JF yapata ushindi mwingine dhidi ya ufisadi

Mwafrika wa Kike

JF-Expert Member
Jul 5, 2007
5,185
56
Kulingana na taarifa ya KLHNEWS, serikali na Mukandala wameamua kuwafutia kesi vijana 38 wa chuo kikuu waliokuwa wameshitakiwa eti kwa kusababisha fujo chuoni.

Hii ni baada ya wana JF kusimama kidete na kupinga kitendo cha uongozi wa chuo kuingilia uhuru wa wanafunzi wa kuchagua viongozi wao. Ingawa Afrika inajulikana kwa udikiteta na ukiukwaji wa haki za binadamu. Ninaamini kuwa Mukandala na Maghembe hawatarudi kwenye zama za mawe na kuwakandamiza hawa vijana wasio kuwa na hatia yoyote isipokuwa kudai uhuru wao wa kidemokrasia.

Habari yenyewe hii hapa kwa hisani ya KLHNEWS na mtiifu wetu Mwanakijiji ambaye alipiga simu zaidi ya mia moja kufuatilia hii habari behind the scene na kutoa sikio kuwasikiliza "wavuta bangi hawa" :



WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Jumanne Maghembe, ameridhia wanafunzi 38 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam waliofunguliwa mashitaka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam wakikabiliwa na mashitaka mbalimbali kuondoloewa mashitaka hayo.
Waziri Maghmbe ameridhia uamuzi huo kutokana na maombi yaliyowasilishwa na uongozi wa chuo hicho kuwa masuala hayo yatamalizwa na uongozi huo, wadau mbalimbali na Serikali ya Wanafunzi (DARUSO).

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo jioni (saa za Tanzania) na Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Rwekaza Mukandala, ilieleza kuwa masuala yote yaliyotokana na vurugu chuoni hapo yatashughulikiwa chini ya sheria za chuo hicho.

"Tunafurahi kuwafahamisha kwamba Waziri wa Elimu amekubali ombi letu, hivyo tunaliomba Jeshi la Polisi kufuta kesi dhidi ya wanafunzi 38 zilizofunguliwa Aprili 23 mwaka huu, kwani kesi hizo zitashughulikiwa kwa mujibu wa sheria za chuo, nao pia wamekubali," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Profesa Mukandala alisema uongozi wa chuo na DARUSO pia inafuatilia kwa karibu kesi ya wanafunzi 14 iliyofunguliwa polisi kutokana na matukio ya Februari 17 na 22, ili kubaini wasio na hatia waweze kurejea madarasani

Aidha, alisema uongozi wa chuo hicho umeliomba Jeshi la Polisi kuharakisha kesi ya kukutwa na dawa za kulevya inayowakabili wanafunzi watano, ili wasiopatikana na hatia nao waweze kurejea darasani mara moja.

"Tutaendelea kufuatilia kwa karibu hali ya usalama chuoni hapa ili kuhakikisha hali ya usalama inarejea kama kawaida," alisema.

Makamu Mkuu huyo wa chuo, aliupongeza uongozi wa DARUSO kwa kusisitiza kuwa mazungumzo ndio mwafaka ya kumaliza mgogoro chuoni hapo. Katika hatua nyingine, Serikali ya wanafunzi chuoni hapo imepinga hatua iliyochuliwa na Waziri wa Elimu na Ufundi kuwafutia udahili wanafunzi 339.

Akizungumza na wandishi wa habari chuoni hapo, Rais wa Serikali ya wanafunzi (DARUSO), Deo Daud, alisema hatua hiyo imetolewa kisiasa, kwani haikufanyiwa utafiti.

Baadala yake wanataka mazungumzo ambayo wanaamini ndio njia muafaka yanafanyika kati ya utawala na Daruso ili wanafunzi wote waliofukuzwa wanarejeshwa chuoni na hatua zozote dhidi yao zinazingatia taratibu na kanuni chuo kuliko kumbilia kuwapeleka Polisi.

Katika Tamko lao Daruso wamesema kwamba hatua iliyochukuliwa na Serikali kuwafutia wanafunzi mikopo na usajili ni ya kibabe isiyozingatia utawala bora kwani miongoni mwao waliofukuzwa chuo bado kesi mahakamani hawajatiwa hatiani hivyo kutoa tamko hilo ni kuingilia uhuru wa Mahakama.

