Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,005
- 9,872
Jeshi la Myanmar limethibitisha kulidhibiti taifa hilo baada ya kumuweka kizuizini kiongozi wa taifa hilo Aung San Suu Kyi pamoja na wanasiasa wengine mapema hii leo.
Baada ya kumkamata kiongozi huyo kwa saa kadhaa, televisheni ya taifa imetangaza kuwa katika hali ya dharura kwa muda wa mwaka mmoja.
Aung San Suu Kyi, kiongozi wa Myanmar, ambaye chama chake cha National League for Democracy (NLD) kipo madarakani amekamatwa, msemaji wa chama amesema.
Hatua hiyo ilikuja wakati wa mvutano mkali kati ya raia na wanajeshi wakihofia jeshi kutawala.
Katika uchaguzi uliofanyika mnamo mwezi Novemba, chama cha NLD kilishinda kura nyingi lakini jeshi likadai kuwa kura zilikuwa zimeibwa.
Myanmar ambayo inajulikana kama Burma, ilikuwa ikiongozwa na jeshi mpaka mwaka 2011. Kwa miaka mingi, Bi Suu Kyi alikuwa katika kifungo cha nyumbani.
Wanajeshi walikuwa mitaani katika mitaa ya mji mkuu wa Naypyitaw pamoja na mji wa Yangon. Huduma za simu na mtandao zilizimwa katika miji mikubwa wakati televisheni ya taifa inasema kwamba kulikuwa na itilafu za kiufundi.
Baada ya kumkamata kiongozi huyo kwa saa kadhaa, televisheni ya taifa imetangaza kuwa katika hali ya dharura kwa muda wa mwaka mmoja.
Aung San Suu Kyi, kiongozi wa Myanmar, ambaye chama chake cha National League for Democracy (NLD) kipo madarakani amekamatwa, msemaji wa chama amesema.
Hatua hiyo ilikuja wakati wa mvutano mkali kati ya raia na wanajeshi wakihofia jeshi kutawala.
Katika uchaguzi uliofanyika mnamo mwezi Novemba, chama cha NLD kilishinda kura nyingi lakini jeshi likadai kuwa kura zilikuwa zimeibwa.
Myanmar ambayo inajulikana kama Burma, ilikuwa ikiongozwa na jeshi mpaka mwaka 2011. Kwa miaka mingi, Bi Suu Kyi alikuwa katika kifungo cha nyumbani.
Wanajeshi walikuwa mitaani katika mitaa ya mji mkuu wa Naypyitaw pamoja na mji wa Yangon. Huduma za simu na mtandao zilizimwa katika miji mikubwa wakati televisheni ya taifa inasema kwamba kulikuwa na itilafu za kiufundi.