Jeshi la Polisi Tanzania, wakati wa kuondoa zuio lenu umewadia. Tafadhalini ondoeni!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Zuio lenu la kuzuia mikutano,maandamano na makongamano ya kisiasa ya ndani na nje liliwafikia walengwa. Kuanzia siku lilipotolewa,wahusika wamelitekeleza ima kwa shurti au utii. Malalamiko yakatamalaki.

Mwezi huu,CCM tutakuwa na mkutano wetu mkuu pale Dodoma. Wajumbe wa mkutano wetu mkuu ni wengi kutoka nchi nzima. Dodoma itafurika na kufurahisha. Mkutano wetu wa Dodoma,kwa mujibu wa katazo lenu la kipolisi,nao umekatazwa. Haupaswi kufanyika bila kuondolewa kwa katazo.

Vyama vingine vya siasa nchini navyo vinatamani kufanya mikutano yao. Kujitangaza,kuongea na wananchi na kujiimarisha. Kufanya siasa hasa na si hasi za visasi. Jeshi la polisi,mmekuwa mkifanya kazi kubwa ya kulinda usalama. Mnastahili pongezi. Tafadhalini,ondoeni zuio lenu ili CCM na wengine wafaidi matunda ya demokrasia ya vyama vingi.

Jeshi la polisi,tusaidieni CCM twende Dodoma kwa amani kumkabidhi uenyekiti wa chama Rais mpendwa John Pombe Magufuli. Wakati sisi CCM tukifurahi,wapinzani nao wafurahi. Muda wa kuondolewa zuio umewadia!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Singida)
 
Zuio lenu la kuzuia mikutano,maandamano na makongamano ya kisiasa ya ndani na nje liliwafikia walengwa. Kuanzia siku lilipotolewa,wahusika wamelitekeleza ima kwa shurti au utii. Malalamiko yakatamalaki.

Mwezi huu,CCM tutakuwa na mkutano wetu mkuu pale Dodoma. Wajumbe wa mkutano wetu mkuu ni wengi kutoka nchi nzima. Dodoma itafurika na kufurahisha. Mkutano wetu wa Dodoma,kwa mujibu wa katazo lenu la kipolisi,nao umekatazwa. Haupaswi kufanyika bila kuondolewa kwa katazo.

Vyama vingine vya siasa nchini navyo vinatamani kufanya mikutano yao. Kujitangaza,kuongea na wananchi na kujiimarisha. Kufanya siasa hasa na si hasi za visasi. Jeshi la polisi,mmekuwa mkifanya kazi kubwa ya kulinda usalama. Mnastahili pongezi. Tafadhalini,ondoeni zuio lenu ili CCM na wengine wafaidi matunda ya demokrasia ya vyama vingi.

Jeshi la polisi,tusaidieni CCM twende Dodoma kwa amani kumkabidhi uenyekiti wa chama Rais mpendwa John Pombe Magufuli. Wakati sisi CCM tukifurahi,wapinzani nao wafurahi. Muda wa kuondolewa zuio umewadia!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Singida)


Unaongea kwa kufumba fumba kama Mwanamke, wewe ni lazima mwanamke uliye naye anachepuka kwani wanawake hawapendi wanaume dhaifu!
 
Hivi ki sheria na kikatiba polisi wana hiyo amri au wanaitumia kwa kuwa Watanzania wengi hatujui sheria??
Nijuavyo mimi vyama vya siasa wanatakiwa kutoa taarifa tuu polisi kuhusu kusanyiko lao.
Na ikitokea polisi wanaona haita wezekana wachotakiwa kufanya ni kukutana na pande husika na kushauriana cha kufanya na sio mazuio ya ki intelijensia ambazo huonekana wakati wa mikutanao ya vyama vya upinzani tu. Na hiyo intelijensia haipo wakati wa rangi za kijani.
Polisi inatakiwa kuwa makini sana na hizi intelijensia zao.
 
Mkuu Jangwani hakuna polisi wakutosha siku hiyo kwa hiyo mkutano wa UKAWA hautaruhusiwa. Jeshi la wananchi litalinda Jangwani.

Polisi wote na magari yao yote mapya 700 yatakuwa Dodoma kulinda mkutano wa CCM. Hakuna haja ya kuondoa katazo. Huu wa sasa ni udikteta uchwara siku hiyo tunasimika udikteta pevu. Tega sikio.
 
Mkuu Jangwani hakuna polisi wakutosha siku hiyo kwa hiyo mkutano wa UKAWA hautaruhusiwa. Jeshi la wananchi litalinda Jangwani.

Polisi wote na magari yao yote mapya 700 yatakuwa Dodoma kulinda mkutano wa CCM. Hakuna haja ya kuondoa katazo. Huu wa sasa ni udikteta uchwara siku hiyo tunasimika udikteta pevu. Tega sikio.
Polisi wataondoa wenyewe zuio

Mzee Tupatupa
 
Haya yanaweza kutokea Tanzania pekee chini ya utawala wa hon.dr JPM
 
Kwenye ratiba za Ccm huwa wanamalizia kwa kumtambulisha mwenyekiti wao uwanja wa jamhuri Dodoma....patamu hapo...na bavicha wamesema wataenda pamoja na polisi kuuzuia mkutano huo ndani na nje!!
 
Humu kuna watu wambeya sana sijui wataacha lini! ccm hamuiwezi hata mkaloge.
 
Hivi ki sheria na kikatiba polisi wana hiyo amri au wanaitumia kwa kuwa Watanzania wengi hatujui sheria??
Nijuavyo mimi vyama vya siasa wanatakiwa kutoa taarifa tuu polisi kuhusu kusanyiko lao.
Na ikitokea polisi wanaona haita wezekana wachotakiwa kufanya ni kukutana na pande husika na kushauriana cha kufanya na sio mazuio ya ki intelijensia ambazo huonekana wakati wa mikutanao ya vyama vya upinzani tu. Na hiyo intelijensia haipo wakati wa rangi za kijani.
Polisi inatakiwa kuwa makini sana na hizi intelijensia zao.
Hakuna intelijensia yoyote. Wakishaambiwa kwamba wapinzani hawatakiwi kukutana wanatekeleza tu. Stori za intelijensia ni changa la macho tu. Na nina hakika katazo hawataliondoa, na CCM watafanya mkutano wao. Na siku hiyo kama kuna chama kingine kitapanga mkutano popote nchini nina hakika watakwenda kusambaratisha wahudhuriaji kwa sababu zile zile za hali tete ya amani nchini. na hoja hii ni kituko cha kuwatisha wananchi eti kuna hali tete ya amani, hivi ingekuwa kama Kenya ambako Alshabab wanafanya matukio ya kihalifu kila wiki, si tungeambiwa hata chooni tusiende?
 
Yani hawa policcm wanataka kuwageuza wapinzani kuwa kundi la ALQADA mana kila wakitaka kufanya mikutano yao policcm wanadai utafiti wa kiintelijensia zinaonyesha mkutano utapelekea uvunjifu wa amani? Mara mkutano sio halali na wakati policcm ndo katoa kibali cha kufanya mkutano, ila sishangai sana mana vyombo vya usalama hufundishwa kutumia nguvu na sio akili
 
Back
Top Bottom