JF Photo Library: Mada maalum ya Picha za Zamani

c5884f1c7f390dc09a65f74aae586288.jpg
 
LEO KATIKA HISTORIA

By Malisa GJ,

Mwaka 1952 Baraza kuu la dola ya Wachagga (Chagga Supreme council) liliketi kumchagua Mangi Mkuu. Wagombea walikua watano. Abdieli Shangali wa Machame, Jackson Kitali wa Mbokomu, Petro Marealle wa Vunjo, John Maruma wa Rombo, na Thomas Marealle wa Marangu.

Baada ya mchujo walibaki Abdiel Shangali (kushoto), Petro Marealle (katikati) na Thomas Marealle (kulia). Baada ya kila mgombea kunadi sera zake, kura zilipigwa na Thomas Marealle kutangazwa mshindi.

Dola ya wachagga ilikua na muundo sawa na dola ya Uingereza (United Kingdoms). Kulikua na "nchi" kadhaa zilizounda dola hiyo. Kwa mfano Old Moshi ilikua na serikali yake, Mangi wake na jeshi lake, vivyo hivyo Uru, Kibosho, Machame, Marangu, Keni etc.

Jumla ya "nchi" 10 zilijiendesha independently, kisha zikaunda serikali ya pamoja (Federal government). Mangi Mkuu ndiye aliyekuwa Kiongozi mkuu wa "Federal government" iliyounganisha "nchi" zote 10. Alichaguliwa na Baraza la kuu la uongozi (Supreme council) ambacho kilikua chombo kikuu cha kusimamia utendaji wa serikali. Kiliundwa na Wamangi na Wachili.

Federal government ilisimamia mambo ya pamoja kama vile uchumi, diplomasia na mambo ya nje, huku mambo mengine kama miundombinu, elimu na afya yakiachwa kwa serikali za "nchi" husika.

Federal government ilifanikiwa kuanzisha sarafu yake, kuunda bendera ya shirikisho na kufungua ofisi za ubalozi Uingereza, Zanzibar na Oman. Pia mwaka 1920 ilianzisha gazeti lake lililoitwa KOMKYA, ambalo lilikua gazeti la kwanza la wazawa Afrika mashariki kabla ya Buruuli la Buganda na Imperial la Zanzibar yaliyoanzishwa 1930.

Moja ya sababu iliyomfanya Thomas Marealle kushinda kiti cha Umangi Mkuu ni elimu. Alikua mgombea pekee mwenye shahada ya uzamili (masters degree) wakati huo.

Wakati Tanganyika inapata Uhuru kulikua wachumi wawili tu wazawa ambao ni Thomas Marealle na Fredrick Mchauru. Wote wawili walisoma London School of Economics na kutunukiwa shahada za uchumi. Lakini Marealle alipata ufadhili kwenda Cambridge University (Trinity College) kufanya shahada ya pili ya uchumi.

NB: Picha ya pili, Mangi Marealle akihutubia "Chagga Supreme Council" mara baada ya kutangazwa mshindi.!
FB_IMG_1709970711989.jpg
FB_IMG_1709970708593.jpg
 
Sheria za ngumi enzi za utoto zilikuwa ni kama ifuatavyo:-
.Kupigana mara nyingi ilikuwa ni mpaka mchonganishwe
.Kabla hamjapigana mlipewa nafasi kwanza ya kuvua mashati na kama Kuna mwenye viatu ñae atavua
.Wakati mnazichapa ukitoka damu au ukitoka nundu basi unakuwa umepoteza pambano
FB_IMG_1710064485939.jpg
 
CHIFU ALIYEZUNGUKA NA HOT POT SAFARINI

Alexander (Aliki) Bandekile Mwamakula (1914 - 1996), alizaliwa Kijiji cha Iponjola, Kajunjumele ambapo sasa huitwa Isyeto (Makaburi ya Chifu Mwamakula). Alikuwa mtoto wa pili wa kiume wa Malafyale (Chifu) Bandekile Mwamakula wa Itunge, Kyela. Mwaka 1940 alikwenda Kambofi (Zambia) kufanya kazi za ukarani katika migodi ya Shaba. Taarifa zinasema kuwa aliishi miji ya Kitwe, Ndola, Shesheke, Lusaka, nk.

Mwaka 1945, akiwa Kabofi (Zambian) alipata taarifa kuwa baba yake mzazi, Chifu Bandekile Mwamakula alikuwa amefariki dunia. Alirejea nchini kumuombolezea baba yake na akarudi tena Zambia. Taratibu zilitaka kuwa mdogo wa Chifu Bandekile aliyeitwa Chifu Lasili Mwaihojo Mwamakula wa Lugombo, Mwaya ndiye arithi na achukue wake wote wa kaka yake. Mtoto wa kwanza wa kiume wa Chifu Bandekil, aliyeitwa Andalwisye, alikataa mama yake kurithiwa, kwa hiyo, Chifu Lasili akachukua wote wa Bandekile akaenda nao Mwaya isipokuwa mke mkubwa wa Chifu Bandekile, aliyeitwa Basikile Lubanga.

Chifu Andalwisye alimjengea nyumba mama yake katika mji wa mumewe kule Itunge, Kululu ambapo aliishi pale hadi pale alipofariki dunia mwaka 1963. Ndipo Chifu Andalwisye akawa ni mrithi wa mahali pa baba yake hadi alipofariki dunia mwaka 1966. Wakati hayo yakijiri, Chifu Aliki alikuwa nchini Kambofi ila alirejea nchini kumuombolezea mama yake mwaka 1963.