"Lazima Waziri aeleze Umma kuwa ametumia sheria zipi kuweza kufikia maamzi hayo,tatizo tunalolishughulikia hapa ni uvunjivu wa taratibu uliofanywa na wanafunzi lakini DARUSO inaona hatua iliyochukuliwa dhidi ya wanafunzi ndizo zinavunja taratibu na sheria zilipo"alisema Daud

Alitoa mfano kuwa kati ya wanafunzi waliofutiwa udahili wapo wanne wanaodhaniwa kuvuruga madarasa adhabu yake kama wakidhibitika kufanya hivyo ni kusimamishwa masoma si zaidi ya miezi tisa. Alisema kama uchunguzi wa kina ungefanyika bila serikali kukurupuka, ungeweza kubaini kuwa wakati vurugu za juzi zinafanyika hawakuwepo kutokana na kusimamishwa masomo.

Adha, rais huyo wa Daruso alionya serikali kutotumia umasikini wa wanafunzi 415 walioshindwa kujilipia ada kuwakandamiza kuwa ndio waliongoza mgomo huo na kuwaacha walengwa. Kutoka na tamko hilo tamko hilo, wanafunzi hao wametaka hatua zozote kuhusiana na tamko la serikali ziachwe na baadala yake wanafunzi hao kurejeshwa chuoni, ili washitakiwe kulingana na sheria za chuo.

Pia wameomba serikali iruhusu majadiliano kati yake na Daruso, ili kuona namna ya haki za wanafunzi wasio na hatia kati ya wenye hatia zitapatikana. Pia Daruso imelaani kitendo cha askari wa Kutuliza ghasia (FFU) kuwafungia ndani ya mgahawa wa chuo wanafunzi waliokuwa wanakula na kuanza kuwapiga mabomu ya machozi, hivyo kupata nafasi ya kuwashika hata wale wasiohusika.

Juzi, Waziri wa Elimu alitangaza kuwafutia udahili wanafunzi 339 kwa tuhuma za kuhusika kwenye mgomo wa kushinikiza wanafunzi wenzao warejeshwe chuoni akiwemo Waziri Mkuu wa Daruso, Julias Mtatiro.

Tangia kufunguliwa kwa kesi hiyo kampeni ya dhati imekuwa ikifanyika ikiwahusisha Watanzania walio ndani na nje ili kutaka uongozi wa Chuo Hicho Kikubwa kabisa nchini kubadili maamuzi yake na kurejea kwenye meza ya mazungumzo badala ya kutumia vyombo vya dola kujibu hoja za wanafunzi.

KLHN inatarajia kufanya mahojiano na mmoja wa viongozi wa serikali ya wanafunzi wa Chuo hicho mwishoni mwa juma hili.

Source KLHNEWS:

http://www.klhnews.com/index.php/headlines/mashtaka-dhidi-ya-wanachuo-38-yafutwa.php
 
Hii ni habari njema sana! Mimi nilikuwa bado sijaelewa iweje hii serikali ianze kupeleka watoto mahakamani! Hii ilikuwa sawa na kumpeleke mtoto uliyzaa mahakamani! Nilishangaa pia kwa msomi wa utawala Prof. Mkandala kudhani suluhisho ni kupeleka watoto mahakamani! Nilishawishika kuamini kuwa ilikuwa ni amri kutoka kwa wakubwa wake wakitaka kupoza mambo ya ufisadi ambayo yamesambaa kila mahali! Nashukuru hili halikufanikiwa! Ufisadi uzi ni uleule akina Karamagi watajuta kwa nini walichanganya biashara na siasa! Hao vijana warudishwe chuo waende madarasani. Hii waliyopata ni adhabu tosha! Sitaki kuamini kuwa hawa wakubwa wanaweza kuwapeleka mahakamani watoto wao wakiwakuta na bangi! Mbona tunasikia wengine ni waathirika wa madawa ya kulevya kwa nini hawapeleki mahakamani wakiwa miteja - ushahidi wa wazi kabisa! Watu tuko serious na issue za akina EPA na vijisent, rechmound nk watu wanapeleka watoto wa kapuku mahakamani tena bila aibu! FFU kakamate hao akina KIWIRA COAL, EPA nk! Hao ndio haswaa wahalifu!
 
taratibu lakini tutafika tu,safari ni hatua

Tunapambana na watu wasiojali utu kabisa. Wewe huwezi kufungia watu kwenye cafeteria na ukaanza kuwapiga mabomu ya machozi. Ni uphill battle lakini fight lazima iendelezwe kwenye front zote tukianzia na hili la kuingilia uhuru wa wanafunzi kujichagulia viongozi wao.
 
Hii ni habari njema sana! Mimi nilikuwa bado sijaelewa iweje hii serikali ianze kupeleka watoto mahakamani! Hii ilikuwa sawa na kumpeleke mtoto uliyzaa mahakamani! Nilishangaa pia kwa msomi wa utawala Prof. Mkandala kudhani suluhisho ni kupeleka watoto mahakamani! Nilishawishika kuamini kuwa ilikuwa ni amri kutoka kwa wakubwa wake wakitaka kupoza mambo ya ufisadi ambayo yamesambaa kila mahali! Nashukuru hili halikufanikiwa! Ufisadi uzi ni uleule akina Karamagi watajuta kwa nini walichanganya biashara na siasa! Hao vijana warudishwe chuo waende madarasani. Hii waliyopata ni adhabu tosha! Sitaki kuamini kuwa hawa wakubwa wanaweza kuwapeleka mahakamani watoto wao wakiwakuta na bangi! Mbona tunasikia wengine ni waathirika wa madawa ya kulevya kwa nini hawapeleki mahakamani wakiwa miteja - ushahidi wa wazi kabisa! Watu tuko serious na issue za akina EPA na vijisent, rechmound nk watu wanapeleka watoto wa kapuku mahakamani tena bila aibu! FFU kakamate hao akina KIWIRA COAL, EPA nk! Hao ndio haswaa wahalifu!

Haki tupu karibu sana JF,

WEwe jiulize swali kuwa serikali na uongozi wa chuo vinatumia masaa chini ya 24 kujua na kukamata "watumiaji wa dawa za kulevya hapo chuoni" na kutumia zaidi ya miaka miwili kukamata wauzaji wa dawa za kulevya hapo Tanzania pamoja na kuwa wamepewa hints (which is not necessary anyway) na wananchi.
 
Jamani, hii kwa kweli ni efforts ya watu wengi kuliko wakati mwingine wowote ule. Kazi kubwa imefanywa na wenzetu nyumbani wengine tumedandia tu na kupulizia moto ulioanza kuwashwa. Hongereni watu wa DARUSO na TAHLISO.

Na wana JF ambao walitoa mchango wa mawazo yao.
 
Jamani, hii kwa kweli ni efforts ya watu wengi kuliko wakati mwingine wowote ule. Kazi kubwa imefanywa na wenzetu nyumbani wengine tumedandia tu na kupulizia moto ulioanza kuwashwa. Hongereni watu wa DARUSO na TAHLISO.

Na wana JF ambao walitoa mchango wa mawazo yao.

Najua hupendi credit na ulikuwa hutaki kuwasikiliza hawa vijana kwa kudhani kuwa ni kweli ni wavuta bangi kama Mukandala anavyowaita ...lol
 
watu wengine kwa kupenda sifa. Sasa unataka watu wakuamini kuwa ulifanya chochote kuwasaidia hawa vijana?
 
Haki tupu karibu sana JF,

WEwe jiulize swali kuwa serikali na uongozi wa chuo vinatumia masaa chini ya 24 kujua na kukamata "watumiaji wa dawa za kulevya hapo chuoni" na kutumia zaidi ya miaka miwili kukamata wauzaji wa dawa za kulevya hapo Tanzania pamoja na kuwa wamepewa hints (which is not necessary anyway) na wananchi.

Sasa hili la kuuza madawa ya kulevya analoshughulikia Kikwete lina uhusiano gani na hao wanafunzi waliokamatwa na madawa ya kulevya na ambao bado watafikishwa mahakamani muda wowote ule?

Soma alichosema Prof Mukandala hapa:

Aidha, alisema uongozi wa chuo hicho umeliomba Jeshi la Polisi kuharakisha kesi ya kukutwa na dawa za kulevya inayowakabili wanafunzi watano, ili wasiopatikana na hatia nao waweze kurejea darasani mara moja.
 
