Al Watani
JF-Expert Member
- Dec 28, 2014
- 20,517
- 30,580
Hivi kulikuwa na uhujumu uchumi au sera mbovu na mitazamo hasi ya kijamaa ndiyo iliyopelekea watawala wetu kuwaona matajiri wanahujumu uchumi ?
Mimi sijawahi kulielewa hili suala la uhujumu uchumi ulikuwa ni uporaji wa kidola tu na wala haukuwa na msaada wowote kwa wananchi badala ya kuzalisha mateso na ufukara.
Watu wanamsifia Sokoine kwa kupora Mali za watanzania ambao walizipata kwa uhalali no wonder hata sasa kuna uporaji wa kidola na unyanyasaji unaitwa vita ya kiuchumi while in fact ni matokeo ya sera mbovu tu za watawala wetu.
Mimi sijawahi kulielewa hili suala la uhujumu uchumi ulikuwa ni uporaji wa kidola tu na wala haukuwa na msaada wowote kwa wananchi badala ya kuzalisha mateso na ufukara.
Watu wanamsifia Sokoine kwa kupora Mali za watanzania ambao walizipata kwa uhalali no wonder hata sasa kuna uporaji wa kidola na unyanyasaji unaitwa vita ya kiuchumi while in fact ni matokeo ya sera mbovu tu za watawala wetu.
Ni kweli alikuwa mzalendo, lakini alionea wananchi katika kampeni dhidi ya walioitwa wahujumu uchumi.
Mwalimu Nyerere na Sokoine walishindwa kuendesha uchumi wa nchi, badala yake wakaanza kulaumu na kusingizia kuwa hali mbaya ya uchumi imesababishwa na wahujumu uchumi na walanguzi.
Nawaelewa zaidi wanaomkubali Sokoine kwa kutambua mchango wake alipokuwa waziri mkuu wakati wa Vita vya Kagera, na siyo wakati wa vita dhidi ya wahujumu uchumi.