Chifu Aliki, alirejea nchini mwaka 1970 kabla ya kustaafu baba ya kaka yake kufariki dunia. Kwa hiyo, ilikuwa lazima Chifu Aliki arejee kwa ajili ya kurithi mamlaka ya Chifu Bandekile. Wakati hayo yote yakijiri, Chifu Korosso Mwamakula ambaye ndiye alikuwa undagili (chifu mtawala) wa nNkirwa alikuwa hai. Na alisimamia vizuri sana utaratibu wa kupeana madaraka katika ile Nyumba ya Chifu Bandekile ambaye alikuwa ni baba mdogo wa Chifu Korosso Mwamakula.

Katika kipindi chote cha miaka 4 baada ya kifo cha Chifu Andalwisye, mamlaka ilikuwa chini ya Chifu Timoti Bandekile Mwamakula ambaye alikuwa mdogo wa Chifu Aliki. Lakini utaratibu haukuruhusu yeye kuendelea kukalia Kiti cha Chifu Bandekile wakati kaka yake yungali hai. Hii ndiyo sababu iliyomfanya Chifu Aliki arejee nchini mwaka 1970.

Waliomfahamu Chifu Aliki, wanamkumbuka kwa mambo yafuatayo: Alikuwa mtu mwenye utani mwingi, hakupenda watu wavivu ingawa hakuwa mchoyo kwa wavivu. Aliwapa chakula lakini baadaye ni lazima awaseme. Alikuwa ni mtu mtanashati sana. Mahali popote alipokuwa akisafiri alikwenda na 'hot pot' zake zikiwa na chakula. Alitembea na 'hot pot' zenye ngazi alizotoka nazo Zambia. Alipenda kun'gata ulimi wake kila akifanya kazi. Wanyakyusa huitwa ni 'ukuluma ing'asi'!

Chifu Aliki alikuwa baba yangu mkubwa. Baada ya yeye walizaliwa shangazi wawili na ndipo akazaliwa baba yangu Chifu Timoti Bandekile Mwamakula (1924 - 2014). Mamlaka ya Serikali ya Mtaa imetambua Nyumba ya Bandekile kwa kutoa jina la Barabara ya Timoti, aliyekuwa ni mmoja wa watoto wake.

Picha hii chini ilipigwa Kambofi (Zambia) kati ya mwaka 1964. Chifu Aliki alinipatia picha hii mwaka 1987 kama kumbukumbu na hii ndiyo picha pekee ambayo iliyobakia katika sehemu ya kumbukumbu muhimu. Mwaka 1987 ndio mwaka ambao niliishi na Chifu kwa mara ya mwisho. Nilipokwenda nyumbani kwa likizo ya masomo niliamua kutumia muda ule kuishi na yeye kupata historia zaidi ya ukoo. Hata hivyo, Chifu Aliki hakuwa anasimulia sana habari za ukoo wake zaidi kupenda sana kusimulia zile habari za Zambia na habari za mama yake.

Mwaka 1987, Chifu Elukaga (Mzaramo), mtoto wa mwisho wa Chifu Bandekile kwa mke wake mkubwa aliyeitwa Basikakile Lubanga alifariki dunia. Habari za Chifu Elukaga Mwamakula ambaye alikuwa ni afisa katika Jeshi la Polisi Hadi Mwanzoni mwa miaka ya 1960s tutakuja kusimulia baadaye kama Mungu atatupa kibari na neema ya kuendelea kuishi.

Simulizi hii inaweza kuwa na thamani ndogo kwa ukoo wa Chifu Mwamakula na matawi yake ingawa inaweza isiwavutie wasomaji wengine. Hata hivyo, yale tusiyoyapenda na kuyathamini yanaweza kuwa na manufaa zaidi kwetu kuliko yale tunayoyapenda. Prof. Janabi anasema kuwa nyama choma, ice cream hata perfume zinaweza ziwe na manufaa kidogo kwa afya zetu kuliko kisamvu na dagaa kauzu!
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Dar es Salaam, 10 Machi 2024; 7:00 mchana
FB_IMG_1710068098069.jpg
 
WAHENGA NGOJA NIWAPE MADINI

Huko kisiwa cha Ukerewe kulikuwa na mwanamke mmoja aliyeitwa Regina. Regina na jamaa yake waliishi pamoja katika kijiji cha Namagondo. Regina alikuwa mzuri sana lakini alikuwa na mume aliyemtesa. Regina alikuwa na binti watano; Rosa Mistika, Flora, Honorata, Stella, na Sperantia. Mume wa Regina aliitwa Zakaria na alitaka sana kupata mtoto wa kiume. Regina alikuwa na mimba sasa na alimwomba Mungu ampe mtoto wa kiume.

……….

Usiku mmoja, Regina alikuwa akila chakula cha jioni pamoja na watoto wake. Alizungumza nao juu ya mambo ya malezi. Baadaye walikwenda kulala. Wakati huo huo, Zakaria alikuwa akirudi kutoka mahali pa kunywa pombe. Alilewa sana na alimwambia Regina kwamba alitaka kuwaona watoto wake. Watoto waliitwa isipokuwa Rosa kwa sababu Rosa alikuwa ameanza kuwa mtu mzima. Zakaria aliwaambia waimbe na kufanya mazoezi ya kijeshi. Mara Stella alimwambia baba yake kwamba Rosa alipokea barua pamoja na pesa. Zakaria alikasirika. Hakutaka binti zake watembee na mvulana ye yote. Rosa aliitwa na Zakaria na aliulizwa juu ya barua hiyo.
FB_IMG_1710638633514.jpg
 
Back
Top Bottom