JF Kuwa Chama Tishio Cha Siasa?

Jamiiforums Kugeuzwa Chama?

  • Yawezekana

    Votes: 44 71.0%
  • Haiwezekani

    Votes: 19 30.6%

  • Total voters
    62
  • Poll closed .
Kwa nini chama cha siasa? Kwani chama cha siasa pekee ndicho chenye nafasi ya kuwakomboa watanzania?
 
Nyie mnaoishi huko ng'ambo hamjui nini kipo hapa; Kwanza JF ni zaidi ya chama cha siasa; kwa nini mnataka kujisumbua namna hii; kuna vyama; vinawasikiliza kama JF kwa mawazo na michango; naona lengo ni kujenga; vyama vilivyoppo pia vilianza na vimefanya kazi inayoonekana; sasa mie naona tunataka kupotea njia hasa kwa kudanganywa na watu wasio kuwa huku nyumbani; JF ibaki JF na kazi yake inajulikana sasa kama chanzo cha habari; mie nina wazo la kuona kama tunaweza kuanzisha ALL_BRAIN TEAM (ili wazalendo wenye malengo ya maendeleo; ubunifu wowote; biashara nk waweze kupata msaada) to name it good JF ThinkTankers..
 
Wakulu,

Kwa mawazo ya haraka haraka ni wazo jipya na geni kwa watanzania ila ni wazo zuri kama kukiwa na mikakati iliyo bora na siyo kukurupuka kama walivyofanya wakati wanaunganisha Vyama vya CUF,CHADEMA na NCCR.

Kunahitajika kufahamu ni nini lengo la kuwa na chama hiki,Je tutatumia Mbinu zipi kupata wananchama na tutafganyaje kukaa na hawa wananchama wasiweze kurubuniwa?

Pia tujue Kazi ya CCCM ni kuweka mamluuki katika vyama hivi,je tuna uwezo kiasi gani kuweza kuwalinda watu hawa wasitekwe na vyama vingine.

Ukiangalia kwa udanni kabisa masuala hayo yote nadhani sasa tuendelee na kukata ishu tu kwa sasa mpaka hapo baadaye.Ateleat tuone Upinzani ukipata Nguvu(aU kuvunjika kwa CCM kama wengine wanavyotaka iwe isivyo)
 
Nyie mnaoishi huko ng'ambo hamjui nini kipo hapa; Kwanza JF ni zaidi ya chama cha siasa; kwa nini mnataka kujisumbua namna hii; kuna vyama; vinawasikiliza kama JF kwa mawazo na michango; naona lengo ni kujenga; vyama vilivyoppo pia vilianza na vimefanya kazi inayoonekana; sasa mie naona tunataka kupotea njia hasa kwa kudanganywa na watu wasio kuwa huku nyumbani; JF ibaki JF na kazi yake inajulikana sasa kama chanzo cha habari; mie nina wazo la kuona kama tunaweza kuanzisha ALL_BRAIN TEAM (ili wazalendo wenye malengo ya maendeleo; ubunifu wowote; biashara nk waweze kupata msaada) to name it good JF ThinkTankers..

Tumeisha anza kubaguana, wa ng'ambo, wa ndni, tutaendelea wa DSM, KIGOMA, zanzibar, tukifika mbeya tutaanza wa mwanjelwa, kyela, rungwe mpaka vijiji!

Please msiweke aina yeyote ya nani yuko wapi ndiyo anaweza kufanya kitu fulani, sisi ni watanzania na tutakuwa hivyo no matter who is where doing what!

Ili ni wazo tu, hata wazo lako linaweza kukosolewa pia.

Mimi nadhani mtoa maada hana lingine bali amechoshwa na mwenendo wa vyama vingi vya siasa tulivyonavyo, kimoj tu kiko laivu kati ya 12 tulivyonavyo na nina hakika vingine watu hawavijui!!

Hii maada ya uchokozi!
 
