Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,480
- 30,152
Ibara ya 13 ya Katiba yetu ya Jamhuri ya Tanzania inatamka hivi "Watu wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki bila ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sheria" mwisho wa kunukuu.
Nimetanguliza kunukuu ibara hiyo ya Katiba yetu, ili tutafakari kwa pamoja ili tuweze kujiridhisha kama kweli Jeshi letu la polisi linatekeleza kikamilifu ibara hiyo kwa vitendo.
Tujaribu kuangalia matukio kadhaa ya uhalifu, na jinsi yalivyoshughulikiwa na jeshi letu la polisi.
Alimwagiwa tindikali msaidizi wa Mufti wa Zanzibar, Sheikh Soraga, hadi hivi sasa hakujawahi kukamatwa watuhumiwa wowote wa tukio hilo.
Ameuawa kwa kupigwa risasi huko Zanzibar, Padri Mushi, wa kanisa katoliki. Hadi hivi leo, hakuna dalili yoyote, kama kuna kesi yoyote inayoendelea kuhusiana na tukio hilo.
Aliuawa mwandishi Mwangosi, huko MUfindi Iringa, na ushahidi wa picha ulimwonyesha wazi, askari aliyemfyatulia risasi, mwandishi Mwangosi, lakini pamoja na jeshi kufanya "maigizo" ya kumfikisha yule askari "masked" mahakamani, lakini hivi sasa, serikali yetu, imeifuta kimya kimya kesi hiyo!!
Ameteswa mwandishi nguli, Absolom Kibanda, hadi kunyofolewa jicho, na pamoja na afande Kova kutuhakikishia waTZ, wakati tukio hilo linatokea kuwa wote waliohusika na unyama huo, watatiwa mkononi mwa polisi, hivi sasa ni zaidi ya miezi 6, hakuna hata mtuhumiwa mmoja aliyetiwa mbaroni!!
Yalitokea mauaji kule Arusha kanisani, kutokana na bomu la kurushwa, pamoja na dereva wa bodaboda kutoa ushirikiano kwa polisi, kuhusiana na abiria aliyempakia, ambaye alimuona akirusha bomu hilo, jeshi la polisi hadi leo halijafanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo!
Kwenye mkutano wa Chadema, uliofanyika kwenye viwanja vya Soweto pale Arusha, palirushwa bomu lililosababisha mauaji ya raia kadhaa wasio na hatia, pamoja na kuwa mkutano huo ulikuwa na ulinzi wa jeshi la polisi, lakini mrushaji huo alifanikiwa "kuescape" toka eneo la tukio, na hadi leo hakuna hata mtu mmoja aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo!!
Lakini alipouawa RPC wa Mwanza. kamanda Barlow. iliwachukua polisi chini ya wiki wa 2, kuwakamata watuhumiwa wote, na kuwafikisha mahakamani!!
Kulipotumbukizwa clip kwenye mtandao, inayohusisha mazungumzo kati ya Kiongozi wa CDM, Wilfred Lwakatare na "Bukoba boy" iliwachukua masaa machache sana, jeshi la polisi, kukamilisha uchunguzi wao, na kuweza kumpandisha kizimbani Lwakatare na mwenzake, wakituhumiwa kwa kosa la jinai, la kutekeleza vitendo vya ugaidi!!
Hivi karibuni kumetolewa tuhuma nzito sana, zinazomhusisha, mbunge wa CCM, Juma Kapuya, akituhumiwa kwa kukabaka kabinti ka miaka 16, ambaye anasoma shule, na vile vile binti huyo huyo,anamtuhumu pia mbunge huyo, kwa kumtishia maisha, kwa kutuma sms kwa kutumia simu namba, ambayo imekuwa registered TCRA, kwa jina la Juma Kapuya, na pamoja na binti huyo kufungua jalada la mashtaka, kwenye kituo cha polisi cha Oysterbay, lakini hadi hivi leo, jeshi la polisi, linaendelea kushikwa na "kigugumizi" kwa kushindwa kumkamata, mbunge Kapuya na kumfungulia mashitaka!!
Lakini siku chache zilizopita, wakati Zitto Kabwe, alipoenda Central Police, na kufungua jalada la malalamiko kuwa Henry Kilewo, Katibu wa Chadema, mkoa wa Dar-es-salaam, anamtishia kumwuua, fasta sana polisi hao hao, wakamwita Henry Kileo kituoni na kumuhoji kwa masaa kadhaa!!
Miezi michache iliyopita, wakati mbunge Sugu, alipopost kwenye page yake ya facebook, kuwa Pinda ni m.p.u.m.b.a.v.u, haraka sana jeshi la polisi, lilimwita kituoni mbunge Sugu, kwa mahojiano ya masaa kadhaa!!
Hivi karibuni tumesikia kukamatwa kwa shehena kubwa ya pembe za ndovu huko Zanzibar na zile zilizokamatwa Mikocheni, Dar-es-salaam,lakini hadi hivi sasa, hakuna kesi yoyote, tunayosikia inaendelea kuhusiana na matukio hayo!
Kutokana na mlolongo wa matukio hayo niliyoyataja, zipo dalili za wazi na ushahidi usio na shaka yoyote kuwa, jeshi la polisi,inaelekea, linaelekezwa na watawala wetu, kuhusu wahalifu gani wa kuwakamata na nani wa kuwaacha, na hivyo kuifanya ibara ya 13 ya kwenye Katiba yetu, ambayo inataka usawa, kwa watu wote mbele ya sheria, kuonekana kama aina fulani ya "PAMBO" lililochomekwa tu, ndani ya Katiba yetu ya Jamhuri ya Tanzania!!!
