beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Marekani na Umoja wa Ulaya wameuonya utawala wa kijeshi nchini Sudan, kutofanya uamuzi wa upande mmoja juu ya uteuzi wa waziri mkuu mpya baada ya kiongozi wa kiraia Abdallah Hamdok kujiuzulu, katikati ya maandamano ya kuupinga utawala huo wa kijeshi
Katika taarifa ya pamoja Marekani, Uingereza, Norway na Umoja wa Ulaya wamesema hawatamuunga mkono waziri mkuu atakayeteuliwa, iwapo wadau wengi wa kiraia hawatahusishwa
Taarifa hiyo ya pamoja pia imetoa mwito wa kuendelea kwa maandalizi ya uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwaka 2023 chini ya makubaliano ya kipindi cha mpito, lakini pia kuimarishwa kwa mfumo huru wa mahakama na bunge, huku ikionya hatua ya upande mmoja ya kuteua waziri mkuu mpya na baraza la mawaziri inaweza kudhoofisha uaminifu wa taasisi hizo.
Katika taarifa ya pamoja Marekani, Uingereza, Norway na Umoja wa Ulaya wamesema hawatamuunga mkono waziri mkuu atakayeteuliwa, iwapo wadau wengi wa kiraia hawatahusishwa
Taarifa hiyo ya pamoja pia imetoa mwito wa kuendelea kwa maandalizi ya uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwaka 2023 chini ya makubaliano ya kipindi cha mpito, lakini pia kuimarishwa kwa mfumo huru wa mahakama na bunge, huku ikionya hatua ya upande mmoja ya kuteua waziri mkuu mpya na baraza la mawaziri inaweza kudhoofisha uaminifu wa taasisi hizo.