Serikali ya kifisadi utaijua tu. Wanashindwa kuwafungulia mashtaka mafisadi wanaoiangamiza nchi wanaenda kuwaonea vijana wanaotafuta elimu. Bora kesi imefutwa.
 
Jamani nimepitwa kidgo kwenye hili

hivi kuna mtu anaweza kunifahamisha role ya JF kwenye hili ilikuwa ni ipi mkapa ikapata ushindi?maana nimesoma article nzima sijaona reference ya JF
 
Jamani, hii kwa kweli ni efforts ya watu wengi kuliko wakati mwingine wowote ule. Kazi kubwa imefanywa na wenzetu nyumbani wengine tumedandia tu na kupulizia moto ulioanza kuwashwa. Hongereni watu wa DARUSO na TAHLISO.

Na wana JF ambao walitoa mchango wa mawazo yao.
Tumedandia ama wamekuja kuomba ushauri?mhn..anyways its a good news for all the reformers and progressives!
 
Jamani nimepitwa kidgo kwenye hili

hivi kuna mtu anaweza kunifahamisha role ya JF kwenye hili ilikuwa ni ipi mkapa ikapata ushindi?maana nimesoma article nzima sijaona reference ya JF
Either its a coincidence kwamba kuja kwao hapa jf kuomba msaada wa kimawazo na uchangiaji wetu sambamba na uamuzi wa kuwafutia kesi kutoka serikalini is remained to be seen!However it will make sense that pepole wants to feel like their contribution wasn't in vain!
 
Jamani nimepitwa kidgo kwenye hili

hivi kuna mtu anaweza kunifahamisha role ya JF kwenye hili ilikuwa ni ipi mkapa ikapata ushindi?maana nimesoma article nzima sijaona reference ya JF

Mukandala alipokea simu nyingi sana toka kwa wanajambo ambao hawataki kutajwa majina hapa. Ukiona pia kuwepo kwa ile thread ya kufukuzwa kwa wanafunzi wa chuo kikuu hapa jamboforums ilikuwa ni presha tosha kwa Mukandala na serikali.

Mengine ni historia ila Maghembe ameonja joto ya jiwe kipindi hiki kwa vile alivyopigiwa simu kutoka ndani na nje ya Tanzania bila kujua kutegemea.
 
Tatizo kubwa la akina Mukandara na Maghembe ni kwamba wao pia wanapokea shinikizo kutoka kwa Mafisadi wa Serikali ya CCM na chama.

Ili kulinda Unga usimwagike inabidi watoe maamuzi yanayopingana na ukuu wa elimu yao na uwezo wao wa kushughulikia matatizo.

Ndiyo maana huku majuu kuna Utitiri wa PhD holders kutoka Tanzania wakiwa walimu na Ma Expert kwenye Field nyingi.
wengi walikimbia ujinga huu tunaouona kupitia kwa akina Mukandara

Nani yuko tayari kupokea amri za kishenzi kutoka kwa mtu kilaza kama Makamba eti kwa sababu yeye ni katibu mkuu wa CCM?

Nani yuko tayari kuendesha chuo kikuu kwa itikadi ya CCM iliyokwisha buma miaka kibao iliyopita?

UDSM siyo chuo cha kufundisha itikadi ya CCM. Pale ni mahali rasmi pa kuwaivisha wataalamu wetu.

Kuna majuha huko ndani ya CCM, kwa vile wao walienda na viroba kuiba BOT huku wakiwa hawana elimu ya kutakata, hawaoni umuhimu wa elimu ya chuo kikuu na hivyo kushindwa pia kuona umuhimu wa UDSM.

Effect ya ujinga wa Makada wa CCM katika mfumo wa elimu inajitokeza wazi wazi kila penye jiko la kuokea wataalamu wetu, UDSM ikiwa mojawapo.
Hawa wazee na vijana Muflisi ndani ya CCM mawazo yao ni mafupi na hayakui, wanadhani shule ni mahali pa kuwaweka vijana ili kuwazuia wasizagae mitaani na kuleta fujo.

