JF members asanteni sana kwa maombi yenu

Chakorii

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
18,579
50,666
Awali ya yote kabisa nimshukuru Mungu wa Mbinguni ambaye ndiye tegemeo letu sote iwe kwenye raha au shida. Na azidi kushukuriwa Mungu huyu huyu kwa kunrejesha katika hali yangu ya mwanzo, Amen.

Wana JF nawashukuru sanaaaa kwa maombi yenu ndugu zangu.maombi yenu yameninyanyua kitandani, yamenipa nguvu, yamenipa faraja ndg si mpaka nitoke naye tumbo moja, hapana!ninyi pia ni ndugu zangu.Nawashukuru sana, nilijaribu kuingia JF baada ya kuambiwa kuwa Mondray kanianzishia uzi huu; Get well soon Chakorii:Member mwenzetu wa jf Anaumwa sana..

Nilipitia baadhi ya comments nikajikuta natabasamu ingawa sikuwa vizuri kabisa baada ya hapo nikajikuta nimepata faraja ya ajabu kuona mnaniombea.

Ashukuriwe Mwenyezi Mungu aliyapokea maombi yenu akaniponya.asanteni sana.

Nimeshindwa kumshukuru mtu mmoja mmoja katika huo uzi wa Mondray na ndo maana nikafungua uzi wa shukrani kwa all JF members. Nawashukuru sana jamani. Ninamaanisha kutoka moyoni ninaposema "nawashukuru". Mungu azidi kuwabariki ndugu zangu.NAWAPENDA SANA.

Mondray asante sana mkuu, barikiwa sana mpaka ushangae.hahahahahahahahahaha hongera kwa kupunguza ban maana na wewe baba loh!!!NAKUPENDA SANA best yangu.
 
Chakorii, me & You 4 Ever...!!
Furaha yangu ni kukuona umerudi tena ukiwa na afya njema, Muda wote ule Jf niliiona chungu kwa kutokuwepo wewe..

Nataman kuandika mengi hapa ila haitakua busara kufanya hivyo but ashukuriwe Mungu wako na wangu kwa kukuponya..

I love you, to the rest of my life and you know how am I to you..

JR Forever..
 
Chakorii, me & You 4 Ever...!!
Furaha yangu ni kukuona umerudi tena ukiwa na afya njema, Muda wote ule Jf niliiona chungu kwa kutokuwepo wewe..

Nataman kuandika mengi hapa ila haitakua busara kufanya hivyo but ashukuriwe Mungu wako na wangu kwa kukuponya..

I love you, to the rest of my life and you know how am I to you..

JR Forever..
Aisee...
Is it brotherly love?
Well, glad your 'best friend' is back.
 
Back
Top Bottom