Ibrah
JF-Expert Member
- Mar 22, 2007
- 2,729
- 528
Wana JF,
Tumekuwa tukifuatilia kampeni na Uchaguzi wa Tarime ambapo Mtu mzima pwaa! LAkini matukio yaliyoendela wakati wa Kampeni yalimuhusisha sana mtu aitwaye Peter Zakaria kwa mambo yafuatayo:
1. Kuwalisha Polisi waliopelekwa Tarime chini ya Kamanda wa Operation Venance Tossi. Hii ni fedheha kubwa kwa nchi na jeshi letu la Polisi kwani ilismekana hawakuwa hata na posho na hata chakula kilikuwa cha shida kwa Askari hawa na hivyo kupelekea Zacharia kuwalisha Askari wetu ili wapate nguvu ya kuwanyamazisha Wana TArime.
2. Katika tukio la kujeruhiwa kwa Wafuasi 4 wa CHADEMA kwa kukatwa mapanga na Wana CCM, ni gari la ZAcharia ambalo nilo lililokamatwa kwa kuwa liliwabeba Wakereketwa hawa waliokuwa na silaha aina ya mapanga.
Nataka kujua Wajameni, huyu mtu ni nani na ana nguvu na jeuri gani ya kufanya haya? Anajiamini kitu gani kuweza kuwatendea hivi wana TArime kwa kufadhili ugaidi na ujambazi huu? Polisi wameshthibitisha kuwa ni gari lake ndilo liliwabeba wale jamaa waliowakata mapanga Wanachadema waliokuwa wakisubiri helkopta ya Chama chao kutelemka na kwa nini hatujasikia amekamatwa na kufikishwa mahakamani? Au ndo Polisi wanaogopa wakimkamata basi hakuna chakula Tarime na watakufa njaa?
Hivi ni kweli Jeshi la Polisi lilikuwa halina pesa za kuwahudumia askari wake hata kwa Chakula jamani? Habari nilizonazo hapa Arusha ni kuwa Askari wengi waligwaya na kutoa vizingizio kibao ili kuepuka kupelekwa TArime kwenye Operation hiyo Maalumu ya kuwasaidia CCM na Watu wao.
Tumekuwa tukifuatilia kampeni na Uchaguzi wa Tarime ambapo Mtu mzima pwaa! LAkini matukio yaliyoendela wakati wa Kampeni yalimuhusisha sana mtu aitwaye Peter Zakaria kwa mambo yafuatayo:
1. Kuwalisha Polisi waliopelekwa Tarime chini ya Kamanda wa Operation Venance Tossi. Hii ni fedheha kubwa kwa nchi na jeshi letu la Polisi kwani ilismekana hawakuwa hata na posho na hata chakula kilikuwa cha shida kwa Askari hawa na hivyo kupelekea Zacharia kuwalisha Askari wetu ili wapate nguvu ya kuwanyamazisha Wana TArime.
2. Katika tukio la kujeruhiwa kwa Wafuasi 4 wa CHADEMA kwa kukatwa mapanga na Wana CCM, ni gari la ZAcharia ambalo nilo lililokamatwa kwa kuwa liliwabeba Wakereketwa hawa waliokuwa na silaha aina ya mapanga.
Nataka kujua Wajameni, huyu mtu ni nani na ana nguvu na jeuri gani ya kufanya haya? Anajiamini kitu gani kuweza kuwatendea hivi wana TArime kwa kufadhili ugaidi na ujambazi huu? Polisi wameshthibitisha kuwa ni gari lake ndilo liliwabeba wale jamaa waliowakata mapanga Wanachadema waliokuwa wakisubiri helkopta ya Chama chao kutelemka na kwa nini hatujasikia amekamatwa na kufikishwa mahakamani? Au ndo Polisi wanaogopa wakimkamata basi hakuna chakula Tarime na watakufa njaa?
Hivi ni kweli Jeshi la Polisi lilikuwa halina pesa za kuwahudumia askari wake hata kwa Chakula jamani? Habari nilizonazo hapa Arusha ni kuwa Askari wengi waligwaya na kutoa vizingizio kibao ili kuepuka kupelekwa TArime kwenye Operation hiyo Maalumu ya kuwasaidia CCM na Watu wao.