Tumeisha anza kubaguana, wa ng'ambo, wa ndni, tutaendelea wa DSM, KIGOMA, zanzibar, tukifika mbeya tutaanza wa mwanjelwa, kyela, rungwe mpaka vijiji!...


Na huo ndio moja ya ubaya wa siasa, nashangaa sana watu wanashabikia kwenda kwenye mrengo huo, tutaharibikwia huko jamani. Tufikiria jingine ambalo linaweza kufanikisha azma yetu, tusiingie kwenye sias, at least in the near future
 
Ni wazo zuri! Suggestion of name, Democratic Forum of Tanzania. Vitu vingi vya maana vilianzishwa kimzahamzaha! Even if you think we are delusional and daydreaming, let us continue to play with the idea, we might get some real interesting result.
Kwa upande wa Rev Kishoka, ana waraka wake ambao tayari ni mwongozo mzuri kwa chama chochote kile. Let the initiator of this thread, take apprpriate steps.
 
Kwa nini chama cha siasa? Kwani chama cha siasa pekee ndicho chenye nafasi ya kuwakomboa watanzania?

Tupe mawazo ni kipi mbadala kinachoweza kuwakomboa Watanzania kwa ukamilifu na kivipi? SACCOS? NGO? What? Tuelimishe!
 
Nyie mnaoishi huko ng'ambo hamjui nini kipo hapa; Kwanza JF ni zaidi ya chama cha siasa; kwa nini mnataka kujisumbua namna hii; kuna vyama; vinawasikiliza kama JF kwa mawazo na michango; naona lengo ni kujenga; vyama vilivyoppo pia vilianza na vimefanya kazi inayoonekana; sasa mie naona tunataka kupotea njia hasa kwa kudanganywa na watu wasio kuwa huku nyumbani; JF ibaki JF na kazi yake inajulikana sasa kama chanzo cha habari; mie nina wazo la kuona kama tunaweza kuanzisha ALL_BRAIN TEAM (ili wazalendo wenye malengo ya maendeleo; ubunifu wowote; biashara nk waweze kupata msaada) to name it good JF ThinkTankers..

Tujikumbushe . . . .

Nyerere alikuwa Mwanachama wa TAA

Baada ya TAA kuonekana haina meno ya kutosha, wakaibadilisha TAA kuwa TANU

Akaacha kazi ili kuiimarisha TANU.

I am assuming the messgae is clear!
 
Na huo ndio moja ya ubaya wa siasa, nashangaa sana watu wanashabikia kwenda kwenye mrengo huo, tutaharibikwia huko jamani. Tufikiria jingine ambalo linaweza kufanikisha azma yetu, tusiingie kwenye sias, at least in the near future

Mkuu; hata watoto wa familia moja wanatofautiana wakati mwingine. Ya kawaida hayo.

Clinton na Obama, good example.
 
What will be our fundermental goals?? This will help having political focus and direction. Will it be iParty? What are the milestone?
 
GM, Jafar, Jasusi, KatuleJ, Malunde-malundi, Mbassa, Mpita Njia, Mwita Maranya, Mzuzu, Waberoya . . . . .

Kweli hatuwezi Wakuu?
 
Tupe mawazo ni kipi mbadala kinachoweza kuwakomboa Watanzania kwa ukamilifu na kivipi? SACCOS? NGO? What? Tuelimishe!

Nyerere huyohuyo inayenukuu maandishi yake alisema ilituendelee tunahitaji mambo manne... chama cha siasa si moja kati ya mambo hayo
 
Umemuelewa sana na alichosema ni kweli kabisaaaaaa, na mimi kwa kuongezea, vipi chadema imewakifu?

Kama unalazimisha kuwa tumeelewa sawa, kama unania ya kufafanua, tutashukuru. The question was so simple and clear.

Kuna yeyote aliyesema CHADEMA imemkifu au haujamkifu? What happened to Mbeya?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom