Jicho langu la Tatu kutoka ukumbi wa Magogoni Feri

Yote tisa kumi ni kua asitake kudanganya watu kwamba uzalendo ni kumuunga mkono yeye kwamba kua tofauti nae unakua sio mzalendo, na mwisho inawezekana ukaichukia serikali yako ila ukaipenda nchi yako tusilazimishe watu waipende serikali iliyopo madarakani....
 
Hawa MCL tumeshawaonya na kuwahusia sana humu Jamvini JF ila naona ' dharau ' zimezidi na masikio yao wameweka ' pamba ' ila nadhani kwa maneno ya ' Taita ' wa Magogoni leo ' Mabosi ' wao sasa ' Kitu ' kinagonga katika ' Pichu ' na kurudi tumboni. Kuna wengine uwepo wetu humu JF ni kama vile ' Malaika ' wema hivyo tukikuonya au kukushauri jambo jitahidi unakuwa nalo makini sana. MCL kama itatokea na yakawakuta wala wasilaumu Mtu kwani Members wengi sana humu walishawaonya na namkumbuka mmoja wao aliyewaonya mapema kuwa ni Ruttashobolwa.
mkuu"GENTAMYCINE" bado makengeza yangu yananituma kuchunguza zaidi kuwa nina muonya nani? ujue tu kuwa huyu ni king maker, huyu ni zaidi Ya jiwe kuu la pembeni. kuna tawala zilijikwaa kwake na zikaangamia kabisa
 
So swali kwako ni je tuungane na watu aina ya waliommimina risasi zote zile Lissu, nimejaribu k
mkuu, just thinking aloud, mimi sifungamani na rangi yoyote hivyo naendelea KUJIULIZA : itakuwaje tutakapo gundua pasipo Shaka kuwa huyu tumayemdhania kuwa mhusika wa risasi za Lisu siye?
 
1. Tanzania yatupasa tuwe na moyo wa Uzalendo hasa na tuache majungu, chuki na uchochezi

2. Rais sasa ameanza kuelewa jinsi ya Kuiongoza / Kuitawala Tanzania

3. Profesa Kabudi awa ‘ turufu ‘ nzuri ya Rais hasa katika ‘ kusawazisha ‘ mambo magumu

4. Waziri Nchemba ‘ confidence ‘ yake mbele ya Rais sasa ni ‘ minus ‘ zero na ‘ anaogopa ‘ mno hadi anatia huruma na anasikitisha pia

5. Siku za uwepo wa Kampuni ya Magazeti ya MCL zinaanza ‘ Kuhesabika ‘ Kisheria

6. Rais ‘ anakerwa ‘ kwa kiasi Kikubwa na Vyombo vya Habari nchini

7. Gavana ‘ Mteule ‘ Luoga aliingia Ikulu akiwa ‘ mtiifu ‘ ila mara baada ya ‘ Kuteuliwa ‘ na alipokuwa anaenda kupiga picha kidogo ‘ mikogo ‘ ilianza japo kwa mbali kwani hajaamini kabisa kama ‘ ameukata ‘ zaidi maishani

8. Waziri Kairuki sasa ‘ confidence ‘ yake imekuwa ‘ maradufu ‘ na anaongea ‘ kiukakamavu ‘ kabisa huku akiwa hana ‘ aibu ‘ ya hadhira iliyokuwepo pale kama kwa wengineo

9. Rais anaidharau mno ‘ tasnia ‘ ya Habari na Mawasiliano hasa pale ambapo alisema kwamba Waandishi wa Habari wa Tanzania wanatakiwa kuwa ‘ Wazalendo ‘ kwa nchi yao ili hata siku moja ikija Kampuni hapa Tanzania basi wanaweza kupata Kazi ya kuwa Afisa Habari ( ila Yeye Rais alisema neno hili namnukuu “ linaweza hata likawa Liafisa Habari la hiyo Kampuni “. Nadhani Rais alisahau kwamba hii ‘ dharau ‘ yake hata ‘ Watendaji ‘ wake Wakuu akina Gerson Msigwa na Dkt. Hassan Abbas nao pia inawagusa

