Jeshi lijitathimini kuhusu uadilifu na uaminifu wake kwa Watanzania wote

Whitesmith

JF-Expert Member
Aug 12, 2017
386
517
Ndg wanajamvi habari za jumapili.
Niende kwenye mada moja kwa moja, “Jeshi lijitathimini” ndiyo Jeshi letu kwa macho ya nje limejivika vazi nzuri la uaminifu macho pa Watanzania wote lakini kwa ndani linapokuja suala la Ajira ndani ya Jeshi hasa hili tunaloliona la vijana wa JKT siyo Waaminifu kabisa. Wakuu wetu hawa wajitathimini tena kwanini wanazipoka haki za vijana wetu hawa hasa ambao hawana mahala pakuegemea.

Sakata la “Uasi wa Vijana wa JKT”
Jambo hili litazamwe upya na hawa vijana wasaidiwe hata km siyo ndani ya JWTZ lkn wapewe ajira maana hii ilikuwa ahadi ya Rais wa awamu ya tano. Kuna michezo mibaya sana labda kama Rais Samia hajui atadanganywa. Kabla vijana hawa kuna vijana ambao walishiriki shughuli mbalimbali za ujenzi kuanzia ngerengere, Dodoma nk ambao km ilivyo kwa hawa “Waasi”, wao walipewa ahadi nawakatimiziwa lakini haikuwa rahisi.

Ilianza kama ilivyokuwa kwa hawa “waasi” wakarejeshwa vikosini nakupewa Vyeti vyakumaliza mkataba wakatakiwa kuondoka huku wakipewa maagizo kuwa watatafutwa kukiwa na mabadiliko. Vijana wale wakafanya jitihada za kuwasiliana na uongozi lkn wakapewa maagizo kuwa waondoke hatua ya mwisho wakahangaika kupata mawasiliano ya alikuwa Rais Marehemu JPM wakafanikiwa, wakamweleza kuwa tumerudishwa nyumbani, JPM alishangaa kwann warudishwe wakati taarifa aliyonayo wanafanyiwa mchakato wa ajira na ana list amepelekewa?

Ndipo alipomwagiza Brigedia Mbuge ampelekea list ya vijana walioshiriki ujenzi kuanzia ukuta wa mererani, Ngerengere na Dodoma, uzuri Mbuge alishtuka akapeleka list iliyohalisi ndipo JPM akagundua kuna waliochomekwa. Akaagizwa vijana waliositishiwa mkataba warejeshwe na hatimaye sasa ni Wanajeshi.

Natoa hii historia ili kwa wale ambao hawaelewi figisu zilipopo Jeshini linapokuja suala la Ajira watambue kuwa vijana wale walijua wazi kuwa wanaondolewa kijanja ili wengine wachomekewe. Rais wangu Samia wangalie vizuri hao wakuu na uchukue hatua vijana hawa wanapigania haki zao walioahidiwa na Rais JPM. Pili, Jeshi linaongozwa na binadamu usije fikiria hakuna maovu huku ndani hapana yapo tu.

Linapokuja suala la maslahi huwa kuna misemo kama “Mbanga na Mbuyu” linakuwa na nguvu. Wakuu wetu katika hili siyo waaminifu wala waadilifu wao wanaangalia ndugu zao na watoto wao kwanza linapokuja suala la kuingia Jeshini.

Mjitathimini, Mjisahihishe “Jeshi la Ulinzi Wawananchi wa Tanzania” siyo vizuri kulisha nyumbu yako kwa jasho na damu za wengine
 
Wewe nadhani ni kati ya hao waliolazimisha ikaamriwa mrudishwe ilihali hamkidhi kulingana na vigezo, sasa mpo na ni Askari tayari. Kwahiyo unapigania na hawa walioonyesha migomo na kuandamana nao warejeshwe na kuingizwa Jeshini!!!!!.


Msitake kutuharibia Nchi yetu.
 
Na wakupewa fursa na wale wote walioko mtaani nao wafikiriwe hivi serikali kwa nini isiwapeleke hata mbungani huko wakalinde nyumbu mbona tuna mapori kibao tuu ya hifadhi za taifa?
 
Na wakupewa fursa na wale wote walioko mtaani nao wafikiriwe hivi serikali kwa nini isiwapeleke hata mbungani huko wakalinde nyumbu mbona tuna mapori kibao tuu ya hifadhi za taifa?

Sent using Jamii Forums mobile app
kulinda mbuga ni zaidi ya mafunzo ya kijeshi. ndio maana taasis zilizoko chini ya wizara ya maliasili tanapa ,tawa,tfs huchukua vijana jkt na kuwapeleka kozi maalumu kwa miezi sita..
kozi ina include paramilitary training na uhifadhi wa wanyama pori.

and yes hizo taasisi zinachukua vijana kila mwaka jkt.
 
Mabeyo kutoka hadharani, tena mbele ya Rais na kutoa tamko la kuwatimua haikuwa bahati mbaya!

Kwenye hafla moja hivi, Mabeyo alisema jeshi lipo tayari kumtii Rais ambaye ni Mama Samia, lakini akataka kusema kitu mwishoni akamezea kuwa atamwasilishia Rais ofisini, ni nani anayejua alichotaka kusema...!?
Kuna waliong'amua kuwa kuna nyuma ya pazia!

Hivyo hao vijana hawajatimuliwa kwa bahati mbaya, jeshi linataratibu zake!
 
kulinda mbuga ni zaidi ya mafunzo ya kijeshi. ndio maana taasis zilizoko chini ya wizara ya maliasili tanapa ,tawa,tfs huchukua vijana jkt na kuwapeleka kozi maalumu kwa miezi sita..
kozi ina include paramilitary training na uhifadhi wa wanyama pori.

and yes hizo taasisi zinachukua vijana kila mwaka jkt.
Kwani si nao watapelekwa kozi kwani shida iko wapi
 
Hao madogo wenge tu limewasumbua
Na wangekuwa wanajeshi full na kwa kitendo
Hicho wangefanywa kitu mbaya

Ova
 
Wewe nadhani ni kati ya hao waliolazimisha ikaamriwa mrudishwe ilihali hamkidhi kulingana na vigezo, sasa mpo na ni Askari tayari. Kwahiyo unapigania na hawa walioonyesha migomo na kuandamana nao warejeshwe na kuingizwa Jeshini!!!!!.


Msitake kutuharibia Nchi yetu.
 
Wewe nadhani ni kati ya hao waliolazimisha ikaamriwa mrudishwe ilihali hamkidhi kulingana na vigezo, sasa mpo na ni Askari tayari. Kwahiyo unapigania na hawa walioonyesha migomo na kuandamana nao warejeshwe na kuingizwa Jeshini!!!!!.


Msitake kutuharibia Nchi yetu.
Uko kihisia zaidi mzee, wale wamepewa ahadi ya moja kwa moja wakikamilisha mission waajiriwe Jeshini direct sasa labda ndo moja ya maasi kwa Mwendazake
 
Uko kihisia zaidi mzee, wale wamepewa ahadi ya moja kwa moja wakikamilisha mission waajiriwe Jeshini direct sasa labda ndo moja ya maasi kwa Mwendazake
Magufuli alikosea PERIOD.

Jeshi haliendeshwi kwa hotuba za kuwapendezesha wapiga kura.

Lipo pale kikazi zaidi.

Vyombo vingine vya ulinzi na usalama walijazwa huko kina Makonda, Musiba na wengine.

Wamekuwa kituko.

Vyombo hivi haviingiliwi ili vifanye kazi ya Taifa, siyo ya mtu.
 
Back
Top Bottom