Uchaguzi 2020 Jicho la tatu: Huu ndio utofauti wa Tundu Lissu na John Magufuli

Dam55

JF-Expert Member
Oct 8, 2015
5,592
11,831
Tumia jicho lako la tatu kutueleza utofauti wa hawa viongozi wawili wenye ushawishi mkubwa kwenye uchaguzi mkuu wa 2020.

Baada ya kumalizika kwa kampeni za leo kwa wagombea wote wawili mmoja akiwa Dodoma na mmoja akiwa Dar es salaam wote waliandike jumbe kwenye kurasa zao za Twitter.

Kwa kauli hizi inatupa picha namna wagombea hawa wanavyo tofautiana katika mambo mengi.

Lissu

Hili ndilo jibu letu kwa waliokuwa wanadai kwamba hatuna sera!!Uhuru, Haki na Maendeleo ya Watu! Njia ya kupata maendeleo sio lazima iwe iliyojaa damu, mateso na vilio. Uhuru, Haki na Maendeleo ya Watu ndio njia bora zaidi.
Screenshot_20200830-004647.png

Magufuli

Nawashukuru wana CCM wote na Watanzania wa vyama vyote kwa kujitokeza katika uzinduzi wa kampeni za CCM 2020 Jijini Dodoma. Pia nawashukuru wasanii, waandishi wa habari, viongozi wa Dini, n.k waliojitokeza kuniunga mkono katika uzinduzi huu. Maendeleo hayana chama. Tanzania Hoyee
Screenshot_20200830-005059.png


  • Kwa upande wangu naona Kuna mmoja amejawa Chuki na visasi n.k alafu Kuna mmoja yuko na moyo mweupe wenye furaha bila vinyongo, chuki, visasi n.k
  • Kuna mmoja anapangilia sana maneno kuepuka kuropoka ovyo, alafu Kuna mmoja huongea tu kile kinachomjia kichwani kwa wakati huo.
  • Kuna mmoja anapenda Sana utani unao tokana na utamaduni wa kitanzania, alafu Kuna mmoja yeye kwake kila kitu ni nongwa kwakifupi hana jema kwake kila kitu ni kibaya.
  • Kuna mmoja ana siasa za asili ya kiuhuni uhuni yani haziko ki presidential alafu Kuna mwingine ni mtulivu sana.
  • Mmoja anaweka sana utaifa mbele alafu mwingine ni mwanaharakati zaidi yupo tayari kwa chochote ikiwa tu kinamletea political popularity.
 
Umesahau mkuu point hizi:-
- Kuna mmoja anatumia dola kufanya atakalo hata kama ni kukandamiza wengine na kuna mwengine hana nguvu ya dola
- Kuna mmoja analazimisha ushindi wa mezani kwa chama chake na kuna mwengingine wagombea wao wameenguliwa na chama cha huyu anaejitia ustaarabu wa kirongo rongo.
- Kuna mmoja anaongea kiupole kinafiki na huyu mwengine amekerwa kwa kuwa upande wao umekuwa ukidhulumiwa kila leo
 
Eti Rais wa Tanzania atatengeneza ajira 8,000,000 kwa watanzania, mwenye maswali ajibu ndiyooooooooo
 
Mmoja ni mzalendo wa madaraja na flyovers kama makaburu mwingne anataka uhuru wa kuongea,uhuru na haki za raia

Mmoja anajifanya binadamu kipindi cha kampeni,akiwa serikalini anawambia wananchi kwa nini UKIMWI ni nyie mwingne anapinga sheria za kukandamiza raia kama asilimia 15 % ya loan board na utitiri wa kodi kwa wafanyabiashara

Mmoja amejaaa visasi vya wazi wazi, alikataza vyombo vya dola kutochunguza tukio la watu kupigwa risasi,akakataa kwa makusudi kuidhinisha matibabu kwa mhanga ,mfano akamwambia Dr Shien mtu anakataa kukupa mkono halafu siku akiugua unatumia huo Mkono aliokataa kuidhinisha hela za matibabu hiiiiiiiii,mwingne yeye anapigania haki kwa watu wenye matatizo

Mmoja anahistoria ya kuumiza watu bila fidia mwingne anatetea haki

Mmoja anaubaguzi wa kimaeneo hasa kanda ya ziwa huku akibeza kaskazini ,mwingne anapigania haki kwa kila mtu
 
Back
Top Bottom