10. Japo Profesa Lipumba alialikuwa kutoa neno ila mwishoni alipiga ‘ Kijembe ‘ cha ‘ akili ‘ na cha ‘ Kimafumbo ‘ hasa aliposema kwamba leo ameongea sana kwakuwa sasa ‘ hawaruhusiwi ‘ kufanya Siasa nchini

11. Mzee John Momose Cheyo ameongea kifupi sana ila ametoa maneno ‘ Kuntu ‘ kabisa kwamba imefika mahala Watanzania sasa ‘ tujiamini ‘ na tuache ‘ kujidharau ‘ kwani tunaweza na pia ‘ Siasa ‘ za Tanzania zisiwe ‘ Kiwanda ‘ cha ‘ machafuko ‘ nchini

12. Kuna wengine leo ‘ Suti ‘ walizozivaa hazikuwakaa vyema hali ambayo imenifanya nihisi kwamba huenda kuna ‘ walioazima ‘ ili waende nazo pale Ikulu

13. Mara baada ya kutoka ‘ tangazo ‘ kwamba leo kutakuwa na Chakula cha pamoja na Rais pale pale Ikulu ukumbi wote ulionyesha Sura za furaha ikiwa ni ‘ Kiashirio ‘ tosha na cha ‘ Kutukuka ‘ kabisa kwamba Wageni wengi walikuwa na ‘ njaa ‘ mno na pengine hata ‘ Pesa ‘ mifukoni mwao zilikuwa hakuna hivyo Rais kaokoa ‘ jahazi ‘ kimtindo vinginevyo wengi wangepiga ‘ pasi ndefu ‘ leo

14. Rais ameonyesha wazi wazi kwamba ‘ hamkubali ‘ Gavana Ndullu na anatamani hata leo aondoke na kama vile ‘ amemchoka ‘ japo kuna wakati alimsifia ila kwa ‘ Wataalam ‘ wa diplomasia na mawasiliano tulimwelewa mapema sana alichokuwa anamaanisha

15. Rais hafurahishwi na baadhi ya ‘ Sheria ‘ ambazo tayari zimeshatungwa lakini ‘ Wahusika ‘ hawazitumii ili kuleta nidhamu na ‘ kuwaadabisha ‘ wale ambao ‘ wanawashwawashwa ‘ nchini

16. Waziri wa Ardhi William Lukuvi amezidi kuonyesha kwamba Yeye ni ‘ Jembe ‘ na ‘ hazina ‘ kubwa kwa Chama cha CCM na Serikali yake kwa ‘ Utendaji ‘ wake uliotukuka wa hiyo Wizara

17. Rais anaonekana ana nia njema na nzuri sana kwa Watanzania na Tanzania kama nchi ila tu kuna uwezekano mkubwa kwamba ‘ anahujumiwa ‘ na alionao karibu na ambao pengine anawaamini mno

18. Uwepo wa Mzee Reginald Mengi ukumbini na jinsi Rais alivyokuwa akisisitiza kuwa ‘ Wazawa ‘ waaminiwe ni dhahiri shahiri kwamba ‘ dongo ‘ kwa Profesa Muhongo limefika na tayari katika Vita yake na Mengi kwa sasa Mzee Mengi ameshakuwa mshindi

19. Rais ameendelea kuonyesha kwamba bado si ‘ mtunza ‘ taarifa ‘ nyeti ‘ mzuri hasa pale alipokuwa anasema hadharani harakati za ‘ Kiintelijensia / Kijasusi ‘ waziwazi dhidi ya wale ‘ maadui ‘ wa Uchumi wa Tanzania hali ambayo kwa maoni yangu Mimi GENTAMYCINE nadhani yalipashwa yajulikane tu Kwake na kwa wale Viongozi Wakuu wa Idara za Ulinzi na Usalama za nchi hii hasa ukizingatia kwamba bado Vita inaendelea na pengine Yeye ( Rais ) kutoa vile zile ‘ Siri ‘ anaweza akawapa mwanya ‘ maadui ‘ wa Uchumi na wakajipanga upya na kivingine

