Uchaguzi 2020 Jeshi la Polisi linawashikilia wanachama watatu wa CHADEMA kwa kughushi barua za chama cha SAU ili wachukue fomu za Ubunge!

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,615
141,443
Polisi mkoani Morogoro inawashikilia wanachama watatu wa Chadema walioghushi barua za utambulisho wakijifanya ni wanachama wa chama cha SAU na kutaka kuchukua fomu za kugombea ubunge kwa njia ya udanganyifu.

------
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Wilbrod Mutafungwa, alisema jeshi hilo lilipokea taarifa kutoka kwa Msimamizi wa Uchaguzi wa jimbo hilo, Sheila Lukuba, akitilia shaka barua ya utambulisho kutoka kwa Edga Msigwa akidai kuwa ni mwanachama wa SAU.

“Tulipopata taarifa ya kutilia shaka kutoka kwa msimamizi wa uchaguzi, tulifika ofisini kwake na tulipokagua hiyo barua tulikuta ina mapungufu na hata tulipochunguza tumebaini chama cha SAU hakina hata ofisi ya wilaya au mkoa ndani ya Morogoro,” alisema Mutafungwa.

Alisema baada ya kumhoji alikiri kuwa si mwanachama wa chama hicho bali alipewa barua hiyo na Christian Daniel ambaye ni mratibu wa uchaguzi wa madiwani wa manispaa ya Morogoro pamoja na dereva wa mgombea ubunge Jimbo la Morogoro Mjini kupitia CHADEMA aliyetambulika kwa jina moja la David.

Kamanda Mtagungwa alisema watuhumiwa wote watatu wanaendelea kuhojiwa ili kujua sababu zilizopelekea kufanya udanganyifu huo.

“Tunamshikiria huyu ni dereva wa Devotha Minja, mgombea kupitia CHADEMA, ndiye alitumia gari ya mbunge huyo kumbeba Edga Msigwa, ambaye alikuwa na barua ya kughushi kwa hiyo tumemkamata yeye pamoja na gari alilolitumia,” alisema Mutafungwa.

IPPMedia
 
Wamewakuta na kadi za uanachama wa chadema au wamedhibitisha vipi kama hao ni wanachama wa chadema ?
Polisi mkoani Morogoro inawashikilia wanachama watatu wa Chadema walioghushi barua za utambulisho wakijifanya ni wanachama wa chama cha SAU na kutaka kuchukua fomu za kugombea ubunge kwa njia ya udanganyifu.

Chanzo: EATV

Maendeleo hayana vyama!
 
JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro linawashikilia watu watatu kwa tuhuma za kufanya udanganyifu kwa kutengeneza barua bandia ya utambulisho kutoka Chama cha Sauti ya Umma (SAU) na kutaka kuchukua fomu ya kugombea ubunge Jimbo la Morogoro Mjini.

polisi.jpg


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Wilbrod Mutafungwa, alisema jeshi hilo lilipokea taarifa kutoka kwa Msimamizi wa Uchaguzi wa jimbo hilo, Sheila Lukuba, akitilia shaka barua ya utambulisho kutoka kwa Edga Msigwa akidai kuwa ni mwanachama wa SAU.

“Tulipopata taarifa ya kutilia shaka kutoka kwa msimamizi wa uchaguzi, tulifika ofisini kwake na tulipokagua hiyo barua tulikuta ina mapungufu na hata tulipochunguza tumebaini chama cha SAU hakina hata ofisi ya wilaya au mkoa ndani ya Morogoro,” alisema Mutafungwa.

Alisema baada ya kumhoji alikiri kuwa si mwanachama wa chama hicho bali alipewa barua hiyo na Christian Daniel ambaye ni mratibu wa uchaguzi wa madiwani wa manispaa ya Morogoro pamoja na dereva wa mgombea ubunge Jimbo la Morogoro Mjini kupitia CHADEMA aliyetambulika kwa jina moja la David.

Kamanda Mtagungwa alisema watuhumiwa wote watatu wanaendelea kuhojiwa ili kujua sababu zilizopelekea kufanya udanganyifu huo.

“Tunamshikiria huyu ni dereva wa Devotha Minja, mgombea kupitia CHADEMA, ndiye alitumia gari ya mbunge huyo kumbeba Edga Msigwa, ambaye alikuwa na barua ya kughushi kwa hiyo tumemkamata yeye pamoja na gari alilolitumia,” alisema Mutafungwa.


IPPMedia
 
Back
Top Bottom