figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,888
Mkuu wa majeshi ya Thailand, Jenerali Prayuth Chan-ocha ametangaza mapinduzi, akisema jeshi la Thailand limetwaa madaraka na kuiondoa madarakani serikali ya uangalizi. Pia limetangaza kusimamisha kwa muda utekelezaji wa katiba , lakini baraza la juu la bunge la nchi hiyo litaendelea kufanya kazi.
Akitoa hotuba kwenye televisheni, Jenerali Prayuth amesema jeshi limechukua hatua hiyo ili kuepuka vifo na majeruhi zaidi kwa raia na kuzuia hali ya sasa izidi kuwa mbaya. Lakini, waziri mkuu wa serikali ya uangalizi amesisitiza kuwa hatajiuzulu na kutangaza kuwa leo ataitisha mkutano wa baraza la mawaziri.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bw. John Kerry amesema, anasikitishwa na kitendo cha jeshi la Thailand kusimamisha utekelezaji wa katiba, na kusema mapinduzi hayo ya kijeshi yataathiri uhusiano kati ya Marekani na Thailand.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki-moon ametoa taarifa kupitia msemaji wake akisema anafuatilia kwa karibu hali ya Thailand, na kutoa wito kwa Thailand kurudi kwenye utawala wa kiraia. Pia amehimiza pande zote husika kujitahidi kuepuka mapambano na kuheshimu haki za binadamu.mia
Chanzo:CRI