JF ni balaa kwa Mafisadi walioko Serikalini

Indume Yene

Platinum Member
Mar 17, 2008
2,948
709
Sina budi kutoa hongera kwa wana JF wote ambao wamekuwa wakichangia hoja hapa. Siku za karibuni nilisoma thread moja hapa kuhusu Mh. SU-PIKA ooh samahani, I meant SPIKA Sitta jinsi na yeye anavyoendesha UFISADI wake kwa kutumia nafasi yake. Katika hiyo thread mtoa hoja alidokeza kuwa kuna kamati mojawapo ya Bunge iligundua huo uchafu lakini wakanyamazishwa kwa kutishiwa kukatiwa unono wa posho pamoja na trip za nje.

Jambo Forums wakaikalia hiyo ishu kidedea, watu wakatoa data n.k
Sasa nimesoma katika gazeti moja Bongo kuwa ofisi ya Katibu wa Bunge wameanzisha uchunguzi kuhusu hizo tuhuma. Ingawa sina uhakika kama hiyo ofisi itakuwa huru kumchunguza SPIKA lakini hii inaonyesha kuwa JF ni BALAA kwa Serikali yetu maana inafichua uchafu wanaofanya hao WAHESHIMIWA.

Kama kweli hizo tuhuma zitakuwa za kweli na wakam-muadhibu Spika kwa mujibu wa Katiba, nilikuwa nina dokezo dogo ambalo ni la kupiga kampeni ya kumuondoa John Cheyo kwenye huo Uenyekiti wa hiyo kamati ya Bunge kwa kufumbia macho huo uchafu wa Spika. Naamimi kutakuwa na wabunge wengine kutoka Upinzani wanaweza kufanya hiyo shughuli. Sitapenda kumuhukumu kabla hizo tuhuma hazijathibitishwa. Ila kama zitakuwa za kweli itabidi Cheyo aachie ngazi kwenye hiyo nafasi.

Again napenda kuipongeza JF na wanachama wake wote kwa kazi nzuri mnayofanya kwa faida ya Taifa letu tukufu.
MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI JAMBO FORUMS.
 
JF ni balaa kwa wale wote wasioitakia mema TANZANIA....kuanzia..SERIKALI,VYAMA,NGO'S,INDIVIDUALS,PROFFESSIONALS nk......!
ROSTAM,KARAMAGI,MBOWE,NDALU,SITA,POLISI,JEETU PATEL,na wengine wengi...kwao hawaJF is no good...!
 
JF ni balaa kwa wale wote wasioitakia mema TANZANIA....kuanzia..SERIKALI,VYAMA,NGO'S,INDIVIDUALS,PROFFESSIONALS nk......!
ROSTAM,KARAMAGI,MBOWE,NDALU,SITA,POLISI,JEETU PATEL,na wengine wengi...kwao hawaJF is no good...!

Ndio maana wakataka kuiua kwa visingizio vya JF ni "wachochezi" lakini wamegundua hakuna uchochezi bali wote tuna mapenzi ya kweli na Tanzania wala hakuna anayepigia debe kuingia msituni, bali tunapiga debe kupambana na mafisadi katika kila kona ya Tanzania.
 
JF ni balaa kwa wale wote wasioitakia mema TANZANIA....kuanzia..SERIKALI,VYAMA,NGO'S,INDIVIDUALS,PROFFESSIONALS nk......!
ROSTAM,KARAMAGI,MBOWE,NDALU,SITA,POLISI,JEETU PATEL,na wengine wengi...kwao hawaJF is no good...!

absolutely ! that was the point i intended to make. Ukisema ni balaa kwa serikali, its as if serikali ndio target, whether they are right or wrong, and i dont think thats the way it is !

Ni balaa kwa wale ambao hawasimamii haki za msingi za binadam !
 
Sawa sawa kabisa
umewasahau na mamluki wengine wa humu JF, kama Kadampinzani, Chinga na wengine wengi tuu, hawa ni vijibaraka na wanafiki wakubwa kabisa.

Mbona Mamluki ni neno zito sana? Tushindane kwa hoja na sio kuitana majina!
 
Mbona Mamluki ni neno zito sana? Tushindane kwa hoja na sio kuitana majina!
ina maana hujui kama chinga na kadampinzania ni mamluki ktk hii jf au na wewe unataka kutuletea uh****** wako hapa, ujue sisi wana jf wanatuudhi sana maana wanaonyesha msimamo wao wazi wazi wakuwatetea mafisadi,ila hawatatuweza maana nijuavyo mimi KTK VITA MUNGU YUPO UPANDE WA HAKI.
 
ina maana hujui kama chinga na kadampinzania ni mamluki ktk hii jf au na wewe unataka kutuletea uh****** wako hapa, ujue sisi wana jf wanatuudhi sana maana wanaonyesha msimamo wao wazi wazi wakuwatetea mafisadi,ila hawatatuweza maana nijuavyo mimi KTK VITA MUNGU YUPO UPANDE WA HAKI.
Bado unashindwa kuelezea ni kwa namna gani hao memba wa JF ni mafisadi...!
Kutofautiana katika kujadili hoja isiwe sababu ya kunyosha vidole..
 
