Ntambaswala
JF-Expert Member
- Dec 7, 2008
- 255
- 78
Kwako Malaria Sugu,
Kwa kweli nimekuwa nikivutiwa sana na uwezo wako katika kukabiliana na hoja za wapinzani wako au niseme wachangiaji wasiokubaliana na hoja zako. Huna hasira, unajibu kwa kifupi na unajua kuanzisha mada chokonozi.
Kwa kweli MS umefuzu vema katika fani yako hii ya propaganda. Japo hoja zako zaweza kuwa sio sawa upande wangu lakini uwezo wako wa kuziwakilisha katika namna ya kukera na kuudhi unajimudu vilivyo.
Kwa kuwa mimi ni mwanajamvi ambaye bado ni ''learner'' sana nahitaji sana kujifunza mengi toka kwako, maana nataka unifundishe huo ujasiri (sio hoja zako). Sijui kutuma hiyo mnaita PM sijui.. kwa hiyo nakuomba unielekeza naweza kukuona vipi ana kwa ana. Au kama unaweza kunipatia namba yako ya simu. Kwa vile wewe unajua ku pm basi naomba kama hutapenda kunijibu hadharani ni pm basi ili tuonane mkuu.
Nimeweka hapa kwa vile najua ni watu wengi watapenda kufahamiana na wewe na kupata huo utaalmu wako wa propaganda
Kwa kweli nimekuwa nikivutiwa sana na uwezo wako katika kukabiliana na hoja za wapinzani wako au niseme wachangiaji wasiokubaliana na hoja zako. Huna hasira, unajibu kwa kifupi na unajua kuanzisha mada chokonozi.
Kwa kweli MS umefuzu vema katika fani yako hii ya propaganda. Japo hoja zako zaweza kuwa sio sawa upande wangu lakini uwezo wako wa kuziwakilisha katika namna ya kukera na kuudhi unajimudu vilivyo.
Kwa kuwa mimi ni mwanajamvi ambaye bado ni ''learner'' sana nahitaji sana kujifunza mengi toka kwako, maana nataka unifundishe huo ujasiri (sio hoja zako). Sijui kutuma hiyo mnaita PM sijui.. kwa hiyo nakuomba unielekeza naweza kukuona vipi ana kwa ana. Au kama unaweza kunipatia namba yako ya simu. Kwa vile wewe unajua ku pm basi naomba kama hutapenda kunijibu hadharani ni pm basi ili tuonane mkuu.
Nimeweka hapa kwa vile najua ni watu wengi watapenda kufahamiana na wewe na kupata huo utaalmu wako wa propaganda