Nimetanguliza kunukuu ibara hiyo ya Katiba yetu, ili tutafakari kwa pamoja ili tuweze kujiridhisha kama kweli Jeshi letu la polisi linatekeleza kikamilifu ibara hiyo kwa vitendo.
Tujaribu kuangalia matukio kadhaa ya uhalifu, na jinsi yalivyoshughulikiwa na jeshi letu la polisi.
Alimwagiwa tindikali msaidizi wa Mufti wa Zanzibar, Sheikh Soraga, hadi hivi sasa hakujawahi kukamatwa watuhumiwa wowote wa tukio hilo.
Ameuawa kwa kupigwa risasi huko Zanzibar, Padri Mushi, wa kanisa katoliki. Hadi hivi leo, hakuna dalili yoyote, kama kuna kesi yoyote inayoendelea kuhusiana na tukio hilo.
Aliuawa mwandishi Mwangosi, huko MUfindi Iringa, na ushahidi wa picha ulimwonyesha wazi, askari aliyemfyatulia risasi, mwandishi Mwangosi, lakini pamoja na jeshi kufanya "maigizo" ya kumfikisha yule askari "masked" mahakamani, lakini hivi sasa, serikali yetu, imeifuta kimya kimya kesi hiyo!!
Ameteswa mwandishi nguli, Absolom Kibanda, hadi kunyofolewa jicho, na pamoja na afande Kova kutuhakikishia waTZ, wakati tukio hilo linatokea kuwa wote waliohusika na unyama huo, watatiwa mkononi mwa polisi, hivi sasa ni zaidi ya miezi 6, hakuna hata mtuhumiwa mmoja aliyetiwa mbaroni!!
Yalitokea mauaji kule Arusha kanisani, kutokana na bomu la kurushwa, pamoja na dereva wa bodaboda kutoa ushirikiano kwa polisi, kuhusiana na abiria aliyempakia, ambaye alimuona akirusha bomu hilo, jeshi la polisi hadi leo halijafanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo!
Kwenye mkutano wa Chadema, uliofanyika kwenye viwanja vya Soweto pale Arusha, palirushwa bomu lililosababisha mauaji ya raia kadhaa wasio na hatia, pamoja na kuwa mkutano huo ulikuwa na ulinzi wa jeshi la polisi, lakini mrushaji huo alifanikiwa "kuescape" toka eneo la tukio, na hadi leo hakuna hata mtu mmoja aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo!!
Lakini alipouawa RPC wa Mwanza. kamanda Barlow. iliwachukua polisi chini ya wiki wa 2, kuwakamata watuhumiwa wote, na kuwafikisha mahakamani!!
Kulipotumbukizwa clip kwenye mtandao, inayohusisha mazungumzo kati ya Kiongozi wa CDM, Wilfred Lwakatare na "Bukoba boy" iliwachukua masaa machache sana, jeshi la polisi, kukamilisha uchunguzi wao, na kuweza kumpandisha kizimbani Lwakatare na mwenzake, wakituhumiwa kwa kosa la jinai, la kutekeleza vitendo vya ugaidi!!
Hivi karibuni kumetolewa tuhuma nzito sana, zinazomhusisha, mbunge wa CCM, Juma Kapuya, akituhumiwa kwa kukabaka kabinti ka miaka 16, ambaye anasoma shule, na vile vile binti huyo huyo,anamtuhumu pia mbunge huyo, kwa kumtishia maisha, kwa kutuma sms kwa kutumia simu namba, ambayo imekuwa registered TCRA, kwa jina la Juma Kapuya, na pamoja na binti huyo kufungua jalada la mashtaka, kwenye kituo cha polisi cha Oysterbay, lakini hadi hivi leo, jeshi la polisi, linaendelea kushikwa na "kigugumizi" kwa kushindwa kumkamata, mbunge Kapuya na kumfungulia mashitaka!!
Lakini siku chache zilizopita, wakati Zitto Kabwe, alipoenda Central Police, na kufungua jalada la malalamiko kuwa Henry Kilewo, Katibu wa Chadema, mkoa wa Dar-es-salaam, anamtishia kumwuua, fasta sana polisi hao hao, wakamwita Henry Kileo kituoni na kumuhoji kwa masaa kadhaa!!
Miezi michache iliyopita, wakati mbunge Sugu, alipopost kwenye page yake ya facebook, kuwa Pinda ni m.p.u.m.b.a.v.u, haraka sana jeshi la polisi, lilimwita kituoni mbunge Sugu, kwa mahojiano ya masaa kadhaa!!
Hivi karibuni tumesikia kukamatwa kwa shehena kubwa ya pembe za ndovu huko Zanzibar na zile zilizokamatwa Mikocheni, Dar-es-salaam,lakini hadi hivi sasa, hakuna kesi yoyote, tunayosikia inaendelea kuhusiana na matukio hayo!
Kutokana na mlolongo wa matukio hayo niliyoyataja, zipo dalili za wazi na ushahidi usio na shaka yoyote kuwa, jeshi la polisi,inaelekea, linaelekezwa na watawala wetu, kuhusu wahalifu gani wa kuwakamata na nani wa kuwaacha, na hivyo kuifanya ibara ya 13 ya kwenye Katiba yetu, ambayo inataka usawa, kwa watu wote mbele ya sheria, kuonekana kama aina fulani ya "PAMBO" lililochomekwa tu, ndani ya Katiba yetu ya Jamhuri ya Tanzania!!!