Bado unashindwa kuelezea ni kwa namna gani hao memba wa JF ni mafisadi...!
Kutofautiana katika kujadili hoja isiwe sababu ya kunyosha vidole..

binafsi nasubiri kwa hamu sana aje atueleze ni kwa namna gani member JF ni mafisadi, kumbe JF pia inalea mafisadi ! sikujua, labda hiyo ndio sababu ilikuwa ikiandamwa, now i get it !
 
Kutofautiana kwa hoja inawezekana kabisa isiwe ni kigezo cha kusema kuwa fulani ni Fisadi, ila inategemea na mchangiaji wa hoja anaelekea upande gani wa hoja

Ikiwa wazi kuwa mchangiaji atakuwa wazi kabisa kwa kumsaport EL, RA na wengineo kwenye sakata la Richmonduli ambalo ushahidi wa tume teulu unaonya wazi kuwa hawa watu ni Mafisadi kabisa, hapa tunalazimika kumuita mtanchiaji Fisadi

Ikiwa wazi mchangiaji anakubaliana na mwenendo wa serikali yetu kwa kila jambo hata ambalo linaonekana wazi kuwa ni la kurudisha maendeleo ya Taifa nyuma (Kuchagua viongozi wa nchi kwa kujuana hapa nazungumzia Mawakili wakuu wa IMMA na nyadhifa zao za sasa serikali na ukitaka kujua angalia pia utendeji kazi wao kwa sasa baada ya kupata nyadhifa hizo) huyu nae atakuwa ni kwenye group la Mafisadi.

Ikiwa mchangiaji hayuko kwa ajili ya Maslahi ya wananchi na nchi kwa ujumla bali kwa ajili yake binafsi na chama chake tu, then huyu nae ni Fisadi (wachangiaji wamekuwa wakitetea hoja za vyama vyao lakini hata pale chama kinapoonyesha kuipeleka nchi mahali pabaya,(Kutumia raslimali za nchi vibaya) then unakuta mchangiaji akiendelea kukisifia na kukimwagia sifa lukuki chama)

Ikiwa hapa ndani ya JF mchangiaji anaonyesha wazi kutokuwa na moyo wa kizalendo kwa nchi yake, je inakuwaje uko kazini kwake anakofanya kazi (BOT. Wizarani, na sehemu zingine)

Na sifa nyingine nyingi sana ndugu zinafanya mchangiaji aweze kuonekana na kujajiwa kama naye ni Fisadi.

you hit the right target ! Lakini unajua hii inawalenga akina nani humu ? Nikutajie ?
 
ina maana hujui kama chinga na kadampinzania ni mamluki ktk hii jf au na wewe unataka kutuletea uh****** wako hapa, ujue sisi wana jf wanatuudhi sana maana wanaonyesha msimamo wao wazi wazi wakuwatetea mafisadi,ila hawatatuweza maana nijuavyo mimi KTK VITA MUNGU YUPO UPANDE WA HAKI.

maybe thats the way am destined to be ! Kwisha kazi ! Kama unajua kada ni fisadi, then i guess anzisha thread na umjulishe kila member kwamba kada ni fisadi ili wapate kujua zaidi !
Ninachoamini mimi sivyo utakavyoamini wewe ! JF inajitahidi sana katika kuleta maendeleo katika nchi yetu jambo ambalo silipingi hata kidogo (angalau wengine wanadai naiponda JF, which is nonsense). Majority ya JF inaangalia chama tawala ambacho kipo serikalini, kitu ambacho ni kizuri sana, na kuwakosoa pale wanapokosea ! Sasa Kada anaangalia upande wa wapinzani kabla hawajaingia ikulu na kujua uovu wao uko wapi ili tujue mapema kabla ya uovu wao haujawa kidonda baada ya wao kuingia ikulu (tutaanza tena kuikosoa wakati muda wa kuwakosoa tunao sasa hivi)watu wanasema kada hivi kada vile, but trust me i know what am doing, and i will do what i believe.
HATUTAKI WAPINZANI KESHO WAINGIE IKULU BILA YA KUCHAMBULIWA NA KUWA EXPOSED ! Lazima watakuwa magnified hata 10 times !
Nafikiri hapa ni kama tumegawana kazi, majority wanaangalia chama tawala, kada anaangalia opposition, sasa tatizo liko wapi ??
Au mmekuwa wagumu kuelewa ??
 
