

PUUUUMBAAAVVVVVVVV
 
usulebritee bongo kaaazi kweli kweli gggggggggggrrrrrrrrrrrrrrrrrrrhhhhhhhhhh!!!!

:),mi ni hapo tu,mengineyo sitiii neno,kwani kila mtu na maisha yake bwana,hata ka akikamua mahela yake yoooote,sidhani ka kesha wahi kwenda kumgongea SEMANYA ,,,ngo ngo ngo!!!!!,"Baba nsaidie tu utumbo twa kuku ili nirumangie na ka ugali kangu ka muhogo",,,,Jamani wazee life is too short bana,kamua leoleo,ukichelewa watakuja zichoma ndugu zako au wajinga wajinga wengine tu.
 
Last edited:
Mawazo ya kijamaa!! Sasa kazi ya TTB na Wizara ya Utalii na Maliasili ni nini?
 
mwacheni mwenzenu atoe tongotongo. Kwani kinauma nini ilhali anatumia hela yake. Tangu nimesikia dada huyu akiimba kwa takribani miaka kumi sasa, hii ndiyo mara ya kwanaza kumsikia akienda vacation wakati watu wengine huenda kila mwaka. Tatizo lake ni kujitangaza kuwa yuko wapi; angeenda kimya kimya na kujirudia kimya kimya kama wengine tunavyofanya, ni dhahiri hizi kelele zote tusingezisikia. Nina imani kuwa huko hatotumia zaidi ya $4000 ambazo ni sawa na shilingi milioni nne tu za kitanzania; kelele za nini sasa.
 
mwacheni mwenzenu atoe tongotongo. Kwani kinauma nini ilhali anatumia hela yake. Tangu nimesikia dada huyu akiimba kwa takribani miaka kumi sasa, hii ndiyo mara ya kwanaza kumsikia akienda vacation wakati watu wengine huenda kila mwaka. Tatizo lake ni kujitangaza kuwa yuko wapi; angeenda kimya kimya na kujirudia kimya kimya kama wengine tunavyofanya, ni dhahiri hizi kelele zote tusingezisikia. Nina imani kuwa huko hatotumia zaidi ya $4000 ambazo ni sawa na shilingi milioni nne tu za kitanzania; kelele za nini sasa.

Tatizo Michuzi ndiye aliyeanzisha haka kamchezo ka kujitangaza tangaza kila mara anapotaka nje ya nchi.Sasa na wengine wameanza kuiga....kazi kwelikweli!!!
 
the angle should be every Tanzanian for example one from tandahimba, Mkuranga, Mwakaleli should have enough cash from the national cofers or from their efforts to enable them be tourists. Je unaweza amini kuwa kuna watanzania hawajawahi kuona twiga pamoja na kuwa entrance fee mbugani Mikumi ni shs 1,000/=.

Kwanza hana nauli ya kutoka mkuranga kwenda mikumi na kama anayo basi ina kazi ya michango ya mwenge , madawati, kumkaribisha DC, dawa ya watoto ( alu ay duo cotexin) ambayo dozi ni shs 10,000/=.

vile vile maisha yake yote anajaribu kubalance maisha hawezi kufikiria kupumzika, mtanzania wa kweli kupumzika kwake ni kifo na sio kwenda vacatation. Vacation wanaenda watanzania elites,, politicians na first class citizens.wengine vacation ni heaven au hell kutegemeana na jinsi walivyoishi.
 
Mimi sioni kosa la jayde na mume wake kwenda kutembea, yupo likozi ameamua kupumzika sisi inatuhusua nini? na hizo picha amewawekea wapenzi wa blog yake ambao wamekuwa wanamuomba awawekee picha zaidi. na kama wewe hutaki kujua anafanya nini usiende kwenye blog yake kuangalia,
na kuna mtu kasema kwa nini asivae nguo yenye bendera ya Tanzania , kama ulianagalia vizuri wakati anaenda alivaa scafu iliyokuwa ni bendera ya Tanzania, kutoka airport mpaka huko alikoenda. sas aavae hiyo kila siku kwa ni haifuliwwi.
Halafu swala la mtot hayo ni mapenzi ya Mungu, nadhani hakuna mwanamke ambaye hataki kuwa na mtoto kila mtu anatamani, siku yake ikifika Mungu atampa sisi siyo tunaotoa watoto mpaka uulize kwa nini hazai? Mungu hachelewi wala hawahi siku yake bado na yeye ataitwa Mama.
Kuhusu kupiga picha samaki wa Tanzania nenda kwenye blog yake kwenye kumbukumbu utaona mara nyingi amepiga picha samaki wa ferry, na kule msasani baharini yuko kwa wavuvi ananunua samaki amewapiga picha.
 
some pipo bwana, yaani mtu anatafuta pesa kwa jasho lake mtake kumfundisha jinc ya kuzitumia kama vile mwamsaidia kuzitafuta, aitangaze serengeti my foot, kama nyie mlishawahi kutangaza vile, majungu/wivu kitu kibaya! na huyo alieuliza kama ana mtoto inahusu? mbona watu mnafatilia maisha ya watu kiac hicho...khaaa mnakera sana! jalini yenu wajameni.
 
some pipo bwana, yaani mtu anatafuta pesa kwa jasho lake mtake kumfundisha jinc ya kuzitumia kama vile mwamsaidia kuzitafuta, aitangaze serengeti my foot, kama nyie mlishawahi kutangaza vile, majungu/wivu kitu kibaya! na huyo alieuliza kama ana mtoto inahusu? mbona watu mnafatilia maisha ya watu kiac hicho...khaaa mnakera sana! jalini yenu wajameni.


Mimi nakubaliana na akina Gadner kwa chochote wanachokifanya au walichofanya kuanzia kuzaa mpaka matumizi ya hela zao.

ILA tu....


Kama wangevaa fulana yenye bendera ya Tanzania pale au yenye Mount Kilimanjaro au Mbuga ya Serengeti.... hapo walipotembelea gereza, wangesaidia kutangaza TZ.......Uzalendo.

Ningewafagilia zaidi.

Mambo yao mengine personal
 
Kama mtu huna hobby ya kutalii stop critisizing others. You just better shut and keep it to yourself that if it is me I won't travel. When you are in Cape Town, Roben Island and Boats tour is something you wouldn't like to miss. if you have never been there you may surely critisize. Wazungu wakifanya mnaona sawa, wabantu tukifanya tunatumia fedha vibaya.. lazima ujithamini mwenyewe ndio watu wakuthamini. Jipe thamani Semenya.
 
some pipo bwana, yaani mtu anatafuta pesa kwa jasho lake mtake kumfundisha jinc ya kuzitumia kama vile mwamsaidia kuzitafuta, aitangaze serengeti my foot, kama nyie mlishawahi kutangaza vile, majungu/wivu kitu kibaya! na huyo alieuliza kama ana mtoto inahusu? mbona watu mnafatilia maisha ya watu kiac hicho...khaaa mnakera sana! jalini yenu wajameni.

Wajameni, naona kama tunaingilia privacy ya watu kwa kiasi kikubwa mno... Namuomba PDiddy a "wrap-up" hii mada for the interest of our sister and brother.

Its painful to read some of the comments made
 
Back
Top Bottom