20. Kuteuliwa kwa Profesa Florens Luoga ambaye ni ‘ Mtaalam ‘ hasa wa Sheria za Kodi ( Taxation Laws ) kunaonyesha kwamba ‘ Wanasheria ‘ wengi hasa waliopo Serikalini ni ‘ goi goi ‘ tupu kwani muda wote Taifa linaingia katika ‘ hasara ‘ kubwa ya ‘ Kiuchumi ‘ wao walikuwa hawajali na hawatumii ‘ utaalam ‘ wao katika kutetea na kulinda ‘ rasilimali ‘ za nchi ambazo zilikuwa ‘ zinanyakuliwa ‘ kwa udhaifu wa hao Wanasheria ‘ goi goi ‘ wa Serikalini ambao wengi wao wapo Benki Kuu na Mamlaka ya Mapato vile vile

Hayo ndiyo ambayo ‘ jicho la Tatu ‘ la “ Purely Talented and Charismatic Fella “ GENTAMYCINE limeweza kuyaona, kuyagundua na kuyaelewa pia ila na Mimi kwa kumalizia tu niseme kwamba ndiyo inawezekana kukawa na ‘ mapungufu ‘ ya hapa na pale ya Kiutendaji kutoka ‘ juu ‘ ila sasa umefika muda kwa Watanzania wote kujenga tabia ya Kuungana na Kuonyesha ‘ Uzalendo ‘ pindi panakuwa na suala lenye umuhimu na maslahi kwa nchi yetu ya Mama Tanzania. Tunavyozidi ‘ Kugombana ‘ na ‘ Kuzozana ‘ sisi kwa sisi tunawapa ‘ mwanya ‘ hata ‘ maadui ‘ zetu kutucheka, kutudharau na hata kujipanga zadi kuweza kutugawa na kuzidi kututawala na sisi kubakia hapa hapa na ‘ maendeleo ‘ yetu duni.

Nawasilisha.
Vipi issue ya mfalme Daud kupeleka Uria front line ili apate nafasi ya kuvinjari vizuri na mkewe?
 
Hata hivyo hakuna mahala popote pale ambapo leo Rais ama aliongelea au aligusia suala lolote lile la Tundu Lissu na nimeshangaa kuona Wewe umelileta na kulihusisha hapa katika huu ' uzi ' wangu wakati hata si mahala pake. Naomba ukimjaza / ukimpachika / ukimweka / ukimtwisha / ukimngono Mkeo mimba nyingine akizaliwa Mtoto wa Kiume basi muite Tundu Lissu ili kuonyesha ' mahaba ' yako zaidi Kwake.
Kumbe na wewe ni wale per day was Lumumba!
 
Haiwezi kuwa nyepesi kama hukujiandaa na ulikuwa tu unajaribu.,kuna watu walijiandaa kwa nafasi hii kiakili na kisaikolojia kwa muda mrefu kubeba majukumu haya....sepa na kupisha watu waliojiandaa tangu zaman .,maandalizi yako ya mtihani ndiyo ufaulu wako ,hii principle iko hivyo hata ktk maisha yetu ya kila siku.
Unalia kazi ngumu halafu unaanzisha propaganda za kutaka uongezewe term iwe miaka saba???

Pumbafu kabisaa....

Nakubaliana na wewe..
Lakini kushinda mtihani si lazma upitie changamoto..
Mkulu wetu ndo kwanza mwaka wa pilii huu bado mitatu tuweze kumpima UFAULU wake..

Kifupi hakuna mtu hata wewe/ anayefanya jambo bila kujiandaa..hayo aliyosema yalikua mameno tuu ya kuchomekea..
Kifupi huyu Rais alikua kashandaliwa..sio kama unavyodhani kua niwakustukiza..
 
Siyo wote tulikuwa na muda wa kuangalia TV kama wee ulifuatilia kausha tu mkuu.

Mkuu usipoteze nae muda huyo ' Mpuuzi ' na si unaona tokea nimpe ile ' dozi ' yangu hajarudi tena mpaka sasa hivi? Na nilimtamani sana arudi ili nimalize Kazi kabisa. Ana bahati mno!
 
foa shudu zako hapa hapo kuna mafumbo gani kama hizo sentense ni mafumbo je ukiwekewa mafumbo yenyewe si utasema hizo ni methali

Mkuu unaonyesha hupendi sana kusoma sijui hata kama umewahi kusoma biblia, jamaa ameandika kwa staha mno kuondoa kadhia yeyote ile. Endelea kusoma vitu kama hadithi za usiku bila kutafakari.
 
15 Reactions
Reply
Back
Top Bottom