(Kuchagua viongozi wa nchi kwa kujuana hapa nazungumzia Mawakili wakuu wa IMMA na nyadhifa zao za sasa serikali na ukitaka kujua angalia pia utendeji kazi wao kwa sasa baada ya kupata nyadhifa hizo) huyu nae atakuwa ni kwenye group la Mafisadi.

1. Kutokujua unachosema na kujaribu kuharibu majina ya viongozi bila sababu, pia ni ufisadi kuliko the proven mafisadi kama kina Lowassa, Msabaha, na Karamagi.

2. Mawakili wawili wa IMMA wametajwa rasmi kuhusika na kampuni moja inayoshukiwa kuhusika na upotevu wa hela BOT, lakini none of them ni viongozi wa taifa, sasa kuwa na chuki binafsi na viongozi wa taifa bila a proven charges, nafiki ni ufisadi kuliko mafisadi wenyewe.

3. Uzalendo sio kuwasingizia viongozi wa taifa charges ambazo hazipo, na uzalendo sio kuwa na chuki binafsi na viongozi wa taiafa bila sababu, na uzalendo sio uwezo wa kuja hapa JF na kuanza kurusha matusi na lugha za choooni dhidi ya CCM na viongozi wa taifa, uzalendo sio kuja hapa JF na kuanza kuwashambulia wasiokubaliana na uzandiki wako dhidi ya viongozi wetu wa taifa, na uzalendo pia sio kuja hapa JF na kuanza kuita wengine mafisadi na vijibaraka, wakati ukweli ni kwamba wewe mwenyewe ndiye kijibaraka na fisadi mkubwa, mawakili wawili wa IMMA ambao ni viongozi wa taifa ni Waziri Masha na Judge Mujuluzi, hebu weka hapa mkuu ufisadi wao uliothibitishwa ni nini? Maaana so far tunajua kuwa mafisadi wameshatajwa rasmi na ushahidi unaokubalika,

1. Mkapa - (Kiwira, ANBEN, Bandari)
2. Lowassa, Karamagi, Msabaha - Richimonduli.
3. Mahalku - Hela za walipa kodi ubalozi Italy.

Wengine kuna tume nyingi zinaendelea kuwachunguza, kwa hiyo mkuu sisi wote hapa ni watu wazima, hatuhitaji kukumbushwa kila wakati kuhusu what is uzalendo na what is ufisadi, tuko hapa kwa ajili ya taifa letu, tulipokuwa tunachokonoa ufisadi kuanzia na Richimonduli wewe hukuwepo hapa, hujui jinsi tulivyowahi kutishiwa hapa personally na mafisadi, wewe umeikuta treni iko safarini, sasa usije hapa kuwafundisha watu on how ku-define ukweli na uongo,

Hatuko hapa kuwasingizia viongozi na kuwaita mafisadi, just for the fun of it, huu uwanja ni mkubwa sana mkuuu na una watu makini sana ambao walikuwepo hapa kabla hujaja hapa, tunajua ukweli, ujinga na uongo, na fisadi ni nani, ninakuomba kwa mara ya mwisho maana nimekuomba mara nyingi sana on this kuwa jaribu kuwa mstaarabu na utumiaji wa maneno, kwa sababu kila mmoja wetu hapa anaweza kuyatumia maneno as you do, kutokubaliana na hoja zako hazimafanyi member mwingine kuwa fisadi, especially zinapokuwa ni za uongo na chuki za binafsi as you always do,

Sisi wotye hapa hatuwezi kuwa vijibaraka wa uongo kama unayotaka tuwe, na hatuwezi kuwa vijibaraka wako wa kukubali tu unayosema ya uongo dhidi ya viongozi ili tu kukufurahisha wewe, au kwa kuogopa kuitwa majina yako, kwanza we are bigger than that na very smart than you think,

Acha mikwara mkuu weka hoja, na stop name calling maana most of the time huwa unajisema wewe mwenyewe mkuu. Ninarudia tena kuwa Waziri Masha na Judge Mujulusi, sio mafisadi sasa kama unao ushahidi wa ufisadi wao uliothibitishwa na jamii yetu basi uweke hapa, kama huna acha name calling! Ni mimi ninaowatetea hao mawakili wa wawili wa IMMA ambao ni viongozi wa taifa, na ninawatetea kwa sababu hakuna usahidi wa kuwahusisha na ufisadi, and I am not fisadi au kijibaraka kwa kudai ukweli, nafikiri unakuwa kijibaraka na fisadi unapojaribu ku-create uongo kwa sababu ya chuki za binafsi kwa viongzi wa taifa, sidahni kama ndio lengo la kuwepo hapa JF.

Na uzalendo sio kuwaisingizia viongozi bila makosa.

Ahsante Mkuu.
 
Back
Top Bottom