Sisi tunatambua kwamba shule ni mahali pa kuelimisha na kujielimisha ili kujenga uwezo wa kutatua matatizo yanayolikabiri taifa letu.

Kama shule hailengi kutoa elimu yenye kuamsha uwezo wa kutatua matatizo basi shule hiyo haina maana yeyote, ni heri kujiengua kutoka kwenye shule hiyo na kwenda kuchunga mbuzi.

Ukichunga mbuzi walau unaweza ambulia maziwa na kisusio siku akichinjwa.

Ninyi makada wa CCM mlegee, tena mlegee mpaka mpate tumbo la kuendesha.

Mkome kama mlivyo koma kunyonya maziwa ya mamazenu kuingilia mambo makuu ya elimu , mambo msiyoyajua.
 
Jamani nimepitwa kidgo kwenye hili hivi kuna mtu anaweza kunifahamisha role ya JF kwenye hili ilikuwa ni ipi mkapa ikapata ushindi?maana nimesoma article nzima sijaona reference ya JF

Nafurahi mno nikiona watu wasiokubali kudandia mikokoteni ya mawazo ya kundi bila kuuliza huu mkokoteni unaenda wapi. Ahsante mwanangu!
 
Ushindi unaoongelewa hapa ni ushindi katika kupambana na uoza kitu ambacho JF inapigania.

Tuko 5000 sasa hivi, mayowe yetu yanasikika na yanafanyiwa kazi.

Pia, wakati mwingine kitendo cha kufungua Thread kuhusu jambo fulani kinaleta jamba jamba kwa Waheshimiwa kiasi cha kuona ni bora yaishe kuliko kuanza kuchambuliwa kama alivyochambuliwa Demu wa Rais mstaafu, sijui mama nani yule?
 
Jamani nimepitwa kidgo kwenye hili

hivi kuna mtu anaweza kunifahamisha role ya JF kwenye hili ilikuwa ni ipi mkapa ikapata ushindi?maana nimesoma article nzima sijaona reference ya JF

Mkuu Jambo Forums huwa kuna baadhi ya watu hawakurupuki, ukiona wamesema kitu ujue kuna something behind it, na hawapendi iwepo hapa wazi na kwa sababu nyingi mbali mbali, labda unmgemuuliza mkulu kwa pm au kwa simu.

Mkuu Kuhani,

Mambo mengine upunguze jazba kidogo sio kila ishu ni malumbano na jazba tu, kuna mengi sana yanafanyika hapa JF ambayo hayawezi kuwekwa hapa usoni, ila ukiwasiliana na watu hapa kwa nje kama unaaminika utaambiwa, maana kuaminika nalo ni another story of its own!

Mambo mengine ni kuyaona na kuyaacha kama yalivyo!
 
Kuna mambo tulijifunza tuliposhughulikia suala la vijana wa Ukraine, mpambanaji asiyeadjust mbinu zake hafai kupambana. JF (na hapa tuna maana wanachama.. and believe me wapo wenye ujiko wao..) wameshiriki kwa namna ya ajabu na majina yao yatabakia nameless. Sasa, mna uamuzi wa kukubali au kukataa it doesn't matter kilichotakiwa kufanyika kimefanyika.

a. Mashtaka yaondolewe
b. Matatizo ya mlimani yatatuliwe kwa njia ya mazungumzo.
 
Najua hupendi credit na ulikuwa hutaki kuwasikiliza hawa vijana kwa kudhani kuwa ni kweli ni wavuta bangi kama Mukandala anavyowaita ...lol


Hivi wangapi katika viongozi wetu kuanzia hao (wakufunzi n.k.) ni watumiaji wa pombe ambayo ni dawa ya kulevya iliyohalalishwa? Wangapi katika hao ambao hawajawahi kuvuta bangi au kuwa na marafiki waliokuwa wanavuta bangi? Wangapi katika hao, kama ilivyoulizwa hapo juu, watoto wao ama ni walevi wa kutupwa au wanavuta bangi? Tuache kuwa hypocritical katika hii jamii. Mimi si mtumiaji wa pombe au hayo majani lakini nakubaliana na marehemu Peter Tosh aliposema "legalize it and don't criticize it, doctors smoke it and even lawyers too!" naona natoka nje ya mada. Samahani sana.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom