Jeshi la Polisi Zanzibar lapiga marufuku kutibiwa majeraha hospitalin bila PF3

Fredwash

JF-Expert Member
Oct 27, 2009
1,041
1,375
jaman naomba wajuze wa mambo mtujuze.. je hii sheria ya pf3 kwel haijapitwa na wakat...

kwangu mm naona ilitakiwa walau wailegeze kuwa mtu atibiwe lakin kila hospt iwe na free toll call kwa vituo vya polis wakipokea mgonjwa wanamtibu wakat huo huo wanatoa taarifa zake kamil kwa polisi.. kwa maana ya jina, umri, anapoishi, alivyoumia then haruhusiw kutoka bila hiyo pf3, yaan ndio itumike wakat wa kumdischarge, la sivyo watu watakuwa wanafia mapokez ama eneo la tukio kisa hawez pelekwa hospt bila pf3

===============

Jeshi la Polisi Zanzibar latoa onyo kwa hospitali zinazotibu watu walioumia bila PF3.

Jeshi la Polisi Zanzibar limepiga marufuku na limesisitiza kuwa litawachukulia hatua za kisheria madaktari na hospitali ambazo zinawatibu watu waliojeruhiwa au kuumia bila ya fomu ya polis-PF3 huku ikisema haina uhusiano wowote na vikundi vinavyoitwa Zombie.

Kauli hiyo ya polisi imetolewa na naibu mkuurgenzi wa upelelezi na makosa ya jinai Zanzibar naibu kamishna Salum Msangi wakati akiongea na waandishi wa habari katika makao makuu ya jeshi hilo hapa Zanzibar ambapo amesema pamekuwepo na baadhi ya wahalifu wamekuwa wakitiwa na madaktari bila ya utaratibu hali ambayo inahatarisha jamii hivyo amesema polisi iko makini itachukua hatua.

Akizungumzia malalamiko ya kuwepo kikundi kianchitwa Zombie ambacho kinalalamikiwa kuwapiga wananchi kamishna Msangi amesema polisi haina taarifa yeyote yakuhusika na kikundi hicho na kuwataka wananchi kutoa taarifa polisi wanapokutana au kupigwa na kikundi hicho kwa vile hadi sasa hakuna taraifa yeyote polisi inayuhusu kikundi hicho.

Mkuu huyo wa upelelezi Zanzibar pia ametahadharisha watu walioanza kupeperusha vipeperushi vya kuhatarisha amani huku pia akisisitiza jeshi hilo lemejipanga kuhakikisha usalama na amani inakuwepo wakati wa uchaguzi mkuu wa Zanzibar Machi 20.

Chanzo: ITV
 
Jeshi la Polisi Zanzibar limepiga marufuku na
limesisitiza kuwa litawachukulia hatua za kisheria
madaktari na hospitali ambazo zinawatibu watu
waliojeruhiwa au kuumia bila ya fomu ya polis-PF3
huku ikisema haina uhusiano wowote na vikundi
vinavyoitwa Zombie.

Kauli hiyo ya polisi imetolewa na naibu mkuurgenzi wa
upelelezi na makosa ya jinai Zanzibar naibu kamishna
Salum Msangi wakati akiongea na waandishi wa habari
katika makao makuu ya jeshi hilo hapa Zanzibar
ambapo amesema pamekuwepo na baadhi ya wahalifu
wamekuwa wakitiwa na madaktari bila ya utaratibu
hali ambayo inahatarisha jamii hivyo amesema polisi
iko makini itachukua hatua.

Akizungumzia malalamiko ya kuwepo kikundi
kianchitwa Zombie ambacho kinalalamikiwa kuwapiga
wananchi kamishna Msangi amesema polisi haina
taarifa yeyote yakuhusika na kikundi hicho na
kuwataka wananchi kutoa taarifa polisi wanapokutana
au kupigwa na kikundi hicho kwa vile hadi sasa hakuna
taraifa yeyote polisi inayuhusu kikundi hicho.

Mkuu huyo wa upelelezi Zanzibar pia ametahadharisha
watu walioanza kupeperusha vipeperushi vya
kuhatarisha amani huku pia akisisitiza jeshi hilo
lemejipanga kuhakikisha usalama na amani inakuwepo
wakati wa uchaguzi mkuu wa Zanzibar Machi 20.

› Jeshi la Polisi Zanzibar latoa onyo kwa
hospitali zinazotibu watu walioumia bila
PF3.

Chanzo: ITV
 
jaman naomba wajuze wa mambo mtujuze.. je hii sheria ya pf3 kwel haijapitwa na wakat...

kwangu mm naona ilitakiwa walau wailegeze kuwa mtu atibiwe lakin kila hospt iwe na free toll call kwa vituo vya polis wakipokea mgonjwa wanamtibu wakat huo huo wanatoa taarifa zake kamil kwa polisi.. kwa maana ya jina, umri, anapoishi, alivyoumia then haruhusiw kutoka bila hiyo pf3, yaan ndio itumike wakat wa kumdischarge, la sivyo watu watakuwa wanafia mapokez ama eneo la tukio kisa hawez pelekwa hospt bila pf3

Fredwash,
Mazombie wanapiga watu wanawajeruhi.
Waziri Mdogo wa Mambo ya Ndani Hamad Masauni alipoulizwa na Mbunge wa Malindi
Mheshimiwa Ally Saleh kuhusu ''Mazombie'' alijibu kuwa hana taarifa hizo.

Baada ya siku chache tu Polisi Zanzibar ikasema kuwa Mazombie ni ''Polisi Shirikishi.''
Soma maelezo ya ziada hapo chini:
Salma Said
5 hrs ·
Jeshi la Polisi Zanzibar limetoa onyo kali kwa madaktari wanaowahudumia watu wanaokwenda hospitali baada ya kupigwa na kikundi cha Mazombi bila ya kuwa na karatari ya PF3 kutoka Polisi. Onyo hilo limetolewa leo na Mkurugenzi wa Upelelezi Zanzibar, Salum Msangi wakati akizungumza na waandishi wa habari, Makamo Makuu ya jeshi hilo Kilimani Mkoa wa Mjini Magharibi. Pia limetoa onyo kwa watu wenye kusambaza vipeperushi na wenye kuwapigia X nyumba zao. aidha wananchi wamehakikishiwa kuwa uchaguzi utafanyika kwa usalama na amani kabisa na kupewa onyo kali ambao watahatarisha amani ya nchi. Picha hii ni Kamishna Hamdan kwa kuwa yeye ndio Boss na sio Salum Msangi.

12670258_1564621547162668_2816280455941648077_n.jpg



Mohamed Said SS askari watesaji wa Hitler walikuta kikundi cha Wayahudi katika kambi ya mateso na mauaji Auschwitz, Poland wakati wa Vita Vya Pili Vya Dunia, kinatoka kufanya kazi basi wakakiingilia kukipiga kwa magongo na vitako vya bunduki.

Wayahudi walikuwa hawawezi kujibu mashambulizi yale kwani kufanya hivyo mtu anapigwa risasi hapo hapo kwa hiyo hali ilikuwa heri nusu shari kupigwa ukabaki na uhai wako kuliko shari kamili kumkabili adui ukauliwa.

Baada ya kuwapiga kefu yao wale SS wakawauliza wale Wayahudi,''Mnajua kwa nini tunakupigeni?''

Wayahudi wakajibu kuwa hawakuwa wanajua. ‘’Tunakupigeni kwa sababu tunasikia raha kukupigeni.’’ Hili ndilo lilikuwa jibu la askari wa Hitler.

Zanzibar nchi ya Kiislam iliyokuwa inasifika kwa ustaarabu na uungwana na kitovu cha elimu ya Kiislam leo Zanzibar imekuwa nchi ya kishenzi...
 
Anayedhani wanzanzibari watakabiliana na jwtz AK 47 kwa mawe anajidangaya . Mbadala upo.
 
Jinsi magazeti ya Tanganyika yanavyoandika na ukifika Zanzibar hali ipo tofauti..naona kama kuna propaganda za siasa kuliko uhalisia..ngoja sasa tuwaone hao majeruhi
 
The rights are taken,they are not given
Haki huchukuliwa,HAIOMBWI.
kuomba haki yako ni ama woga,uchizi au kutojitambua,ila ukijitambua wakati wa kuchukua haki si lelemama,hili napenda alitambue yeyote anaenidhulumu.
Get up stand up,stand up for your rights!(BOB MARLEY AND THE WAILING WAILERS).ni wimbo tu.
 
Hao police wanamiliki hizo hospital??? Kwanini wasithibiti hao zombies wao???
 
Back
Top Bottom