Hii ni nyimbo mpya ya jide,inaitwa YAHAYA,kwa kweli hii ngoma imetulia,mziki wa kijanja wenye hadhi ya kisasa,haijakaa kishari,ukikaa chumbani na kuitafakari hii nyimbo aiseeh inagusa,hongera Man walter na jide,napenda sana mdundo wake,umetulia ukipata speaker zinazogonga vyema hakika uta enjoy huu wimbo.Jide kamchora yahaya kama kijana tapeli,mzushi,smart lakini hana hela,ni mtu mwenye fix nyingi,hana kazi maalumu,kazi yake kupiga mizinga,kujifanya matawi ya juu,anajifanya yeye ndo anajua kila kitu.Ki ukweli kwenye jamii yetu wapo watu wa namna hii,yaani wakina yahaya,watu wanaopenda vya bure,kujifanya matawi kumbe matapeli,mtunzi amefanikiwa kumchora yahaya,hongera sana jide,u always rock